Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

5. Kuharibu dunia

5. Kuharibu dunia

5. Kuharibu dunia

“[Mungu] ataharibu wale wenye wanaharibu dunia.”​—UFUNUO 11:18.

● Mwanaume mwenye kuitwa Pirri anatengenezaka pombe ya muti ya ngazi mu muji wa Kpor, Nigeria. Mafuta mingi ilimwangika fasi kwenye muto Niger unajigawanya, na ile iliharibisha biashara yake. Anasema hivi: “Inaua samaki, inaharibisha ngozi yetu, na inachafua mito yetu. Sina tena kazi ya kunisaidia kupata mambo yenye niko nayo lazima.”

USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Watu fulani wenye kufanya uchunguzi wanasema kama tone milioni 6.5 za uchafu zinaingiaka mu bahari za mu dunia kila mwaka. Karibu nusu ya ile uchafu ni vitu vya plastike vyenye vitabakia mu maji kwa miaka mingi mbele vifikie kuoza. Zaidi ya kuharibu dunia, wanadamu wako wanatumia mali ya dunia haraka sana. Uchunguzi umeonyesha kama dunia iko na lazima ya mwaka moja na miezi tano ili kutokeza tena vitu vyenye wanadamu wametumia mu mwaka moja. Gazeti moja ya Australia inasema hivi: “Kama watu wanaendelea kuongezeka na kutumia sana mali ya dunia, kufikia mwaka wa 2035, tutakuwa na lazima ya dunia mbili.”​—Sydney Morning Herald.

WATU FULANI WANASEMA NINI? Wanadamu wako na akili sana. Wanaweza kumaliza ile matatizo na kuokoa dunia.

ILE NI KWELI? Vikundi mbalimbali na watu fulani-fulani wamejikaza sana kuelezea watu faida ya kutunza dunia yetu. Lakini dunia inaendelea kuchafuliwa sana.

UNAWAZA NINI? Inaomba Mungu afanye jambo fulani juu ya kuokoa dunia, sawa vile amesema?

Zaidi ya maunabii tano yenye tumezungumuzia, Biblia ilitabiri pia mambo fulani ya muzuri yenye ingetokea mu siku za mwisho. Moja kati ya ile mambo inazungumuziwa mu unabii wa sita.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 8]

“Zamani, kwenye ninaishi kulikuwa sawa vile paradiso, lakini sasa ninaishi fasi kwenye kunayala uchafu wenye unayala sumu​—MANENO YA ERIN TAMBER KUHUSU MATOKEO YA MAFUTA (PETROLE) YENYE ILIMWANGIKA KWENYE GUBA YA MEKSIKO MU 2010. ANAISHI PEMBENI YA BAHARI, MU INCHI YA AMERIKA.

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

Ni Kosa ya Mungu?

Juu Biblia ilitabiri mambo ya mubaya yenye tuko tunaona leo, ni kusema ni kosa ya Mungu kama ile mambo iko inatokea? Yeye njo anatuleteaka mateso? Unaweza kupata majibu ya ile maulizo mu sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? yenye ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 8]

U.S. Coast Guard photo