Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“kamata maamuzi yenye inamutukuza Yehova”

“kamata maamuzi yenye inamutukuza Yehova”

“kamata maamuzi yenye inamutukuza Yehova”

“Mwerevu anafikiria sana kila hatua.”​—MEZ. 14:15.

1, 2. (a) Nia yetu kubwa inapaswa kuwa nini wakati tuko nakamata maamuzi? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

 TUNAKAMATAKA maamuzi ya mingi kila siku. Matokeo ya maamuzi ya mingi inakuwaka ya muda fulani tu. Lakini, maamuzi ingine inaweza kuwa na matokeo juu ya maisha yetu. Wakati tunakamata maamuzi, ikuwe ya maana sana ao ya kidogo-kidogo, nia yetu kubwa inapaswa kuwa: kumutukuza Mungu.​—Soma 1 Wakorinto 10:31.

2 Unaonaka kama ni mwepesi ao ni nguvu kukamata maamuzi? Juu tumutumikie Yehova muzuri, tunapaswa kujifunza kutofautisha mema na mabaya. Ile itatusaidia tukamate maamuzi yenye inategemea mambo yenye tunaamini, hapana mambo yenye wengine wanatuambia. (Ro. 12:1, 2; Ebr. 5:14) Juu ya nini tujifunze kukamata maamuzi ya muzuri? Juu ya nini wakati fulani inakuwaka nguvu kukamata maamuzi ya muzuri? Tunaweza kufanya nini juu tukamate maamuzi yenye itamutukuza Mungu?

JUU YA NINI TUJIFUNZE KUKAMATA MAAMUZI YA MUZURI?

3. Hatupaswe kuacha nini ituchochee wakati tuko nakamata maamuzi?

3 Kama tunasita kufanya mambo yenye Biblia inasema, wafanyakazi wenzetu ao wanafunzi wenzetu wanaweza kuwaza kama hatuamini Biblia, na wanaweza kutuchochea kufanya mambo yenye wao wanapenda. Wanaweza kusema uongo, kudanganya, ao kuiba, na kisha wanaweza kutuchochea “kufuata watu wengi.” Ni kusema wanaweza kutuchochea tuwaige ao tufiche mambo yenye walifanya. (Kut. 23:2) Lakini, kama mutu anajua kukamata maamuzi yenye inamutukuza Mungu, hataacha woga ao tamaa ya kupenda kukubaliwa na wengine imuchochee afanye mambo yenye Biblia inakataza.​—Ro. 13:5.

4. Juu ya nini wengine wanaweza penda kutukamatia maamuzi?

4 Haiko kusema kama watu wote wenye wanapenda kutukamatia maamuzi wako na nia ya mubaya. Marafiki wenye kuwa na nia ya muzuri wanaweza kukazia kama tunapaswa kufuata mashauri yao. Hata kama tunaishi mbali, pengine watu wa familia yetu wangali natuhangaikia sana, na wanaweza kuona kama wanapaswa kutusaidia kukamata maamuzi ya maana. Kwa mufano, tufikirie mambo ya matunzo. Biblia inakataza kabisa kutumia damu. (Mdo. 15:28, 29) Lakini kuko matunzo ingine yenye inaomba mutu aamue yeye mwenyewe kama ataikubali ao hapana. * Watu wa jamaa yetu wanaweza kutukaza tufuate mawazo yao. Lakini, wakati tuko nakamata maamuzi, tunapaswa kukumbuka kama kila Mukristo mwenye kubatizwa, anapaswa ‘kubeba muzigo wake mwenyewe.’ (Gal. 6:4, 5) Nia yetu kubwa inapaswa kuwa: kuendelea kuwa na zamiri safi mbele ya Mungu, hapana kupendeza wanadamu.​​—1 Ti. 1:5.

5. Tunapaswa kufanya nini juu imani yetu isiharibike?

5 Kusitasita kunaweza kututia mu hatari. Mutume Yakobo aliandika kama mutu mwenye kusitasita ni mutu “mwenye haiko imara katika njia zake zote.” (Yak. 1:8) Sawa vile mutu mwenye anashindwa kuongoza mashua yake mu bahari yenye upepo mukali, mutu mwenye kusitasita anaweza kuchochewa kwa vyepesi na mawazo ya watu wengine. Imani yake inaweza kuharibika kama mashua yenye kuvunjika, na kisha anaweza kusema kama ni kosa ya wengine! (1 Ti. 1:19) Tunapaswa kufanya nini juu imani yetu isiharibike? Tunapaswa “kufanywa imara katika imani.” (Soma Wakolosai 2:6, 7.) Juu imani yetu ikuwe imara, tunapaswa kujifunza kukamata maamuzi yenye inaonyesha kama tunaamini mambo yenye Biblia inasema. (2 Ti. 3:14-​17) Lakini, nini njo inaweza fanya ikuwe nguvu kwetu kukamata maamuzi ya muzuri?

Juu ya Nini Inaweza Kuwa Nguvu Kukamata Maamuzi

6. Woga inaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

6 Woga inaweza kufanya ikuwe nguvu kukamata maamuzi ya muzuri. Kwa mufano, tunaweza kuogopa kukamata uamuzi mubaya, tunaweza kuogopa kushindwa, ao tunaweza kuogopa kama wengine watatuona kuwa wapumbafu. Ile inaeleweka. Hakuna mutu mwenye anapendaka kukamata maamuzi yenye itamuletea magumu ao yenye itamupatisha haya. Lakini, kumupenda Mungu na kupenda Neno yake Biblia kunaweza kutusaidia tusiogope. Namna gani? Kama tunamupenda Mungu, tutachunguza Neno yake na vichapo mbele ya kukamata maamuzi ya maana. Kama tunafanya vile, tutaepuka makosa mingi. Juu ya nini? Juu Biblia inaweza “kumupatia werevu mutu mwenye hana uzoefu; [na] kumupatia kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.”​—Mez. 1:4.

7. Mufano wa Mufalme Daudi unatufundisha nini?

7 Ni kusema tutakuwa nakamata maamuzi ya muzuri kila siku? Hapana. Siye wote tunafanyaka makosa. (Ro. 3:23) Kwa mufano, Mufalme Daudi alikuwa na hekima na alikuwa muaminifu kwa Yehova. Lakini, wakati fulani alikamataka maamuzi ya mubaya yenye ilifanyaka yeye na wengine wateseke. (2 Sa. 12:9-12) Hata vile, Daudi hakuacha makosa yake imuzuie kukamata maamuzi yenye inamutukuza Mungu. (1 Fa. 15:4, 5) Tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri hata kama tulifanyaka makosa zamani. Tutaweza kufanya vile kama tunamuiga Daudi. Kama Daudi, tunapaswa kukumbuka kuwa Yehova anakuwaka anasamehe makosa yetu na kama ataendelea kutegemeza wale wenye kumupenda na kumutii.​—Zb. 51:1-4, 7-10.

8. Mambo yenye Mutume Paulo alisema juu ya ndoa inatufundisha nini?

8 Kuko jambo yenye inaweza kutusaidia tusikuwe naogopa kukamata maamuzi. Ni jambo gani? Ni kukumbuka kama mu hali fulani, watu wawili wanaweza kukamata maamuzi tofauti, lakini yote ni ya muzuri. Fikiria mambo yenye mutume Paulo alisema kuhusu ndoa. Aliandika hivi: “Kama mutu yeyote anawaza kwamba anajiendesha mubaya kwa kubakia bila kuoa ao kuolewa, na kama amepita mwanzo wa kipindi cha ujana, basi inapaswa kuwa hivi: Afanye vile anataka; hafanye zambi. Aoe ao aolewe. Hata hivyo, kama mutu yeyote ametulia katika moyo wake na hajisikie kuwa analazimika, lakini iko na mamlaka juu ya nia yake mwenyewe na amefanya uamuzi katika moyo wake kubakia bila kuoa ao kuolewa, atafanya muzuri. Vilevile mutu yeyote mwenye anaoa ao anaolewa anafanya muzuri, lakini mutu yeyote mwenye haoe ao haolewe atafanya muzuri zaidi.” (1 Ko. 7:36-38) Paulo alisema kama ni muzuri zaidi kama mutu anabakia bila kuoa ao kuolewa, lakini hakumaanisha kama ni mubaya kama mutu anaoa ao kuolewa. Yote ni maamuzi ya muzuri.

9. Juu ya nini tunapaswa kuhangaikia namna wengine wataona maamuzi yetu? Fasiria.

9 Wakati tunakamata maamuzi, tunapaswa kuhangaikia mambo yenye wengine watawaza? Ndiyo, kwa kadiri fulani. Wakati mutume Paulo alikuwa nazungumuzia ikiwa Mukristo anaweza kula ao hapana vyakula vyenye vilikuwa vimetolewa zabihu kwa sanamu, alionyesha kuwa hata kama haiko mubaya kufanya jambo fulani, ni muzuri kuepuka kuifanya kama itakwaza wengine. Paulo aliamua nini? Aliandika hivi: “Kama chakula kinamukwaza ndugu yangu, mimi sitakula nyama tena hata kidogo, ili nisimukwaze ndugu yangu.” (1 Ko. 8:4-​13) Na siye tunapaswa fikiria ikiwa maamuzi yetu itakwaza wengine ao hapana. Lakini, jambo kubwa yenye tunapaswa kufikiria ni ikiwa maamuzi yetu itafanya urafiki wetu na Yehova ukuwe nguvu ao hapana. (Soma Waroma 14:1-4.) Ni kanuni gani za Biblia zenye zitatusaidia kukamata maamuzi yenye inamutukuza Mungu?

Mambo Sita Yenye Itatusaidia Kukamata Maamuzi ya Muzuri

10, 11. (a) Namna gani tunaweza kuepuka kimbelembele mu familia? (b) Wazee wanapaswa kukumbuka nini wakati wako nakamata maamuzi kwa ajili ya kutaniko?

10 Uepuke kimbelembele. Mbele ya kukamata uamuzi fulani, unapaswa kujiuliza hivi: ‘Miye njo wakuamua mu hii hali?’ Mufalme Sulemani aliandika hivi: “Wakati kimbelembele kinakuja, haya itafuata, lakini wenye kiasi wako na hekima.”​—Mez. 11:2.

11 Wazazi wanaweza kupatia watoto ruhusa ya kukamata maamuzi fulani, lakini kuko maamuzi yenye watoto hawapaswe kukamata bila ruhusa ya wazazi wao. (Kol. 3:20) Mu familia, bibi anaweza kukamata maamuzi fulani, lakini anapaswa kukumbuka kama, bwana njo kichwa cha familia. (Mez. 1:8; 31:10-18; Efe. 5:23) Vilevile, bwana anapaswa kukumbuka kama mamlaka yake iko na mipaka na kama anapaswa kujitiisha kwa Kristo. (1 Ko. 11:3) Wazee wanakamataka maamuzi fulani kwa ajili ya kutaniko. Lakini, wanapaswa kuwa waangalifu juu ‘wasipite mambo yenye yaliandikwa’ mu Neno ya Mungu. (1 Ko. 4:6) Na wanajikazaka sana kufuata muongozo wenye mutumwa muaminifu na mwenye busara anawatolea. (Mt. 24:45-47) Tutaepuka magumu mingi kama tunaonyesha kiasi kwa kuepuka kukamata maamuzi yenye hatuna haki ya kukamata.

12. (a) Juu ya nini tunapaswa kufanya utafiti? (b) Fasiria namna mutu anaweza kufanya utafiti.

12 Ufanye utafiti. Sulemani aliandika hivi: “Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.” (Mez. 21:5) Kwa mufano, kama uko nafikiria kuanza biashara fulani, usifuate tu mambo yenye moyo wako uko nakuambia. Tafuta habari zote zenye uko nazo lazima, tafuta mashauri ya watu wenye wanaelewa muzuri ile biashara, na utafute kanuni za Biblia zenye zinaweza kukusaidia mu ile hali. (Mez. 20:18) Juu ufanye utafiti muzuri, fanya liste mbili. Ku moja, uandike faida zenye utapata, na ku ingine, uandike magumu yenye unaweza kupata. Mbele ya kukamata uamuzi, “hesabia garama.” (Lu. 14:28) Usifikirie tu makuta yenye utapata, lakini ujiulize pia ikiwa ile biashara itafanya urafiki wako na Yehova ukuwe namna gani. Inaomba wakati na nguvu juu ya kufanya utafiti. Lakini kama unafanya vile, unaweza kuepuka kukamata maamuzi ya haraka-haraka yenye inaweza kukuletea mahangaiko.

13. (a) Yakobo 1:5 inatuhakikishia nini? (b) Tutapata faida gani kama tunamuomba Mungu atupatie hekima?

13 Umuombe Mungu akupatie hekima. Maamuzi yetu itamutukuza Mungu kama tunamuomba atupatie hekima. Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila kulaumu, na atapewa hiyo.” (Yak. 1:5) Hatupaswe kusikia haya ya kuomba Mungu hekima juu siye wote tuko na lazima ya hekima juu tuweze kukamata maamuzi ya muzuri. (Mez. 3:5, 6) Kama tunawaza kuwa hatuna lazima ya hekima ya Mungu, tutakamata maamuzi ya mubaya. Wakati tunamuomba Mungu atupatie hekima na tunatafuta kanuni za Biblia, tunaruhusu roho takatifu itusaidie kuchunguza nia yenye inatuchochea kufanya jambo fulani.​—Ebr. 4:12; Soma Yakobo 1:22-25.

14. Juu ya nini tunapaswa kuepuka tabia ya kungoya-ngoya?

14 Ukamate uamuzi. Usikimbilie kukamata uamuzi kama hauyafanya utafiti na kumuomba Mungu akupatie hekima. Mutu mwenye hekima, hakuwake haraka-haraka. ‘Anafikiria sana kila hatua.’ (Mez. 14:15) Lakini uepuke pia tabia ya kungoya-ngoya. Mutu mwenye iko na tabia ya kungoya-ngoya, mara mingi anajiteteaka kwa kuleta visingizio vyenye havina maana. (Mez. 22:13) Kwa kufanya vile, anaacha wengine waongoze maisha yake.

15, 16. Nini njo itasaidia mutu afanye mambo yenye ameamua kufanya?

15 Ufanye mambo yenye umeamua kufanya. Wakati yote na nguvu yote yenye tulitumia juu ya kukamata uamuzi muzuri, inaweza kufa bure kama hatufanye mambo yenye tuliamua kufanya. Sulemani aliandika hivi: “Jambo lenye mukono wako unapata kufanya, ulifanye kwa nguvu zako zote.” (Muh. 9:10) Juu tupate matokeo ya muzuri, tunapaswa kuwa tayari kufanya mambo yenye itatusaidia kutimiza uamuzi wetu. Kwa mufano, tuseme muhubiri anaamua kuwa painia. Ataweza? Ataweza kama haache kazi yake, na mambo ya kujifurahisha imufanye akose nguvu na wakati ya kuhubiri.

16 Hata kama tunakamata maamuzi ya muzuri, inaweza kuwa nguvu kufanya mambo yenye tuliamua kufanya. Juu ya nini? Juu “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yo. 5:19) Tunapaswa kupambana na “watawala wa ulimwengu wa giza hili, na majeshi ya pepo wachafu katika mahali pa kimbingu.” (Efe. 6:12) Mutume Paulo na mwanafunzi Yuda, wote walionyesha kama ikiwa mutu anaamua kumutukuza Mungu, maisha yake haitakuwa mwepesi.​​—1 Ti. 6:12; Yud. 3.

17. Kuhusu maamuzi yenye tunakamata, Yehova anapenda tufanye nini?

17 Uchunguze tena uamuzi wako na kama ni lazima ufanye mabadiliko. Wakati fulani, mambo haikuwake vile tulipanga. “Wakati na matukio yenye hayatazamiwe” inatufikiaka siye wote. (Muh. 9:11) Lakini Yehova anapenda tuendelee kushikamana na maamuzi fulani, hata kama tunapata magumu. Kwa mufano, kama mutu alishajitoa kwa Yehova, ao alishaoa ao kuolewa, hapaswe kubadilisha ile maamuzi. Mungu anapenda tuendelee kuheshimia ile maamuzi. (Soma Zaburi 15:1, 2, 4.) Lakini kuko maamuzi ingine ya mingi, yenye haiko ya maana sana, yenye tunaweza kubadilisha. Mutu mwenye hekima anapaswa kuchunguza mara kwa mara maamuzi yenye alishakamata. Hapaswe kuruhusu kiburi ao kichwa nguvu imuzuie kubadilisha maamuzi fulani, kama ni lazima. (Mez. 16:18) Jambo ya maana sana yenye tunapaswa kuhangaikia ni kumutukuza Yehova mu maisha yetu.

Saidia Wengine Wajifunze Kukamata Maamuzi Yenye Kumutukuza Mungu

18. Wazazi wanaweza kufanya nini juu ya kusaidia watoto wao wajue namna ya kukamata maamuzi ya muzuri?

18 Wazazi wanaweza kujikaza kusaidia watoto wao wajue namna ya kukamata maamuzi yenye inamutukuza Mungu. Njia ya muzuri zaidi ya kuwafundisha ni kupitia mufano wao. (Lu. 6:40) Wakati inafaa, wazazi wanaweza kufasiria watoto wao mambo mbalimbali yenye walifanya juu wafikie kukamata uamuzi fulani. Wanaweza pia kuacha watoto wao wakamate maamuzi fulani, na kuwapongeza ikiwa ile maamuzi inaleta matokeo ya muzuri. Halafu kama mutoto anakamata uamuzi mubaya? Muzazi anaweza kupenda kulinda mutoto wake juu asipate matokeo ya mubaya ya uamuzi wake. Lakini kufanya vile haiko kumusaidia. Kwa mufano, tuseme muzazi anaruhusu mutoto wake apate kikaratasi ya kumuruhusu kutembeza gari. Kisha ule mutoto haheshimie sheria za mu barabara na anaombwa alipe amande. Muzazi anaweza kuamua kumulipia ile amande. Lakini, kama anamuambia atumike juu yeye peke apate makuta ya kulipa ile amande, ile itamusaidia siku ingine akuwe muangalifu.​—Ro. 13:4.

19. Tunapaswa kufundisha wanafunzi wetu wa Biblia kufanya nini, na tutafanya vile namna gani?

19 Yesu aliambia wanafunzi wake wafundishe wengine. (Mt. 28:20) Kukamata maamuzi ya muzuri, iko kati ya mambo ya maana sana yenye tunaweza kufundisha wanafunzi wetu wa Biblia. Juu ya kuwasaidia wajue namna ya kukamata maamuzi ya muzuri, tunapaswa kuepuka kuwaambia mambo ya kufanya. Ni muzuri zaidi tuwafundishe namna ya kutumia kanuni za Biblia ili waweze kujikamatia maamuzi ya muzuri. Tusisahau kama “kila mumoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu.” (Ro. 14:12) Kwa hiyo, siye wote tunapaswa kujifunza kukamata maamuzi ya muzuri, yenye itamutukuza Mungu.

[Maelezo ya chini]

^ Ili kupata habari zaidi, ona nyongeza “Ninaona Namna Gani Sehemu za Damu na Namna Mbalimbali za Matunzo Zinazoomba Kutumia Damu Yangu Mwenyewe?” yenye ilitolewa mu Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 11, 2006, ukurasa wa 3-6.

Utajibia Namna Gani?

• Juu ya nini tujifunze kukamata maamuzi ya maana?

• Woga inaweza kuwa na matokeo gani juu yetu, na tunaweza kufanya nini juu ya kushinda woga?

• Ni Mambo gani sita yenye itatusaidia kukamata maamuzi yenye inamutukuza Mungu?

[Maulizo ya Funzo]

[Kisanduku/​Picha kwenye ukurasa wa 16]

Mambo Yenye Itatusaidia Kukamata Maamuzi ya Muzuri

1 Uepuke kimbelembele

2 Ufanye utafiti

3 Umuombe Mungu akupatie hekima

4 Ukamate uamuzi

5 Ufanye mambo yenye umeamua kufanya

6 Uchunguze tena uamuzi wako na kama ni lazima ufanye mabadiliko

[Picha kwenye ukurasa wa 15]

Mutu mwenye kusitasita iko sawa vile mutu mwenye anashindwa kuongoza mashua yake mu bahari yenye upepo mukali