Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ni lazima tu tulipe kodi?”

“Ni lazima tu tulipe kodi?”

“Ni lazima tu tulipe kodi?”

WATU wengi hawapendake kulipa kodi. Wanawazaka kama makuta yenye wanalipa haitumiwake muzuri. Wakaaji wa muji fulani wa mashariki ya kati walisema hivi wakati walikuwa nafasiria juu ya nini wanakatala kulipa kodi: “Hatutapatia serikali makuta ya kuuza masasi yenye itatumiwa kuua watoto wetu.’’

Watu wengi wako na ile mawazo. Wanakatala kulipa kodi juu hawapendi makuta yao itumiwe mubaya. Mohandas K. Ghandi, mwenye alikuwa kiongozi wa Wahindu, alisemaka hivi ili kufasiria juu ya nini zamiri yake haikumuruhusu kulipa kodi: “Kila mutu mwenye anategemeza serikali yenye kuwa na maaskari ikuwe kwa njia ya moja kwa moja ao hapana, anafanya zambi. Kila mutu, akuwe kijana ao muzee, anafanya ile zambi kwa kulipa serikali kodi.”

Vilevile filozofe Henry David Thoreau, mwenye aliishi mu miaka ya 1900, alikatala kulipa kodi juu ile makuta inatumiwaka juu ya kutegemeza vita. Aliona kama haiko muzuri wakubwa wa serikali wakaze watu wategemeze jambo fulani yenye wanawaza kama haiko muzuri. Alionyesha kama kila mutu anapaswa kutumia zamiri yake juu ya kuamua.

Hii jambo inahusu Wakristo juu Biblia inasema kama wanapaswa kuwa na zamiri safi mu mambo yote. (2 Timoteo 1:3) Lakini, Biblia inasema tena kama serikali iko na haki ya kulipisha kodi. Inasema hivi: “Kila mutu ajitiishe kwa mamlaka zenye kuwa kubwa, kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa ruhusa ya Mungu; mamlaka zenye ziko zimewekwa [serikali za wanadamu] na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri. Kwa hiyo kuko sababu ya lazima kwenu kujitiisha, haiko kwa sababu ya ile kasirani kali tu, lakini pia kwa sababu ya zamiri yenu. Ndiyo sababu munalipa kodi pia; kwa maana wao ni watumishi wa Mungu kwa watu wote, na wanatumika bila kuacha kwa kusudi hili. Mupatie wote haki zao: ule mwenye anataka kodi, kodi.”​—Waroma 13:1, 5-7.

Njo maana Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa nalipa kodi hata kama sehemu kubwa ya makuta yenye walikuwa nalipa ilikuwa natumiwa juu ya kutegemeza jeshi. Mashahidi wa Yehova wanalipaka pia kodi. * Juu ya nini wanalipaka kodi hata kama wanajua kuwa kiasi fulani ya makuta yenye watalipa itatumiwa mu mambo yenye haipatane na Maandiko? Mukristo anapaswa kukatala kusikiliza zamiri yake wakati anaombwa kulipa kodi?

Ili Kuwa na Zamiri Safi Tunapaswa Kulipa Kodi

Kwa kweli, wakati wa mitume, makuta mingi yenye watu walilipa kodi ilitumiwa juu ya kutegemeza jeshi. Ni ileile sababu njo ilifanya Gandhi na Thoreau, wenye tulishataya, wakatale kulipa kodi.

Wakristo walitii amri yenye kuwa mu Waroma sura ya 13 haiko tu juu waliogopa azabu lakini pia ‘kwa sababu ya zamiri yao.’ (Waroma 13:5) Kwa hiyo, hata kama Mukristo hafurahie namna makuta ya kodi inatumiwa, anapaswa tu kulipa kodi juu akuwe na zamiri safi. Juu ya kuelewa ile jambo, tunapaswa kujua namna zamiri inatumikaka. Zamiri iko sawa vile sauti ya ndani yenye inatuambia ikiwa jambo fulani ni ya muzuri ao ni ya mubaya.

Kila mutu iko na ile sauti ya ndani sawa vile Thoreau alionyeshaka. Lakini wakati fulani inaweza kutudanganya. Juu tumupendeze Mungu, tunapaswa kuzoeza zamiri yetu ili ipatane na kanuni zake. Sababu gani? Kwa sababu mawazo ya Mungu iko juu sana kupita mawazo yetu. Mara kwa mara tunapaswa kubadilisha mawazo yetu juu ipatane na mawazo yake. (Zaburi 19:7) Njo maana tunapaswa kujikaza kuelewa mawazo ya Mungu kuhusu serikali za wanadamu. Anazionaka namna gani?

Mutume Paulo aliita serikali za wanadamu kuwa “watumishi wa Mungu kwa watu wote.” (Waroma 13:6) Alipenda kusema nini? Ni kusema, ziko na daraka ya kuleta utaratibu na kufanyia watu mambo fulani ya muzuri. Hata serikali yenye kuongoza mubaya sana inasaidiaka kufanya mambo mbalimbali sawa vile kutuma barua, kushugulikia mambo ya masomo, kuzimisha moto, na kuhakikisha kama watu wanatii sheria za inchi. Mungu anajua mambo ya mubaya yenye viongozi wa serikali za wanadamu wanafanyaka. Lakini, anawaacha waendelee kutawala. Anatuambia tulipe kodi juu ya kuonyesha kama tunamuheshimia yeye mwenye anaruhusu zile serikali za wanadamu ziendelee kutawala.

Lakini hataziruhusu ziendelee kutawala milele. Atatosha serikali zote za wanadamu na kuleta Ufalme wake. Na ule Ufalme utatosha mambo yote ya mubaya yenye serikali za wanadamu zimeletea watu kwa miaka mingi. (Danieli 2:44; Matayo 6:10) Lakini, wakati Wakristo wako nangoya Mungu afanye vile, wanapaswa kuendelea kutii wenye mamlaka kwa kulipa kodi na kufanya mambo ingine yenye wanawaomba.

Sasa, ufanye nini kama uko na mawazo sawa ya Gandhi, mwenye alikuwa nawaza kama ni zambi kulipa kodi juu ile makuta inatumiwaka mu mambo ya vita? Tukumbuke kama mawazo ya Mungu iko juu sana kupita mawazo yetu na anajua mambo mingi sana kutupita. Kwa hiyo, siye njo tunapaswa kubadilisha mawazo yetu. Kupitia nabii Isaya, Mungu alisema hivi: “Kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia, Ni vile njia zangu ziko juu kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.”​—Isaya 55:8, 9.

Serikali Ziko na Mamlaka Yote?

Wakati Biblia inasema kama tunapaswa kulipa kodi, haimaanishe kama tunapaswa kufanya mambo yote yenye serikali za wanadamu zinatuomba. Yesu alifundisha kama Mungu amepatia serikali za wanadamu mamlaka, lakini ile mamlaka iko na mipaka. Wakati mutu fulani aliuliza Yesu ikiwa ni sawa kulipa kodi yenye Waroma walikuwa nalomba, Yesu alijibia hivi: “Mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”​—Marko 12:13-​17.

“Kaisari,” ni kusema serikali, zinatengenezaka makuta na kuamua samani ya ile makuta. Kwa hiyo, kulingana na mawazo ya Mungu, serikali ziko na haki ya kutuomba tuwarudishie ile makuta kwa kulipa kodi. Lakini Yesu alionyesha kama hakuna serikali yenye tunapaswa kupatia “vitu vya Mungu,” ni kusema uzima wetu na ibada yetu. Wakati sheria za wanadamu zinatuomba tufanye mambo yenye sheria ya Mungu inakataza, siye Wakristo “tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.”​—Matendo 5:29.

Pengine Wakristo leo hawafurahie namna makuta yenye wanalipa kodi inatumiwa, lakini hawajaribu kupinga serikali ao kukatala kulipa kodi. Wakifanya vile, wataonyesha kama hawaamini kuwa Mungu tu njo atamaliza magumu ya wanadamu. Wanangoya kwa hamu wakati wenye Mungu atamaliza magumu yetu yote kupitia utawala wa Mwana wake Yesu, mwenye alisemaka hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.”​—Yohana 18:36.

Utapata Faida Kama Unafuata Mambo Yenye Biblia Inasema

Kuko faida mingi zenye utapata ikiwa unafuata mambo yenye Biblia inasema kuhusu kulipa kodi. Utaepuka azabu yenye wale wenye wanavunjaka sheria wanapewaka na hautakuwa na wasiwasi kuwa watakukamata. (Waroma 13:3-5) Zaidi ya ile, utaendelea kuwa na zamiri safi, na mwenendo wako wa kutii sheria utamutukuza Mungu. Hata kama unaweza kuwa na makuta kidogo kuliko wale wenye wanakatalaka kulipa kodi ao wenye wanasemaka uongo juu walipe kodi kidogo, ukuwe hakika kama Yehova atakuhangaikia. Daudi, mwandikaji fulani wa Biblia, alisemaka hivi: “Nilikuwa kijana na sasa nimezeeka, Lakini sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa, wala watoto wake wakitafuta mukate.”​—Zaburi 37:25.

Na tena, kuelewa amri ya Mungu yenye inatuomba kulipa kodi kutafanya ukuwe na amani ya akili. Tuseme unalipiaka nyumba, na mwenye-nyumba anazoea kutumia makuta yenye unalipa juu ya kufanya mambo ya mubaya. Weye njo serikali itafunga? Hapana. Vilevile, kama serikali inatumia mubaya kodi yenye unalipa, mbele ya Mungu hauna kosa. Fikiria mufano wa Stelvio mwenye alikuwa naishi kusini mwa Ulaya. Mbele ajifunze Biblia, alikuwa napenda kuleta mabadiliko mu inchi yake. Wakati alifasiria juu ya nini aliacha kutafuta kuleta mabadiliko, alisema hivi: “Nililazimika kukubali kama mwanadamu hawezi kuleta haki, amani na kusaidia watu wapendane mu dunia. Ni Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kuleta ile mambo na kuletea watu maisha ya muzuri.”

Kama Stelvio, na weye unaweza kuwa hakika kama Mungu atamaliza ukosefu wa haki ikiwa unaendelea kumulipa Mungu vitu vya Mungu. Utajionea wakati Mungu ataleta utawala wa haki mu dunia yote, na kutosha mambo ya mubaya na ukosefu wa haki wenye utawala wa wanadamau umeleta.

[Maelezo ya chini]

^ Juu ya kupata ushuhuda wenye kuonyesha kama Mashahidi wa Yehova wanalipaka kodi, ona Munara wa Mulinzi wa 1 Mwezi wa 11, 2002, ukurasa wa 13, fungu ya 15, na wa 1 Mwezi wa 5, 1996, ukurasa wa 17, fungu ya 7.

[Wazo ya fungu kwenye ukurasa 22]

Tunapaswa kubadilisha mawazo yetu juu ipatane na mawazo ya Mungu kwa sababu mawazo yake iko juu sana kupita mawazo yetu

[Wazo ya fungu kwenye ukurasa 23]

Wakati Wakristo wanalipa kodi, wanaendelea kuwa na zamiri safi mbele ya Mungu na wanaonyesha kuwa wako hakika kama Mungu atawasaidia kupata mambo yenye wako nayo lazima

[Picha kwenye ukurasa wa 22]

“Mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu”

[Kwenye Picha Ilitoka]

Copyright British Museum