Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Mungu anaweza kukufanya uwe tajiri katika njia gani?

Zamani, Yehova aliwabariki watu fulani kama vile Abrahamu na Sulemani kwa kuwapa utajiri wa kimwili. Lakini utajiri ambao Wakristo wanahitaji zaidi na ambao Mungu anaweza kuwapa unatia ndani imani, amani, uradhi, na furaha.—9/1, ukurasa wa 3-7.

• Ni somo gani tunalojifunza kutokana na hatua ya Yesu ya kumwokoa Petro alipokuwa akizama baharini? (Mt. 14:28-31)

Tukitambua kwamba ndugu fulani anaonekana hana imani, tunaweza kuunyosha mkono wetu kwa njia ya mfano na kumsaidia kuwa na imani zaidi.—9/15, ukurasa wa 8.

• Yehova alijidhabihu kadiri gani ili kutukomboa?

Yehova alivumilia kumwona Mwana wake akiteswa na kudhihakiwa. Utayari wa Abrahamu wa kumtoa mwana wake, ulionyesha jinsi ambavyo Yehova alivumilia kumwona Mwana wake akiuawa kama mhalifu.—9/15, ukurasa wa 28-29.

• kwa nini Kodeksi ya Vatikani ni yenye thamani sana?

Ni hati ya Kigiriki iliyoandikwa miaka isiyozidi 300 baada ya Biblia kukamilishwa. Ina karibu Maandiko yote ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Inatumiwa na wasomi ili kujua mambo yaliyokuwa katika maandishi ya awali ya Biblia.—10/1, ukurasa wa 18-20.

• Tunajifunza somo gani kwenye andiko la Methali 24:27 kuhusu ‘kujenga nyumba’?

Mwanamume ambaye anataka kuoa anahitaji kujitayarisha kwa ajili ya daraka hilo. Hilo linatia ndani kujitayarisha kuiandalia familia mahitaji ya kimwili na kuiongoza katika mambo ya kiroho.—10/15, ukurasa wa 12.

• kwa nini haifai kusema kwamba Mashahidi wa Yehova ni dini ya Kiprotestanti?

Uprotestanti ulianza karne ya 16 huko Ulaya katika jitihada za kuleta marekebisho katika Dini ya Katoliki. Neno “Uprotestanti” linawahusu wale wanaounga mkono malengo ya Marekebisho hayo Makubwa ya Kidini. Mashahidi wa Yehova hawatambui mamlaka ya ulimwenguni pote ya papa na wanaunga mkono kwa moyo wote mamlaka ya Biblia, hata hivyo, wanapinga mazoea na mafundisho mengi yasiyo ya kimaandiko ambayo yako katika dini za Kiprotestanti.—11/1, ukurasa wa 19.

• Je, mtu anahitaji kujifunza Kiebrania na Kigiriki ili aelewe Biblia?

Hapana. Kujua lugha hizo hakumaanishi kwamba mtu ataweza kuelewa ujumbe wa Biblia. Mtu ambaye amejifunza lugha hizo bado anategemea kamusi na vitabu vya lugha. Uhakika wa kwamba Mungu alitumia roho yake kuhifadhi maneno ya Mtumishi wake mkuu zaidi katika tafsiri, unaonyesha kwamba mtu anaweza kutumia Biblia zilizotafsiriwa katika lugha za sasa na kujifunza kweli.—11/1, ukurasa wa 20-23.

• Yehova na Yesu walituwekea jinsi gani mfano katika kuonyesha adabu?

Hata ingawa Yehova ana cheo kikubwa, anawatendea wanadamu kwa fadhili na heshima. Yehova alipozungumza na Abrahamu na Musa, alitumia neno la Kiebrania ambalo mara nyingi linatafsiriwa “tafadhali.” (Mwa. 13:14; Kut. 4:6) Pia, Mungu anawasikiliza wanadamu. (Mwa. 18:23-32) Yesu pia aliwasikiliza, na alikuwa tayari kuwasaidia wengine, na mara nyingi hata aliwaita kwa majina yao.—11/15, ukurasa wa 25.

• kwa nini Wakristo wa kweli wanaepuka kusherehekea Mwaka Mpya?

Sherehe ya Mwaka Mpya ni sherehe muhimu katika kalenda za Asia. Mara nyingi sherehe hiyo imekusudiwa kuwatakia watu bahati nzuri na kuonyesha heshima kwa pepo. Wakristo wanawaheshimu wazazi wao, lakini hawashiriki karamu ambazo zimekusudiwa kutafuta ulinzi wa mababu waliokufa au kuipendeza miungu ya familia.—12/1, ukurasa wa 20-23.