Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?

Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?

▪ Katika Biblia, Yesu aliwaamuru wafuasi wake hivi: ‘Kwa hiyo nendeni mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na kuwafundisha.’ (Mathayo 28:19, 20) Je, Wakristo wote wanapaswa kutii amri hiyo ya kuhubiri na kufundisha? Wafuasi wa kwanza wa Yesu walielewa kama wote walipaswa kufanya hivyo. Kwa mufano, mutume Petro alisema hivi: “[Yesu] alituagiza sisi tuwahubirie watu na kutoa ushahidi kamili.” (Matendo 10:42) Na mutume Paulo aliandika hivi: “Nimewekewa sharti. Kwa kweli, ole wangu mimi ikiwa sitangazi habari njema!”​—1 Wakorintho 9:16.

Si Paulo na Petro tu ndio walitii amri hiyo ya kuhubiri na kufundisha, lakini Wakristo wote wa wakati wa Yesu walifanya hivyo pia. Kazi ya kuhubiri ndio ilikuwa kazi ya lazima zaidi katika maisha yao. (Matendo 5:28-32, 41, 42) Leo, Mashahidi wa Yehova nao wanajikaza kufanya hivyo. Wanahubiri ujumbe uleule ambao Yesu alikuwa anahubiri, ni kusema, “ufalme wa mbinguni.”​—Mathayo 10:7.

Ni nani wanaopaswa kuhubiriwa ujumbe wa Ufalme? Yesu alionyesha kama ni watu wa mahali pote wanaopaswa kuhubiriwa. Aliwaambia wafuasi wake hivi: ‘Mutakuwa mashahidi wangu mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Matendo 1:8) Na alitabiri pia kama, mbele ya mwisho wa ulimwengu huu kuja, “habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi.” (Mathayo 24:14) Ndiyo sababu, Wakristo wa kwanza walijikaza kuhubiria watu wote. Hawakuhubiria tu watu waliofahamiana nao wala watu wasio na dini. (Wakolosai 1:23; 1 Timotheo 2:3, 4) Leo, Mashahidi wa Yehova nao wanajikaza kuhubiria kila mutu. *

Ni njia gani iliyo nzuri zaidi ya kukutana na watu wengi ili kuwahubiria ujumbe wa Ufalme? Yesu, alijua namna ya kukutana na watu wengi zaidi; ndiyo maana aliwatuma wafuasi wake katika miji, vijiji, na kwenye nyumba za watu. (Mathayo 10:7, 11, 12) Kisha kufa na kufufuka kwa Yesu, wafuasi wake waliendelea kuhubiri “nyumba kwa nyumba.” (Matendo 5:42) Kama Yesu, wao pia walihubiri mahali popote walipokuta watu. (Yohana 4:7-26; 18:20; Matendo 17:17) Leo, Mashahidi wa Yehova wanatumia pia njia hizo ili kuhubiria watu wote.

Yesu alionyesha kama si kila mutu atakayesikiliza ujumbe wa Ufalme. (Mathayo 10:14; 24:37-39) Je, hilo linapaswa kuwazuia Wakristo kuhubiri? Tuchukue mufano: Wazia uko katika kikundi cha kuokoa watu kisha mutetemeko mukubwa wa inchi. Je, utaacha kutafuta kwa sababu, kisha kutafuta kwa muda mufupi, mumepata watu wachache tu? Hapana, utaendelea kutafuta ikiwa tu kuna tumaini la kupata tena hata mutu mumoja. Yesu aliwaamuru wafuasi wake waendelee tu kuhubiri ikiwa kungali tumaini kama watu fulani watasikiliza habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 10:23; 1 Timotheo 4:16) Mashahidi wa Yehova wanawatafuta watu kama hao nyumba kwa nyumba. Kwa kufanya hivyo, wanaonyesha kama wanamupenda Mungu na majirani wao, ambao wanaweza kuokolewa ikiwa wanasikiliza ujumbe wa Ufalme.​—Mathayo 22:37-39; 2 Wathesalonike 1:8.

Gazeti ambalo unasoma sasa linakutolea ujumbe huo unaotoka katika Biblia. Lakini kama unapenda kupata habari zingine, tafazali, uzungumuze na Mashahidi wa Yehova wakati watakutembelea, ao uandikie wachapishaji wa gazeti hili.

[Maelezo ya chini]

^ Sasa, Mashahidi wa Yehova wanahubiri katika inchi 236. Mwaka jana, walihubiri saa 1 707 094 710 na waliongoza mafunzo ya Biblia 8 490 746 duniani pote.