Ona video zinazopatikana

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Nini njo ilichochea Rasta fulani akate nywele zake na aache kubagua wazungu? Nini njo ilichochea kijana mwanaume mwenye alikuwa nakusanya makuta kwa ajili ya watu wenye kuuzisha dawa za kulewesha abadilishe maisha yake? Tuache watuelezee.

“Nilifikia kuachana na ubaguzi.”​—HAFENI NGHAMA

IKO NA MIAKA: 34

INCHI: ZAMBIA

ALIKUWA: RASTA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa mu kambi ya wakimbizi mu inchi ya Zambia. Mama yangu alikuwa amekimbia kutoka Namibia wakati wa vita na alikuwa amejiunga na Shirika ya Watu wa Kusini Mangaribi mwa Afrika (SWAPO). Ile shirika ilikuwa inapinga serikali ya Afrika ya Kusini yenye ilikuwa natawala Namibia ile wakati.

Niliptisha miaka 15 ya kwanza-kwanza ya maisha yangu mu kambi mbalimbali za wakimbizi. Watoto wenye walikuwa mu kambi za SWAPO walifundishwa kupigania uhuru. Tulifundishwa mambo ya politike na tulifundishwa pia kuchukia wazungu.

Wakati nilikuwa na miaka 11, nilipenda kuwa Mukristo na kuwa muamini wa kanisa fulani yenye ilikuwa mu kambi. Mu ile kanisa, Wakatoliki, Waluteri, Waanglikani na watu wa dini zingine, walikuwa naabudu pamoya. Pastere mwenye nilizungumuza naye, aliniambia nisifanye vile. Kuanzia ile wakati, nikaacha kuamini kama Mungu anakuwaka. Lakini wakati nilikuwa na miaka 15, nilijiunga na kikundi ya Warasta juu nilikuwa napenda muziki wa reggae na nilipenda kupiganisha ukosefu wa haki wenye Waafrika weusi walitendewa. Nilikomalisha nywele, nikaanza kuvuta marijuana, nikaacha kukula nyama, na nikaanza kupigania uhuru wa watu weusi. Lakini, sikuacha mwenendo wangu muchafu na sikuacha kuangalia filme za jeuri. Na niliendelea kutumia maneno machafu.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Mu 1995, wakati nilikua na miaka 20, nilianza kufikiria sana pia namna nitatumia maisha yangu. Nilikuwa nasoma vitabu vyote vya Warasta vyenye nilikuwa napata. Vitabu fulani vilikuwa vinataya Biblia, lakini nilikuwa naona kama mafasirio yenye vilikuwa vinatoa haiko ku mustari. Kwa hiyo niliamua kujisomea Biblia miye peke.

Kisha, rafiki yangu mwenye naye alikuwa Rasta alinipatia kitabu ya kusaidia kujifunza Biblia yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Nilijifunza ile kitabu miye peke na niko nailinganisha na Biblia. Kisha, nilikutana na Mashahidi wa Yehova na nikaendelea kujifunza nao Biblia.

Nilijikaza sana, na nikafikia kuacha kuvuta na kunywa sana pombe. (2 Wakorinto 7:1) nilibadilisha namna yangu ya kuonekana, nikakata nywele zangu, nikaacha kuangalia pornografia na filme za jeuri na nikaacha kutumia maneno machafu. (Waefeso 5:3, 4) Nilifikia hata kuacha kubagua wazungu. (Matendo 10:34, 35) Juu niweze kufanya ile mabadiliko, niliacha kusikiliza miziki yenye ilichochea ubaguzi wa rangi, na nikaachana na marafiki wangu wa zamani wenye walikuwa najaribu kunichochea nirudilie maisha yangu ya zamani.

Kisha kufanya ile mabadiliko, nilitafuta Jumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova, na nikaomba niingie mu dini yao. Walikuwa najifunza Biblia na miye. Wakati niliamua kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, familia yangu haikufurahi. Mama yangu aliniambia nichague “dini ingine,” lakini hapana ya Mashahidi wa Yehova. Mujomba wangu fulani, mwenye alikuwa na cheo mu guvernema, mara mingi alinichambua-chambua juu ya uamuzi wangu wa kujiunga na Mashahidi wa Yehova.

Lakini, kujifunza namna Yesu alitendea watu na kutumikisha mashauri yake kulinisaidia kuvumilia wakati watu walikuwa nanipinga na kunicheka. Wakati nililinganisha mambo yenye Mashahidi wanafundisha na mambo yenye Biblia inasema, nilikuwa hakika kama nimepata dini ya kweli. Kwa mufano, wanafuata amri ya Biblia ya kuhubiria wengine. (Matayo 28:19, 20; Matendo 15:14) Pia, hawajiingize mu mambo ya politike.​—Zaburi 146:3, 4; Yohana 15:17, 18.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yangu kumenisaidia mu mambo mingi. Kwa mufano, kuacha kuvuta marijuana kumenisaidia nisikuwe napoteza makuta mingi kila mwezi. Sionake tena mambo yenye mutu anaonaka kisha kuvuta bangi, na akili yangu iko natumika muzuri zaidi, na afya yangu pia imekuwa muzuri zaidi.

Sasa niko na maisha ya muzuri na yenye furaha yenye nilikuwaka natafuta tangu wakati nilikuwa kijana. Na zaidi ya yote, nimekuwa rafiki ya Mungu.​—Yakobo. 4:8.

“Nimejifunza kuzuia kasirani yangu.”​—MARTINO PEDRETTI

IKO NA MIAKA: 43

INCHI: AUSTRALIA

ALIKUWA: NAUZISHA DAWA ZA KULEWESHA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Wakati nilikuwa mudogo, familia yetu ilikuwa nahama-hama. Tuliishi mu miji ya kidogo-kidogo, mu muji mukubwa, na kwa wakati fulani mu eneo ya mashamba ya wenyeji wa Australia. Ningali nakumbuka mambo ya muzuri yenye tulikuwa nafanya na binamu zangu na wajomba wangu; tulikuwa navua samaki, tulikuwa nawinda, tulikuwa natengeneza vitu vya kuwinda navyo, na kuchonga vitu vingine.

Baba yangu alikuwa boxeur na alianza nifundisha kupigana tangu wakati nilikuwa mudogo sana. Nilipenda jeuri sana. Wakati nilikuwa kijana, nilikuwa nakunywa sana, fasi za kukunyia pombe. Miye na marafiki wangu tulikuwa nachokoza watu juu tu tupigane. Tulikuwa natumia visu na fimbo za kuchezea besiboli juu ya kushambulia vikundi vya watu 20 ao zaidi.

Juu nipate makuta, nilikuwa nauzisha dawa za kulewesha na vitu vyenye watu wenye walikuwa natumika ku bandari walikuwa naiba. Nilikuwa nalipisha makuta kwa ajili ya wenye kuuzisha dawa za kulewesha, Nilikuwa natumia bunduki juu ya kuogopesha wenye walikuwa na madeni ili walipe. Nilipenda kuwa mutu mwenye watu watakuwa nalipa juu ya kuua wengine. Nilikuwa najiambia hivi: Ua mbele wakuue.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Wakati nilikuwa nakomala, nilisikiaka mambo fulani kuhusu Mashahidi wa Yehova. Wakati nilikuwa na miaka 20 hivi, ninakumbuka, niliulizaka mama yangu ikiwa anajua kwenye ninaweza kupata Shahidi wa Yehova. Kisha siku mbili, Shahidi mwenye kuitwa Dixon aligonga ku mulango yangu. Tulizungumuza naye kwa wakati fulani, na kisha akanialika ku mukutano wa Mashahidi wa Yehova. Nilienda ku ile mukutano. Miaka 20 imepita tangu ile wakati na siyaachaka kuenda ku mikutano. Shahidi wa Yehova alitumia Biblia ili kujibia maulizo yote yenye nilikuwa nayo.

Nilifurahi kujifunza kama Yehova anahangaikia kila mutu, hata wale wenye hawamutumikie. (2 Petro 3:9) Nilijifunza kama Yehova ni Baba mwenye upendo, mwenye atanihangaikia hata kama wengine wote wananiacha. Pia, nilitiwa moyo kujua kama atasamehe zambi zangu kama ninabadilika. Andiko ya Waefeso 4:22-24 ilinigusa sana. Ile andiko ilinitia moyo ‘niondoe utu wa zamani’ na “kuvaa utu mupya wenye uliumbwa kupatana na mapenzi ya Mungu.”

Haikukuwa mwepesi kwangu kubadilika. Sikutumia dawa za kulewesha kuanzia Siku ya Kwanza mupaka Siku ya Tano, lakini wakati nilikutana tena na marafiki wangu siku ya Posho na Siku ya Yenga, nilitumia tena dawa za kulewesha. Nilitambua kama nilipaswa kuenda mbali na marafiki wangu juu niweze kusafisha maisha yangu. Kwa hiyo, niliamua kuhamia mu jimbo ingine. Marafiki fulani waliomba wanisindikize, na nikakubali. Wakati tulikuwa mu safari, walianza kuvuta marijuana na wakanipatia na miye nivute. Niliwaambia kama nilishaachana na ile tabia, kwa hiyo, wakati tulifika ku mipaka, wakaniacha na nikaendelea miye peke na safari yangu. Kisha wakati fulani, nilipata habari kama wale marafiki wangu walishambulia banke fulani kwa kutumia bunduki na wakaiba makuta.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Kisha tu kuachana na wale marafiki, ilikuwa mwepesi zaidi kubadilisha maisha yangu. Mu 1989, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Kisha kubatizwa, dada yangu, mama yangu, na baba yangu, nao walikubali kweli na wakaanza kumutumikia Yehova.

Sasa nimefanya miaka 17 mu ndoa na niko na watoto wa tatu wazuri. Nimejifunza kuzuia kasirani yangu, hata wakati watu wananichokoza. Na nimejifunza kupenda watu kila ‘kabila na kikundi cha watu na luga.’ (Ufunuo 7:9) Nimeona kama Yesu alisemaka kweli wakati alisemaka hivi: “Kama munakaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, na mutajua kweli, na kweli itawaweka ninyi huru.”​—Yohana 8:31, 32.

[Wazo ya fungu]

Juu niweze kubadilika, niliacha kusikiliza miziki yenye ilichochea ubaguzi wa rangi

[Wazo ya fungu]

Miye na marafiki wangu tulikuwa nachokoza watu juu tu tupigane. Tulikuwa natumia visu na fimbo za kuchezea besiboli juu ya kushambulia vikundi vya watu 20 ao zaidi