Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Onyesha Usadikisho!

Onyesha Usadikisho!

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Onyesha Usadikisho!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yeremia, Ebed-meleki, Mfalme Sedekia

Muhtasari: Yeremia anapingwa vikali sana anapotangaza ujumbe wa Mungu kwamba watu wa Yuda wanapaswa kujisalimisha kwa Wakaldayo.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA YEREMIA 38:1-5.

Unafikiri Yeremia alihisi namna gani alipokuwa akizungumza na watu wa Yuda?

․․․․․

Unafikiri sauti ya Yeremia ilionyesha hisia gani alipotangaza onyo la Yehova?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Yeremia alikuwa na usadikisho gani ambao ulimwezesha kutoa tangazo hilo kwa ujasiri?

․․․․․

2 CHUNGUZA TUKIO HILO.—SOMA YEREMIA 38:6-13.

Unawazia tangi hilo la maji lilikuwa na umbo, upana, kina, na harufu gani?

․․․․․

Huenda Yeremia alikuwa na mawazo gani alipoanza “kuzama katika yale matope”? (Soma tena mstari wa 6.)

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Ukitumia vifaa vya kufanyia utafiti unavyoweza kupata, chunguza jambo ambalo hukujua kuhusu matangi ya maji yaliyotumiwa nyakati za Biblia.

․․․․․

Ebed-meleki alisadiki nini alipoomba Yeremia aokolewe? (Soma tena mistari ya 7-9.)

․․․․․

Kwa nini Sedekia alishawishiwa kwa urahisi sana, kwanza na wakuu na baadaye na Ebed-meleki? (Soma tena mstari wa 5 na 10.) Hilo linaonyesha nini kuhusu utu wake? jinsi alivyokosa usadikisho?

․․․․․

Ni watu gani katika simulizi hili ambao walionyesha usadikisho wenye nguvu, na ni nani ambaye hakuonyesha? Kwa nini unajibu hivyo?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Ujasiri.

․․․․․

Usadikisho.

․․․․․

Jinsi Yehova anavyowalinda wale wanaomtii bila kuogopa.

․․․․․

Kuwa na usadikisho kunaweza kukusaidia jinsi gani kufanya yaliyo sawa unapokabili mkazo?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

SOMA HABARI ZAIDI ZA BIBLIA, KWENYE INTANETI www.watchtower.org