Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunapaswa Kusali kwa Nani?

Tunapaswa Kusali kwa Nani?

MUNGU anasikilizaka sala zote? Vile njo watu wengi wanawazaka leo. Watu wengi wanawazaka kama dini zote ni za muzuri. Kwa hiyo, hata usali kwa mungu gani, ni sawa tu. Lakini, ile ni kweli kabisa?

Biblia inafundisha kama mara mingi watu hawakuwake wanasali kwa Mungu wa kweli. Zamani wakati Biblia iliandikwa, watu walizoea kusali kwa sanamu. Lakini, mara kwa mara Mungu aliwapatia angalisho juu ya ile tabia. Kwa mufano, Zaburi 115:4-6 inasema hivi juu ya sanamu: “Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia.” Mambo iko wazi: Kusali kwa mungu mwenye hawezi kukusikia, ni kuchokea bure.

Habari fulani ya Biblia inatusaidia kuelewa ile jambo. Nabii wa kweli Eliya aliambiaka manabii wa Baali wasali kwa mungu wao, na kisha yeye atasali kwa Mungu wake. Eliya alisema kama Mungu wa kweli atajibia, lakini mungu wa uongo hatajibia. Manabii wa Baali waliitika kufanya vile. Walisali kwa bidii kwa wakati murefu, na walilia kwa sauti. Lakini, mungu wao hakuwajibia! Biblia inasema hivi: “Hakuna mutu yeyote mwenye alijibu; hakuna mwenye aliwasikiliza.” (1 Wafalme 18:29) Lakini mambo ilikuwa namna gani wakati Eliya alisali?

Kisha Eliya kusali, Mungu wake alijibia palepale. Alituma moto na ukateketeza zabihu ya Eliya. Juu ya nini sala ya Eliya njo ilijibiwa? Mu sala ya Eliya, yenye inapatikana mu 1 Wafalme 18:36, 37, muko jambo fulani ya maana yenye ilifanya Mungu ajibie sala ya Eliya. Sala yake haikukuwa hata ya murefu. Mu Kiebrania ya zamani, ile sala iko tu na maneno 30 hivi. Lakini, mu ile maneno kidogo, Eliya alisali kwa Mungu na kutaya jina yake ya pekee, Yehova, mara tatu.

Baali, mwenye jina yake inamaanisha “mumiliki” ao “bwana,” alikuwa mungu wa Wakanaani, na walikuwa wanamuita mu majina mbalimbali kulingana na fasi kwenye walikuwa wanaishi. Lakini, Yehova ni jina ya pekee ya Mungu mumoja tu mu ulimwengu wote muzima. Ule Mungu aliambiaka watu wake hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; sipatie mutu yeyote utukufu wangu.”​—Isaya 42:8.

Juu ya nini sala ya Eliya ilijibiwa lakini sala za manabii wa Baali hazikujibiwa? Wakati watu walikuwa wanaabudu Baali, walikuwa wanafanya uasherati na kumutolea Baali zabihu za wanadamu. Lakini, ibada ya Yehova iliheshimisha watu wake, Waisraeli, na iliwaepusha na ile matendo ya mubaya. Wazia hii jambo: Kama unapenda kutumia barua rafiki yako mwenye unaheshimia sana, utaituma ku jina ya mutu mwingine na mwenye iko na tabia za mubaya zenye ziko tofauti na zile za rafiki yako? Hapana!

Mambo yenye Eliya aliambiaka manabii wa Baali wafanye inaonyesha kama Mungu hasikilizake sala zote

Wakati unasali kwa Yehova, unasali kwa Muumbaji na Baba ya wanadamu wote. * Nabii Isaya alisali hivi: “Wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu.” (Isaya 63:16) Na ule njo Mungu mwenye Yesu alizungumuzia wakati aliambia wanafunzi wake hivi: “Ninapanda kuenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.” (Yohana 20:17) Yehova njo Baba ya Yesu. Yeye njo Mungu mwenye Yesu alikuwa anasali kwake na kufundisha wanafunzi wake wakuwe wanasali kwake.​—Matayo 6:9.

Je, Biblia inasema kama tunapaswa kusali kwa Yesu, kwa Maria, kwa watakatifu, ao kwa malaika? Hapana. Tunapaswa kusali kwa Yehova tu. Juu ya nini? Tuone sababu mbili. Ya kwanza, sala ni ibada, na Biblia inasema kama Yehova tu njo tunapaswa kuabudu. (Kutoka 20:5) Ya pili, Biblia inaonyesha kama yeye tu njo “musikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Hata kama Yehova anapatiaka wengine kazi mbalimbali, hakuna mwenye alishakapatia kazi ya kusikiliza sala. Ameahidi kusikiliza sala zetu yeye mwenyewe.

Njo maana, kama unapenda Mungu asikilize sala zako, usisahau hii maneno yenye Biblia inasema: “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.” (Matendo 2:21) Lakini, Yehova anasikilizaka sala zote? Ao kuko mambo ingine yenye tunapaswa kujua kama tunapenda akuwe anasikiliza sala zetu?

^ Watu wa dini fulani wanasema kama ni mubaya kutaya jina ya pekee ya Mungu, hata mu sala. Lakini, ile jina inapatikana karibu mara 7000 mu luga zenye zilitumiwa kuandika Biblia, zaidi sana mu sala za watumishi waaminifu wa Yehova zenye ziko mu kitabu ya Zaburi.