Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Ajili ya Vijana

Musa Apokea Mgawo wa Pekee

Musa Apokea Mgawo wa Pekee

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yehova Mungu na Musa

Muhtasari: Yehova anamwagiza Musa awaongoze Waisraeli kutoka Misri.

1 CHUNGUZA MATUKIO HAYA.​—SOMA KUTOKA 3:1-14; 4:1-17.

Eleza jinsi mti uliokuwa ukiteketea ulivyoonekana, kama unavyowazia.

․․․․․

Eleza jinsi unavyowazia uso na sauti ya Musa alipokuwa akijibu maneno ya Mungu kama ilivyoandikwa kwenye andiko la Kutoka 3:4?

․․․․․

Unawazia Musa alikuwa na hisia gani alipomuuliza Yehova maswali yaliyo andikwa kwenye andiko la Kutoka 3:11, 13 na 4:1, 10?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Ukitumia vifaa vya kufanyia utafiti unavyoweza kupata, chunguza zaidi kuhusu maneno “nitakuwa kile nitakachokuwa.” (Kutoka 3:14) Kwa nini Yehova alisema maneno hayo alipokuwa akijibu swali la Musa kuhusu jina Lake? *

․․․․․

Unafikiri ni kwa nini Musa alisita kuzungumza na Farao? (Dokezo: Soma Hesabu 12:3.)

․․․․․

Kwa nini huenda Musa alisita kuzungumza na Waisraeli wenzake?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Mwelekeo wa wanadamu wa kutojiamini.

․․․․․

Uthibitisho wa kwamba Yehova ana uhakika kukuelekea na kuelekea uwezo wako.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAZOWEZA KUTUMIA HABARI HIYO.

Ni katika sehemu gani za maisha yako ambazo unakosa kujiamini?

․․․․․

Yehova Mungu anaweza kukutumia kwa njia zipi licha ya udhaifu wako?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Unaweza kupakua na/au kuchapisha makala hii kwenye Tovuti ya www.pr418.com

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au uisome katika Intaneti kwenye Tovuti ya www.watchtower.org/sw

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 14 Mashahidi wa Yehova huchapisha vitabu na broshua kadhaa ambazo zinaweza kukusaidia uchimbe zaidi unapojifunza Biblia. Kwa habari zaidi, wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au uwaandikie barua wachapishaji wa gazeti hili.