Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

5 Mungu Anakubali Ibada Yoyote Ile Ikiwa Tu Inatoka Moyoni—Je, Ni Kweli?

5 Mungu Anakubali Ibada Yoyote Ile Ikiwa Tu Inatoka Moyoni—Je, Ni Kweli?

5 Mungu Anakubali Ibada Yoyote Ile Ikiwa Tu Inatoka Moyoni​—Je, Ni Kweli?

Jambo ambalo huenda umesikia: “Kama vile tu kulivyo na njia na barabara nyingi za kwenda mahali fulani, ndivyo pia kulivyo na njia nyingi za kumfikia Mungu. Kila mtu anapaswa kutafuta njia yake mwenyewe ya kumfikia Mungu.”

Biblia inafundisha nini?: Ni lazima tumwabudu Mungu kwa unyofu wa moyo, bila unafiki. Yesu aliwaambia viongozi wa kidini wa siku zake sababu iliyofanya Mungu awakatae: “Isaya kwa kufaa alitoa unabii juu yenu wanafiki, kama ilivyoandikwa, ‘Watu hawa huniheshimu mimi kwa midomo yao, bali mioyo yao iko mbali nami.’” (Marko 7:6) Hata hivyo, unyofu wa moyo peke yake si uhakikisho wa kwamba Mungu atakubali ibada yetu.

Yesu alionyesha jambo hilo waziwazi kwa kufunua kasoro kubwa katika ibada iliyotolewa na viongozi hao wa kidini na wafuasi wao. Alitumia maneno haya ya Mungu kuwahusu: “Wao huniabudu bure, kwa sababu wao hufundisha amri za wanadamu kuwa mafundisho.” (Marko 7:7) Ibada yao ilikuwa ya “bure,” au isiyo na maana yoyote, kwa sababu badala ya kutanguliza matakwa ya Mungu walitanguliza mapokeo yao ya kidini.

Biblia haiungi mkono wazo la kwamba kuna njia nyingi zinazokubalika za kumfikia Mungu, badala yake, inafundisha kwamba kuna njia moja tu. Andiko la Mathayo 7:13, 14 linasema: “Ingieni kupitia lango jembamba; kwa sababu barabara inayoongoza kwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanaoipitia; lakini lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.”

Jinsi kujua ukweli kunavyokusaidia: Wazia jinsi ambavyo ungehisi kama ungefanya mazoezi kwa miezi kadhaa, kisha ushiriki katika mbio za masafa marefu na kushinda, lakini kwa sababu ya kuvunja sheria fulani bila kujua, unapokonywa taji lako. Ungehisi kwamba jitihada zako zote zilikuwa za bure. Je, inaweza kuwa hivyo kuhusiana na ibada yetu kwa Mungu?

Akilinganisha ibada yetu na mashindano ya mbio, mtume Paulo aliandika: “Kama yeyote akishindana hata katika michezo, havikwi taji isipokuwa awe ameshindana kulingana na sheria.” (2 Timotheo 2:5) Tunapata kibali cha Mungu kwa kumwabudu “kulingana na sheria,” yaani, katika njia ambayo yeye anakubali. Hatuwezi kujichagulia njia yetu wenyewe ya kumfikia Mungu kama vile tu mkimbiaji asivyoweza kukimbia jinsi anavyotaka na atazamie kutangazwa mshindi.

Ili kumfurahisha Mungu, ni lazima tuepuke kuchanganya ibada yetu na mafundisho ya uwongo kumhusu. Yesu alisema: “Waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli.” (Yohana 4:23) Tunajifunza kuhusu njia ya kweli ya kumfikia Mungu katika Neno lake Biblia.—Yohana 17:17. *

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 8 Kwa habari zaidi kuhusu ibada ambayo Mungu anakubali, ona sura ya 15 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

[Blabu katika ukurasa wa 8]

Je, dini zote zinawafundisha watu wamwabudu Mungu kwa njia ambayo yeye anakubali?