Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

5 Tusali Wakati Gani na Mahali Gani?

5 Tusali Wakati Gani na Mahali Gani?

Sala

5 Tusali Wakati Gani na Mahali Gani?

BILA shaka, umeona kwamba dini nyingi kubwa zinakazia kuwa na majengo ya sala yenye madoido na zinapanga wakati hususa wa kusali. Je, Biblia inasema ni lazima tuwe na mahali hususa na wakati hususa wa kusali?

Biblia inaonyesha kwamba kuna nyakati zinazofaa za kusali. Kwa mfano, kabla ya kula na wafuasi wake, Yesu alitoa sala ya kumshukuru Mungu. (Luka 22:17) Na wanafunzi wake walipokutana ili kuabudu, walisali pamoja. Hivyo, waliendeleza desturi iliyokuwa ikifuatwa tangu zamani katika masinagogi ya Wayahudi na katika hekalu huko Yerusalemu. Mungu alikusudia hekalu liwe “nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”—Marko 11:17.

Watumishi wa Mungu wanapokusanyika na kusali pamoja, maombi yao yanaweza kuwa na matokeo mazuri. Mungu hufurahi ikiwa wanakusanyika wakiwa na nia moja na sala inayotolewa kwa ajili yao inapatana na kanuni za Maandiko. Sala hiyo hata inaweza kumchochea Mungu afanye jambo ambalo huenda hangefanya. (Waebrania 13:18, 19) Mashahidi wa Yehova husali kwa ukawaida katika mikutano yao. Unakaribishwa kwa uchangamfu uende kwenye Jumba la Ufalme ambalo liko karibu nawe ili usikie sala hizo.

Hata hivyo, Biblia haisemi ni lazima tuwe na mahali hususa na wakati hususa wa kusali. Katika Biblia, tunasoma kuhusu watumishi wa Mungu waliosali wakati na mahali tofauti-tofauti. Yesu alisema: “Unaposali, ingia ndani ya chumba chako cha faragha na, baada ya kufunga mlango wako, sali kwa Baba yako aliye mahali pa siri; ndipo Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.”—Mathayo 6:6.

Bila shaka, huo ni mwaliko wenye kupendeza, sivyo? Unaweza kusali kwa Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote wakati wowote, hata ukiwa faraghani, na kuwa na hakika kwamba atakusikiliza. Si ajabu kwamba mara nyingi Yesu alihitaji kuwa peke yake ili asali! Wakati fulani alisali kwa Mungu usiku kucha, bila shaka, akitafuta mwongozo wa kufanya uamuzi fulani mzito.—Luka 6:12, 13.

Wanaume na wanawake wengine katika Biblia walisali walipotaka kufanya maamuzi mazito au walipopatwa na hali fulani ngumu. Nyakati fulani walisali kwa sauti na nyakati nyingine wakasali kimyakimya; walisali walipokuwa katika kikundi na hata walipokuwa peke yao. Jambo muhimu ni kwamba walisali. Hata Mungu huwaambia watumishi wake hivi: “Salini bila kuacha.” (1 Wathesalonike 5:17) Yuko tayari kuwasikiliza bila kuchoka wale wanaofanya mapenzi yake. Je, huo si mwaliko wenye upendo?

Bila shaka, katika ulimwengu huu wenye shaka, wengi wanataka kujua ikiwa sala inaweza kuwasaidia. Huenda ukauliza, ‘Je, kweli sala inaweza kunisaidia?’

[Blabu katika ukurasa wa 9]

Tunaweza kusali wakati wowote, mahali popote