Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

3. Magonjwa

3. Magonjwa

3. Magonjwa

“Kutakuwa . . . magonjwa.”​—LUKA 21:11.

● Bonzali, alikuwa munganga mu inchi moja ya Afrika kwenye watu wameteseka kwa sababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe. Alifanya yake yote juu ya kutunza kikundi fulani ya wafanyakazi wenye walikuwa wanakufa kwa sababu ya ugonjwa wa Marburg. * Aliomba musaada kwa wakubwa wa serikali wenye walikuwa mu muji ingine mukubwa zaidi, lakini hawakumusaidia. Musaada ulifika kisha miezi ine, lakini Bonzali alikuwa alishakufa. Wafanyakazi wenye alikuwa anajaribu kuokoa walimuambukiza ugonjwa wa Marburg.

USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Magonjwa ya mapafu (sawa vile pneumonie), magonjwa ya kuhara, SIDA, tuberculose, na malaria iko kati ya magonjwa ya mubaya yenye inatesa sana wanadamu. Mu mwaka wa 2004, ile magonjwa tano iliua watu karibu milioni 10.7. Ni kusema ile mwaka yote, ile magonjwa ilikuwa inaua mutu moja kila segonde tatu.

WATU FULANI WANASEMA NINI? Watu wanaendelea kuongezeka mu dunia, njo maana hesabu ya wagonjwa inapaswa tu kuwa mingi. Kuko watu wengi wenye wanaweza kuambukizwa.

ILE NI KWELI? Watu wemeongezeka sana mu dunia. Lakini pia, uwezo wa mwanadamu wa kupima magonjwa, kuizuia, na kuitunza umeongezeka. Kwa hiyo, magonjwa na matokeo ya ile magonjwa inapaswa kupunguka. Lakini mambo haiko vile, iko njo inaongezeka.

UNAWAZA NINI? Watu wako wanateseka kwa sababu ya magonjwa ya mubaya, sawa vile Biblia ilisemaka?

Matetemeko ya inchi, njala, na magonjwa inafanya watu wengi sana wateseke. Watu wengine wengi wako wanateswa na wanadamu wenzao; wengi wanateswa na watu wenye wanapaswa kuwalinda. Ona mambo yenye Biblia ilisema kama ingetokea.

[Maelezo ya chini]

^ Marburg ni homa ya kutokwa na damu, yenye inaletwa na virusi fulani yenye inafanana na virusi ya Ebola.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 6]

“Sawa vile ni mubaya sana kukuliwa na simba ao munyama mwingine wa pori, vilevile ni mubaya sana kukuliwa na ugonjwa wenye kuwa ndani ya mwili wetu na kuona vile ule ugonjwa uko unaua watu wengine.”​—MICHAEL OSTERHOLM, MUTU MWENYE KUJIFUNZA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA.

[Kwenye Picha Zilitoka ukurasa wa 6]

© William Daniels/​Panos Pictures