Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunapaswa Kusali Wakati Gani na Wapi?

Tunapaswa Kusali Wakati Gani na Wapi?

BILA shaka, umeona kama dini za mingi zinahangaikia sana kujenga nyumba za sala na zinapanga wakati wa kusali. Lakini, Biblia inasema kama tunapaswa kusali tu wakati fulani na fasi fulani?

Biblia inaonyesha kama kuko wakati mbalimbali wenye tunapaswa kusali. Kwa mufano, mbele ya kula na wafuasi wake, Yesu alisali juu ya kumushukuru Mungu. (Luka 22:17) Na wakati wanafunzi wake walikutana juu ya ibada, walikuwa wanasali. Kwa kufanya vile, waliendelesha desturi yenye Wayahudi walikuwa wanafuata tangu zamani mu masinagogi yao na mu hekalu kule Yerusalemu. Mungu alipenda hekalu ikuwe “nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”​—Marko 11:17.

Wakati watumishi wa Mungu wanakutana na kusali pamoja, Mungu anasikilizaka maombi yao. Kama wanasali na wako na nia moja na wanafanya vile kupatana na kanuni za Biblia, Mungu anafurahia sala yao. Sala yao inaweza hata kumuchochea Mungu afanye jambo yenye pengine hangefanya. (Waebrania 13:18, 19) Mashahidi wa Yehova wanakuwaka wanasali ku mikutano yao yote. Tunakutia moyo uende ku Jumba ya Ufalme ya karibu na kwako juu ujisikilie vile wanakuwaka wanasali.

Lakini, Biblia haiseme kama tunapaswa kusali wakati fulani tu ao fasi fulani tu. Mu Biblia muko habari za watumishi wa Mungu wenye walisali wakati na fasi mbalimbali. Yesu alisema: “Wakati unasali, ingia ndani ya chumba chako cha peke yako, na kisha kufunga mulango, sali kwa Baba yako mwenye kuwa mahali pa siri. Halafu Baba yako mwenye kuona akiwa mahali pa siri atakulipa.”​—Matayo 6:6.

Tunaweza kusali wakati yoyote na fasi yoyote

Mualiko muzuri sana, hauone vile? Unaweza kusali kwa Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi mu ulimwengu wote wakati yoyote, na unaweza kufanya vile na uko peke yako na kuwa hakika kama atakusikiliza. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini mara mingi Yesu alikuwa anapenda kusali na iko yeye peke! Wakati fulani alisali kwa Mungu usiku muzima. Bila shaka alifanya vile juu ya kumuomba Mungu amuongoze mbele ya kukamata uamuzi fulani wa maana sana.​—Luka 6:12, 13.

Wanaume na wanamuke mbalimbali wenye Biblia inazungumuzia walikuwa wanasali mbele ya kukamata maamuzi ya maana sana ao wakati walikuwa na magumu ya nguvu. Wakati fulani walisali kwa sauti na wakati ingine walisali kimyakimya. Walisali wakati walikuwa na watu wengine na hata wakati walikuwa peke yao. Ya maana ni vile tu walisali. Hata Mungu anaambia watumishi wake hivi: “Musali bila kuacha.” (1 Watesalonike 5:17) Iko tayari kusikiliza wale wenye wanafanya mapenzi yake, hata wasali mara ngapi. Ile inaonyesha kama Yehova anapenda kabisa tukuwe tunasali kwake.

Leo, watu wengi hawaamini kama sala inaweza kuwasaidia. Pengine na weye unajiulizaka: ‘Sala inaweza kabisa kunisaidia?’