Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Ni Kitabu Tofauti Kabisa!

Biblia Ni Kitabu Tofauti Kabisa!

Biblia Ni Kitabu Tofauti Kabisa!

‘Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida, ili mutu wa Mungu awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’​—2 TIMOTHEO 3:16, 17.

WATU fulani hawakubali maneno hayo. Wewe una mawazo gani juu ya Biblia? Unawaza Biblia ni:

• Kitabu kinachozungumuzia tu mambo mazuri?

• Kitabu kama vile vitabu vingine vitakatifu vya dini?

• Kitabu cha hadisi za kutunga zinazofundisha watu namna ya kuishi?

• Ao ni Neno la Mungu?

Kwa hiyo, ujiulize: Je, mambo ninayoamini juu ya Biblia ni ya kweli? Biblia yenyewe inasema hivi: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.” (Waroma 15:4) Kupitia maneno hayo, Biblia inaonyesha kama iliandikwa ili kutufundisha, kutufariji, na kutupatia tumaini.

Ikiwa Biblia ni kitabu kinachozungumuzia tu mambo mazuri ao ni kitabu kama vile vitabu vingine vitakatifu vya dini, je, ungekitumainia na kukubali kikufundishe na kuongoza familia yako, ikiwa habari iliyo ndani haipatane na mambo unayowazia kuwa sawa? Ikiwa Biblia ni kitabu cha hadisi za kutunga tu, unawaza ahadi zilizo ndani zingekufariji na kukupatia tumaini?

Lakini, ujue kama mamilioni ya watu ambao wamejifunza Biblia wanaamini kabisa kama Biblia ni Neno la Mungu. Sababu gani wanaamini hivyo? Ni nini kinachoifanya Biblia iwe tofauti na vitabu vingine vyote? Ili upate majibu ya maulizo hayo, tafazali, uchunguze mambo matano yanayozungumuziwa katika habari zinazofuata.