Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Anasikilizaka na Kujibia Sala?

Mungu Anasikilizaka na Kujibia Sala?

WATU wengi wanapendaka sana kujua kama Mungu anasikilizaka na kujibia sala zetu. Biblia inaonyesha kama hata leo Yehova anasikilizaka sala. Lakini juu Mungu asikilize sala zetu, kuko mambo yenye tunapaswa kufanya.

Yesu alilaumu viongozi wa dini wa wakati wake. Aliwaita wanafiki juu walikuwa wanasali juu tu ya kuonyesha kama wao njo wazuri. Alisema kama “watapata zawabu yao kikamili.” Alipenda kusema kama watapata tu jambo yenye walihangaikia sana, ni kusema, kuonekana na watu; lakini hawangepata jambo yenye walikuwa nayo lazima, ni kusema, kusikiwa na Mungu. (Matayo 6:5) Vilevile, leo watu wengi wanasali kupatana na mapenzi yao, hapana mapenzi ya Mungu. Juu hawafuate kanuni za Biblia zenye tumezungumuzia, Mungu hasikilize sala zao.

Halafu weye? Mungu atasikiliza na kujibia sala zako? Haiko rangi yako ya ngozi, inchi yako, ao cheo yako njo itafanya Mungu asikilize na kujibia sala zako. Biblia inatuhakikishia hivi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” (Matendo 10:34, 35) Na weye uko unafanya vile? Kumuogopa Mungu maana yake kumuheshimia sana na kuepuka kufanya mambo yenye haimufurahishe. Kufanya mambo yenye kuwa sawa ni kufuata mawazo ya Mungu, hapana mawazo yetu ao mawazo ya wanadamu wenzetu. Unapenda kabisa Mungu asikilize sala zako? Biblia inaonyesha namna unaweza kusali juu Mungu asikilize sala zako. *

Watu wengi wanapenda Mungu ajibie sala yao kwa kuwafanyia muujiza. Lakini hata mu wakati wa Biblia, Mungu hakukuwaka nafanya miujiza kila wakati. Wakati fulani, kisha muujiza moja kufanyika, kulikuwa kunapita mamia ya miaka njo muujiza ingine inafanyika. Zaidi ya ile, Biblia inaonyesha kama kipindi ya miujiza ilimalizika kisha wakati wa mitume. (1 Wakorinto 13:8-​10) Ni kusema Mungu hajibiake sala leo? Hapana! Tuone mambo fulani yenye anafanyaka juu ya kujibia sala leo.

Mungu anapatiaka watu hekima. Hekima yote ya kweli inatoka njo kwa Yehova. Anafurahiaka kuipatia wale wenye wanapenda awaongoze na wenye wanajikaza kufuata kanuni zake mu maisha yao.​—Yakobo 1:5.

Mungu anatupatiaka roho yake takatifu. Roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kutimiza mambo mbalimbali. Hakuna nguvu yenye inaipita. Inaweza kutusaidia tuvumilie magumu. Inatusaidia tukuwe na amani wakati tuko na mahangaiko. Inaweza kutusaidia tukuwe na sifa za muzuri. (Wagalatia 5:22, 23) Yesu aliambiaka wanafunzi wake kama Mungu anapatiaka watu roho takatifu, haiimake mutu.​—Luka 11:13.

Mungu anasaidiaka wale wenye kumutafuta kwa bidii wamujue. (Matendo 17:26, 27) Mu dunia yote kuko watu wenye wako wanatafuta kabisa kweli. Wanapenda kujua jina ya Mungu, mambo yenye anapanga kufanya juu ya dunia na wanadamu, na mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake. (Yakobo 4:8) Mara mingi Mashahidi wa Yehova wanakutanaka na watu wa vile na wanafurahiaka kuwafasiria ile mambo kwa kutumia Biblia.

Na weye uko unamutafuta Mungu? Ile njo sababu yenye ilifanya ukamate hii gazeti? Pengine hii gazeti njo jibu ya sala yako.

^ Kama unapenda kupata habari zaidi juu ya namna ya kusali na mambo yenye unaweza kufanya juu Mungu asikilize sala yako, ona sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova.