Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko Thesalonike

Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko Thesalonike

Mapambano kwa Ajili ya Habari Njema Huko Thesalonike

Muji wa Thesalonike, unaoitwa leo Thessaloníki ao Salonika, ni muji wenye kuendelea ulio na bandari ao nafasi ambapo mashua zinaegesha, ngambo ya kaskazini-mashariki mwa inchi ya Ugiriki (ao Grèce). Muji huo ulikuwa wa lazima sana katika historia ya Wakristo wa wakati wa mitume, zaidi sana katika kazi ya kuhubiri ya Paulo, aliyekuwa mutume Mukristo kwa mataifa.​—MATENDO 9:15; WAROMA 11:13.

PAULO na Sila aliyesafiri pamoja naye, walifika huko Thesalonike katika mwaka wa 50 hivi. Walikuwa katika safari ya pili ya Paulo ya umisionere, na ilikuwa mara yao ya kwanza kufikisha habari njema juu ya Kristo katika eneo linaloitwa leo Ulaya.

Walipofika Thesalonike, ni wazi kama walikuwa wangali wanakumbuka namna walivyopigwa na kufungwa huko Filipi, muji mukubwa wa Makedonia. Ndiyo sababu wakati Paulo alipowatembelea Wathesalonike baadaye aliwaambia kama alikuwa amehubiri “habari njema ya Mungu kwa kupambana sana.” (1 Wathesalonike 2:1, 2) Je, hali ingekuwa nzuri zaidi huko Thesalonike? Namna gani watu wangepokea habari njema katika muji huo? Je, kazi ya kuhubiri ingekuwa na matokeo mazuri? Acheni tuzungumuzie kwanza historia ya muji huo wa zamani.

Historia Yenye Mivurugo

Jina Thesalonike lenyewe linatokana na maneno mawili ya Kigiriki yanayomaanisha pambano na ushindi. Watu wengi wanaamini kama katika mwaka wa 352, Mufalme Philippe II wa Makedonia, baba ya Alexandre le Grand, alishinda kabila fulani katika muji unaoitwa Thessalie, katikati ya Ugiriki. Wanasema kama ili kukumbuka ushindi huo, Mufalme alimupa binti yake mumoja jina la Thessalonice, ambaye baadaye aliolewa na Cassandre. Cassandre alitawala mahali pa Alexandre, ndugu ya Thessalonice. Katika mwaka wa 315 hivi, Cassandre alijenga muji upande wa mangaribi ya Rasi ya Chalcidique na akaupatia muji huo jina la bibi yake. Katika Thesalonike kulitokea kila mara vita muda wote wa historia yake yenye mivurugo.

Muji wa Thesalonike ulikuwa pia na utajiri mwingi. Ulikuwa na bandari ao nafasi moja nzuri ya kuegeshea mashua pembeni ya Bahari Égée. Wakati wa utawala wa Waroma, muji huo ulikuwa kwenye barabara kubwa inayoitwa Via Egnatia. Kwa sababu muji huo ulipatikana mahali penye kufaa, utawala wa Waroma uliona nafasi hiyo kuwa nafasi nzuri ya kufanyia biashara. Kwa miaka mingi, mataifa mengine kama vile Wagoti, Waslovani, Wafrank, Waturuki na wakaaji wa muji wa Venice walitamani sana muji huo kwa sababu ya utajiri wake. Wamoja kati yao walichukua muji huo kwa kutumia nguvu na kuua watu wengi. Acheni sasa tuzungumuzie matembezi ya Paulo katika muji huo wakati alianza mapambano kwa ajili ya habari njema.

Paulo Anafika Thesalonike

Kila mara, Paulo alipofika katika muji fulani, kwa kawaida alikuwa akizungumuza kwanza na Wayahudi kwa sababu wao walifahamu Maandiko. Kufanya hivyo kulimuwezesha kuanzisha mazungumuzo na kuwasaidia waelewe habari njema. Mutu fulani mwenye elimu anasema kama Paulo alizoea kufanya hivyo kwa sababu aliwahangaikia sana watu wa taifa lake ao alipenda kutumia Wayahudi na watu wengine wenye kumuogopa Mungu ili kuchochea Watu wa Mataifa wakubali habari njema.​—Matendo 17:2-4.

Ndiyo sababu, wakati Paulo alifika huko Thesalonike, aliingia kwanza katika sinagogi, na ‘[kufikiri na Wayahudi] kwa kutumia Maandiko, akieleza na [kuonyesha kabisa kwa kutaja maandiko] kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu, akisema: Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu ninayewatangazia ninyi.’​—Matendo 17:2, 3, 10.

Ujumbe wa Paulo ulitokeza ubishi kwa sababu alipenda kusaidia Wayahudi wamutambue Masiya na daraka lake. Wayahudi walitumaini kama Masiya atakuja kuwapigania ili kuwakomboa kutoka utawala wa Waroma. Kwa hiyo, wazo la kusema kama Masiya angeteseka na kufa halikupatana na tumaini lao. Ili kuwasaidia Wayahudi wakubali wazo hilo, Paulo “[alifikiri nao],” ‘akieleza,’ na ‘[kuonyesha kabisa kwa kutaja Maandiko]’​—huo ndio ufundi ambao mwalimu muzuri anatumia. * Lakini, je, wale waliomusikiliza Paulo walikubali mafundisho hayo mazuri?

Magumu na Matokeo Mazuri

Wayahudi fulani na Wagiriki wengi waliokubali dini ya Kiyahudi na pia “[wanawake wengi] wenye vyeo” walikubali ujumbe wa Paulo. Maneno “wanawake wenye vyeo” ni yenye kufaa kabisa kwa sababu katika Makedonia wanawake walikubaliwa kuwa na vyeo vya juu. Walipewa vyeo katika guvernema, walikuwa na mali, walipewa haki fulani za uanainchi na pia walikuwa wanafanya biashara. Hata monuma zilijengwa ili kuwatukuza wanawake. Katika Filipi, Lidia, mwanamuke mufanyabiashara alikuwa amekubali habari njema. Sasa katika Thesalonike pia wanawake wengi wenye vyeo walikubali habari njema, kwa mufano, mabinti wa familia zenye kuheshimika, wake wa watu wenye kujulikana sana.​—Matendo 16:14, 15; 17:4.

Kwa sababu watu wengi walikubali habari njema, Wayahudi wakawa na wivu sana. Wakajiunga na ‘wanaume waovu kati ya wazururaji wa sokoni na kufanyiza kikundi chenye gasia ili kuzusha fujo jijini.’ (Matendo 17:5) Watu hao walikuwa watu wa namna gani? Mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia alisema kama walikuwa “watu waliokuwa na mwenendo muchafu na wasiofaa kitu.” Alisema tena hivi: “Inaonekana kama hawakupendezwa hata kidogo na ujumbe wa Paulo; lakini walikuwa watu wanaokasirika haraka na walio tayari kutenda kwa ujeuri, kama vikundi vingine vyenye jeuri.”

Watu mbalimbali waliounda kikundi hicho “wakaishambulia nyumba ya Yasoni [aliyemukaribisha Paulo na Sila] na kuanza kujaribu kuwaleta mbele ya watu wenye kufanya [fujo].” Walipowakosa, wakaenda kwa watawala wa muji. “Wakamukokota Yasoni na akina ndugu fulani na kuwapeleka kwa watawala wa jiji, wakipaaza sauti hivi: ‘Watu hawa ambao wameipindua dunia inayokaliwa wapo hapa pia.’”​—Matendo 17:5, 6.

Muji wa Thesalonike ulikuwa na uhuru kwa sababu ulikuwa muji mukubwa wa Makedonia. Muji huo ulikuwa na guvernema iliyoundwa na baraza la muji, ambalo lilishugulikia mambo ya watu katika eneo. “Watawala wa jiji,” ao politarques, * walikuwa watu wenye vyeo vya juu, ambao walikuwa na daraka la kulinda amani na kushugulikia hali ambazo zingefanya Waroma wakuje na hivyo wapoteze mamlaka yao. Kwa sababu hiyo, wangehangaishwa sana kusikia kama amani ya muji wao ilivurugwa na watu hao “wanaozusha fujo.”

Kisha hapo Wakristo walishitakiwa tena jambo nzito sana. Tunasoma katika Biblia hivi: ‘Watu hawa wanapingana na maagizo ya Kaisari, wakisema kuna mufalme mwingine, Yesu.’ (Matendo 17:7) Kitabu kimoja kinasema kama kupitia maneno hayo, walisingizia Wakristo kama “wanaasi wafalme wa Roma na wanachochea watu pia waasi.” Jambo hilo waliloshitakiwa lilikuwa nzito sana kwa sababu, kulingana na kitabu hicho, wafalme wa Roma “hawakukubali jina la mufalme [mwingine] litajwe katika maeneo yote ambayo walikuwa wameshinda, isipokuwa wao wenyewe waruhusu jambo hilo.” Tena, kwa sababu Paulo alihubiri kama Yesu ni Mufalme, na kwa sababu ni watawala wa Roma ndio waliokuwa wamemuua Yesu kwa kumusingizia kama alichochea watu wamuasi Kaisari, hilo lilifanya ionekane kama shitaka hilo juu ya Paulo na wenzake lilikuwa la kweli.​—Luka 23:2.

Kwa hiyo, watawala wa muji walikasirika sana. Lakini, kwa sababu hakukuwa jambo lolote lililoonyesha kama mambo waliyoshitaki Wakristo yalikuwa ya kweli na kwa sababu hawakumupata Paulo, ‘baada ya kuchukua zamana ya kutosha kutoka kwa Yasoni na wale wengine wakawaacha waende zao.’ (Matendo 17:8, 9) Inawezekana zamana hiyo ni kiasi fulani cha feza ambacho Yasoni na Wakristo wengine walilipa kwa watawala wa muji ili kuwahakikishia kama Paulo atatoka katika muji na hatarudi tena ili kuzusha fujo. Labda Paulo alikuwa anakumbuka tukio hilo aliposema kama “Shetani aliizuia njia [yake]” ili asirudi tena katika muji huo.​—1 Wathesalonike 2:18.

Kwa sababu ya hali hiyo, Paulo na Sila walisafirishwa usiku na kwenda Beroya. Huko Beroya, kazi ya Paulo ilikuwa pia na matokeo mazuri, lakini hilo likawakasirisha Wayahudi waliomupinga huko Thesalonike. Wapinzani hao wakasafiri mupaka Beroya, safari ya kilometre 80, ili kuwachochea watu wamupinge Paulo. Bila kukawia, Paulo akaondoka na kwenda Athene, lakini huko pia aliendelea kupambana kwa ajili ya habari njema.​—Matendo 17:10-14.

Kutaniko Jipya na Mapambano

Jambo la kufurahisha ni hili: Kutaniko jipya lilianzishwa huko Thesalonike. Lakini, zaidi ya upinzani, Wakristo walipambana na matatizo mengine mengi katika muji huo. Waliishi katika muji uliojaa desturi za kipagani na walizungukwa na watu waliokuwa na mwenendo muchafu. Jambo hilo lilimuogopesha Paulo sana. Hangaiko lake lilikuwa ni hili: Ndugu zake katika muji huo watafanya nini ili kupambana na matatizo hayo?​—1 Wathesalonike 2:17; 3:1, 2, 5.

Wakristo huko Thesalonike walijua kama marafiki wao wa zamani wangewachukia na kuwakasirikia kwa sababu waliacha kujiunga nao katika mambo ya kidini na mambo mengine ya kujifurahisha yaliyofanywa katika muji. (Yohana 17:14) Tena, muji wa Thesalonike ulijaa mazabahu ya miungu ya wanainchi wa Ugiriki kama vile Zeus, Artemis, na Apollo, na pia miungu ya wakaaji wa Misri. Ibada ya Kaisari ilikuwa pia ya lazima, na watu wote wenye kujulikana na pia wakaaji wote wa muji walipaswa kushika desturi za ibada hiyo. Mutu aliyekataa kushiriki katika desturi za ibada hiyo alionekana kuwa anaasi utawala wa Roma.

Mara nyingi ibada ya sanamu ilifanya watu wajiingize katika mwenendo muchafu. Ibada ya Cabirusi, mungu mulinzi wa Wathesalonike; Dionisio na Afrodito; na Isisi mungu wa Misri zilifanana katika njia hii: desturi nyingi zilizofanywa wakati wa ibaba ya miungu hiyo yote zilijaa karamu za uasherati na ulevi. Tabia ya kukaa na mwanaume ao mwanamuke bila kufunga ndoa na umalaya (ukahaba) ilionwa kuwa jambo la kawaida tu. Na watu hawakuona kama uasherati ni zambi. Katika muji huo, watu waliiga kabisa tabia za Waroma. Juu ya jambo hilo, mutu fulani mwenye elimu anasema kama “kulikuwa wanaume na wanawake wengi katika muji ambao kazi yao ilikuwa tu kumutimizia kila mutu tamaa ambayo alikuwa nayo—na wale wanaojifunza tabia za watu walishauria watu kama hawapaswe kujizuia kutimiza tamaa zao.” Kwa hiyo, tunaweza kuelewa sasa sababu gani Paulo aliwashauria Wakristo wa muji huo ‘wajiepushe na uasherati’ na “hamu yenye tamaa ya ngono” na “uchafu.”​—1 Wathesalonike 4:3-8.

Walishinda Pambano

Wakristo katika muji wa Thesalonike walipaswa kupambana sana ao kupigana vita kwa ajili ya imani yao. Lakini, ijapokuwa walipingwa na kuteswa, ijapokuwa waliishi katika muji uliojaa desturi za kipagani na ijapokuwa walizungukwa na watu waliokuwa na mwenendo muchafu, Paulo aliwapongeza kwa sababu ya ‘kazi yao ya uaminifu, kazi yao ya jasho yenye upendo, na uvumilivu wao’ na kwa sababu walisaidia sana ili kueneza habari njema katika sehemu za mbali.​—1 Wathesalonike 1:3, 8.

Katika mwaka wa 303, Wakristo walianza kuteswa sana katika utawala wa Roma. Mutawala Muroma César Galère aliyekaa huko Thesalonike ndiye aliyeanzisha mateso hayo. Mutawala huyo alijenga majengo mazuri sana huko Thesalonike na mabomoko ya majengo hayo yangali mupaka leo. Waturiste wanaotembelea huko wanaona masalio ya majengo hayo.

Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiria majirani zao katika muji wa Thessaloníki, mara nyingi mbele ya majengo hayo yaliyojengwa na adui huyo mukubwa wa Wakristo. Hata ikiwa katika miaka ya 1900 kuna wakati ndugu waliteswa sana walipokuwa wakifanya kazi yao ya kuhubiri, sasa kuna makutaniko karibu 60 ya Mashahidi wa Yehova wanaofanya kazi kwa bidii. Bidii yao inaonyesha kama mapambano kwa ajili ya habari njema yaliyoanza tangu zamani hayajakwisha na Wakristo wanaendelea kuyashinda.

[Maelezo ya chini]

^ Labda Paulo alitaja maandiko ambayo leo ni Zaburi 22:7; 69:21; Isaya 50:6; 53:2-7; na Danieli 9:26.

^ Neno hili halikupatikana katika vichapo vya Kigiriki. Lakini, maandishi fulani yaliyo na neno hilo yalivumbuliwa katika Thesalonike. Kati ya maandishi hayo, kulikuwa yale yaliyoandikwa katika miaka ya 100 mbele ya Yesu kuzaliwa, na hilo linaonyesha kama kitabu cha Matendo kinasema kweli.

[Karte kwenye ukurasa wa 18]

(Ili kuona maelezo hayo, ona kitabu)

Via Egnatia

MAKEDONIA

Filipi

Amfipoli

Thesalonike

Beroya

THESSALIE

Bahari ya Égée

ATHENE

[Picha katika ukurasa wa 20, 21]

Juu: Thessaloníki leo

Chini: magaze na jengo la Waroma lililo na vyumba vya kuogea katika soko kubwa

[Picha katika ukurasa wa 21]

Jengo la Waroma la muviringo karibu na monuma ya mutawala Galère; sanamu ya César Galère; Mashahidi wanahubiri karibu na jengo la Galère

[Maneno ili kueleza mahali picha zilitokea, ukurasa wa 18]

Médaille: © Bibliothèque nationale de France; stone inscription: Thessalonica Archaeological Museum, copyright Hellenic Ministry of Culture and Tourism

[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 20]

Picha mbili za mwisho kushoto: 16th Ephorate of Prehistoric and Classical Antiquities, copyright Hellenic Ministry of Culture and Tourism

[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 21]

Picha ya katikati: Thessalonica Archaeological Museum, copyright Hellenic Ministry of Culture and Tourism