Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Bustani ya Edeni, Ilikuwaka Kabisa?

Bustani ya Edeni, Ilikuwaka Kabisa?

Bustani ya Edeni, Ilikuwaka Kabisa?

UNAJUA habari kuhusu Adamu na Eva na bustani ya Edeni? Mu dunia yote, watu wengi wanaijua. Na weye ungependa kuisoma? Inapatikana mu Mwanzo 1:26–3:24. Hii njo kifupi ya ile habari:

Yehova Mungu * anaumba mutu kwa kutumia mavumbi, anamupatia jina Adamu, kisha anamutia mu bustani, mu eneo yenye inaitwa Edeni. Mungu yeye peke njo alipanda ile bustani. Mu ile bustani muko maji ya kutosha na muko miti mingi ya matunda. Katikati kuko “muti wa ujuzi wa mema na mabaya.” Mungu anakataza mwanadamu kula matunda ya ile muti, na anamuambia kama akiikula, atakufa. Kisha wakati fulani, Yehova anaumba mwanamuke na kumuleta kwa Adamu ili akuwe bibi yake. Anamuumba kwa kutumia ubavu moja wa Adamu, na ule mwanamuke jina yake Eva. Mungu anawapatia kazi ya kutunza bustani ya Edeni na anawaambia wazale na kujaza dunia.

Wakati Eva iko yeye peke, nyoka anazungumuza naye. Anamuchochea akule tunda yenye Mungu aliwakataza. Anamuambia kama Mungu alimudanganya na iko namuima jambo fulani ya muzuri, yenye inaweza kufanya akuwe sawa Mungu. Eva anaamini nyoka na anakula ile tunda. Kisha, Adamu naye anakosa kumutii Mungu juu anaitika kula ile tunda. Kwa hiyo Yehova anahukumu Adamu, Eva na nyoka. Anafukuza Adamu na Eva mu bustani ya Edeni, na anaweka malaika juu walinde njia ya kuenda mu ile bustani.

Zamani, watu wengi wenye elimu waliamini kama ile habari yenye kitabu ya Mwanzo inazungumuzia ni ya kweli. Lakini leo watu wengi wako na mashaka juu ya mambo yenye Biblia inasema. Juu ya nini hawaamini mambo yenye kitabu ya Mwanzo inasema juu ya Adamu, Eva, na bustani ya Edeni? Tuone mawazo ine yenye wako nayo.

1. Bustani ya Edeni Haikukuwaka Kabisa

Juu ya nini wanawaza kama bustani ya Edeni haikukuwaka kabisa? Inawezekana filozofia iko kati ya mambo yenye imewafanya wakuwe na mashaka sana. Kwa miaka mingi, viongozi fulani wa dini walikuwa nasema kama inawezekana bustani ya Edeni ingali fasi fulani. Walisema vile juu walichochewa na mawazo ya wafilozofe Wagiriki, sawa vile Plato na Aristote, wenye walikuwa nasema kama ku dunia hakuwezi kuwa kitu yoyote yenye inakamilika. Mbinguni tu njo kunaweza kuwa vitu vyenye kukamilika. Njo maana, viongozi wa dini waliwaza kama paradiso ya kwanza ilikuwa fasi fulani karibu na mbinguni. * Wengine waliwaza kama bustani ya Edeni ilikuwa juu ya mulima murefu sana, mbali na hii dunia yenye kuharibika. Wengine walikuwa nasema kama ilikuwa ku sehemu ya mwisho-mwisho ya kaskazini ao ya kusini ya dunia. Na tena wengine walikuwa nasema kama ilikuwa ku mwezi ao karibu na mwezi. Ile mambo yote ilifanya watu waanze kuwaza kama bustani ya Edeni haikukuwaka kabisa. Leo watu fulani wenye elimu wanasema kama habari ya Biblia juu ya bustani ya Edeni ni upumbavu na wanasema kama ile fasi haikukuwaka hata kidogo.

Lakini, Biblia haiseme vile wakati inazungumuzia bustani ya Edeni. Mwanzo 2:8-14 inatuambia mambo yenye kuwa wazi kabisa juu ya ile bustani. Inasema kama ilikuwaka mu eneo ya mashariki yenye kuitwa Edeni. Inatuambia kama maji yenye ilikuwa mu ile bustani ilikuwa natoka mu muto yenye ilikuwa najigawanya mu mito ine. Inatuambia majina ya ile mito ine, na inatoa maelezo fulani juu ya kila muto. Watu wengi wenye elimu ya Biblia wametumia zile habari juu ya kutafuta fasi kwenye bustani ya Edeni ilikuwaka. Lakini, wameshindwa kuipata na wameshindwa kuelewana juu ya fasi kwenye ile bustani ilikuwaka. Juu ya wameshindwa, ni kusema mambo yenye Biblia inazungumuzia juu ya bustani ya Edeni na mito yake ni ya uongo, na ni hadisi ya kuwazia tu?

Fikiria hii jambo: Mambo yenye inahusu bustani ya Edeni ilifanyika miaka 6 000 hivi yenye imepita. Ni wazi kama Musa njo aliandikaka ile mambo. Inawezekana alitumia habari zenye watu walikuwa namuelezea ao hata maandishi yenye ilikuwaka ile wakati. Hata vile, wakati Musa aliandika ile habari, kulikuwa kulishapita miaka 2 500 hivi tangu ile mambo itokee. Kwa hiyo, hata ile wakati, habari kuhusu bustani ya Edeni ilikuwa historia ya zamani. Kisha miaka mingi kupita, inawezekana alama za asili, sawa vile mito, zibadilike. Dunia inabadilikaka, haibakiake tu vile iko. Mu eneo yenye bustani ya Edeni ilikuwaka, munakuwaka matetemeko mingi ya inchi. Asilimia 17 (ao 17%) ya matetemeko makubwa ya inchi yenye inatokeaka mu dunia, inafanyikaka mu ile eneo. Mu maeneo ya vile, mabadiliko ni jambo ya kawaida. Zaidi ya ile, Garika yenye ilitokeaka mu siku za Noa ilibadilishaka mambo mingi mu dunia mu njia yenye hatuwezi kujua leo. *

Lakini, hii njo mambo kidogo yenye tunajua: Kitabu ya Mwanzo inaonyesha kama bustani ya Edeni ilikuwaka kabisa. Mito mbili kati ya mito ine yenye Biblia inazungumuzia, ni kusema Efrati na Tigri ao Hidekeli, ingali mupaka leo. Na chemchemi ya ile mito mbili iko tu mu eneo ileile. Biblia inataya hata majina ya ma eneo kwenye ile mito ilipita na inazungumuzia vitu vyenye samani vyenye vilikuwa mu ile maeneo. Wakati watu wa zamani wangesoma zile habari, wangezielewa.

Hadisi hazielezake mambo waziwazi vile. Na hazionyeshake waziwazi habari zenye watu wanaweza kushuhudia kama ni za kweli ao wanaweza kupinga. Mara mingi zinaanzaka tu hivi: “Kulikuwaka.” Lakini habari za kweli zinaonyeshaka mambo waziwazi sawa vile habari kuhusu bustani ya Edeni.

2. Haiwezekane Mungu Akuwe Aliumba Adamu kwa Kutumia Mavumbi na Eva kwa Kutumia Ubavu wa Adamu

Leo sayansi inaonyesha kama mwili wa mwanadamu unafanyizwa na vitu mbalimbali sawa vile hidrojeni, oksijeni, na karbone. Na vile vitu vyote vinapatikana pia mu udongo. Lakini namna gani vile vitu vilitiwa pamoja juu ya kufanyiza kiumbe yenye uzima?

Wanasayansi wengi wanaamini kama vitu vyenye uzima vilijitokeza. Wanasema kama kulikuwaka kwanza vitu vyenye uzima vya burebure tu. Kisha vikaanza kubadilika polepole, na kisha mamilioni ya miaka, vikakuwa vya ajabu zaidi. Lakini, ni kukosea kutumia neno “burebure” juu vitu vyote vyenye uzima, hata vya kidogo sana vyenye hatuwezi kuona na macho, vyenye kuwa na chembe moja, ni vya ajabu sana. Hakuna ushuhuda yenye inaonyesha kama kitu fulani yenye uzima ilishakajitokeza, ao inaweza jitokeza. Lakini, ukichunguza vitu vyote vyenye uzima, utaona kama kuko mutu fulani mwenye akili kutupita mwenye alivifanya. *​—Waroma 1:20.

Tuseme uko nasikiliza muziki muzuri sana, uko nafurahia muchoro wenye kupendeza, ao kitu fulani ya teknolojia ya ajabu; utasema kama ile mambo yote ilijitokeza? Hapana! Lakini ile mambo yote haiko kitu kama unailinganisha na mwili wa mwanadamu wenye kufanywa kwa njia ya ajabu na wenye kupendeza sana. Namna gani mutu anaweza kuwazia kama hakuna mutu mwenye alifanya mwili wa mwanadamu? Zaidi ya ile, kitabu ya Mwanzo inasema kama, kati ya vitu vyote vyenye uzima vyenye kuwa ku dunia, mwanadamu tu njo aliumbwa kwa mufano wa Mungu. (Mwanzo 1:26) Njo maana, hapa ku dunia ni mwanadamu tu njo anaweza kuiga uwezo wa Mungu wa kuumba. Kwa mufano anaweza kutunga muziki, kuchora picha, na kutengeneza vyombo mbalimbali. Kwa hiyo hatushangale kuona kama Mungu iko na uwezo mukubwa sana wa kuumba kuliko wanadamu.

Basi, kuumba mwanamuke kwa kutumia ubavu wa mwanaume, haiko hata kitu kwake. * Angependaka, angetumikishaka njia ingine juu ya kuumba mwanamuke. Lakini kuko sababu yenye ilifanyaka amuumbe vile. Alifanyaka vile juu alipendaka mwanaume na mwanamuke waoane na wakuwe “mwili mumoja.” (Mwanzo 2:24) Namna mwanaume na mwanamuke waliumbwa, juu wakuwe na uhusiano wa karibu sana na watumike kwa umoja, inaonyesha kama Mungu iko na hekima na anatupenda.

Zaidi ya ile, watu wenye kuchunguza chembe za uriti wanasema kama inawezekana wanadamu wote walitokana na mwanaume na mwanamuke mumoja. Kwa kweli, tunaweza kuamini mambo yenye kitabu ya Mwanzo inasema juu ya uumbaji.

3. Muti wa Ujuzi na Muti wa Uzima Ni Mambo ya Kuwazia Tu

Kitabu ya Mwanzo haiseme kama ile miti ilikuwa na nguvu fulani yenye haiko ya kawaida. Lakini, ilikuwa tu miti ya kawaida yenye Yehova alipatia maana fulani ya mufano.

Wanadamu nao, hawafanyake vile? Ndiyo. Kwa mufano, muamuzi anaweza kuambia mutu asizarau jumba ya tribinali. Ile haimaanishe kama iko naambia mutu asizarau viti, meza, na ukuta wenye kuwa mu ile jumba ya tribinali. Anapenda tu kumuambia asizarau sheria yenye ile jumba ya tribinali inawakilisha. Watawala fulani wametumia pia fimbo ya ufalme na taji kuwa alama ya mamlaka yao.

Sasa, ile miti mbili ilifananisha nini? Watu wametoa mawazo mingi juu ya mambo yenye ile miti mbili ilifananisha. Lakini, jibu ya kweli ya ile ulizo ni ya mwepesi lakini yenye maana sana. Muti wa ujuzi ulifananisha haki yenye Mungu tu njo iko nayo, ya kuamua mema na mabaya. (Yeremia 10:23) Njo maana ilikuwa kosa kubwa sana kuiba matunda ya ile muti. Na muti wa uzima ulifananisha zawadi yenye Mungu tu njo anaweza kutoa, ni kusema, zawadi ya uzima wa milele.​—Waroma 6:23.

4. Haiwezekane Nyoka Aseme

Ni kweli kama, habari juu ya nyoka yenye kitabu ya Mwanzo inazungumuzia, inaweza kuvuruga akili, zaidi sana kama musomaji hafikirie habari zingine za Biblia. Lakini, maandiko ingine ya Biblia inatusaidia kuelewa ile habari.

Ni nini ao ni nani njo alifanya ionekane sawa vile nyoka iko nasema? Waisraeli wa zamani walijua habari fulani zenye zingewasaidia kuelewa mambo yenye ilifanyikaka mu bustani ya Edeni. Walijua kuwa hata kama wanyama hawawezi kusema, kiumbe wa roho anaweza kufanya munyama aonekane sawa vile iko nasema. Kwa mufano, Musa aliandika habari juu ya Balaamu. Mungu alituma malaika afanye punda ya Balaamu iseme sawa vile mwanadamu.​​—Hesabu 22:26-31; 2 Petro 2:15, 16.

Pepo wachafu wanaweza pia kufanya miujiza? Musa aliona namna makuhani wa Misri, wenye walikuwa nafanya uchawi, wanaiga muujiza fulani wa Mungu sawa vile kugeuza fimbo ikuwe nyoka. Ni pepo wachafu njo waliwapatia uwezo wa kufanya vile.​—Kutoka 7:8-12.

Bila shaka, ni Musa njo aliandika kitabu ya Yobu. Ile kitabu inaonyesha namna, Shetani, adui mukubwa wa Mungu, alitilia mashaka uaminifu wa watumishi wote wa Yehova. (Yobu 1:6-11; 2:4, 5) Inaonekana kama Waisraeli wa zamani waliamini kuwa Shetani njo alifanya ionekane kuwa nyoka iko anasema. Waliamini kama alifanya vile juu ya kumudanganya Eva na kumufanya asimutii Mungu.

Ni kweli kabisa kama Shetani njo alikuwa nazungumuza kupitia nyoka? Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alimuita Shetani kuwa “muongo na baba ya uongo.” (Yohana 8:44) Ni wazi kama ule “baba ya uongo” njo alisemaka uongo wa kwanza. Ule uongo wa kwanza unapatikana mu maneno yenye nyoka aliambiaka Eva. Nyoka alipinga maneno ya Mungu kwa kusema kama ikiwa Eva anakula ile tunda yenye Mungu aliwakataza, ‘hatakufa.’ (Mwanzo 3:4) Bila shaka, Yesu alijua kama Shetani njo alitumiaka nyoka juu ya kuzungumuza na Eva. Ufunuo wenye Yesu alipatiaka mutume Yohana unaonyesha waziwazi ule nyoka ni nani. Unamuita Shetani, “ule nyoka wa zamani.”​​—Ufunuo 1:1; 12:9.

Inawezekana kabisa kiumbe wa roho mwenye nguvu afanye ionekane sawa vile nyoka njo iko nasema? Ndiyo, inawezekana. Juu hata wanadamu wenye hawana uwezo mingi sawa vile viumbe vya roho wanaweza kufanya sanamu ionekane sawa vile iko nasema, kumbe ni mutu njo iko nasema.

Jambo Ingine Yenye Kuonyesha Kabisa Kama Bustani ya Edeni Ilikuwaka

Hauone kama wale wenye kuwa na mashaka juu ya mambo yenye kitabu ya Mwanzo inasema hawana kabisa sababu za kusadikisha za kuwa na ile mashaka? Kuko ushuhuda wenye kuonyesha wazi kabisa kama kitabu ya Mwanzo inasema kweli.

Kwa mufano, Biblia inaita Yesu kuwa “shahidi muaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu alikuwa mutu mukamilifu, hakuna siku alisemaka uongo, ao kugeuza kweli kuwa uongo. Zaidi ya ile, alisema kama aliishi kwa muda murefu sana mbinguni mbele akuwe mwanadamu hapa ku dunia. Aliishi pamoja na baba yake, Yehova, “mbele ya ulimwengu kuwa.” (Yohana 17:5) Ni kusema, alikuwa pale wakati Mungu aliumba vitu vyenye uzima ku dunia. Sasa, Yesu, ule shahidi mwenye kutumainika, naye alisemaka nini?

Yesu alionyesha kama Adamu na Eva ni watu wenye walikuwaka kabisa. Alizungumuzia ndoa yao wakati alikuwa nafasiria kanuni ya Yehova juu ya kufunga ndoa na bibi ao bwana mumoja tu. (Matayo 19:3-6) Kama Adamu na Eva hawakukuwaka, na kama bustani ya Edeni ni hadisi ya kuwazia tu, ni kusema Yesu naye walimudanganyaka ao yeye njo alikuwaka nadanganya watu. Haiwezekane kabisa kukuwe mutu mwenye alidanganya Yesu, ao Yesu aseme uongo! Yesu alikuwa mbinguni, na aliona namna Adamu na Eva walikosa kumutii Mungu mu bustani ya Edeni. Kuko ­ushuhuda ingine yenye inapita ile ya Yesu? Hakuna kabisa.

Kusema kweli, kukatala kuamini mambo yenye kitabu ya Mwanzo inasema, nikukatala kuamini mambo yenye Yesu alisema. Na kama hatuamini mambo yenye kitabu ya Mwanzo inasema juu ya bustani ya Edeni, hatutaelewa mafundisho ingine ya maana ya Biblia, na hatutaelewa mambo ya muzuri yenye Mungu anasema atatufanyia, yenye Biblia inazungumuzia. Tuone juu ya nini tunasema vile.

[Maelezo ya chini]

^ Biblia inaonyesha kama jina ya Mungu ni Yehova.

^ Lakini ile mawazo haipatane na Biblia. Biblia inafundisha kama vitu vyote vyenye Mungu aliumbaka vilikuwaka vikamilifu, na kama mambo ya mubaya ilitokeaka kisha yeye kumaliza kuumba kila kitu. (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Wakati Yehova alimaliza kuumba vitu vyote ku dunia, alisema kama kila kitu chenye aliumba kilikuwa “kizuri sana.”​—Mwanzo 1:31.

^ Wakati Mungu alileta Garika, bila shaka bustani ya Edeni ilipotea kabisa. Andiko ya Ezekieli 31:18 inaonyesha kama kufikia karne ya saba mbele ya kuzaliwa kwa Yesu “miti ya Edeni” haikukuwa tena. Kwa hiyo, mutu yeyote mwenye alikuwa natafuta bustani ya Edeni kisha ile wakati, hangeipata.

^ Ona broshua Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?​—Maulizo 5 ya Kujiuliza, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova.

^ Leo wanganga wamevumbula kama, ubavu uko na uwezo wa kupona. Tofauti na mifupa ingine, unaweza kuota tena.