Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Nini njo ilifanya kijana mwenye alikuwa muasi, na mwenye hakukuwa nahangaikia watu aanze kupenda watu na kuwasaidia? Nini njo ilifanya mwanaume fulani wa Meksiko aachane na maisha yake ya uasherati? Nini njo ilifanya mwanaume fulani wa Japani mwenye alikuwa napata sana ushindi mu mashindano ya kutembeza kinga, aachane na ile mashindano na aanze kumutumikia Mungu? Acha tuone.

“Nilikuwa mukosa-adabu, mwenye kiburi, na mukali sana.”​—DENNIS O’BEIRNE

ALIZALIWA MWAKA WA: 1958

INCHI: ENGLAND

ALIKUWA: MUASI NA MWENYE HAHANGAKIE WATU

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Baba yangu alikuwa mutu wa Irlande. Kwa hiyo, wakati nilikomala, nilikuwa mu kanisa Katoliki ya Irlande. Nilikuwa naenda ku kanisa miye peke hata kama sikukuwa napenda kuenda. Lakini, nilikuwa napenda kujua mambo mingi juu ya Mungu. Nilizoea kusali sala ya Baba yetu. Ninakumbuka usiku fulani nilikuwa najinyoosha ku kitanda, na kujiuliza ikiwa ile sala inamaanisha nini. Nilikuwa naigabula mu sehemu mbalimbali na kujaribu kutafuta maana ya kila sehemu.

Wakati nilikuwa na miaka 15 hivi, niliingia mu kikundi ya Warasta. Niliingia pia mu vikundi fulani vya politike, sawa vile kikundi fulani ya kupinga Wanazi. Lakini nilifikia kuwa muasi sana na mwenye haangaikie watu. Nilikuwa natumia dawa za kulewesha, zaidi sana marijuana, na nilikuwa naivuta karibu kila siku. Juu sikikuwa “nahangaikia kitu,” nilikuwa na kunywa sana, nilikuwa natia maisha yangu mu hatari, na sikuhangaikia wengine. Ningezungumuza tu na mutu kama ningeona kuwa ile mazungumuzo iko na faida fulani. Na hata nilikatala mutu asinikamate picha. Wakati ninakumbuka ile miaka ya zamani, ninaona kama nilikuwa mukosa-adabu, mwenye kiburi, na mukali sana. Mutu mwenye ninajua sana, njo tu nilikuwaka natendea muzuri na kumuonyesha ukarimu.

Wakati nilikuwa na miaka 20, nilianza kupenda kujifunza Biblia. Rafiki yangu fulani mwenye alikuwaka nauzisha dawa za kulewesha, alianzaka kusoma Biblia wakati alikuwaka mu gereza, na tulizungumuza sana juu ya dini, kanisa na mambo yenye Shetani iko nafanya mu dunia. Niliuza Biblia na nikaanza kujifunza Biblia miye peke. Miye na rafiki yangu tulikuwa nasoma sehemu fulani za Biblia, tulizizungumuzia pamoja, na kisha tulikuwa nafikia uamuzi fulani juu ya mambo yenye tulijifunza. Tulifanya vile kwa miezi mingi.

Hii njo mambo yenye tulifikia kuelewa, wakati tulikuwa nasoma Biblia: Tunaishi mu siku za mwisho; Wakristo wanapaswa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu; hawapaswe kuwa sehemu ya ulimwengu, ni kusema hawapaswe kujiingiza mu mambo ya politike; na Biblia iko na mashauri ya muzuri. Tulifikia kuelewa kama Biblia inasemaka kweli na kama kunapaswa kuwa dini ya kweli. Lakini ya wapi njo ya kweli? Tulifikiria dini kubwa-kubwa zenye kuwa na majengo na desturi za kushangaza na namna zinajiingizaka mu mambo ya politike, na tukaona kama Yesu hakukuwaka vile. Tulielewa kama Mungu hakubali zile dini. Kwa hiyo, tuliamua kuchunguza dini za kidogo-kidogo.

Tulikuwa nakutana na watu wa zile dini na kuwauliza maulizo fulani. Tulijua mambo yenye Biblia inasema juu ya ile maulizo, kwa hiyo tungeweza kuona ikiwa majibu yao inapatana na mambo yenye Biblia inasema ao hapana. Kisha ile mazungumuzo, nilikuwa nasali kwa Mungu na kumuambia hivi: ‘Kama hawa watu njo wako mu dini ya kweli, tafazali, unipatie hamu ya kuzungumuza nao siku ingine.’ Lakini kisha kufanya ile mazungumuzo kwa miezi mingi, sikupata dini yenye ilijibia maulizo yetu kwa kutumia Biblia na hakuna siku nilisikiaka hamu ya kuzungumuza nao tena.

Ku mwisho, miye na rafiki yangu tulikutana na Mashahidi wa Yehova. Tuliwauliza ileile maulizo, lakini walikuwa wanajibu kwa kutumia Biblia. Majibu yao ilipatana kabisa na mambo yenye tulikuwa tumejifunza. Kwa hiyo, tuliwauliza maulizo yenye tulikuwa hatuyapata majibu yake mu Biblia. Kwa mufano, tuliwauliza Mungu iko na mawazo gani juu ya kuvuta tumbako na kutumia dawa za kulewesha. Tena, walijibia kwa kutumia Biblia. Na tulikubali kuenda kumikutano ku Jumba ya Ufalme.

Haikukuwa mwepesi kwangu kuenda ku mikutano. Hata kama Mashahidi walinichangamukia na walikuwa navala muzuri, sikupenda kuzungumuza nao. Sikuwatumainia, na sikupenda tena kuenda ku mikutano. Lakini, nilisali tena kwa Mungu, anipatie hamu ya kukutana tena na Mashahidi, kama wao njo wako mu dini ya kweli; na kisha nilisikia hamu sana ya kujifunza Biblia na Mashahidi.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Nilijua kama nilipaswa kuacha kutumia dawa za kulewesha. Kwa hiyo, niliacha bila kukawia. Lakini ilikuwa nguvu sana kuacha kuvuta tumbako. Nilijaribu kuacha mara mingi, lakini sikuweza. Wakati nilisikia kama watu fulani waliachaka tu mara moya kuacha kuvuta tumbako na hawayarudiliaka tena ile tabia, niliomba Yehova anisaidie. Na kisha pale, Yehova alinisaidia kuacha kuvuta tumbako. Nimejifunza kama kuambia Yehova waziwazi mambo yenye iko mu moyo, kuko na faida sana.

Jambo ingine yenye nilipaswa kubadilisha kabisa mu maisha yangu, ni namna yangu ya kuvala na kukata nywele. Wakati nilienda kwa mara ya kwanza ku mukutano ku Jumba ya Ufalme, nywele yangu ilikuwa nasimama ku kichwa sawa miba-miba, na mulikuwa kamba ya bleu ya kuangara-angara. Kisha, nikabadilisha rangi ya nywele yangu, ikakuwa rangi ya orange ya kuangara-angara. Nilikuwa navala jeans na koti ya ngozi yenye iko na maandiko-maandiko. Mashahidi walinishauria kwa upole, lakini sikuona kama ni lazima nifanye mabadiliko. Ku mwisho, nilifikiria andiko ya 1 Yohana 2:15-17 yenye inasema hivi: “Musipende ulimwengu ao vitu vyenye viko katika ulimwengu. Kama mutu yeyote anapenda ulimwengu, upendo wa Baba hauko ndani yake.” Nilifikia kuelewa kama namna yangu ya kuvala na kukata nywele, ilionyesha kuwa ninapenda ulimwengu, na kama juu nionyeshe kama ninapenda Mungu, nilipaswa kubadilika. Na ni vile nilifanya.

Kisha wakati fulani, nilifikia kuelewa kama haiko Mashahidi tu njo walipenda nikuee nafika ku mikutano. Waebrania 10:24, 25 ilinisaidia kuona kama Mungu anapenda tukuwe nakusanyika. Kisha nilianza kuenda ku mikutano yote na kufahamiana na ndugu na dada. Na kisha nikaamua kujitoa kwa Yehova na kubatizwa.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Jambo yenye imenigusa sana nikuona namna Yehova anaruhusu tukuwe marafiki wake wa sana. Huruma yake, na kuona namna anatuhangaikia, imenichochea nifuate mufano wake na wa Mwana wake mu maisha yangu. (1 Petro 2:21) Nimeelewa kama kufuata mufano wa Yesu, haimaanishe kama siwezi kuwa na mambo yenye ninafurahiaka kipekee. Nimejikaza kupenda watu na kuwahangaikia. Ninajikazaka kufuata mufano wa Yesu mu namna yangu ya kutendea bibi yangu na mutoto wangu mwanaume. Na ninahangaikiaka sana ndugu na dada zangu mu kutaniko. Kufuata mufano wa Yesu kunanisaidia nijiheshimie na niweze kuonyesha wengine upendo.

“Walinitendea kwa Heshima.”​—GUADALUPE VILLARREAL

ALIZALIWA MWAKA WA: 1964

INCHI: MEKSIKO

ALIKUWA: MUASHERATI

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Mu familia yetu tulikuwa watoto saba. Nilikomalia Hermosillo, katika Sonora, mu inchi ya Mexico, eneo kwenye watu walikuwa maskini sana. Baba yangu alikufa wakati nilikuwa mutoto. Kwa hiyo, mama yangu alikuwa natumika sana juu ya kutimiza mahitaji yetu. Mara mingi, nilikuwa natembea migulu chini juu hatukukuwa na makuta ya kuuza viatu. Wakati nilikuwa ningali mutoto, nilianza tumika juu ya kusaidia familia yangu. Tuliishi mu nyumba ya kidogo sana, sawa vile familia zingine.

Mara mingi, mama hakukuwa nabakia na siye juu ya kutulinda. Wakati nilikuwa na miaka 6, kijana fulani wa miaka 15 alianza kunitendea mubaya kingono. Na aliendelea kufanya vile kwa wakati murefu. Ile ilifanya nivurugike kuhusu mambo ya ngono. Niliwaza ni kawaida kupendezwa kimapenzi na wanaume. Wakati nilitafuta musaada wa wanganga na wa viongozi wa dini, waliniambia kama hakuna shida, ni sawa tu kupendezwa kimapenzi na wanaume wenzako.

Wakati nilikuwa na miaka 14, niliamua kuonyesha waziwazi kama ninapendezwaka kimapenzi na wanaume wenzangu. Na nilikuwa mu ile hali kwa miaka 11 yenye ilifuata, na hata niliishi na wanaume mbalimbali mu ile wakati. Kisha, nikaamua kujifunza kutengeneza watu nywele, na nikafungula fasi ya kutengenezea watu nywele na kuwapamba. Lakini, sikukuwa na furaha. Mara mingi niliteseka na kujisikia kuwa nimesalitiwa. Nilikuwa naona kama mambo yenye nilikuwa nafanya haikukuwa ya muzuri. Nilianza kujiuliza, ‘mu dunia, muko watu wazuri kabisa?’

Nilifikiria dada yangu. Wakati fulani alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova na kisha akabatizwa. Alikuwaka ananielezea mambo yenye alikuwaka anajifunza. Lakini sikukuwaka namusikiliza. Lakini, nilikuwa nafurahia namna yake ya kuishi na ndoa yake. Niliona namna yeye na bwana yake walikuwa napendana na kuheshimiana kabisa. Walikuwa natendeana muzuri. Kisha wakati fulani, Shahidi mumoja wa Yehova alianza kujifunza na miye Biblia. Ku mwanzo, nilikuwa tu najifunza, lakini sikufurahia kabisa funzo. Kisha mambo ikabadilika.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Mashahidi walinialika ku mukutano na nikaenda. Mambo yenye niliona, nilikuwaka siyaionaka. Kwa kawaida, watu walikuwaka nanichekelea, lakini Mashahidi hawakufanya vile. Walinisalimia kwa upendo, na walinitendea kwa heshima. Ile ilinigusa sana.

Nilifurahia zaidi Mashahidi wa Yehova wakati nilifika ku mukusanyiko wao mukubwa. Niliona kuwa hata kama walikuwa wengi sana, walikuwa tu sawa dada yangu; walikua na roho ya muzuri na walihangaikiana. Nilijiuliza kama wao njo watu wazuri wenye nilikuwaka natafuta. Ilinigusa sana kuona namna wanapendana, na namna wako na umoja na pia namna walitumia Biblia juu ya kujibia maulizo yangu yote. Nilitambua kama Biblia njo iliwasaidia wakuwe watu wazuri vile. Na niliona kama, na miye nilipaswa fanya mabadiliko ya mingi sana juu nikuwe kama wao.

Nilipaswa kubadilisha kabisa namna yangu ya kuwa, juu nilikuwa naishi sawa vile mwanamuke. Nilipaswa kubadilisha namna yangu ya kusema, ya kutenda, ya kuvala, ya kukata nywele, na hata marafiki wangu. Marafiki wangu wa zamani walianza kunichekelea, na kusema: “Juu ya nini uko nafanya hivi? Haiko lazima ubadilike. Acha kujifunza Biblia. Uko na kila kitu.” Lakini jambo ya nguvu sana kubadilisha ilikuwa, kuachana na mwenendo wangu wa uasherati.

Lakini, nilijua kama ninaweza kubadilika, juu maneno ya 1 Wakorinto 6:9-11 ilikuwa imegusa moyo wangu. Ile andiko inasema hivi: “Ao je, hamujue kama watu wenye hawako wenye haki hawatariti Ufalme wa Mungu? Musidanganywe. Waasherati, waabudu-sanamu, wazinifu, wanaume wenye wanakubali matendo ya kulalwa na wanaume wenzao, wanaume wenye kulala na wanaume wenzao . . . hawatariti Ufalme wa Mungu.” Yehova alisaidiaka wale watu wazamani kubadilika, na miye alinisaidia. Nilipiganisha kwa miaka mingi juu niweze kuacha ile tabia. Lakini, mashauri na upendo wenye Mashahidi wa Yehova walinionyesha, ilinisaidia sana.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Leo, niko na maisha ya muzuri. Nilishaoa, na miye na bibi yangu tuko nafundisha mutoto wetu mwanaume kutumikisha mashauri ya Biblia mu maisha yake. Siko tena vile nilikuwaka zamani. Niko sasa na urafiki muzuri na Yehova, na ninafurahia kumutumikia. Niko muzee wa kutaniko na nimesaidia wengine wajifunze mafundisho ya kweli ya Biblia. Mabadiliko yenye nilifanya, ilifurahisha sana mama yangu mupaka naye akaamua kujifunza Biblia na akafikia hata kubatizwa. Dada yangu, mwenye naye alikuwa naishi maisha ya uasherati, amekuwa Shahidi wa Yehova.

Na hata watu wenye walinijuaka zamani, wanasemaka kama nimekuwa mutu muzuri zaidi. Ninajua nini njo ilinisaidia kubadilika. Zamani nilitafutaka musaada wa wanganga, lakini walinipatiaka mashauri ya mubaya. Lakini Yehova amenisaidia kabisa. Hata kama nilikuwa najiona mutu wa bure, aliniona na akanionyesha upendo na kunivumilia. Kufikiria tu namna Mungu wa ajabu sana, mwenye akili, na mwenye upendo sana aliniona na kupenda nikuwe na maisha ya muzuri, kulinipatia nguvu ya kufanya mabadiliko.

“Sikutosheka, nilijisikia kuwa peke yangu, na nilijisikia kuwa ninakosa kitu.”​—KAZUHIRO KUNIMOCHI

ALIZALIWA MWAKA WA: 1951

INCHI: JAPANI

ALIKUWA: MUTU MWENYE KUPENDA SANA MASHINDANO YA KUTEMBEZA KINGA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilikomalia mu muji mutulivu wa pembeni ya bahari, mu eneo ya Shizuoka, katika inchi ya Japani. Mu familia yetu tulikuwa watu munane, na tuliishi mu nyumba ya kidogo. Baba yangu alikuwa na duka ya kuuzisha kinga. Wakati nilikuwa mutoto, alikuwa nanipeleka fasi yenye mashindano ya kutembeza kinga ilikuwa nafanywa, na alifanya nianze kupenda michezo. Baba yangu alianza kunitayarisha juu nikuwe mutu wakufanya mashindano ya kutembeza kinga. Wakati nilikuwa ningali ku masomo ya musingi, alianza kunizoeza sana. Ku masomo ya segondere nilipata ushindi mara tatu, ku mashindano ya taifa yenye ilikuwa nafanywa kila mwaka. Nilipewa nafasi ya kusoma masomo ya juu, lakini niliamua kuenda ku masomo ya kujifunza kufanya mashindano ya kutembeza kinga. Wakati nilikuwa na miaka 19, nilijulikana kuwa mutu wa kufanya mashindano ya kutembeza kinga.

Ile wakati, nilikuwa napenda kuwa wa kwanza mu inchi ya Japani mu mashindano wa kutembeza kinga. Nilipenda kupata makuta mingi sana juu nisaidie familia yangu ikuwe na maisha muzuri. Nilikuwa najizoeza sana. Kila mara wakati nilikuwa naona kuwa mazoezi ao mashindano ya kutembeza kinga iko nguvu, nilikuwa najiambia kama nilizaliwaka juu ya kufanya mashindano ya kutembeza kinga, na kama siwezi kurudia nyuma, nitaweza tu, na kwa hiyo niliendelea. Nilianza kuona matokeo ya kujikaza. Mwaka wa kwanza, nilikuwa wa kwanza kati ya watu wenye walikua wapya mu mashindano ya kutembeza kinga. Mwaka wa pili, nilichaguliwa kati ya watu wenye wangeshindana juu ya kuamua nani njo atakua wa kwanza mu Japani. Mara sita, nilitoka wa pili mu ile mashindano.

Juu nilikuwa kati ya watu wenye walikuwa napata ­ushindi, nilijulikana kuwa mutu mwenye miguu ya mwepesi ya Tokai, eneo fulani ya Japani. Nilikuwa napenda sana kupata ushindi. Watu walianza kuniogopa kwa sababu sikukuwa na huruma mu mashindano. Nilianza kupata makuta mingi sana, na ningeweza kuuza kitu yote yenye ningependa. Niliuza nyumba yenye ilikuwa na chumba ya kufanyia mazoezi na mashini za muzuri sana. Niliuza gari ya bei sana, ilikuwa karibu bei moya na nyumba. Juu ya kulinda makuta yangu, nilianza kuiweka mu viwanja na nyumba, na pia mu biashara.

Lakini, sikutosheka, nilikuwa najisikia kuwa peke yangu, na nilijisikia kuwa ninakosa kitu. Ile wakati nilikuwa nilishaoa na nilikuwa na watoto tatu. Lakini sikukuwa naonyesha watu wa familia yangu uvumilivu. Nilikuwa nakasirikia bibi yangu na watoto wangu juu ya mambo ya burebure. Kila mara walikuwa na wasiwasi, na walikuwa naniangalia juu ya kuona ikiwa nilishakasirika ao hapana.

Lakini, kisha wakati fulani, bibi yangu alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ile ilibadilisha mambo mingi. Alisema kama anapenda kuenda ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo nilimuambia tutaenda siye wote mu familia. Ningali nakumbuka namna usiku fulani, muzee mumoja alitutembeleaka na kuanza kujifunza na miye Biblia. Mambo yenye nilijifunza ilinigusa sana.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Siwezi kusahau namna nilijisikia kisha kusoma Waefeso 5:5. Ile andiko inasema hivi: “Hakuna mwasherati ao mutu mwenye haiko safi ao mutu mwenye pupa,​—maana yake kuwa muabudu-sanamu​—mwenye kuwa na uriti wowote katika Ufalme wa Kristo na wa Mungu.” Niliona kama mara mingi watu wenye kufanya mashindano ya kutembeza kinga, walikuwa nacheza michezo ya makuta, na ile mashindano ilichochea watu wakuwe na pupa. Zamiri yangu ilianza kunisumbua. Nilielewa kama, ikiwa ninapenda kumufurahisha Yehova, nilipaswa kuacha mashindano ya kutembeza kinga. Lakini haikukuwa mwepesi kufanya vile.

Nilikuwa tu nimemaliza mwaka wenye nilipata ushindi sana mu mashindano, na sikupenda kuachia pale. Lakini, niliona kama kujifunza Biblia kulinisaidia nitulie, na nikuwe na amani ya akili, tofauti sana na roho yenye nilipaswa kuwa nayo juu nipate ushindi! Kisha kuanza kujifunza Biblia, nilifanyaka mashindano mara tatu tu. Lakini mu moyo wangu ile hamu ya kufanya mashindano ilikuwa haiyaisha kabisa. Tena nilikuwa najiuliza nitafanya nini juu ya kutimiza mahitaji ya familia yangu. Nilikosa nifanye nini, na watu wa jamaa yangu walianza kunipinga juu ya dini yangu ya mupya. Baba yangu alihuzunika sana. Nilivurugika, nikakua na mahangaiko sana mupaka nikagonjwa estomac.

Kuendelea kujifunza na kukusanyika na Mashahidi wa Yehova njo kulinisaidia sana mu ile wakati ya magumu. Imani yangu ilianza kuwa nguvu zaidi na zaidi. Niliomba Yehova asikilize sala zangu na anisaidie nione namna iko najibia sala zangu. Mahangaiko yenye nilikuwa nayo ilipunguka wakati bibi yangu alinihakikishia kama haiko lazima aishi mu nyumba kubwa juu akuwe na furaha. Pole kwa pole, nilifanya maendeleo.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Nilijionea namna maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 6:33 ni ya kweli kabisa. Yesu alisema hivi mu ile andiko: “Basi, muendelee kutafuta kwanza Ufalme na haki yake, na mutaongezewa vitu hivyo vingine vyote.” Hakuna siku tulishakakosa “mambo ingine” yenye Yesu anazungumuzia, ni kusema, mambo ya lazima. Hata kama makuta yenye ninapataka leo ni ya kidogo sana kama ninailinganisha na makuta yenye nilikuwa napata wakati nilikuwa nafanya mashindano ya kutembeza kinga, miye na familia yangu hatuyakosaka kitu mu miaka 20 yenye imepita.

Zaidi ya yote, wakati ninatumikaka na kuabudu na Wakristo wenzangu, ninasikiaka furaha na ninajisikiaka kuwa mwenye kutosheka kuliko zamani. Sionake hata vile wakati iko napita. Maisha ya familia yangu imekuwa muzuri kabisa. Watoto wangu watatu na bibi zao, wote wako namutumikia Yehova kwa uaminifu.