Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1 Mungu Ni Fumbo—Je, Ni Kweli?

1 Mungu Ni Fumbo—Je, Ni Kweli?

1 Mungu Ni Fumbo​—Je, Ni Kweli?

Jambo ambalo huenda umesikia: “Mungu hufanya kazi kwa njia za mafumbo, au zisizoeleweka.”

“Baba haeleweki, Mwana haeleweki, na Roho Mtakatifu Haeleweki.”—Fundisho la Athanasia linalofafanua Utatu ambao unafundishwa na dini nyingi zinazodai kuwa za Kikristo.

Biblia inafundisha nini?: Yesu alisema kwamba wale ‘wanaopata ujuzi juu ya Mungu wa pekee wa kweli,’ watapata baraka. (Yohana 17:3) Lakini tunaweza kupata ujuzi juu ya Mungu jinsi gani ikiwa yeye ni fumbo, au haeleweki? Badala ya kuficha ukweli kujihusu, Mungu anataka kila mtu amjue.—Yeremia 31:34.

Ni kweli kwamba hatuwezi kujua kila kitu kumhusu Mungu. Hiyo ni kwa sababu mawazo na njia zake ziko juu kuliko zetu.—Mhubiri 3:11; Isaya 55:8, 9.

Jinsi kujua ukweli kunavyokusaidia: Ikiwa Mungu ni fumbo, basi kuna sababu gani ya kujaribu kumjua? Mungu anatuwezesha kumjua na pia kuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye. Alimrejelea Abrahamu, mwanamume mwaminifu, kuwa ‘rafiki yake,’ naye Mfalme Daudi wa Israeli akaandika: “Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa.”—Isaya 41:8; Zaburi 25:14.

Je, kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Mungu ni jambo lisilowezekana? Labda inaonekana hivyo, lakini ona andiko la Matendo 17:27 linavyosema: “[Mungu] hayuko mbali na kila mmoja wetu.” Kwa njia gani? Kupitia Biblia, Mungu anaandaa habari tunazohitaji ili tumjue vizuri. *

Anatuambia jina lake ni Yehova. (Isaya 42:8) Anatueleza katika Biblia jinsi ambavyo ameshughulika na wanadamu ili tuweze kujua yeye ni Mungu wa aina gani. Zaidi ya hayo, Mungu anatufunulia hisia zake. Yeye ni “mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo na kweli.” (Kutoka 34:6) Matendo yetu yanaweza kumfurahisha au kumhuzunisha. Kwa mfano, Waisraeli wa kale ‘walimhuzunisha’ walipomwasi, lakini wale ambao kwa hekima wanamtii, wanafanya ashangilie.—Zaburi 78:40; Methali 27:11.

[Maelezo ya Chini]

^ Kwa habari zaidi kuhusu yale ambayo Biblia inasema kumhusu Mungu, ona sura ya 1 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 4]

Kama Mungu angekuwa Utatu usioeleweka, tungemjua jinsi gani?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 4]

The Trinity c.1500, Flemish School, (16th century)/​H. Shickman Gallery, New York, USA/​The Bridgeman Art Library International