Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unabii wa Maana Sana

Unabii wa Maana Sana

Unabii wa Maana Sana

“Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”—MATHAYO 24:14.

WASOMI mbalimbali wa Biblia wanakubali kwamba unabii huo ni wa maana sana. Ni wa maana sana kwa sababu, kazi ambayo unabii huo unazungumzia inapaswa kufanywa duniani pote. Pia, ni wa maana kwa sababu unaonyesha kazi ambayo Wakristo wanapaswa kuwa wakifanya—kazi ya kuhubiri ambayo ingefanywa kabla ya tukio muhimu na kubwa ambalo Yesu aliliita “mwisho.”

Unabii huo unatimizwa leo. Wewe unahusika kwa sababu habari njema inatoa mwaliko na onyo pia. Inakupa nafasi ya kuamua kati ya mambo mawili: Ukubali Ufalme wa Mungu au uukatae. Uamuzi utakaofanya utaathiri maisha yako.

Fikiria mistari mingine inayozunguka mstari huo. Siku kadhaa kabla ya Yesu kuuawa, wanafunzi wake walimwendea na kumuuliza kuhusu wakati ujao. Walitaka kujua kuhusu kuanzishwa kwa Ufalme wa Mungu, ambao Yesu alikuwa ameuzungumzia mara nyingi. Pia, walitaka kujua kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo,” au “mwisho wa dunia” kama vile tafsiri nyingine zinavyosema.—Mathayo 24:3, Union Version.

Katika jibu lake, Yesu alitabiri kwamba kungekuwa na vita vikubwa, njaa, magonjwa ya kuambukiza, na matetemeko makubwa ya ardhi. Pia, alisema kwamba uvunjaji wa sheria ungeongezeka, walimu wa dini wa uwongo wangewapotosha wengi, na Wakristo wa kweli wangechukiwa na kuteswa. Hizo zote zilikuwa habari mbaya.—Mathayo 24:4-13; Luka 21:11.

Lakini pia kulikuwa na habari njema. Yesu alitaja maneno yaliyonukuliwa hapo juu, maneno ambayo yamewasisimua na kuwachochea watu kwa miaka mingi. Ingawa watu wanakubaliana kuhusu umuhimu wa maneno ya Yesu, wana maoni tofauti kuhusu maana ya maneno hayo. Habari njema ni nini hasa? Ufalme ni nini? Unabii huo utatimizwa na nani na wakati gani? Na “mwisho” ni nini? Acheni tuone.

[Picha katika ukurasa wa 2, 3]

Nakala ya Hati ya Washington yenye Vitabu Vinne vya Injili. Andiko la Mathayo 24:14 linaonekana waziwazi

[Hisani]

From the book Facsimile of the Washington Manuscript of the Four Gospels in the Freer Collection 1912