Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mapendekezo ya Kufanya Ibada ya Familia na Funzo la Kibinafsi

Mapendekezo ya Kufanya Ibada ya Familia na Funzo la Kibinafsi

Mapendekezo ya Kufanya Ibada ya Familia na Funzo la Kibinafsi

MWANZONI mwa mwaka wa 2009, makutaniko ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote yalibadili programu yao ya mikutano. Mikutano miwili ya katikati ya juma iliunganishwa, na wote walitiwa moyo watumie jioni hiyo ya ziada kwa ajili ya ibada ya familia au funzo la kibinafsi. Je, umekuwa ukitumia vizuri mpango huo mpya? Je, unafaidika kikamili na mpango huo?

Wengine hawajui wachague habari gani ya kujifunza wakati wa ibada ya familia. Baraza Linaloongoza halina nia ya kuchagua utaratibu mmoja wa kufuatwa na familia zote. Kwa kuwa hali zinatofautiana, inafaa kila kichwa cha familia au kila mtu aamue njia nzuri zaidi ya kutumia nafasi hiyo ya kila juma

Watu fulani wamekuwa wakitayarisha mikutano ya kutaniko, lakini si lazima ibada ya familia itumiwe kwa kusudi hilo tu. Wengine wamekuwa wakisoma, kuzungumzia, na hata kufanya drama zinazotegemea habari za Kimaandiko, hasa kwa faida ya watoto wadogo. Si lazima au hata haifurahishi kutumia sikuzote njia ya maswali na majibu, ambayo inatumiwa katika mikutano ya kutaniko. Mara nyingi watu wanafurahia zaidi kuzungumzia mawazo mbalimbali katika hali zenye kustarehesha. Hali kama hizo zinawachochea watu kutoa mawazo yenye kusisimua, ambayo yanaweza kufanya pindi hiyo iwafurahishe wote na kukumbukwa kwa muda mrefu.

Baba mmoja mwenye watoto watatu anaandika hivi: “Ibada yetu imetegemea hasa usomaji wa Biblia. Kila mmoja anasoma sura hizo mapema, watoto wanachagua habari fulani ya kufanyia utafiti, kisha wanaeleza mambo waliyopata. Mara nyingi Michael [mwenye umri wa miaka saba] anachora picha au kuandika fungu moja. Huenda David na Kaitlyn [wenye umri wa miaka 13 na 15] wakaandika kuhusu simulizi la Biblia wakiwa kama watazamaji. Kwa mfano, tuliposoma kuhusu jinsi Yosefu alivyofasiri ndoto ya mnyweshaji na mwokaji wa mikate wa Farao, Kaitlyn aliandika simulizi hilo akiwa kama mfungwa anayetazama mambo hayo yakitukia.”—Mwa., sura ya 40.

Kwa kawaida hali zinatofautiana. Jambo linalomfaa mtu mmoja au familia moja huenda lisifae mtu au familia nyingine. Sanduku linalofuata lina mapendekezo ambayo mnaweza kutumia wakati wa ibada yenu ya familia au funzo lako la kibinafsi. Inaelekea sana kwamba mnaweza kufikiria mapendekezo mengine mengi.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 6, 7]

Kwa familia zenye matineja:

• Someni na mzungumzie kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.

• Fanyeni mazoezi mkitumia sehemu yenye kichwa “Namna gani ikiwa . . . ?” (Ona Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1996 (15/5/1996), ukurasa wa 14, fungu la 17-18.)

• Zungumzeni kuhusu miradi ya muda mrefu na ya muda mfupi.

• Mara kwa mara, tazameni na kuzungumzia video inayotegemea Biblia.

• Jifunzeni sehemu za Mnara wa Mlinzi zenye kichwa “Kwa Ajili ya Vijana.”

Kwa wenzi wa ndoa ambao hawana watoto:

• Zungumzieni fy sura ya 1, 3, 11-16 ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia.

• Zungumzieni mambo mliyopata mlipofanya utafiti kuhusu usomaji wa Biblia.

• Tayarisheni Funzo la Biblia la Kutaniko au Funzo la Mnara wa Mlinzi.

• Zungumzieni njia za kupanua huduma yenu mkiwa wenzi wa ndoa.

Kwa ndugu na dada waseja au Wakristo walio katika familia zilizogawanyika kidini:

• Jifunzeni vichapo vipya ambavyo tulipokea katika makusanyiko ya wilaya.

• Someni Vitabu vya Mwaka vya hivi karibuni na vya zamani.

• Fanyeni utafiti kuhusu maswali au maulizo ambayo ni ya kawaida katika eneo lenu.

• Tayarisheni njia za kuanzisha mazungumzo katika huduma ya shambani.

Kwa familia zenye watoto wadogo:

• Fanyeni drama za masimulizi ya Biblia.

• Chezeni michezo ya kukumbuka mambo, kama ile iliyo kwenye ukurasa wa 30 na 31 wa Amkeni!

• Mara kwa mara, fanyeni mambo yenye kupendeza. (Ona “Kujifunza Biblia—Katika Hifadhi ya Wanyama!” katika gazeti Amkeni! la Machi 8, 1996 (8/3/1996), ukurasa wa 16-19.)

• Jifunzeni sehemu za Mnara wa Mlinzi zenye kichwa “Wafundishe Watoto Wako.”