Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hadithi ya Sita ya Uwongo: Mungu Anakubali Mifano na Sanamu Zitumiwe Katika Ibada

Hadithi ya Sita ya Uwongo: Mungu Anakubali Mifano na Sanamu Zitumiwe Katika Ibada

Hadithi ya Sita ya Uwongo: Mungu Anakubali Mifano na Sanamu Zitumiwe Katika Ibada

Ni nini chanzo cha hadithi hiyo? “Wakristo wa mapema hawakutumia kamwe sanamu katika ibada yao . . . Kukubaliwa kwa sanamu kanisani katika karne ya 4 na ya 5 kulitetewa kwa msingi wa kwamba watu wasiojua kitu wangejifunza vizuri zaidi mafundisho ya Kikristo kupitia sanamu kuliko kupitia hotuba au vitabu.”— Cyclopedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature, cha McClintock na Strong, Buku la 4, ukurasa wa 503 na 504.

Biblia inasema nini? “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia.” (Kutoka 20:4, 5, Union Version) Mtume Yohana aliwaandikia hivi Wakristo wa karne ya kwanza: “Watoto wadogo, jilindeni na sanamu.”—1 Yohana 5:21.

Je, mifano ni njia tu ya kuabudu na kuheshimu kile ambacho inawakilisha, kama makanisa yanavyodai? Kitabu The Encyclopedia of Religion kinasema kwamba “huenda mwanzoni mifano ilitumiwa kwa ajili ya kufundisha na kupamba majengo; na angalau, ilitetewa kwa msingi huo. Lakini baadaye ilianza kutumiwa katika ibada. Ndivyo ilivyokuwa hasa kuhusu sanamu ambazo zilikuja kuwa sehemu ya maana sana ya Kanisa Othodoksi la Mashariki.” Hata hivyo, nabii Isaya aliuliza swali hili linalofaa: “Mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani?”—Isaya 40:18, UV.

Linganisha mistari hii ya Biblia: Isaya 44:13-19; Matendo 10:25, 26; 17:29; 2 Wakorintho 5:7

UKWELI:

Mungu hakubali mifano na sanamu zitumiwe katika ibada

KATAA HADITHI ZA UWONGO, SHIKAMANA NA KWELI

Tunaweza kukata kauli gani kutokana na mazungumzo hayo mafupi kuhusu hadithi za uwongo ambazo bado zinafundishwa leo na makanisa mengi? ‘Hadithi hizo [Kigiriki, myʹthos] zilizotungwa kwa werevu’ haziwezi kulinganishwa na kweli rahisi na zenye kufariji za Biblia.—2 Petro 1:16, UV.

Kwa hiyo, usisite kulinganisha kwa unyoofu Neno la Mungu, chanzo cha kweli, na mambo ambayo umefundishwa. (Yohana 17:17) Kisha, utaona ahadi hii ikitimizwa katika maisha yako: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.”—Yohana 8:32.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.