Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Juu ya nini mwanamuke mwenye alikuwa na miaka zaidi ya 60 aliamua kuacha kuabudu sanamu? Juu ya nini padri wa dini ya Shinto aliacha kazi yake na kuamua kuwa Shahidi wa Yehova? Nini ilisaidia mwanamuke mwenye wazazi wake waliachaka aache kuhuzunika? Acha tuone.

“Nilishakaacha Kuabudu Sanamu.”​—ABA DANSOU

ALIZALIWA MWAKA WA: 1938

INCHI: BENIN

ALIKUWA: MUABUDU SANAMU

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilikomalia mu kijiji yenye kuitwa So-Tchahoué. Ni kijiji yenye kuwa na maeneo yenye tingi-tingi ao yenye maji-maji, yenye inapatikana pembeni ya ziwa. Watu wa mu ile kijiji wanafanyaka kazi ya kuvua samaki na kufuga wanyama sawa vile ngombe, mbuzi, kondoo, nguruwe na ndege. Hamukuwake barabara, njo maana watu wanatumiaka mashua na mitumbwi juu ya kusafiri. Mara mingi watu wanatumiaka mbao na nyasi juu ya kujenga nyumba zao. Lakini kuko pia nyumba fulani za matofali (ao briques). Watu wengi ni maskini. Hata vile, mambo sawa vile wizi, kuingiliana haikuwake sana, sawa vile mu miji mikubwa.

Baba yangu alinitumaka miye na dada yangu fasi fulani yenye kuwa mbali na watu wengine, na kule tulijifunza desturi za kwetu. Wakati nilikomala, nilianza kuabudu Dudua (Oduduwa) mungu wa Wayoruba. Nilijengea ule mungu nyumba na nilizoea kumutolea zabihu za igname, mafuta ya ngazi, konokono, kuku, njiwa, na wanyama wengine. Zile zabihu zilikuwa bei sana, na mara mingi zilikuwa zinanimaliza makuta.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Wakati nilianza kujifunza Biblia, nilijifunza kama Yehova tu njo Mungu wa kweli. Tena, nilijifunza kama hapendi tutumie sanamu mu ibada. (Kutoka 20:4, 5; 1 Wakorinto 10:14) Nilijua kama nilipaswa kufanya jambo fulani. Kwa hiyo, nilitupa sanamu zangu zote na nikatosha mu nyumba yangu kila kitu yenye ilikuwa na uhusiano na ibada ya sanamu. Niliacha kutafuta habari kwa wafumu, na niliacha kufanya desturi za kwetu zenye hazipatane na Maandiko, na desturi za maziko.

Haikukuwa mwepesi kufanya ile mabadiliko juu nilikuwa na miaka zaidi ya 60. Marafiki wangu, watu wa jamaa yangu, na majirani walinipinga na kunichekelea. Lakini niliomba Yehova anipatie nguvu ya kufanya mambo ya muzuri. Maneno yenye iko mu Mezali 18:10 ilinitia moyo. Ile andiko inasema hivi: “Jina la Yehova ni munara wenye nguvu. Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.”

Jambo ingine yenye ilinisaidia ni kufika ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Kule niliona namna ndugu na dada wanapendana, na namna wanajikaza kutumikisha mu maisha yao mambo yenye Biblia inafundisha. Mambo yenye niliona, ilinihakikishia kama Mashahidi wa Yehova njo dini ya kweli.

FAIDA YENYE NIMEPATA:Kutumikisha kanuni za Biblia kunanisaidia nikuwe na uhusiano muzuri na watoto wangu. Tena, minajisikiaka sawa vile wamenishusha muzigo muzito, wenye nilikuwa nabeba. Nilikuwaka natumikisha makuta yangu ku sanamu zenye hazina uzima na zenye hazikukuwaka hata nanisaidia kitu. Sasa niko namutumikia Yehova, mwenye atamaliza magumu yetu yote. (Ufunuo 21:3, 4) Niko na furaha sana juu siko tena mutumwa wa sanamu, lakini niko mutumwa wa Yehova! Amenisaidia kupata usalama na ulinzi wa kweli.

“Nilikuwa Natafuta Mungu Tangu Wakati Nilikuwa Mutoto.”​—SHINJI SATO

ALIZALIWA MWAKA WA: 1951

INCHI: JAPANI

ALIKUWA: PADRI MU DINI YA SHINTO

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilikomalia mu muji fulani mudogo, mu maeneo ya mashamba ya Japani. Wazazi wangu walikuwa napenda sana mambo ya dini; na tangu wakati nilikuwa mutoto, walinifundisha kuabudu miungu ya dini ya Shinto. Wakati nilikuwa kijana mudogo, mara mingi nilifikiria juu ya wokovu wangu, na nilipenda sana kusaidia watu wenye walikuwa na magumu. Ninakumbuka siku moja wakati niikuwaka ku masomo ya musingi, mwalimu aliombaka kila mwanafunzi aseme anapenda kufanya nini wakati atakomala. Kila mwanafunzi alisema kazi yenye angependa kufanya, sawa vile kuwa mwanasayansi. Miye nilisema kama nitamutumikia Mungu. Kila mutu alinicheka.

Wakati nilimaliza masomo ya segondere, nilienda ku masomo ya kuwa mwalimu wa dini. Wakati nilikuwa ku ile masomo, nilikutana na padiri fulani wa dini ya Shinto. Alikuwa napenda kusoma kitabu fulani yenye ilikuwa na jalada ya mweusi. Siku moja aliniuliza, “Sato, unajua hii ni kitabu gani?” Juu nilikuwa nilishaona jalada ya ile kitabu, nilijibia, “Ni Biblia.” Kisha akasema, “Kila mutu mwenye anapenda kuwa padri wa dini ya Shinto, anapaswa kusoma hii kitabu.”

Palepale nilitoka na kuenda uza Biblia. Niliiweka fasi ya kuonekana muzuri, mu kabati yangu ya vitabu na niliichunga muzuri. Lakini sikukuwa napanga wakati ya kuisoma juu masomo ilikuwa nanikamata wakati yote. Wakati nilimaliza masomo, nikakuwa padri ku hekalu ya Washinto. Nilikuwa sasa namutumikia Mungu sawa vile nilikuwaka napenda tangu wakati nilikuwaka mtoto.

Lakini, kisha wakati fulani, nilitambua kama kuwa padri wa dini ya Shinto, ilikuwa tofauti na vile nilikuwa nawazia. Mapadri wengi hawakukuwa napenda sana watu na hawakukuwa nawahangaikia. Na wengi hawakukuwa na imani. Padri fulani, mwenye alikuwa natusimamia, alifikia hata kuniambia hivi: “Kama unapenda mambo ikuendee muzuri hapa, usikuwe nazungumuza juu ya imani, ukuwe tu nazungumuzia mambo ya filozofia. Inakatazwa kuzungumuzia imani hapa.”

Wakati nilisikia maneno ya vile, sikutumainia tena dini ya Shinto. Hata kama nilikuwa natumika ku hekalu, niliendelea kuchunguza dini zingine. Lakini, hakuna yenye niliona kuwa ya muzuri zaidi. Kadiri niliendelea kuchunguza dini, ni vile niliendelea kuvunjika moyo. Niliona kama hakuna dini yenye inafundishaka kweli.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Mu mwaka wa 1988, nilikutana na Mubuda mwenye alinitia moyo nikuwe nasoma Biblia. Nilikumbuka ule padri wa Shinto, mwenye naye aliniambiaka nikuwe nafanya vile. Niliamua kufanya vile. Nilianza kusoma Biblia, na bila kukawia, niliipenda sana. Wakati fulani nilikuwa naisoma usiku wote mupaka asubui.

Mambo yenye nilisoma, ilinifanya nikuwe na hamu ya kusali kwa Mungu mwenye kuzungumuziwa mu Biblia. Nilianza kusali sala ya mufano yenye kuwa mu Matayo 6:9-​13. Nilirudilia ile sala kisha kila saa mbili, hata wakati nilikuwa nafanya kazi yangu ku hekalu ya Washinto.

Nilikuwa na maulizo mingi juu ya mambo yenye nilikuwa nasoma. Ile wakati, nilikuwaka nilishaowa, na nilijua kama Mashahidi wa Yehova wanafundishaka watu juu ya Biblia, juu walikuwaka walishatembelea bibi yangu. Nilitafuta Shahidi mumoja wa Yehova na nilimumwangia mvua ya maulizo. Nilishangala kuona vile alitumia Biblia juu ya kujibia ile maulizo yote. Aliomba Mashahidi wengine wakuwe najifunza na miye Biblia.

Kisha tu wakati kidogo, nilianza kuenda ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Ile wakati sikutambua kama, kati ya wale Mashahidi, kuko wamoja wenye nilitendeaka kwa ukali zamani. Hata vile, walinisalimia kwa furaha na kunikaribisha muzuri.

Ku ile mikutano, nilijifunza kama, Mungu anapenda bwana apende na aheshimie watu wa familia yake. Lakini, miye nilikuwa nahangaikia sana kazi yangu ya upadri na sikukuwa nahangaikia bibi yangu na watoto wangu wawili. Sasa, nilikumbuka kama nilikuwaka nasikiliza watu wenye walikuwa wanakuya kuabudu ku hekalu, lakini hakuna hata siku moja yenye nilisikilizaka mambo yenye bibi yangu anapenda kusema.

Wakati niliendelea kujifunza Biblia, nilijifunza mambo mingi juu ya Yehova, yenye ilifanya nimukaribie. Andiko yenye ilinigusa moyo sana ni ya Waroma 10:13, yenye inasema hivi: “Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.” Nilikuwa natafuta Mungu tangu wakati nilikuwa mutoto, na sasa, nilikuwa nimemupata!

Nilianza kuona kama, sipaswe kuendelea kutumika ku hekalu. Ku mwanzo, nilijiuliza watu watawaza nini kama ninaacha dini ya Shinto. Lakini, mara mingi nilikuwaka najiambia kama nitaacha dini ya Shinto kama ninapata Mungu wa kweli fasi ingine. Njo maana, mu mwaka 1989, niliamua kusikiliza zamiri yangu. Niliacha dini ya Shinto na nikajitia mu mikono ya Yehova.

Haikukuwa mwepesi kuacha kutumika ku hekalu. Wenye walikuwa nanisimamia walijaribu kunichochea nibakie. Lakini jambo ya nguvu sana, ilikuwa kujulisha wazazi wangu. Wakati nilikuwa mu njia ya kuenda kwao, nilikuwa na wasiwasi sana mupaka kifua ikaanza kuniluma na magoti ikaniregea! Nilisimama mara mingi mu njia na kuomba Yehova anipatie nguvu.

Wakati nilifika kwa wazazi wangu, niliogopa sana kuanza kuzungumuzia ile jambo. Saa zikapita. Ku mwisho, kisha kusali sana, nikaelezea baba yangu mambo yote. Nilimuambia kama nilikuwa nimepata Mungu wa kweli na kama nitaacha dini ya Shinto juu nitumikie ule Mungu wa kweli. Baba yangu alikasirika na kuhuzunika. Watu wengine wa familia walikuya juu ya kujaribu kunichochea nibadilishe uamuzi wangu. Sikupenda kuumiza watu wa familia yangu, lakini pia, nilijua kama jambo ya muzuri ya kufanya ni kumutumikia Yehova. Kisha wakati fulani, watu wa familia yangu walifikia kuheshimia uamuzi wangu.

Hata kama niliacha kutumika ku hekalu, niliendelea kuwaza juu ya mambo yenye nilikuwaka nafanya kule juu ni mambo yenye ilikuwaka ya maana sana mu maisha yangu. Nilijikaza kusahau, lakini kila fasi kulikuwa tu mambo ya kunikumbusha maisha yangu ya zamani.

Kuko mambo mbili yenye ilinisaidia. Kwanza, nilitafuta mu nyumba yangu kila kitu yenye ilikuwa na uhusiano na dini yangu ya zamani. Kisha nikalunguza vile vitu vyote, sawa vile vitabu, picha, na hata vitu vya bei vyenye nilikuwaka nilishajikusanyia. Pili, nilijikaza kupitisha wakati mingi na Mashahidi wa Yehova. Juu walinihangaikia na kunitegemeza, ile linisaidia sana. Polepole, nikaacha kufikiria maisha yangu ya zamani.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Zamani sikukuwaka nahangaikia bibi yangu na watoto wangu, na ile ilikuwa nafanya wakose furaha. Lakini wakati nilianza kupitisha wakati pamoja nao, sawa vile Biblia inaambia bwana wafanye, tukakuwa marafiki sana. Kisha wakati fulani, bibi yangu naye alianza kumutumikia Yehova. Sasa miye na bibi yangu, mutoto wetu mwanaume, mutoto wetu mwanamuke na bwana yake, siye wote tuko namutumikia Yehova.

Wakati ninafikiria namna nilikuwaka napenda kumutumikia Mungu na kusaidia wengine, wakati nilikuwaka mutoto, ninaona kama nimepata jambo yenye nilikuwaka natafuta, na mambo ingine ya mingi. Sijue niseme nini juu ya kumushukuru Yehova.

“Nilijua Kama Kuko Kitu Yenye Nilikuwa Nakosa.”​—LYNETTE HOUGHTING

ALIZALIWA MWAKA WA: 1958

INCHI: AFRIKA KUSINI

ALIKUWA: MWENYE HUZUNI JUU WAZAZI WAKE WALIMUACHAKA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa Germiston, muji mudogo kwenye watu wanachimbulaka majiwe ya bei. Mu ile muji hamukukuwa wizi sana na mambo ya kuingiliana. Juu wazazi wangu waliona kama hawataweza kunihangaikia, waliamua kunipatia wazazi wengine, ili wanikomalishe. Siku 14 kisha kuzaliwa, nilipelekwa kwa wazazi wengine. Wao njo walikuwa sasa baba yangu na mama yangu. Lakini, wakati nilifikia kujua kama ni vile mambo ilikuwa, nilisikia sawa vile wazazi wangu waliniacha. Nilianza kuona kama siko mutoto wa wale wazazi wenye walinikomalisha, na niliona kama hawakukuwa nanielewa kabisa.

Wakati nilikuwa na miaka 16, nilianza kuenda fasi za kukunywia pombe. Kule, miye na marafiki wangu tulikuwa nacheza na kusikiliza muziki. Wakati nilikuwa na miaka 17, nilianza kuvuta tumbako. Nilipenda kuwa mwembamba sana, sawa watu wenye nilikuwa naona mu matangazo ya kuchochea watu kuvuta tumbako. Wakati nilikuwa na miaka 19, nilianza kutumika mu muji wa Johannesburg, na kule nilianza kupitisha wakati na marafiki wabaya. Bila kukawia nilianza kusema maneno machafu, kuvuta sana, na kukunywa sana kila mwisho wa juma.

Hata vile, nilikuwa nafanya mazoezi sana. Na mara mingi nilicheza michezo mbalimbali. Tena, nilikuwa natumika sana juu nijulikane mu mambo ya kutengeneza ordinatere. Kwa hiyo, nilipata makuta mingi, na watu wengi waliona kama niko na maisha ya muzuri. Lakini, sikukuwa na furaha na maisha yangu ilinichokesha. Nilikuwa najisikia sawa vile kuko kitu fulani yenye ninakosa.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Wakati nilianza kujifunza Biblia, nilijifunza kama Yehova ni Mungu mwenye upendo. Tena nilijifunza kama anaonyesha kuwa anatupenda kwa kutupatia Neno yake, Biblia. Biblia iko sawa vile barua yenye ametuandikia juu ya kutuongoza mu maisha. (Isaya 48:17, 18) Niliona kama, ikiwa ninapenda Yehova aniongoze mu maisha, ninapaswa kubadilisha mambo mingi mu maisha yangu.

Kwa mufano, nilipaswa kuachana na marafiki wabaya. Nilifikiria sana maneno yenye iko mu Mezali 13:20, yenye inasema hivi: “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, Lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.” Ile maneno ilinisaidia niache marafiki wangu wa zamani, na nitafute marafiki wa mupya kati ya Mashahidi wa Yehova.

Jambo ya nguvu kufanya ilikuwa kuacha kuvuta tumbako; nilikuwa nilishakuwa mutumwa wa tumbako. Wakati nilijikaza polepole kuacha kuvuta tumbako, nilipata tatizo ingine. Kuacha kuvuta tumbako kulifanya ninenepe. Niliongeza zaidi ya kilo 13.6! Ile ilifanya nijisikie mubaya sana, na ilinikamata miaka kumi juu nipunguze kilo. Lakini, nilijua kama kuacha kuvuta tumbako njo ilikuwa jambo ya muzuri ya kufanya. Niliendelea kusali kwa Yehova na alinipatia nguvu ya kuacha ile tabia.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Sasa niko na afya ya muzuri. Siwazake tena kama kazi, ao kutafuta makuta mingi njo kutaniletea furaha. Lakini, ninapata furaha wakati ninahubiria wengine mafundisho ya kweli ya Biblia. Kufanya vile kumesaidia wanamuke tatu wenye nilikuwaka natumika nao zamani waanze pia kumutumikia Yehova pamoja na miye na bwana yangu. Mbele wazazi wangu wenye walinikomalisha wakufe, nilipata nafasi ya kuambia kila mumoja wao kama Biblia inasema kuwa watu watafufuliwa na kuishi mu dunia paradiso.

Kumukaribia Yehova kumenisaidia nisiendelee kuhuzunika juu wazazi wangu waliniachaka. Sasa niko mu familia ya mu dunia yote ya Wakristo wenzangu. Mule, nimepata mama, baba, ndugu, na dada wengi.​—Marko 10:29, 30.

[Picha kwenye ukurasa wa 12]

Nimejionea upendo wa kweli kati ya Mashahidi wa Yehova

[Picha kwenye ukurasa wa 13]

Hekalu ya Shinto, kwenye nilikuwa naabudia zamani