Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Baba Wanaweza Kufanya Nini Juu Wakuwe Marafiki wa Sana wa Watoto Wao Wanaume?

Baba Wanaweza Kufanya Nini Juu Wakuwe Marafiki wa Sana wa Watoto Wao Wanaume?

Baba Wanaweza Kufanya Nini Juu Wakuwe Marafiki wa Sana wa Watoto Wao Wanaume?

“PAPA, ile mambo yote uliijua namna gani? Mutoto wako mwanaume alishakakukuuliza vile? Kama ni vile, ulifurahi kabisa kuwa baba. Na bila shaka ulifurahi hata zaidi wakati uliona iko natumia mashauri yenye hekima yenye ulimupatia. *​—Mezali 23:15, 24.

Kadiri mutoto wako mwanaume iko nakomala angali anaona kama unajua mambo mingi sawa vile alikuwaka naona wakati alikuwaka mutoto? Ao kadiri iko nakomala anaanza kukuona sawa tu mutu wa kawaida? Unaweza kufanya nini juu uendelee kuwa na urafiki wa sana na mutoto wako mwanaume kadiri iko nakomala na kuwa mutu muzima? Tuone kwanza mambo fulani yenye inafanyaka baba wasikuwe na urafiki wa sana na watoto wao wanaume.

Matatizo Tatu Yenye Baba Wengi Wanakuwaka Nayo

1. KUKOSA WAKATI: Mu inchi za mingi baba njo wanatumikaka sana juu ya kutimiza mahitaji ya familia zao. Mara mingi, kila siku kazi yao inawalazimishaka kupitisha saa mingi mbali na familia zao. Mu maeneo fulani, baba wanapitishaka wakati kidogo sana na watoto wao. Kwa mufano, uchunguzi wenye ulifanywa mu inchi ya Ufaransa hivi karibuni unaonyesha kama, kwa kukadiria, baba wanapitishaka chini ya dakika 12 pamoya na watoto wao.

JAMBO YA KUFIKIRIA: Unapitishaka muda gani na mutoto wako mwanaume? Juma yenye kufuata ao juma mbili zenye kufuata, pima kuandika wakati yenye utapitisha naye kila siku. Utashangala kuona wakati yenye unapitishaka na mutoto wako.

2. KUKOSA MUFANO MUZURI WA KUIGA: Wanaume fulani hawakukuwaka napitisha wakati mingi na baba zao. Jean-Marie, wa Ufaransa, anasema hivi: “Sikukuwa na urafiki wa sana na baba yangu.” Ile imekuwa na matokeo gani juu ya Jean-Marie? Anasema hivi: “Imeniletea magumu yenye sikuwaziaka kama ninaweza kuwa nayo. Kwa mufano, inakuwaka nguvu kuzungumuza na watoto wangu wanaume juu ya mambo fulani ya maana.” Wanaume wengine wanajua baba zao muzuri sana, lakini hawana uhusiano muzuri pamoya nao. Philippe, mwenye kuwa na miaka 43, anasema hivi: “Ilikuwa nguvu kwa baba yangu kunionyesha upendo. Kwa hiyo, imeniomba nijikaze sana juu niweze kuonyesha mutoto wangu mwanaume upendo.”

JAMBO YA KUFIKIRIA: Unawaza uhusiano wako na baba yako njo unafanyaka ukuwe natendea mutoto wako mwanaume kwa njia fulani? Unawaza kama uko nafuata mufano muzuri wa baba yako ao uko naiga tabia zake za mubaya? Uko nafanya vile namna gani?

3. KUKOSA MASHAURI YENYE KUFAA: Mu maeneo ya mingi, watu wanawazaka kama kukomalisha watoto haiko kabisa kazi ya baba. Luca, mwenye alikomalia mu inchi fulani ya Ulaya anasema hivi: “Kwenye nilikomalia watu walikuwa naona kama kazi ya kukomalisha watoto ni ya mama.” Mu maeneo ingine baba wanatiwa moyo wakaripie watoto wao kwa ukali. Kwa mufano, George mwenye alikomalia mu inchi fulani ya Afrika, anasema hivi: “Baba hawachezake na watoto wao juu wanaogopaka kama ile itafanya watoto wasiwaheshimie. Njo maana na miye nimekuwa na magumu ya kupitisha wakati na mutoto wangu mwanaume.”

JAMBO YA KUFIKIRIA: Mu eneo yenu watu wanaonaka kama baba iko na daraka gani? Wanasemaka kama kazi ya kukomalisha watoto ni ya wanamuke? Baba wanatiwa moyo waonyeshe watoto wao wanaume upendo ao wanafundishwa kama haina maana kufanya vile?

Kama uko baba na uko na tatizo moya ao zaidi kati ya matatizo yenye tumezungumuzia, unaweza kufanya nini ili uweze kufanya urafiki na mutoto wako mwanaume? Fikiria mashauri yenye kufuata.

Anza Wakati Mutoto Wako Mwanaume Angali Mudogo

Inaonekana kama mutoto mwanaume anazaliwaka na tamaa ya kuiga baba yake. Njo maana ni muzuri ukuwe unapitisha wakati naye juu akujue muzuri. Unaweza kufanya vile namna gani? Na unaweza kufanya nini juu upate wakati ya kupitisha pamoya naye?

Wakati inawezekana, ambia mutoto wako mwanaume akusaidie kufanya mambo mabalimbali kila siku. Kwa mufano, kama uko nafanya kazi za ku nyumba umuambie akusaidie. Umupatie kifagio ya kidogo ao jembe ya kidogo. Kwa kweli, atafurahi kutumika na weye juu anakuonaka kuwa mutu wa kuiga. Pengine ile kazi itakukamata wakati murefu zaidi juu uko natumika naye. Lakini ile itatia nguvu urafiki wenu na itakusaidia umufundishe namna ya kutumika kazi muzuri. Zamani, Biblia ilitia moyo wazazi wakuwe nafanya kazi mbalimbali za kila siku pamoya na watoto wao, na watumie ile wakati juu ya kuzungumuza nao na kuwafundisha. (Kumbukumbu la Torati 6:6-9) Ile shauri ya Biblia ingali ya maana hata leo.

Zaidi ya kufanya kazi pamoya na mutoto wako mwanaume, tafuta pia wakati wa kucheza naye. Kucheza na mutoto iko na faida ingine, haiko tu kujifurahisha. Uchunguzi unaonyesha kama wakati baba wanacheza na watoto wao wadogo wanawatia moyo wakuwe hodari na wakuwe na tamaa ya kufanya mambo ya mupya.

Wakati baba anacheza na mutoto wake mwanaume, ile iko na faida ya maana hata zaidi. Muchunguzi Michel Fize, anasema hivi: “Wakati mutoto mwanaume iko nacheza na baba yake njo wakati anazungumuzaka naye muzuri zaidi. Wakati wako nacheza, baba anaweza kuonyesha kama anamupenda mutoto wake kupitia maneno na matendo. Wakati anafanya vile anafundisha mutoto wake mwanaume namna ya kuonyesha wengine upendo. “André, baba mwenye kuishi mu inchi ya Alemanye, anasema hivi: “Wakati mutoto wangu mwanaume alikuwa mudogo, nilikuwa nacheza naye mara mingi. Nilikuwa namukumbatia na ile ilifanya naye ajifunze kunionyesha upendo.”

Wakati ya kuenda kulala ni wakati yenye baba wanaweza kutumia juu ya kutia nguvu urafiki wao na watoto wao. Ukuwe na kawaida ya kusomea mutoto wako hadisi, na umusikilize wakati iko nakuambia mambo yenye ilimufurahisha ao yenye ilimuhuzunisha ile siku. Kama unafanya vile, itakuwa mwepesi kwake kuzungumuza na weye wakati yenye atakomala.

Uendelee Kufanya Naye Mambo Yenye Anafurahiaka

Wakati baba wanajaribu kuzungumuza na vijana wao wanaume, vijana wao wanaume wanaweza kuonekana kuwa hawapendi kuzungumuza nao. Kama kijana wako mwanaume iko naepuka maulizo yako, usiwaze mara moya kuwa hapendi kuzungumuza na weye. Anaweza kuwa tayari kuzungumuza na weye kama unabadilisha namna yako ya kuzungumuza naye.

Jacques, baba mwenye kuishi katika Ufaransa, aliona kama wakati fulani ilikuwa nguvu kuzungumuza na mutoto yake mwanaume, Jérôme. Lakini kuliko kumukaza azungumuze, yeye njo alibadilisha namna yake ya kufanya. Alianza kucheza naye kabumbu. Jacques anasema hivi: “Kisha kucheza, tulikuwa naikala chini na kupumuzika kidogo. Ile wakati, mara mingi mutoto wangu mwanaume alikuwa nanifungulia moyo wake. Nawaza kama kukuwa tu siye wawili, miye naye tu, kulifanya urafiki wetu ukuwe wenye nguvu sana.”

Utafanya nini kama mutoto wako mwanaume hapendake michezo? André anakumbuka saa za mingi sana zenye alikuwa anapitisha na mutoto wake mwanaume na wako tu naangalia nyota. André anasema hivi: “Tulikuwa naikala inje ku viti mu baridi wakati ya usiku. Tulikuwa tunavala manguo ya kutulinda na baridi na tulikuwa naangalia anga ya usiku na tuko nakunywa chai. Tulikuwa nazungumuzia ule mwenye aliumbaka nyota, tulikuwa nazungumuzia mambo ya kipekee; kwa kifupi, tulikuwa nazungumuzia karibu kila kitu.”​—Isaya 40:25, 26.

Halafu kama haupendake mambo fulani yenye mutoto wako mwanaume anapendaka? Kama ni vile, inaweza kukuomba uachane na mambo yenye unapendaka juu ujipatanishe na mutoto wako mwanaume. (Wafilipi 2:4) Ian, wa Afrika kusini anasema hivi: “Miye nilikuwa nafurahia sana michezo, lakini mutoto wangu mwanaume Vaughan hakukuwa naifurahia sana. Yeye alikuwa nafurahia mambo yenye ilikuwa inahusu ndege (ao avion) na ordinatere. Kwa hiyo, miye pia nilianza kupendezwa na ile mambo. Nilikuwa namupeleka fasi za kuangalilia namna ndege ziko naruka na nilikuwa nacheza naye michezo ya kutembeza ndege ku ordinatere. Juu tulikuwa nafanya pamoya mambo yenye alifurahia, Vaughan alikuwa najisikia huru kuzungumuza na miye.”

Umusaidie Asikuwe Najiona Kuwa Mutu wa Bure

“Ona, Papa, ona.” Mutoto wako mudogo mwanaume alishakakuambia vile wakati aliweza kufanya jambo fulani ya mupya? Kama alishakuwa sasa kijana, angali nakuonyesha waziwazi mambo yenye alifanya juu umupongeze? Pengine hapana! Lakini ujue kama angali na lazima ya kupongezwa juu afikie kuwa mutu muzima mwenye usawaziko.

Kwa mufano, ona namna Yehova alitendea mumoja wa wana wake. Wakati Yesu alikaribia kuanza sehemu ya maana sana ya maisha yake hapa ku dunia, Mungu alionyesha waziwazi kama anamupenda. Alisema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali.” (Matayo 3:17; 5:48) Ni kweli kama uko na daraka ya kumupatia mutoto wako mwanaume nizamu na kumufundisha. (Waefeso 6:4) Lakini unatafutaka pia nafasi ya kumupongeza juu ya mambo ya muzuri yenye anasema ao kufanya?

Wanaume fulani wanaonaka kama ni nguvu kupongeza watoto wao wanaume na kuwaonyesha upendo. Pengine walikomalia mu familia zenye wazazi walikuwa nakazia sana makosa ya watoto kuliko mambo ya muzuri yenye watoto walikuwa nafanya. Kama ulikomalia mu familia ya vile, unapaswa kujikaza sana juu usaidie mutoto wako mwanaume asikuwe najiona kuwa mutu wa bure. Unaweza kufanya vile namna gani? Luca, mwenye tulishazungumuzia anafanyaka kazi za ku nyumba pamoya na mutoto wake mwanaume Manuel wa miaka 15. Luca anasema hivi: “Wakati fulani ninaambiaka Manuel aanze kazi yeye mwenyewe na nitamusaidia kama iko na lazima yangu. Lakini, mara mingi anawezaka kumaliza ile kazi yeye mwenyewe.” Ile inamuleteaka furaha na inamusaidiaka asikuwe najiona kuwa mutu wa bure. Wakati anawezaka kufanya kazi yenye nilimupatia ninamupongezaka. Na wakati haifanye muzuri vile angependa, ninamupongezaka hata juu ya ile kidogo yenye alijikaza kufanya.”

Unaweza pia kusaidia mutoto wako mwanaume asijione kuwa mutu wa bure kwa kumusaidia afikie miradi ya maana mu maisha. Lakini utafanya nini kama hafikie ile miradi haraka sawa vile ungependa? Halafu kama miradi yake, yenye pengine nayo ni ya muzuri, iko tofauti na miradi yenye umemuwekea? Inaweza kuwa muzuri ubadilishe mawazo yako juu ya mambo yenye unatazamia afanye. Jacques mwenye tulishazungumuzia anasema hivi: “Ninasaidiaka mutoto wangu mwanaume ajitilie miradi yenye anaweza kufikia. Lakini ninahakikishaka kama ni miradi yake, hapana yangu. Kisha ninajikumbushaka kama anapaswa kujikaza kufikia ile miradi kulingana na uwezo wake. Kama unasikiliza mawazo ya mutoto wako mwanaume, unamupongeza juu ya uwezo wake, na unamutia moyo apiganishe vizuizi vyenye anaweza kukutana navyo, utamusaidie afikie miradi yake.

Kusema kweli, ile haimaanishe kama uhusiano wenu utakuwa tu muzuri kila wakati bila matatizo. Lakini kama unafanya yako yote, inawezekana mutoto wako mwanaume ataendelea kukupenda juu ya mambo yote yenye unafanya ili kumusaidia na kumutegemeza.

[Maelezo ya chini]

^ Hii habari inazungumuzia sana uhusiano kati ya baba na mutoto wake mwanaume, lakini kanuni zenye kuzungumuziwa zin ahusu pia uhusiano kati ya baba na mutoto wake mwanamuke.