Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Kusali?

Juu ya Nini Tuko na Lazima ya Kusali?

WATU wengi wanapendaka kujua mambo yenye Biblia inasema juu ya sala. Ona maulizo 7 yenye watu wanazoeaka kujiuliza juu ya sala; kisha tuchunguze pamoja namna Biblia inajibia ile maulizo. Hizi habari ziko na kusudi ya kukusaidia uanze kusali. Na kama tayari unakuwaka unasali, zitakusaidia ukuwe unasali mu njia yenye itafanya Mungu asikilize sala zako.

MU dunia yote, mu kila desturi na dini, watu wanakuwaka wanasali. Wanakuwaka wanasali peke yao, ao mu vikundi. Wanakuwaka wanasali mu makanisa, mu mahekalu, mu masinagogi, mu misikiti, na fasi zingine za ibada. Wanatumikishaka vitu mbalimbali wakati wako wanasali, sawa vile vitabu vya sala, bushanga, sanamu, ao vitu vingine.

Wanadamu wako tofauti na viumbe vingine vyote ku dunia juu wao tu njo wanakuwaka wanasali. Kwa kweli, kuko mambo yenye tunafanyaka yenye wanyama nao wanafanyaka. Kwa mufano, sawa vile wanyama, tunakulaka, tunapumuaka, na tunakunywaka maji. Tena, siye wote tunazaliwaka, tunaishi, tunazeeka, na tunakufaka. (Muhubiri 3:19) Lakini, ni wanadamu tu njo wanakuwaka wanasali. Juu ya nini?

Bila kuenda huku na huku, jibu ni: tuko na lazima ya kusali. Watu wengi wanakuwaka wanasali juu wanapenda kuzungumuza na Mungu. Biblia inaonyesha kama Mungu alituumba na tamaa ya kufanya vile. (Muhubiri 3:11) Yesu Kristo alisemaka hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho.”​—Matayo 5:3.

Kuko nafasi za mingi kwenye watu wanaendaka kuabudu na kusali. Ile yote inaonyesha kama siye wote tuko na mahitaji ya kiroho. Kusema kweli, watu wengi wanawazaka kama wanaweza kujitimizia wao wenyewe mahitaji yao ya kiroho ao kama wengine wanaweza kuwasaidia kutimiza ile mahitaji. Hata vile, hauone kama wanadamu hawana uwezo wa kujitimizia ile mahitaji? Siye wanadamu tuko na mipaka, maisha yetu ni ya mufupi, na kuko mambo mingi yenye hatuelewake. Tuko na lazima ya mutu wa kutusaidia kutimiza mahitaji yetu ya kiroho. Ule mutu anapaswa kuwa na hekima na nguvu kutushinda, na anapaswa kuishi muda murefu kutushinda. Ile mahitaji ya kiroho ni gani?

Waza kidogo: Kuko wakati ulikuwa kabisa na lazima ya kupata muongozo, hekima, ao majibu ya maulizo yenye ulionaka kama hakuna mwanadamu mwenye anaweza kujibia? Kuko siku ulikuwaka na lazima ya faraja kisha mutu mwenye ulikuwa unapenda sana kufa? Ao kuko siku ulikuwaka na lazima ya muongozo juu ukamate uamuzi fulani wa maana sana? Ao kuko wakati ulikuwaka na lazima kabisa ya kusamehewa juu zamiri ilikuwaka inakuhangaisha juu ya jambo fulani yenye ulifanya?

Biblia inaonyesha kama ni sawa kabisa kusali juu ya ile mambo yote. Biblia inaweza kukusaidia ujue namna ya kusali na mambo ya kusema mu sala, juu mu Biblia muko sala za wanaume na wanamuke wenye walikuwaka wanamutumikia Mungu kwa uaminifu. Walisali juu ya kuomba Mungu awafariji, awaongoze, awasamehe, na ajibie maulizo yenye ilikuwa inawahangaisha.​—Zaburi 23:3; 71:21; Danieli 9:4, 5, 19; Habakuki 1:3.

Hata kama hawakusali juu ya mambo ileile, wote walijua jambo moja ya maana sana juu ya sala, jambo yenye watu wengi leo hawajue ao hawatiake mu akili. Walijua ni nani njo tunapaswa kusali kwake.