Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Munakaa Katika Neno Langu”

“Munakaa Katika Neno Langu”

“Munakaa Katika Neno Langu”

“Kama munakaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, na mutajua kweli, na kweli itawaweka ninyi huru.”​—YOHANA 8:31, 32.

Maana yake nini?: “Neno” ya Yesu maana yake mafundisho yake yenye ilitoka kwa Mungu. Yesu alisema hivi: “Baba mwenye alinituma, yeye mwenyewe amenipatia amri juu ya jambo la kusema na la kufundisha.” (Yohana 12:49) Wakati Yesu alikuwa nasali kwa Baba yake wa mbinguni Yehova Mungu, alisema hivi: “Neno lako ni kweli.” Wakati alikuwa nafundisha, mara mingi alikuwa anataya maandiko. (Yohana 17:17; Matayo 4:4, 7, 10) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli wanakaa katika Neno yake, ni kusema wanakubali Neno ya Mungu Biblia kuwa “kweli.” Na wanatosha ndani mambo yote yenye wanaamini na wanajikaza kutumikisha mu maisha yao mambo yenye inasema.

Wakristo wa Kwanza-kwanza Walifanya Vile Namna Gani?: Mutume Paulo mwenye aliandikaka vitabu mingi mu Biblia, alikuwa anaheshimia Neno ya Mungu sawa tu vile Yesu. Aliandika hivi: “Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.” (2 Timoteo 3:16) Wale wenye walikuwa na daraka ya kufundisha mu kutaniko ya Kikristo walipaswa “kushikamana kabisa na neno la uaminifu.” (Tito 1:7, 9) Paulo aliambia Wakristo wa kwanza-kwanza waepuke “filozofia na udanganyifu wa bure kulingana na desturi ya wanadamu, kulingana na mambo ya musingi ya ulimwengu na hapana kulingana na Kristo.”​—Wakolosai 2:8.

Nani Njo Wako Nafanyaka Vile Leo?: Kitabu Catechism of the Catholic Church inasema hivi: “Haiko mu Biblia tu njo kanisa Katoliki inatoshaka mafundisho yake. Njo maana inakubali na kuona mafundisho ingine takatifu kuwa ya maana sawasawa tu na Biblia.” Habari fulani yenye ilichapishwa mu gazeti Maclean ilikuwa na maneno ya kiongozi fulani wa dini wa Toronto, Kanada, mwenye aliuliza hivi: “Tuko kabisa na lazima ya kuongozwa na mawazo yenye iliandikwaka kumepita miaka elfu mbili? Na siye tuko na mawazo yetu ya muzuri. Lakini ile mawazo iko nakosa nguvu wakati tunatafuta kuipatanisha na mawazo ya Yesu na mawazo ya maandiko.

Kitabu New Catholic Encyclopedia inasema hivi kuhusu Mashahidi wa Yehova: “Mafundisho yao yote inatoka mu Biblia na wanatumikishaka mu maisha yao mambo yote yenye Biblia inasema. Juzijuzi wakati Shahidi fulani wa Yehova alikuwa najitambulisha, mwanaume fulani katika inchi ya Kanada alimukatiza na kumuambia hivi: “Ninajua uko nani juu uko na Biblia mu mikono.”