Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wewe Umedanganywa?

Je, Wewe Umedanganywa?

Je, Wewe Umedanganywa?

NI MAMBO machache yanayoumiza zaidi kuliko kujua kwamba mtu fulani unayemwamini amekudanganya. Unaweza kukasirika, kuhisi umedharauliwa au hata kusalitiwa. Udanganyifu unavunja urafiki na ndoa; na unafanya watu wapoteze mamilioni ya pesa.

Basi, wazia jinsi ambavyo ungehisi kama ungejua kwamba umedanganywa kumhusu Mungu. Ikiwa unamwogopa Mungu, matokeo yanaweza kuwa mabaya kama ilivyokuwa kwa watu wafuatao ambao walikuwa wafuasi wa dini:

● “Nilihisi kwamba nimesalitiwa na kanisa.”—DEANNE.

● “Nilikasirika. Nilihisi kuwa nimedanganywa, yaani, nilihisi kuwa matumaini na malengo yangu hayana maana yoyote.”—LUIS.

Huenda hata usiwazie kwamba inawezekana kuwa umedanganywa kumhusu Mungu. Yaelekea mambo unayojua kumhusu uliyasikia kutoka kwa mtu unayemwamini na ambaye hawezi kamwe kukuumiza kimakusudi, kama vile mzazi wako, kasisi, pasta, au rafiki wa karibu. Huenda umeamini fundisho fulani katika maisha yako yote. Lakini je, hukubali kwamba fundisho fulani linaweza kuwa la uwongo ingawa watu wengi wanaliamini? Aliyekuwa rais wa Marekani, Franklin D. Roosevelt alitambua jambo hilo, kwa kuwa alisema: “Kurudia-rudia uwongo hakuufanyi kuwa ukweli.”

Unaweza kujua jinsi gani kwamba umedanganywa? Wakati mmoja Yesu alisali hivi kwa Mungu: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Ndiyo, Neno la Mungu, Biblia, linatusaidia kutofautisha ukweli na uwongo.

Acha tuone mafundisho matano ya uwongo kumhusu Mungu ambayo Biblia inafunua. Utaona jinsi ukweli unavyoweza kubadili maisha yako yawe bora.