Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unaheshimu Kabisa Zawadi ya Ndoa?

Je, Unaheshimu Kabisa Zawadi ya Ndoa?

Je, Unaheshimu Kabisa Zawadi ya Ndoa?

‘Yehova na awape zawadi, na mupate mahali pa kupumuzika kila mumoja katika nyumba ya mume wake.’​—RUT. 1:9.

TAFUTA MAJIBU YA MAULIZO HAYA:

Kwa nini tunaweza kusema kama watumishi wa Mungu wa zamani waliheshimu zawadi ya ndoa?

Tunajua namna gani kama Yehova anaweza kufurahishwa ao kuhuzunishwa na uchaguzi tunaofanya wa mwenzi wa ndoa?

Ni shauri gani la Biblia juu ya ndoa unalowazia kutumia katika maisha yako?

1. Adamu alijisikia namna gani alipopata bibi?

 ‘MWISHOWE huyu ni mufupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu. Huyu ataitwa Mwanamuke, kwa sababu huyu alitolewa katika mwanamume.’ (Mwa. 2:23) Adamu alifurahi sana kupata bibi! Ili kuonyesha furaha yake, Adamu alisema maneno matamu ili kumusifu bibi yake. Yehova alimulalisha Adamu usingizi muzito, akachukua mufupa moja wa ubavu wa Adamu akamufanyia mwanamuke mwenye sura nzuri sana. Kisha Adamu alimupatia jina la Eva. Mungu aliwaunganisha katika ndoa yenye furaha. Kwa kuwa Yehova alitumia mufupa moja wa ubavu wa Adamu ili kumuumba Eva, wenzi hao wawili walipendana sana kuliko watu wengine.

2. Sababu gani wanaume na wanawake wanavutiana?

2 Kwa hekima yake iliyo ya juu zaidi, Yehova alitia katika wanadamu upendo wa kimapenzi unaofanya wanaume na wanawake wavutiane. Kitabu kimoja kinasema hivi: ‘Mwanaume na mwanamuke wanaooana wanatazamia kufanya kitendo cha ndoa na kuendelea kuvutiana kimapenzi.’ Watu wa Yehova wamejionea hilo mara nyingi.

WALIHESHIMU MUPANGO WA NDOA

3. Namna gani Isaka alipata bibi?

3 Mwanaume mwaminifu Abrahamu aliheshimu sana mupango wa ndoa. Kwa hiyo, alimutuma mutumishi wake kwenda Mesopotamia ili kumuoea Isaka. Mutumishi huyo alisali ili Mungu amusaidie, na alipata mwanamuke anayefaa. Rebeka alikuwa binti anayemuogopa Mungu na ni yeye aliyekuja kuwa bibi mupendwa wa Isaka. Yehova alimutumia mwanamuke huyo ili kutimiza ahadi yake ya kuendeleza uzao wa Abrahamu. (Mwa. 22:18; 24:12-14, 67) Hadisi hii haitufundishi kama kazi yetu ni kuwatafutia wengine wenzi wa ndoa hata ikiwa hatukuombwa kufanya hivyo. Leo, watu wengi wanajichagulia wao wenyewe wenzi wa ndoa. Kwa kweli, si Mungu anayechagulia watu wenzi wa ndoa kama wengine wanavyosema, lakini Mungu anaweza kumusaidia Mukristo afanye uamuzi muzuri katika jambo hili na mambo mengine ya maisha ikiwa anasali ili kutafuta uongozi wa Mungu, na ikiwa anakubali kuongozwa na roho takatifu yake.​—Gal. 5:18, 25.

4, 5. Tunajua namna gani kwamba Mushulami na muchungaji walipendana sana?

4 Binti mwenye sura nzuri Mushulami wa Israeli hakutaka marafiki wake wamulazimishe kuwa mumoja wa wanawake wa Sulemani. Yeye alisema: ‘Nimewaapisha ninyi, enyi binti za Yerusalemu kwamba musijaribu kuamusha ao kuwasha upendo ndani yangu mupaka wenyewe utake.’ (Wim. 8:4) Mushulami pamoja na muchungaji fulani walipendana sana. Mushulami alisema hivi kwa unyenyekevu: ‘Mimi ni zafarani tu ya inchi tambarare ya pwani, yungiyungi la inchi tambarare za chini.’ Muchungaji naye akajibu: ‘Kama yungiyungi katikati ya magugu yenye miiba, ndivyo alivyo musichana mwenzi wangu katikati ya mabinti.’ (Wim. 2:1, 2) Walipendana kweli kweli!

5 Ndoa ya Mushulami na muchungaji ilikuwa na musingi wenye nguvu kwa sababu kwanza walimupenda Mungu. Ndiyo maana Mushulami alimuambia muchungaji wake aliyemupenda hivi: ‘Nitie kama muhuri juu ya moyo wako, kama muhuri juu ya mukono wako; kwa maana upendo una nguvu kama kifo, musisitizo juu ya kujitoa kikamili ni wenye kudai kama Kaburi. Miwako yake ni miwako ya moto, mwali wa moto wa Yah [kwa kuwa unatoka kwake]. Maji mengi hayawezi kuuzima upendo, wala mito haiwezi kuufagilia mbali. Kama mutu angetoa vitu vyote vyenye samani vya nyumba yake kwa ajili ya upendo, hakika watu wangevizarau.’ (Wim. 8:6, 7) Mutumishi wa Yehova anapofikiria kuoa ao kuolewa, anapaswa kutafuta mutu anayemupenda kwelikweli.

MUNGU ANAPENDEZWA NA UCHAGUZI TUNAOFANYA

6, 7. Ni nini inayoonyesha kama Mungu anaweza kufurahishwa ao kuhuzunishwa na uchaguzi tunaofanya wa mwenzi wa ndoa?

6 Yehova anaweza kufurahishwa ao kuhuzunishwa na uchaguzi tunaofanya wa mwenzi wa ndoa. Waisraeli walipewa sheria hii kuhusu wakaaji wa Kanaani: ‘Nawe usifanye mapatano yoyote ya ndoa pamoja nao. Binti yako usimupe mwana wake, wala binti yake usimuchukue kwa ajili ya mwana wako. Kwa maana atamugeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine; na hasira ya Yehova itawaka kwelikweli juu yenu, naye hakika atakuangamiza haraka.’ (Kum. 7:3, 4) Miaka mingi baadaye, kuhani Ezra aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Ninyi wenyewe mumetenda kwa kukosa uaminifu kwa vile mumewapa makao wanawake wa kigeni ili kuongezea hatia ya Israeli.’ (Ezra 10:10) Mutume Paulo pia aliwaambia Wakristo wenzake hivi: ‘Muke amefungwa wakati wote ambao mume wake yuko hai. Lakini mume wake akilala usingizi katika kifo, yeye yuko huru kuolewa na yeyote anayemutaka, katika Bwana tu.’​—1 Kor. 7:39.

7 Mutumishi wa Yehova akioa ao kuolewa na mutu asiye Shahidi, hilo lingekuwa tendo la kutomutii Mungu. Waisraeli wa siku za Ezra walikosa uaminifu kwa ‘kuwapa makao wanawake wa kigeni,’ na ilikuwa kosa kujaribu kupunguza uzito wa maagizo yaliyo wazi ya Maandiko. (Ezra 10:10; 2 Kor. 6:14, 15) Mukristo anayeoa ao kuolewa na mutu asiye Shahidi yeye si mufano muzuri na hilo linaonyesha kama haheshimu zawadi ya ndoa. Mukristo aliyebatizwa akifanya hivyo, anaweza kupoteza mapendeleo yake katika kutaniko. Ni jambo lisilopatana na akili Mukristo akisali hivi: ‘Ee, Yehova, hata kama nimekukosea kwa makusudi. Tafazali, unibariki.’

YEHOVA ANAJUA VIZURI MAMBO YA NDOA KULIKO SISI

8. Kwa nini ni vizuri kufuata muongozo wa Mungu kuhusu ndoa? Eleza.

8 Mutu aliyetengeneza mashine fulani ndiye anayejua kabisa namna inavyotumika. Anaweza kutoa maagizo yanayofaa ili kuonyesha namna ya kuunganisha sehemu mbalimbali za mashini hiyo. Matokeo yatakuwa nini ikiwa tunapuuza maagizo hayo na kuunganisha sehemu hizo kulingana na mawazo yetu? Labda mashini hiyo inaweza kuanza kutumika, lakini matokeo yatakuwa mabaya sana. Bila shaka, tukitaka kuwa na ndoa yenye furaha, tunapaswa kufuata maagizo ya yule aliyeanzisha ndoa, yaani, Yehova.

9. Tunajua namna gani kama Yehova anaelewa namna mutu anavyojisikia anapokuwa peke yake, na furaha inayotokana na kufunga ndoa?

9 Yehova anajua mambo yote kuhusu wanadamu na ndoa. Alitia katika wanadamu tamaa ya kufanya kitendo cha ndoa ili ‘wazae na wawe wengi.’ (Mwa. 1:28) Mungu anaelewa namna mutu anavyojisikia anapokuwa peke yake, kwa kuwa mbele ya kumuumba mwanamuke wa kwanza, yeye mwenyewe alisema hivi: ‘Si vema huyo mwanamume aendelee kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi, awe kikamilisho chake.’ (Mwa. 2:18) Tena, Yehova anajua kabisa kama kufunga ndoa kunaweza kuleta furaha.​—Soma Methali 5:15-18.

10. Wenzi wa ndoa wanapaswa kufuata mashauri gani kuhusu kitendo cha ndoa?

10 Kila ndoa ina matatizo kwa sababu ya kutokukamilika na zambi tuliyoriti kutoka kwa Adamu. Lakini, Wakristo wanaweza kuwa na ndoa yenye furaha ikiwa wanafuata maagizo ya Neno la Mungu. Kwa mufano, fikiria shauri lililo wazi la Paulo kuhusu kitendo cha ndoa kati ya bwana na bibi. (Soma 1 Wakorintho 7:1-5.) Maandiko hayafundishi kama kitendo cha ndoa kinafanyika tu ili kuzaa watoto. Kitendo hicho kinaweza pia kuwaletea furaha wenzi waliooana na kuwatimizia uhitaji wao wa kimwili. Lakini matendo yaliyo kinyume cha asili yanamuchukiza Mungu. Kwa hiyo, ni vizuri ikiwa kila mwenzi wa ndoa atatenda kwa kumufikiria mwenzake na kumuonyesha upendo wa kweli. Tena, wenzi wa ndoa watajikaza kuepuka matendo yote yanayomuchukiza Yehova katika jambo hilo.

11. Ruthu alibarikiwa namna gani kwa kuwa alifanya mambo kama vile Yehova anavyopenda?

11 Maisha ya ndoa yanapaswa kuwa yenye kufurahisha, wala si yenye kuhuzunisha ao kuchokesha. Zaidi sana nyumba ya Mukristo inapaswa kuwa mahali penye utulivu na amani. Fikiria mambo yaliyotokea miaka 3 000 hivi iliyopita wakati Naomi na binti-wakwe zake Orpa na Ruthu, walipokuwa njiani kutoka Moabu kuelekea Yuda. Naomi aliwaomba warudi kwao. Lakini, Ruthu Mumoabu aliyekataa kumuacha Naomi alikuwa mwaminifu kwa Mungu, na kwa hiyo, alipata ‘malipo kamili kutoka kwa Yehova, ambaye chini ya mabawa yake alikuja kutafuta kimbilio.’ (Rut. 1:9; 2:12) Kwa kuwa aliheshimu sana zawadi ya ndoa, Ruthu alikubali kuolewa na Boazi, muabudu wa kweli wa Yehova; ingawa Boazi alikuwa mwenye umri mukubwa. Atakapofufuliwa katika paradiso duniani, Ruthu atafurahi sana kujua kama alikuwaka nkambo ao tate wa Yesu Kristo. (Mt. 1:1, 5, 6; Lu. 3:23, 32) Kwa kweli alibarikiwa sana kwa kuwa alifanya mambo kama vile Yehova anavyopenda.

MASHAURI MAZURI ILI KUWA NA NDOA YENYE FURAHA

12. Ni wapi tunaweza kupata mashauri yenye hekima kuhusu ndoa?

12 Yehova, aliyeanzisha ndoa anatutolea mashauri tunayohitaji ili kuwa na ndoa yenye furaha. Yeye anajua mambo mengi kuliko wanadamu. Biblia inasema kweli siku zote, na ikiwa mutu anataka kutoa mashauri mazuri kuhusu ndoa anapaswa kuyachukua katika Neno la Mungu. Kwa mufano, mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kila mutu mumoja​-mumoja kati yenu na amupende hivyo muke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, muke anapaswa kumuheshimu sana mume wake.’ (Efe. 5:33) Wakristo waliokomaa wanaelewa vizuri shauri hilo. Lakini ulizo ni, Je, watatumia mashauri hayo ya Neno la Mungu? Watafanya hivyo ikiwa wanaheshimu kabisa zawadi ya ndoa iliyotoka kwa Mungu. *

13. Matokeo yanaweza kuwa nini ikiwa bwana hatii shauri lililo kwenye 1 Petro 3:7?

13 Mwanaume Mukristo anapaswa kumutendea bibi yake kwa upendo. Mutume Petro aliandika hivi: ‘Enyi waume, endeleeni kukaa nao vivyo hivyo kulingana na ujuzi, mukiwapa heshima kama chombo zaifu zaidi, yaani, mwanamuke, kwa kuwa ninyi pia ni wariti pamoja nao wa pendeleo lisilostahiliwa la uzima, kusudi sala zenu zisizuiwe.’ (1 Pet. 3:7) Sala za mwanaume Mukristo zinaweza kuzuiwa ikiwa hatii shauri hilo la Yehova. Kwa hiyo, hali ya kiroho ya wenzi wa ndoa inaweza kuharibika sana, na hilo linaweza kutokeza mahangaiko, fujo, kugombana na kutendeana vibaya.

14. Mwanamuke anayependwa anaweza namna gani kuisaidia familia yao?

14 Mwanamuke Mukristo anayejiacha kuongozwa na Neno la Yehova na roho yake anaweza kufanya mengi ili nyumba yake iwe na amani na furaha. Hilo litamuchochea bwana yake anayemuogopa Mungu kumupenda na kumulinda kimwili na kiroho. Mwanamuke anatamani sana kupendwa, kwa hiyo ni lazima aonyeshe sifa zitakazomufanya bwana yake amupende zaidi. Methali 14:1 inasema: ‘Mwanamuke mwenye hekima kwelikweli amejenga nyumba yake, lakini aliye mupumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.’ Mwanamuke mwenye hekima na anayependwa anaweza kusaidia sana ili familia yao iwe na furaha. Kwa kufanya hivyo, yeye pia anaonyesha kama anaheshimu sana zawadi ya ndoa.

15. Ni mashauri gani yanayopatikana katika Waefeso 5:22-25?

15 Wanaume na wanawake wanaoiga mufano wa Yesu, namna alivyokuwa akilitendea kutaniko, wanaoonyesha kama wanafurahia na kuheshimu zawadi ambayo Mungu alitutolea, yaani, ndoa. (Soma Waefeso 5:22-25.) Wenzi wa ndoa watapata baraka nyingi ikiwa wanapendana kweli kweli na ikiwa hawataacha kiburi, kukataa kuongea, ao tabia nyingine zisizo za Kikristo ziharibu ndoa yao.

MUTU YEYOTE ASIWATENGANISHE

16. Kwa nini Wakristo fulani wamebaki bila kuoa ao kuolewa?

16 Ijapokuwa watu wengi wanapanga kufunga ndoa siku moja katika maisha yao, watumishi fulani wa Yehova wamebaki bila kuoa ao kuolewa kwa sababu hawajapata mwenzi anayewafaa ao anayefaa kulingana na Yehova. Wengine wamezaliwa na zawadi ya kubaki waseja, hali hiyo inawafanya wamutumikie Yehova bila kukengeushwa. Bila shaka, tunaweza kufurahia useja ikiwa tunautumia kulingana na sababu zinazokubaliwa na Yehova.​—Mt. 19:10-12; 1 Kor. 7:1, 6, 7, 17.

17. (a) Ni maneno gani ya Yesu kuhusu ndoa ambayo hatupaswi kusahau? (b) Ikiwa Mukristo anaanza kutamani bwana ao bibi ya mutu mwengine, anapaswa kufanya nini bila kuchelewa?

17 Sisi wote, iwe tumefunga ndoa ao hapana, hatupaswi kusahau maneno haya ya Yesu: “Je, hamukusoma kwamba yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamuke na kusema, ‘Kwa sababu hiyo mwanamume atamuacha baba yake na mama yake naye atashikamana na muke wake, na hao wawili watakuwa mwili mumoja’? Hivi kwamba wao si wawili tena, bali mwili mumoja. Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.” (Mt. 19:4-6) Ni kosa kabisa kutamani bwana ao bibi ya mutu mwingine. (Kum. 5:21) Ikiwa Mukristo yeyote anaanza kuwa na tamaa hiyo chafu, anapaswa kutenda haraka ili kuiongoa katika moyo wake, hata ikiwa kufanya hivyo kutamuumiza sana moyoni. (Mt. 5:27-30) Ni jambo la maana sana kuachana na mawazo hayo na kuondoa tamaa hiyo yenye zambi ya moyo mudanganyifu.​—Yer. 17:9.

18. Unawaza tunapaswa kuiona namna gani zawadi ya ndoa ambayo Mungu alitutolea?

18 Ikiwa watu ambao hawajui mambo mengi juu ya Yehova Mungu ao hawajui lolote juu ya Yehova na zawadi nzuri ya ndoa wameheshimu ndoa kwa kiasi fulani, basi sisi ambao tumejitoa kwa Yehova, “Mungu mwenye furaha,” hatupaswi kufurahia mipango yake yote na kuonyesha kama tunaheshimu kabisa zawadi ya ndoa kuliko watu hao?​—1 Tim. 1:11.

[Maelezo ya chini]

^ Ili kupata habari zaidi juu ya ndoa, soma sura ya 10 na 11 ya kitabu “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu.”

[Maulizo ya Funzo]

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 6]

Ndoa nzuri inamuletea Yehova sifa na inafurahisha kila mushiriki wa familia

[Picha katika ukurasa wa 5]

Ruthu aliheshimu zawadi ya ndoa

[Picha katika ukurasa wa 7]

Je, wewe unaheshimu kabisa zawadi ya ndoa iliyotoka kwa Mungu?