Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunapaswa Kusali Namna Gani?

Tunapaswa Kusali Namna Gani?

DINI za mingi zinakazia kama mutu anapaswa kuwa mu hali fulani wakati iko anasali. Kwa mufano, anapaswa kusali na iko mwenye kusimama, kuikala, ao kupiga magoti. Tena, zinatia mukazo juu ya maneno yenye anapaswa kutia mu sala, na desturi fulani zenye anapaswa kufuata wakati iko anasali. Lakini, Biblia inatusaidia tujue mambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kufikiria juu ya namna ya kusali.

Biblia inaonyesha kama watumishi waaminifu wa Mungu walikuwa wanasali mu hali mbalimbali. Wamoja walisali kimya-kimya, na wengine walisali kwa sauti, kupatana na hali yenye walikuwa ndani. Wamoja walisali na wako wanaangalia mbinguni, na wengine walisali na wako wenye kuinama. Hawakukuwa wanatumia sanamu, bushanga, ao vitabu vya sala. Lakini walikuwa wanamuambia Mungu maneno yenye inatoka mu moyo wao. Ni nini ilifanya Mungu asikilize sala zao?

Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, walikuwa wanasali kwa Mungu mumoja tu, Yehova. Kuko jambo ingine ya maana yenye ilifanya Mungu asikilize sala zao. 1 Yohana 5:14 inaonyesha ile jambo. Inasema hivi: “Huu ndio uhakika wenye tuko nao kwake, kwamba hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” Tunapaswa kusali kupatana na mapenzi ya Mungu. Maana yake nini?

Juu tusali kupatana na mapenzi ya Mungu, tunapaswa kwanza kuijua. Njo maana, kujifunza Biblia ni jambo ya maana yenye itatusaidia tujue namna ya kusali juu Mungu atusikie. Ni kusema juu Mungu atusikie, inaomba tu tujue sana Biblia? Hapana, lakini Mungu anapenda tujifunze mapenzi yake, tujikaze kuielewa, na tutumikishe mu maisha yetu mambo yenye tuko tunajifunza. (Matayo 7:21-​23) Tunapaswa kusali kupatana na mambo yenye tunajifunza.

Juu Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kusali kupatana na mapenzi yake, kuwa na imani, na kusali mu jina ya Yesu

Wakati tunajifunza juu ya Yehova na mapenzi yake, imani yetu inaongezeka. Na ile ni jambo ingine ya maana, juu tunapaswa kuwa na imani juu Mungu asikilize sala zetu. Yesu alisema hivi: “Mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.” (Matayo 21:22) Imani haimaanishe kuitika-itika tu mambo bila kufikiri. Lakini, ni kuamini jambo yenye hata kama hatuione, kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama ni ya kweli. (Waebrania 11:1) Mu Biblia muko ushuhuda mbalimbali wenye kuonyesha kama hata kama hatumuonake Yehova, yeye ni mutu wa kweli, mwenye tunaweza kutumainia, na iko tayari kujibia sala za wale wenye wanamuamini. Zaidi ya ile, tunaweza kila mara kumuomba Yehova atupatie imani zaidi, na iko tayari kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima.​—Luka 17:5; Yakobo 1:17.

Kuko jambo ingine ya maana yenye inaweza kufanya Yehova asikilize sala zetu. Yesu alisema hivi: “Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yohana 14:6) Yesu njo njia yenye inatusaidia kumukaribia Baba, Yehova. Njo maana, Yesu aliambia wanafunzi wake wasali mu jina yake. (Yohana 14:13; 15:16) Ile haimaanishe kama tunapaswa kusali kwa Yesu. Lakini, tunapaswa njo kusali mu jina ya Yesu, juu yeye njo alifanya iwezekane tumukaribie Baba yetu mukamilifu na mutakatifu.

Siku moja, wanafunzi wa Yesu walimuambiaka hivi: “Bwana, utufundishe kusali.” (Luka 11:1) Inaonekana kama hawakuwa wanamuomba Yesu awaambie mambo ya musingi yenye tumezungumuzia. Walipenda kabisa kujua mambo ya kutia mu sala. Ni sawa vile walimuuliza, ‘Tunaweza kusali juu ya mambo gani?’