Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Bustani ya Edeni, Njo Ilikuwaka Makao ya Kwanza ya Wanadamu?

Bustani ya Edeni, Njo Ilikuwaka Makao ya Kwanza ya Wanadamu?

Bustani ya Edeni, Njo Ilikuwaka Makao ya Kwanza ya Wanadamu?

WAZIA uko mu bustani. Hakuna makelele, ao fujo yenye inakuwaka mu miji mikubwa. Bustani ni ya kabambi, na muko amani. Zaidi ya ile, hauna mahangaiko, uko na afya ya muzuri, na hausikie maumivu yoyote. Unafurahia kila kitu yenye inakuzunguka.

Unaangalia maua ya mingi ya rangi mbalimbali, maji yenye kutakata ya muto mudogo, mayani ya mubichi, na nyasi. Unasikia upepo mutulivu ku ngozi ya mwili yako na harufu ya muzuri ya maua. Unasikia sauti za majani yenye iko natingizwa na upepo, sauti ya maji yenye iko nateremuka ku majiwe, na sauti za ndege zenye ziko naimba na sauti za vidudu. Wakati unafikiria ile mambo yote, bila shaka unaweza kupenda kuishi fasi ya vile.

Ku dunia yote, watu wengi wanaamini kama fasi ya vile njo wanadamu wa kwanza walikuwaka naishi. Kwa miaka mingi, watu wa dini ya Wayahudi, dini zenye kujiita kuwa za Kikristo, na dini ya Waislamu wamefundishwa juu ya bustani ya Edeni, kwenye Mungu aliwekaka Adamu na Eva. Biblia inaonyesha kama Adamu na Eva walikuwa na maisha yenye amani na furaha. Walikuwa na amani kati yao, walikuwa na amani na wanyama, na walikuwa na urafiki muzuri na Mungu, mwenye aliwapatia tumaini ya kuishi milele mu ile fasi ya muzuri.​—Mwanzo 2:15-24.

Wahindu nao wanaamini kama zamani kulikuwaka paradiso. Na Wabuda nao wanaamini kama viongozi wao walitokeaka wakati fulani ya muzuri sana, wakati yenye dunia ilikuwaka paradiso. Na dini za mingi mu Afrika zinafundishaka hadisi zenye zinafanana na habari ya Adamu na Eva.

Kusema kweli, watu wa dini mbalimbali na desturi mbalimbali wanaamini kama zamani kulikuwaka paradiso. Muandikaji fulani alisema hivi: “Watu wa wakati mbalimbali wanaamini kama kulikuwaka paradiso ku mwanzo wa historia ya wanadamu. Mu ile paradiso, mulikuwa ukamilifu, uhuru, amani, furaha, vitu mingi sana, na hamukukuwa mahangaiko, mateso, na magumu. . . . Njo maana watu wengi walitamani sana ile paradiso yenye ilipoteaka na kujaribu kutafuta namna ya kuipata tena.”

Inawezekana zile habari zote zilitokea fasi moya? Inawezekana namna gani “watu wa desturi za mingi” wakuwe na hadisi zenye zinafanana kuhusu paradiso? Bustani ya Edeni ilikuwaka kabisa? Adamu na Eva walikuwaka kabisa?

Watu wenye mashaka hawaamini ile jambo. Hii wakati yenye sayansi imeendelea sana, watu wengi wanasema kama zile habari ni za kuwazia tu. Lakini jambo ya kushangaza ni kwamba, hata watu wa dini wako na ile mawazo. Viongozi wengi wa dini wanaendelea kufundisha kama bustani ya Edeni haikukuwaka. Wanasema kama ile habari ni hadisi ya kuwazia tu, ao ni habari ya mufano.

Ni kweli kwamba, mu Biblia muko mifano mingi. Hata Yesu alitoaka mifano mingi, yenye inajulikana sana. Lakini wakati Biblia inazungumuzia bustani ya Edeni, inaizungumuzia sawa vile historia ya kweli kabisa na ya mwepesi kuelewa, hapana sawa vile habari ya mufano. Sasa, kama tunasema bustani ya Edeni haikukuwaka, ni sawa vile tunasema kama mambo yote yenye Biblia inasema haiko ya kweli. Tuone juu ya nini watu fulani wako na mashaka juu ya bustani ya Edeni, na tuone ikiwa wako kabisa na sababu za kuwa na ile mashaka. Kisha tutaona juu ya nini habari kuhusu bustani ya Edeni ni ya maana kwetu.