Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Biblia Ni Kitabu cha Kawaida Tu?

Je, Biblia Ni Kitabu cha Kawaida Tu?

Je, Biblia Ni Kitabu cha Kawaida Tu?

“Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida . . . , ili mtu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.”​—2 TIMOTHEO 3:16, 17.

SI KILA mtu anayekubaliana na maneno kama hayo. Wewe una maoni gani kuhusu Biblia?

• Je, ni kitabu cha fasihi kilichoandikwa kwa ustadi?

• Ni mojawapo ya vitabu vitakatifu vinavyokubaliwa?

• Ni kitabu cha hadithi za kale zenye mafundisho mazuri?

• Au ni Neno la Mungu

Swali ambalo unapaswa kujiuliza ni, Je, ni muhimu kuchunguza unaloamini? Fikiria yale ambayo Biblia yenyewe inasema: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.” (Waroma 15:4) Hivyo, Biblia inataja kwamba kusudi lake ni kutufundisha na kutupatia faraja na tumaini.

Hata hivyo, ikiwa Biblia ingekuwa tu kitabu cha fasihi au mojawapo ya vitabu vitakatifu, je, ungetazamia ikufundishe na iongoze familia yako, hasa ikiwa ujumbe wake ungekuwa tofauti na yale unayofikiria kuwa sawa? Ikiwa Biblia ingekuwa kitabu cha hadithi za kale, je, ungeweza kupata faraja na tumaini kutokana na ahadi zake?

Kwa upande mwingine, watu wengi ambao wamejifunza Biblia wameamini kwamba ni Neno la Mungu na ni kitabu cha kipekee. Kwa nini? Ni nini kinachoifanya Biblia iwe tofauti na vitabu vingine? Tunakutia moyo uchunguze mambo matano yanayotajwa katika makala zifuatazo yanayoifanya Biblia kuwa kitabu cha kipekee.