Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Biblia inabadilisha maisha ya watu

Nini njo ilisaidia mwanaume mwenye alikuwa nacheza michezo ya makuta na kuiba aachane na zile tabia na abadilishe maisha yake? Soma habari juu ya maisha yake.

“Nilikuwa Napenda Sana Mashindano ya Kutembeza Farasi”​—RICHARD STEWART

ALIZALIWA MWAKA WA: 1965

INCHI: JAMAIKA

ALIKUWA: NACHEZA MICHEZO YA MAKUTA NA ALIKUWA MWIZI

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilikomalia mu eneo ya Kingston, muji mukubwa wa Jamaika. Mu ile eneo mulikuwa watu wengi sana na walikuwa maskini. Watu wengi hawakukuwa na kazi, na kulikuwa jeuri sana. Watu walikuwa naishi mu woga juu kulikuwa watu wengi sana wenye jeuri. Nilikuwa nasikia sauti ya masasi karibu kila siku.

Mama yangu alikuwa natumika sana juu ya kutimiza mahitaji yangu, ya ndugu yangu mudogo, na ya dada yangu. Alijikaza sana juu tuende ku masomo. Sikukuwa napenda masomo, lakini nilipenda sana mashindano ya kutembeza farasi. Kuko siku nilikuwa nakosa masomo juu ya kuenda fasi ya kufanyia mashindano ya farasi. Nilikuwa hata natembeza farasi.

Kisha nilianza kucheza michezo ya makuta fasi ya kufanyia mashindano ya farasi. Nilikuwa nafanya uasherati na wanamuke wengi. Nilikuwa navuta marijuana na nilikuwa naiba juu nipate makuta ya kufanya ile mambo yote. Nilikuwa na bunduki za mingi, lakini ninafurahi juu sikuuaka mutu wakati nilikuwaka naenda kuiba.

Ku mwisho, polisi walinikamata na nikafungwa mu gereza. Kisha kutoka mu gereza, niliendelea na maisha yangu ya mubaya. Niliharibika sana kupita hata na zamani. Kama mutu angeniangalia ku sura, angewaza niko mutu muzuri. Lakini nilikuwa kichwa-nguvu, nilikuwa nakasirika haraka, na sikukuwa na huruma. Nilijiangaikia tu miye peke.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Wakati nilikuwa nafanya ile mambo yote, mama yangu alikuwa najifunza Biblia na akakuwa Shahidi wa Yehova. Niliona vile alibadilika sana na kuwa mutu muzuri zaidi. Kwa hiyo nilipenda kujua nini njo ilifanya abadilike. Na miye nilianza kuzungumuza na Mashahidi wa Yehova kuhusu Biblia.

Nilivumbula kwamba mafundisho ya Mashahidi wa yehova iko tofauti na mafundisho ya dini zingine, na kama mafundisho yao yote inategemea Biblia. Wao tu njo walikuwa nahubiri nyumba kwa nyumba sawa vile Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwaka nafanya. (Matayo 28:19; Matendo 20:20) Wakati niliona upendo wa kweli wenye walikuwa naonyeshana, nilikuwa hakika kama nimepata dini ya kweli.​—Yohana 13:35.

Mambo yenye nilijifunza mu Biblia, ilinisaidia kuona kama nilipaswa kubadilisha mambo mingi mu maisha yangu. Nilijifunza kama Yehova anachukia uasherati, na kama juu nimupendeze ninapashwa kuachana na tabia zenye zinachafua mwili wangu. (2 Wakorinto 7:1; Waebrania 13:4) Nilifurahi sana wakati nilijifunza kama Yehova naye anakuwaka na hisia, ni kusema matendo yetu inaweza kufanya afurahi ao ahuzunike. (Mezali 27:11) Kwa hiyo, niliamua kuacha kuvuta marijuana, nikaachana na bunduki zangu, na nikajikaza kuachana na tabia za mubaya. Ilikuwa nguvu kuachana na mambo fulani sawa vile uasherati, na michezo ya makuta.

Ku mwanzo, sikupenda marafiki wangu wajue kama niko najifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Lakini nilibadilisha mawazo yangu wakati nilisoma Matayo 10:33. Mu ile andiko, Yesu anasema hivi: “Lakini kila mutu mwenye ananikana mbele ya wanadamu, mimi pia nitamukana mbele ya Baba yangu wa mbinguni.” Ile maneno ilinichochea nielezee marafiki wangu kama nilikuwa najifunza na Mashahidi wa Yehova. Walishtuka sana. Walijiuliza namna gani mutu sawa miye anaweza kupenda kuwa Mukristo. Lakini niliwaambia kama sipendi tena kuendelea na maisha yangu ya zamani.

FAIDA YENYE NIMEPATA: Mama yangu alifurahi sana wakati aliona ninaanza kutumikisha mambo yenye Biblia inasema. Sasa hakuwake na wasiwasi kama nitafanya mambo fulani ya mubaya. Tumekuwa marafiki sana juu siye wote tunamupenda Yehova. Wakati fulani ninafikiriaka maisha yangu ya zamani na kushangala wakati ninaona mabadiliko yenye Mungu amenisaidia kufanya. Sipendi kurudilia tena maisha yangu ya uasherati, na kupenda sana vitu vya kimwili.

Kama singejifunzaka Biblia, pengine kama leo niko mu kaburi, ao mu gereza. Lakini, sasa, niko na familia ya muzuri na yenye furaha. Ninafurahi sana kumutumikia Yehova pamoya na bibi yangu mwenye kunitegemeza, na mutoto wangu mwanamuke mwenye kuwa mutiifu. Ninamushukuru sana Yehova kwa kunikubali mu familia ya Kikristo yenye upendo. Na ninashukuru juu kuko mutu mwenye alijikazaka kunifundisha Biblia. Tena, ninafurahia pendeleo yenye niko nayo ya kuelezea wengine mambo yenye Biblia inafundisha. Na zaidi sana ninamushukuru Yehova juu alinionyesha fazili zake zenye upendo kwa kunivuta kwake.

[Wazo ya fungu kwenye ukurasa wa 11]

“Nilijifunza kama Yehova naye anakuwaka na hisia, ni kusema matendo yetu inaweza kufanya afurahi ao ahuzunike”

[Picha kwenye ukurasa wa 11]

Miye na bibi yangu na mutoto wetu mwanamuke

[Picha kwenye ukurasa wa 11]

Niliona namna mama yangu alibadilika na kuwa mutu muzuri zaidi