Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Wakati Uliowekwa” Umekaribia

“Wakati Uliowekwa” Umekaribia

“Wakati Uliowekwa” Umekaribia

KAMA nabii Habakuki, wanafunzi wa Yesu walitamani sana kuona kuteseka kukiisha. Baada ya kujua yale ambayo Ufalme wa Mungu utafanya ili kurekebisha mambo duniani, walimwuliza Yesu hivi: “Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako [katika mamlaka ya Ufalme] na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3) Yesu aliwaambia kwamba Yehova Mungu peke yake ndiye anayejua wakati hususa ambapo Ufalme huo utatawala kwa ukamili juu ya dunia. (Mathayo 24:36; Marko 13:32) Hata hivyo, Yesu na wengine walitabiri mambo fulani ambayo yangetukia duniani kuonyesha kwamba wakati huo ulikuwa umekaribia.—Ona  sanduku upande wa kulia.

Je, hukubali kwamba hayo ni mambo ya kawaida leo? Yesu pia alitabiri kwamba kazi ya kuwaelimisha watu itafanywa duniani pote. Alisema: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.

Kazi hiyo inatimizwa leo na Mashahidi wa Yehova. Katika nchi 236 hivi, Mashahidi zaidi ya milioni saba wanawaambia watu mambo ambayo Ufalme utatimiza, na wanawasaidia kupatanisha maisha yao na matakwa ya uadilifu ya Mungu, ambaye mapenzi yake ni kukomesha kuteseka na maumivu. Endelea kujifunza kuhusu Ufalme wa Mungu, nawe utakuwa na tumaini la kuishi milele katika ulimwengu usio na kuteseka.

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

 Maandiko Yanayoonyesha Tunaishi Siku za Mwisho

MATHAYO 24:6, 7; UFUNUO 6:4

• Vita visivyo na kifani

MATHAYO 24:7; MARKO 13:8

• Matetemeko makubwa ya nchi

• Upungufu wa chakula

LUKA 21:11; UFUNUO 6:8

• Tauni

MATHAYO 24:12

• Kuongezeka kwa uasi-sheria

• Upendo kupoa

UFUNUO 11:18

• Kuharibiwa kwa dunia

2 TIMOTHEO 3:2

• Kupenda pesa kupita kiasi

• Kutotii wazazi

• Kujipenda kupita kiasi

2 TIMOTHEO 3:3

• Kutokuwa na upendo wa asili

• Watu wasiotaka makubaliano yoyote

• Watu wa matabaka yote ya jamii wanakosa kujizuia

• Kutopenda mema kwaenea

2 TIMOTHEO 3:4

•Kupenda raha badala ya kumpenda Mungu

2 TIMOTHEO 3:5

• Wengi wanadai kwa unafiki kuwa ni Wakristo

MATHAYO 24:5, 11; MARKO 13:6

• Kuwepo kwa manabii wengi wa uwongo

MATHAYO 24:9; LUKA 21:12

•Kuteswa kwa Wakristo wa kweli

MATHAYO 24:39

• Watu hawajali maonyo ya Biblia

[Picha katika ukurasa wa 8]

Duniani pote, Mashahidi wa Yehova wanawafundisha watu kuhusu Ufalme wa Mungu