Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vitabu Vyote vya Biblia Vinapatana

Vitabu Vyote vya Biblia Vinapatana

Vitabu Vyote vya Biblia Vinapatana

“Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”​—2 PETRO 1:21.

SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Mara nyingi vitabu vya zamani vinapingana, hata ikiwa viliandikwa wakati mumoja. Ni vigumu kabisa vitabu vipatane ikiwa viliandikwa na watu tofauti, mahali tofauti, wakati tofauti. Lakini, ijapokuwa Biblia iliandikwa na watu tofauti, vitabu vyote 66 vilivyo ndani vina ujumbe wenye kupatana kwa sababu Mutu aliyeiandikisha ni mumoja.​—2 Timotheo 3:16.

KWA MUFANO: Katika kitabu cha kwanza cha Biblia, Musa, aliyekuwa muchungaji wa kondoo katika miaka ya 1 500 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, aliandika juu ya “uzao” ambao ungekuja kuokoa wanadamu. Baadaye, kitabu hicho kilitabiri kama uzao huo ungetokea katika kizazi cha Abrahamu, Isaka, na Yakobo. (Mwanzo 3:15; 22:17, 18; 26:24; 28:14) Miaka 500 hivi kisha hapo, nabii Nathani alionyesha kama uzao huo ungetokea katika kizazi cha mufalme Daudi. (2 Samweli 7:12) Miaka 1 000 baadaye, mutume Paulo alieleza kama uzao huo ungefanyizwa na Yesu na kikundi cha wafuasi wake waliochaguliwa. (Waroma 1:1-4; Wagalatia 3:16, 29) Mwishowe, katika mwaka wa 96 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mutume Yohana alitabiri katika kitabu cha mwisho cha Biblia kama wale wanaofanyiza uzao huo wangetoa ushahidi juu ya Yesu duniani, wangefufuliwa na kwenda mbinguni, na kutawala pamoja naye kwa miaka 1 000. Uzao huo unaoundwa na Yesu na wafuasi wake utamuharibu Shetani na kuokoa wanadamu.​—Ufunuo 12:17; 20:6-10.

YALE WACHUNGUZI WA MAMBO YA BIBLIA WANASEMA: Kisha kujifunza kwa uangalifu vitabu 66 vya Biblia, Louis Gaussen aliandika katika kitabu chake (Théopneustie ou Inspiration Plénière des Saintes Écritures) kama alishangazwa sana na “upatano wenye kuvutia wa kitabu hicho, kilichoandikwa na watu wengi, . . . ambao yaonekana walikuwa na kusudi moja, hata ikiwa hawakuelewa kusudi hilo, waliendelea kulifuatilia, mupaka wakatimiza kusudi hilo kubwa, ni kusema, ukombozi wa ulimwengu kupitia Mwana wa Mungu.”

UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine kilichoandikwa na watu tofauti tofauti karibu 40 katika kipindi cha miaka zaidi ya 1 500 ambacho kina ujumbe wenye kupatana kabisa? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 7]

Katika kitabu chake (THE PROBLEM OF THE OLD TESTAMENT), JAMES ORR aliandika hivi: “Maandishi hayo yanapokusanywa pamoja, yanakuwa kitabu kimoja chenye kuundwa vizuri . . . Hakuna kitabu kingine duniani kinachoweza kujilinganisha kabisa na kitabu hicho, ao kinachokikaribia.”