Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu Kristo—Nguvu ya Ujumbe Wake

Yesu Kristo—Nguvu ya Ujumbe Wake

Yesu Kristo—Nguvu ya Ujumbe Wake

“Bila shaka jambo linalothibitisha kwamba mtu huyu mwenye hekima kutoka Kapernaumu alikuwa mtu wa pekee ni kwamba bado watu wanauamini na kuupenda ujumbe wake.” *—MWANDISHI GREGG EASTERBROOK.

MANENO yana nguvu. Yanapochaguliwa vizuri, yanaweza kuchochea mioyo ya watu, kuwapa tumaini, na kubadili maisha yao. Hakuna mtu mwingine ambaye amewahi kusema maneno yenye nguvu kama Yesu Kristo. Mtu fulani aliyesikiliza Mahubiri ya Mlimani ya Yesu, aliandika hivi baadaye: “Basi wakati Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati ukashangazwa na njia yake ya kufundisha.”—Mathayo 7:28.

Mpaka leo hii, watu duniani kote wanajua semi nyingi za Yesu. Fikiria baadhi ya semi zake zenye kujaa maana.

“Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.”—Mathayo 6:24.

“Mambo yote mnayotaka watu wawatendee ninyi, lazima mwatendee wao pia vivyo hivyo.”—Mathayo 7:12.

“Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”—Mathayo 22:21.

“Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.

Yesu alifanya mengi zaidi ya kusema semi muhimu na zisizosahaulika. Ujumbe aliohubiri ulikuwa wenye nguvu kwa sababu ulifunua ukweli kumhusu Mungu, uliwapa watu kusudi maishani, na ulionyesha wazi kwamba suluhisho la matatizo ya wanadamu ni Ufalme wa Mungu. Tunapochunguza mafundisho ya Yesu katika kurasa zinazofuata, tutaona kwa nini mamilioni ya watu bado “wanauamini na kuupenda ujumbe wake.”

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 2 Kapernaumu lilionwa kuwa jiji la nyumbani la Yesu katika eneo la Galilaya.—Marko 2:1.