Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unajifurahishaka na mambo yenye inafaa?

Unajifurahishaka na mambo yenye inafaa?

Unajifurahishaka na mambo yenye inafaa?

“Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.”​—EFE. 5:10.

1, 2. (a) Biblia inasema nini yenye inaonyesha kama Yehova anapenda tufurahie maisha? (b) Kuona mambo ya kujifurahisha kuwa “zawadi ya Mungu” kutatuchochea kufanya nini?

 MU Biblia muko maandiko mingi yenye inaonyesha kama Yehova hapendi tu tuishi, lakini anapenda pia tufurahie maisha. Kwa mufano, Zaburi 104:14, 15 inasema kama Yehova ‘anakomalisha chakula juu ya udongo, na divai yenye inafanya moyo wa mwanadamu ufurahi, mafuta yenye inafanya uso ungae, na mukate wenye unategemeza moyo wa mwanadamu mwenye anaweza kufa.’ Kwa kweli, Yehova anafanyaka mimea yote itoe nafaka, mafuta, na divai juu tupate mambo ya lazima ya kutusaidia kuendelea kuishi. Lakini anatupatia pia divai yenye inafanya ‘moyo ufurahi.’ Divai haiko ya lazima juu tuendelee kuishi, lakini inafanya tufurahie maisha zaidi. (Muh. 9:7; 10:19) Kwa kweli, Yehova anapenda tukuwe na furaha, na mioyo yetu iyale “furaha.”​—Mdo 14:16, 17.

2 Kwa hiyo, hatupaswe kuona kama ni kosa kutia pembeni wakati fulani juu ya ‘kuangalia kwa uangalifu ndege wa mbinguni’ na “maua ya mayungiyungi ya shamba” ao kufanya mambo ingine ya kujifurahisha yenye itafanya tupumuzike na tufurahie maisha. (Mt. 6:26, 28; Zb. 8:3, 4) Maisha ya muzuri ni “zawadi ya Mungu.” (Muh. 3:12, 13) Kuona mambo ya kujifurahisha kuwa sehemu ya ile zawadi, kutatuchochea tujifurahishe mu njia yenye itamupendeza Mungu mwenye alitupatia ile zawadi. *

Chagua kwa Hekima Mambo ya Kujifurahisha

3. Juu ya nini tukubali kama hatuwezi kufurahia mambo ileile ya kujifurahisha?

3 Watu wenye wako na mawazo yenye kusawazika juu ya kujifurahisha, wanajifurahishaka na mambo mbalimbali, lakini wanajua kama wanapaswa kujitilia mipaka fulani. Juu ya nini? Juu ya kujibia ile ulizo, tulinganishe mambo ya kujifurahisha na chakula. Chakula yenye watu wanapendaka mu eneo fulani inaweza kuwa tofauti na chakula yenye watu wanapendaka mu eneo ingine. Na hata chakula yenye watu wa mu eneo fulani wanapenda sana, pengine watu wa mu eneo ingine hawaipendake hata kidogo. Vilevile, mambo ya kujifurahisha yenye Wakristo wa mu eneo fulani wanaweza kufurahia, pengine Wakristo wa mu eneo ingine hawataifurahia. Na hata Wakristo wenye kuishi mu eneo ileile hawafurahiake mambo ileile ya kujifurahisha. Kwa mufano, Mukristo fulani anaweza kuona kama kusoma kitabu ni jambo ya kufurahisha, lakini mwingine anaweza kuona kama kufanya vile kunaleta uvivu. Mwingine anaweza kuona kama kutembeza kinga na iko anaangalia uumbaji ni jambo ya kufurahisha, lakini mwingine anaweza kuona kama ni jambo ya kuchokesha. Lakini tunakubali kama sawa tu vile chakula, mambo ya kujifurahisha ni ya mingi na kila mutu iko na yenye anafurahiaka.

4. Juu ya nini tunapaswa kujitilia mipaka kuhusu mambo ya kujifurahisha yenye tunachagua? Leta mufano.

4 Hata kama kuko mambo mingi ya kujifurahisha, ile haimaanishe kama tunapaswa tu kujiachilia. Tufikirie tena mufano wa chakula. Hata kama tunaweza penda kula chakula ya aina mbalimbali, hatuwezi kula chakula ya kuoza kimakusudi. Kufanya vile itakuwa kukosa akili na kunaweza kuharibisha afya yetu. Vilevile, hata kama tunaweza kupenda kujifurahisha na mambo mbalimbali ya muzuri, tutaepuka kujifurahisha na mambo yenye inaweza kutia uzima wetu mu hatari, mambo ya jeuri ao ya uasherati. Kama tunajifurahisha na ile mambo, tutakuwa tunavunja kanuni za Biblia na kutia mu hatari afya yetu na urafiki wetu pamoja na Mungu. Juu tusivuke mipaka, ni muzuri tujiulize mbele ya wakati ikiwa mambo yetu ya kujifurahisha inafaa ao hapana. (Efe. 5:10) Tunaweza kufanya vile namna gani?—Ro. 14:2-4.

5. Nini njo itatusaidia kujua kama mambo ya kujifurahisha yenye tunapendaka inaheshimia kanuni za Mungu?

5 Juu mambo ya kujifurahisha ituletea faida na imufurahishe Yehova, inapaswa kuheshimia kanuni fulani zenye zinaonyeshwa mu Biblia. (Zb. 86:11) Juu ya kujua kama mambo ya kujifurahisha yenye unapendaka inaheshimia zile kanuni, kuko maulizo tatu yenye unapaswa kujiuliza: Ninajifurahishaka na nini? Ninatumiaka muda gani? Na ninajifurahishaka na nani? Tuzungumuzie basi kila ulizo.

Ninajifurahishaka na Nini?

6. Tunapaswa kuepuka mambo gani ya kujifurahisha, na juu ya nini?

6 Mbele ya kuchagua mambo ya kujifurahisha, ulizo ya kwanza ya kujiuliza ni hii: ‘Ninapendaka kujifurahisha na nini?’ Wakati utakuwa natafuta jibu ya ile ulizo ni muzuri ukumbuke kama kuko aina mbili ya mambo ya kujifurahisha. Aina ya kwanza ni yenye tunapaswa kuepuka kabisa, na aina ya pili ni yenye tunapaswa kutumia zamiri yetu ili kuamua. Mu hii dunia yenye kuharibika, watu wengi wanajifurahishaka na mambo yenye inapingana kabisa na kanuni za Biblia, ao yenye inavunja sheria za Mungu. (1 Yo. 5:19) Wakristo wanakatala kabisa kujifurahisha na mambo ya vile. Kwa mufano, wanaepuka mambo ya kujifurahisha yenye inaonyesha matendo ya bila huruma, mambo ya mashetani, ngono kati ya wanaume na wanaume na ngono kati ya wanamuke na wanamuke, pornografia, jeuri, na mambo ya kujifurahisha yenye inatukuza matendo ingine ya uasherati. (1 Ko. 6:9, 10; soma Ufunuo 21:8.) Wakati tunakatala kujifurahisha na mambo ya vile, hata tukuwe wapi, tunaonyesha Yehova kama ‘tunachukia sana mambo maovu.’​—Ro. 12:9; 1 Yo. 1:5, 6.

7, 8. Namna gani tunaweza kujua ikiwa mambo fulani ya kujifurahisha inafaa? Leta mufano.

7 Aina ya pili ya mambo ya kujifurahisha ni yenye haipingane na mambo yenye Biblia inasema. Mbele ya kujifurahisha na mambo ya vile, tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu kanuni za Biblia juu ya kuona ikiwa ile mambo inapatana na mawazo ya Yehova. (Mez. 4:10, 11) Kisha kila mutu anapaswa kukamata uamuzi wenye utafanya aendelee kuwa na zamiri yenye kuwa safi. (Gal. 6:5; 1 Ti. 1:19) Tunaweza kufanya vile namna gani? Mbele ya kula chakula yenye hatuyakulaka, tunaulizaka kwanza ikiwa ile chakula ilipikwa na nini. Vilevile, mbele ya kujifurahisha na mambo fulani, tunapaswa kwanza kujiuliza ikiwa ile mambo ya kujifurahisha inafanyizwa na nini.​—Efe. 5:17.

8 Kwa mufano, pengine unapendaka michezo, na ile inaeleweka. Michezo mingi inaweza kufurahisha na kuchangamusha. Sasa halafu kama unavutiwa na michezo fulani yenye inafanyaka wachezaji waumie sana, yenye inachochea sana watu wakuwe na roho ya kushindana, wajitie mu hatari, washangilie kwa fujo sana, wapende sana inchi yao, ao yenye kuwa na mambo ingine ya vile? Kisha kuchunguza ile mambo, pengine utafikia kuamua kama ile mambo ya kujifurahisha haipatane na mawazo ya Yehova na haipatane na ujumbe wa amani na upendo wenye tunahubiriaka wengine. (Isa. 61:1; Gal. 5:19-21) Lakini, kama mambo ya kujifurahisha inapatana na mawazo ya Yehova, inaweza kukuletea faida na kufanya ujisikie muzuri.​—Gal. 5:22, 23; soma Wafilipi 4:8.

Ninatumia Muda Gani?

9. Namna tunajibia ulizo, ‘Nitajifurahisha kwa muda gani? inaonyesha nini?’

9 Ulizo ya pili ya kujiuliza ni hii: ‘Nitatumia muda gani mu mambo ya kujifurahisha?’ Namna tunajibia ulizo, ‘Nitajifurahisha na nini?’ inaonyesha mambo yenye tunaona kuwa inafaa na yenye tunaona kuwa haifae. Lakini, namna tunajibia ulizo, ‘Nitajifurahisha kwa muda gani?’ inaonyesha mambo yenye tunatia pa nafasi ya kwanza, ni kusema, mambo yenye tunaona kuwa ya maana na yenye tunaona kuwa haiko ya maana. Sasa nini itatusaidia kujua ikiwa tunatia mambo ya kujifurahisha fasi yake?

10, 11. Namna gani maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 6:33 inatusaidia kuamua muda wenye tutapitisha mu mambo ya kujifurahisha?

10 Yesu Kristo aliambia wanafunzi wake hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Mk. 12:30) Kwa hiyo, jambo ya kwanza mu maisha yetu ni kumupenda Yehova. Tunaonyesha kama kumupenda Yehova njo jambo ya maana zaidi mu maisha yetu wakati tunafuata hii shauri ya Yesu: “Basi, muendelee kutafuta kwanza Ufalme na haki yake, na mutaongezewa vitu hivyo vingine vyote.” (Mt. 6:33) Namna gani ile andiko inaweza kutusaidia kuamua muda wenye tutatumia mu mambo ya kujifurahisha na fasi yenye tutapatia mambo ya kujifurahisha mu maisha yetu?

11 Kama unaangalia muzuri, utaona kama Yesu alituambia, ‘muendelee kutafuta kwanza Ufalme.’ Hakutuambia, ‘tuendelee kutafuta Ufalme tu.’ Yesu alijua kama zaidi ya kutafuta Ufalme, kuko mambo ingine yenye tuko nayo lazima. Tuko na lazima ya fasi ya kuishi, chakula, manguo, tuko na lazima ya kusoma masomo, tuko na lazima ya kazi, tuko na lazima ya kujifurahisha, na mambo ingine. Lakini kati ya mambo yote yenye tunaweza kutafuta, Ufalme wa Mungu njo tunapaswa kutafuta kwanza. Kwa hiyo, kufanya ile mambo ingine yote, hakupaswe kutufanya tukose wakati ya kufanya jambo ya maana zaidi, ni kusema, kumutumikia Yehova. (1 Ko. 7:29-31) Mambo ya kujifurahisha itatuletea faida kama tu tunatia Ufalme pa nafasi ya kwanza.

12. Kanuni yenye kuwa mu Luka 14:28, inaweza kutumiwa namna gani mu mambo ya kujifurahisha?

12 Kwa hiyo, tunapaswa kuhesabia garama, ni kusema, kuamua mbele ya wakati ni muda gani njo itaomba kupitisha mu mambo fulani ya kujifurahisha. (Lu. 14:28) Tunapaswa kuamua muda wenye mambo fulani ya kujifurahisha itatubeba. Kisha tunapaswa kujiuliza ikiwa ni lazima kabisa tutumie ile wakati yote mu mambo ya kujifurahisha. Ikiwa mambo fulani ya kujifurahisha itafanya tukose wakati ya kufanya mambo ya lazima, sawa vile, funzo ya pekee, ibada ya familia, kuhuzuria mikutano ao kuhubiri, ni kusema haiko lazima tuifanye. (Mk. 8:36) Lakini kama mambo fulani ya kujifurahisha inatupaitia nguvu ya kuendelea kufanya mambo ya kiroho, tunaweza kusema kama wakati yenye tulipitisha mu ile mambo ya kujifurahisha iko na faida.

Ninajifurahishaka na Nani?

13. Juu ya nini tunapaswa kuchagua kwa uangalifu watu wenye tutajifurahisha nao?

13 Ulizo ya tatu ya kujiuliza ni hii: ‘Ninapendaka kujifurahisha na nani?’ Ni jambo ya maana kujiuliza ile ulizo. Juu ya nini? Juu watu wenye tunajifurahishaka nao wanaweza kutuchochea tujifurahishe na mambo ya muzuri ao ya mubaya. Sawa vile tunafurahiaka zaidi chakula kama tuko naikula na marafiki wazuri, vilevile tunafurahiaka zaidi mambo ya kujifurahisha kama tuko naifanya na watu wazuri. Kwa hiyo, inaeleweka kuona kama wengi kati yetu, zaidi sana vijana, wanapendaka kujifurahisha na wengine. Lakini juu tujifurahishe mu njia yenye kufaa, ni jambo ya hekima tuamue mbele ya wakati nani njo tutajifurahisha nao na nani njo tutaepuka.​—2 Ny. 19:2; soma Mezali 13:20; Yak. 4:4.

14, 15. (a) Yesu alituachia mufano gani kuhusu kuchagua marafiki? (b) Tunapaswa kujiuliza maulizo gani mbele ya kuamua ikiwa mutu fulani atakuwa rafiki yetu ao hapana?

14 Mufano wa Yesu unaweza kutusaidia sana wakati tuko nachagua watu wa kupitisha nao wakati. Yesu anapendaka sana wanadamu tangu wakati waliumbwa. (Mez. 8:31) Wakati alikuwa ku dunia, alionyesha upendo watu wa aina zote. (Mt. 15:29-37) Yesu alijua tofauti kati ya kutendea kila mutu muzuri na kuwa rafiki wa sana wa mutu. Hata kama alitendea watu wote muzuri, alikuwa rafiki wa sana wa wale tu wenye walitimiza mambo fulani. Aliambia mitume wake waaminifu 11 hivi: “Ninyi ni marafiki wangu kama munafanya mambo yenye ninawaamuru.” (Yoh. 15:14; ona pia Yohana 13:27, 30.) Yesu alifanya urafiki wa sana na wale tu wenye walimufuata na kumutumikia Yehova.

15 Kwa hiyo, wakati uko najiuliza ikiwa mutu fulani anaweza kuwa rafiki yako ao hapana, ni jambo ya hekima ukumbuke ile maneno yenye Yesu alisema. Unaweza kujiuliza hii maulizo: ‘Maneno ya huyu mutu na matendo yake inaonyesha kama anatii amri za Yehova na Yesu? Naye anaheshimia kanuni za Biblia kuhusu mwenendo? Kuwa rafiki yake kutanichochea nitie Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yangu na nimutumikie Yehova kwa ushikamanifu?’ Kama unajibia ndiyo ku ile maulizo, ni kusema umepata rafiki muzuri mwenye unaweza kujifurahisha naye.​—Soma Zaburi 119:63; 2 Ko. 6:14; 2 Ti. 2:22.

Unaona Namna Gani Mambo Yenye Unajifurahishaka Nayo?

16. Juu tujifurahishe kwa njia yenye inafaa, tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

16 Tumezungumuzia mambo tatu kuhusu kujifurahisha. Juu tujifurahishe mu njia yenye inafaa, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Nitajifurahisha na nini? Ni mambo ya muzuri ao ya mubaya?’ (Mez. 4:20-​27) ‘Nitatumia muda gani mu mambo ya kujifurahisha? Itafanya nikose wakati ya kumutumikia Yehova?’ (1 Ti. 4:8) Na nitajifurahisha na nani? Ni marafiki wazuri ao wabaya?’​—Muh. 9:18; 1 Ko. 15:33.

17, 18. (a) Nini njo itatusaidia kujua ikiwa mambo yenye tunachagua kujifurahisha nayo inapatana na kanuni za Biblia? (b) Unaazimia kufanya nini wakati unachagua mambo ya kujifurahisha nayo?

17 Kama mambo fulani ya kujifurahisha inapingana na kanuni za Biblia mu jambo moya ao zaidi kati ya ile mambo tatu, ni kusema haifae. Lakini kama mambo yenye tunajifurahisha nayo inapatana na kanuni za Biblia mu ile mambo tatu, itamutukuza Yehova na itatuletea faida.​—Zb. 119:33-35.

18 Kwa hiyo, wakati tuko nachagua mambo ya kujifurahisha nayo, tujikaze kuchagua mambo ya muzuri, tusiache ile mambo ifanye tukose wakati ya kumutumikia Yehova, na tujifurahisha na watu wazuri. Kwa hiyo, siye wote tujikaze basi kufuata hii shauri ya Biblia: “Ikuwe munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Ko. 10:31.

[Maelezo ya chini]

^ Mu hii habari maneno “mambo ya kujifurahisha,” inatumiwa juu ya kuzungumuzia wakati yenye tunatia pembeni juu ya kufanya mambo yenye inatuletea furaha.

Unaweza kufasiria?

Kuhusu kujifurahisha, namna gani unaweza kutumia kanuni zenye kupatikana mu . . .

Wafilipi 4:8?

Matayo 6:33?

Mezali 13:20?

[Maulizo ya Funzo]

[Muchoro kwenye ukurasa wa 9]

(Juu ya kuona ile maelezo, ona kitabu)

Ninajifurahishaka na Nini?

[Muchoro kwenye ukurasa wa 10]

(Juu ya kuona ile maelezo, ona kitabu)

Ninatumia Muda Gani?

[Muchoro kwenye ukurasa wa 12]

(Juu ya kuona ile maelezo, ona kitabu)

Ninajifurahishaka na Nani?

[Picha kwenye ukurasa wa 10]

Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Yesu wakati tunachagua marafiki na mambo ya kujifurahisha nayo?