Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tia Kazi ya Yehova pa Nafasi ya Kwanza

Tia Kazi ya Yehova pa Nafasi ya Kwanza

Tia Kazi ya Yehova pa Nafasi ya Kwanza

‘Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako, wokovu wako muchana kutwa.’​—ZAB. 71:15.

UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

Ni mambo gani Noa, Musa, Yeremia, na Paulo walitia pa nafasi ya kwanza katika maisha yao?

Ni nini itakayokusaidia ujue namna ya kutumia maisha yako?

Sababu gani unakusudia kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza?

1, 2. (a) Mutu anaonyesha nini anapojitoa kwa Yehova katika sala na kubatizwa? (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na uamuzi ambao Noa, Musa, Yeremia, na Paulo walichukua katika maisha yao?

 MUTU anapojitoa kwa kwa Mungu katika sala na kubatizwa ili kuwa mufuasi wa Yesu, anafanya hatua ya maana sana katika maisha. Kujitoa kwa Mungu ili kufanya mapenzi yake ndio uamuzi wa lazima kuliko uamuzi mwengine wowote ambao mutu anaweza kuchukua katika maisha yake. Unapojitoa kwa Yehova ni kama vile unamuambia hivi: “Yehova, tangu sasa ninataka wewe uwe Bwana wangu, maana yake, uongoze maisha yangu yote. Mimi ni mutumishi wako. Ninapenda uniambie namna ninapaswa kutumia wakati wangu, nini ninapaswa kutia pa nafasi ya kwanza, na namna gani ninapaswa kutumia mali yangu na uwezo wangu mbalimbali.”

2 Hivyo ndivyo ulivyomuahidi Yehova ulipojitoa kwake katika sala na kubatizwa. Tunakushukuru sana kwa uamuzi wako. Uamuzi uliofanya ni muzuri na wenye hekima. Lakini, kwa kuwa ulimukubali Yehova kuwa Bwana wako, namna gani, unapaswa sasa kutumia wakati wako? Maisha ya Noa, Musa, Yeremia, na mutume Paulo yanaweza kukusaidia kujibu ulizo hilo. Wote walijitoa kwa nafsi yote katika kazi ya Yehova. Hali zetu zinafanana na hali zao. Uamuzi ambao walichukua ili kutia mambo ya lazima pa nafasi ya kwanza unaweza kutusaidia ili kuona namna tunavyotumia wakati wetu katika maisha.​—Mt. 28:19, 20; 2 Tim. 3:1.

MBELE YA GARIKA

3. Namna gani siku zetu zinalingana na siku za Noa?

3 Yesu alilinganisha siku za Noa na siku zetu. Yeye alisema hivi: ‘Kama vile siku za Noa zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa. Walikuwa wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiolewa, mupaka siku ambayo Noa aliingia ndani ya safina; nao hawakujali mupaka garika ikaja na kuwafagilia mbali wote.’ (Mt. 24:37-39) Watu wengi leo wanaishi bila kujali kama tunaishi wakati ambao inaomba kutenda kwa haraka. Hawajali maonyo yanayotolewa na watumishi wa Mungu. Kama ilivyokuwa katika siku za Noa, watu wengi leo wanacheka wanapohubiriwa kama karibuni Mungu atawaharibu watu wabaya. (2 Pet. 3:3-7) Lakini, namna gani Noa alitumia wakati wake ijapokuwa alizungukwa na watu wabaya?

4. Namna gani Noa alitumia wakati wake Yehova alipomupatia kazi ya kufanya, na sababu gani alitumia wakati wake hivyo?

4 Mungu alipomuambia Noa kama atawaharibu watu wabaya, alimupatia kazi ya kujenga safina ili watu na wanyama waokoke. (Mwa. 6:13, 14, 22) Tena Noa alitangaza hukumu ya Yehova iliyokuwa imekaribia sana. Mutume Petro anamuita Noa ‘muhubiri wa uadilifu.’ Hilo linaonyesha kama Noa alijikaza kuwaonyesha majirani wake hatari iliyokuwa mbele yao. (Soma 2 Petro 2:5.) Je, unafikiri lingekuwa jambo la hekima ikiwa Noa na familia yake wangetumia wakati wao wote ili kutafuta kuendelea katika mambo ya biashara, kutafuta kuwashinda wengine, ao kutafuta kuwa na maisha ya raha? Bila shaka, hapana! Hawakuruhusu mambo hayo yawakengeushe kwa sababu walijua hatari iliyokuwa mbele yao.

MAMBO AMBAYO MUSA ALICHAGUA

5, 6. (a) Sababu gani Musa alifundishwa hekima yote ya Wamisri? (b) Sababu gani Musa alikataa kuishi kama mwana wa mufalme wa Misri?

5 Acheni tuzungumuzie sasa maisha ya Musa. Musa alikomalia katika nyumba ya mufalme wa Misri, kwa kuwa binti ya Farao alimulea kama mutoto wake. Alipokuwa kijana, mwana huyo wa mufalme alifundishwa “hekima yote ya Wamisri.” (Mdo. 7:22; Kut. 2:9, 10) Labda alifundishwa hivyo ili kumutayarisha atumike katika makao ya Farao. Musa angekuwa mutu mukubwa sana katika serikali kubwa duniani wakati huo, angepata mali nyingi, vitu vingi vizuri, mapendeleo mengi na angeheshimiwa sana. Je, Musa alikaza akili yake juu ya mambo hayo?

6 Wazazi wa Musa walimufundisha mambo mengi juu ya Yehova alipokuwa angali mudogo sana. Kwa hiyo, Musa alijua ahadi ambazo Mungu alitolea mababu zake Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Musa aliamini ahadi hizo. Alifikiri sana juu ya wakati wake ujao na namna gani angeweza kuwa mwaminifu kwa Yehova. Kwa hiyo, wakati ulipofika ili Musa achague ikiwa ataishi kama mwana wa mufalme ao kuishi kama mutumwa pamoja na Waisraeli wenzake, alichagua nini? Musa alichagua ‘kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia zambi kwa muda.’ (Soma Waebrania 11:24-26.) Kisha, alifuata uongozi wa Yehova ili kujua namna gani angetumia maisha yake. (Kut. 3:2, 6-10) Sababu gani Musa alifanya hivyo? Kwa sababu aliamini ahadi za Mungu. Alitambua kama mambo yote ambayo angepata katika Misri ni ya muda. Kwa kweli, hakudanganyika, kwa sababu kisha muda fulani Mungu alileta mapigo kumi juu ya Misri. Sisi, watumishi wa Yehova waliojitoa kwake, tunaweza kujifunza nini kutokana na mufano wa Musa leo? Badala ya kufuatilia tu kazi za kimwili na raha za ulimwengu huu, tunapaswa kutia Yehova na kazi yake pa nafasi ya kwanza.

YEREMIA ALIJUA MAMBO AMBAYO YANGETOKEA

7. Namna gani hali ya Yeremia inafanana na hali yetu?

7 Mutu mwengine aliyetia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yake ni nabii Yeremia. Yehova alimuchagua awe nabii wake ili atangaze ujumbe wa hukumu juu ya wakaaji waasi-imani wa Yerusalemu na Yuda. Tunaweza kusema kama Yeremia aliishi pia “katika siku za mwisho.” (Yer. 23:19, 20) Alijua vizuri kabisa kama ulimwengu wa wakati wake ungefikia mwisho.

8, 9. (a) Kwa nini Baruku alipaswa kubadilisha mawazo yake? (b) Tunapaswa kufikiria nini tunapofanya mipango fulani kwa ajili ya wakati ujao?

8 Mambo ambayo Yeremia aliamini yalimuzuia kufanya nini? Hakutafuta kuwa na maisha mazuri katika ulimwengu ambao ulikuwa karibu kuharibiwa. Ikiwa angefanya hivyo, lingekuwa jambo la upumbavu kabisa. Hata hivyo, mwandishi wake Baruku, alikuwa na mawazo tofauti. Kwa hiyo, Mungu alimutuma Yeremia amuambie Baruku hivi: ‘Tazama! Kile ambacho nimekijenga ninakibomoa, na kile ambacho nimekipanda ninakingoa, ndiyo, inchi yote. Na wewe unaendelea kujitafutia makuu. Usiendelee kuyatafuta. Kwa maana, tazama, ninaleta musiba juu ya wote wenye mwili, asema Yehova, nami nitakupa wewe nafsi yako kuwa nyara katika mahali pote utakapoenda.’​—Yer. 45:4, 5.

9 Ni mambo gani “makuu” ambayo Baruku aliendelea kutafuta? Hatujui. * Lakini, tunajua kama ni mambo ambayo yangeharibiwa wakati Wababiloni wangeshambulia Yerusalemu katika mwaka wa 607 mbele ya Yesu. Historia hii inatufundisha nini? Bila shaka, ili tupate mahitaji ya lazima tunapaswa kufanya mipango fulani. (Met. 6:6-11) Lakini, je, ni jambo la hekima kutumia wakati mwingi na nguvu zetu zote ili kutafuta vitu ambavyo havitadumu? Ni kweli kwamba tengenezo la Yehova linaendelea kufanya mipango kwa ajili ya wakati ujao kwa kujenga Majumba ya Ufalme, Beteli, na kwa kufanya mipango mingine ya kiteokrasi. Lakini, mipango hiyo ni ya lazima sana kwa sababu inasaidia faida za Ufalme zisonge mbele. Ni jambo la hekima kwamba watumishi wote wa Yehova waliojitoa kwake wafikirie kuendeleza faida za Ufalme wanapofanya mipango kwa ajili ya wakati ujao. Je, unaamini kabisa katika moyo wako kama ‘unaendelea kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu [wa Yehova]’?​—Mt. 6:33.

“NAVIONA KUWA TAKATAKA NYINGI”

10, 11. (a) Paulo alifuatilia mambo gani mbele ya kuwa Mukristo? (b) Ni nini kilichomusaidia Paulo abadilishe kabisa mipango yake katika maisha?

10 Tuzungumuzie sasa mufano wa Paulo. Mbele ya kuwa Mukristo, ilionekana kama Paulo angeweza kuwa na kazi nzuri sana katika maisha yake. Alifundishwa sheria ya Kiyahudi na Gamalieli, mwalimu aliyejulikana sana wakati huo. Alipewa mamlaka na kutumainiwa sana na kuhani mukubwa wa Wayahudi. Tena, alikuwa akifanya maendeleo makubwa zaidi katika dini ya Kiyahudi kuliko watu wengine wa wakati wake. (Mdo. 9:1, 2; 22:3; 26:10; Gal. 1:13, 14) Hata hivyo, mambo hayo yote yalibadilika wakati Paulo alitambua kama taifa la Wayahudi halikuwa tena lenye kukubaliwa na Yehova.

11 Paulo alitambua kama kazi ambayo angefuatilia katika ulimwengu wa Kiyahudi haingekuwa na faida yoyote tena mbele za Yehova; na haingedumu. (Mt. 24:2) Mutume huyo aliyekuwa Farisayo hapo zamani, alipoelewa kusudi la Mungu na umaana wa pendeleo la kuhubiri, alisema kama mambo yote ambayo hapo zamani aliona kuwa ya lazima aliyaona sasa kuwa “takataka nyingi.” Kwa hiyo, Paulo aliacha dini ya Kiyahudi na faida zake zote, akatumia maisha yake yote ili kuhubiri habari njema ya Ufalme.​—Soma Wafilipi 3:4-8, 15; Mdo. 9:15.

CHUNGUZA MIPANGO YAKO

12. Namna gani Yesu alitumia maisha yake kisha kubatizwa?

12 Noa, Musa, Yeremia, Paulo, na wengine wengi, walitumia karibu maisha yao yote na nguvu zao katika utumishi wa Yehova. Wao ni mifano mizuri na tunapaswa kuwaiga. Bila shaka, mufano muzuri zaidi kushinda wale wote waliojitoa kwa Yehova ni Yesu. (1 Pet. 2:21) Kisha kubatizwa, Yesu alitumia maisha yake yote katika kazi ya kuhubiri na kumutukuza Yehova. Kwa hiyo Mukristo anayekubali kabisa kama Yehova ndiye Bwana wake, anapaswa kuelewa kama kumutumikia Yehova ndilo jambo la kuweka pa nafasi ya kwanza katika maisha yake. Je, unafanya hivyo? Namna gani tunaweza kutia utumishi wetu kwa Yehova pa nafasi ya kwanza na wakati huohuo kufanya kazi zetu za kimwili?​—Soma Zaburi 71:15; 145:2.

13, 14. (a) Watumishi wote waliojitoa kwa Yehova na kubatizwa wanatiwa moyo kufanya nini? (b) Watu wa Yehova wanaweza kupata furaha gani?

13 Kwa miaka mingi, tengenezo la Yehova limeendelea kuwatia moyo watumishi wote wa Yehova waliobatizwa waone kama wanaweza kufanya kazi ya upainia na wasali kwa ajili ya jambo hilo. Ni kweli kwamba watumishi wengine waaminifu wa Yehova hawawezi kuhubiri saa 70 kila mwezi, kwa sababu hali haziwaruhusu. Hawapaswi kuvunjika moyo kwa sababu ya jambo hilo. (1 Tim. 5:8) Lakini, wewe unawaza nini? Je, unawaza kama ni vigumu kwako kuwa painia?

14 Fikiria furaha ambayo watumishi wengi wa Yehova walipata katika kipindi cha Ukumbusho mwaka huu. Katika mwezi wa 3, kulikuwa mupango fulani wa pekee uliotolea wahubiri uwezekano wa kuwa mapainia wasaidizi kwa kuhubiri saa 30 ao 50. (Zab. 110:3) Wengi walifanya kazi ya upainia musaidizi, na hilo lilitokeza furaha sana katika makutaniko. Je, unaweza kufanya mipango ili ushiriki mara nyingi katika kazi ya upainia? Mukristo yeyote aliyejitoa kwa Yehova anapofanya kazi ya upainia, jambo hilo linamupatia furaha nyingi, na mwishoni mwa kila siku anaweza kumwambia Yehova hivi: “Yehova, mimi nimefanya yote ambayo ningeweza kufanya katika utumishi wako.”

15. Ni muradi gani ambao kijana Mukristo anapaswa kujitilia kuhusu masomo?

15 Ikiwa unakaribia kumaliza masomo, labda una afya nzuri na hauna madaraka mengi. Je, umefikiria kwa uzito uwezekano wa kuwa painia? Bila shaka, walimu wako wanaweza kukutia moyo usome mingi ili upate kazi nzuri; wanapokuambia hivyo wao wanawaza kama wanatafuta faida yako. Lakini, kumbuka kama wao wanafikiria tu mipango ya wanadamu na feza. Kumbuka kama mambo hayo hayatadumu. Lakini, wewe ukifuatilia miradi ya kiroho, utakuwa umetumia maisha yako vizuri na utapata baraka za milele. Na hilo litaonyesha kama unafuata kabisa mufano wa Yesu. Huo ni uamuzi wa hekima; utakuletea furaha na utakulinda. Tena kuchukua uamuzi huo, kunaonyesha kama unataka kuishi kulingana na naziri uliyofanya ya kumutumikia Yehova.​—Mt. 6:19-21; 1 Tim. 6:9-12.

16, 17. Ni maulizo gani tunayoweza kujiuliza kuhusu kazi ya kimwili na mambo mengine tunayofuatilia?

16 Leo, watumishi wengi wa Mungu wanatumika saa nyingi ili kupata mahitaji ya lazima ya familia yao. Lakini, wengine wanatumika saa nyingi hata ikiwa si lazima. (1 Tim. 6:8) Wafanya-biashara wanafanya yote wawezayo ili kutusadikisha kama hatuwezi kuishi ikiwa hatununue vitu vingi na vya kisasa wanavyotengeneza. Lakini, Wakristo wa kweli hawapaswi kuacha ulimwengu wa Shetani uwaambie mambo ya lazima ambayo wanapaswa kufanya. (1 Yoh. 2:15-17) Na kwa wale wanaoacha kazi kwa sababu ya kuzeeka, njia nzuri zaidi ya kutumia wakati wao ni kufanya kazi ya upainia; hilo litaonyesha kama wanatia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza.

17 Watumishi wote waliojitoa kwa Yehova wanaweza kujiuliza hivi: Ni mambo gani ninayotia pa nafasi ya kwanza katika maisha yangu? Je, ninatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza? Je, ninamuiga Yesu kwa kuwa na roho ya kujinyima? Je, ninatii shauri la Yesu la kuendelea kumufuata sikuzote? Je, ninaweza kupanga vizuri programu yangu ili nipate wakati mwingi wa kuhubiri Ufalme ao kufanya mambo mengine ya kiroho? Hata ikiwa hali zangu haziniruhusu kwa sasa kuhubiri zaidi, je, ninaendelea kukomalisha roho ya kujinyima?

‘KUWA NA NIA NA KUTENDA’

18, 19. Tunaweza kusali kwa ajili ya jambo gani, na sababu gani sala hiyo itamupendeza Yehova?

18 Ni jambo lenye kupendeza sana kuona namna watu wa Mungu wanavyomutumikia kwa bidii. Lakini, labda wengine hawana nia ya kufanya kazi ya upainia, ao wanafikiri hawastahili hata ikiwa hali zao zinawaruhusu kufanya kazi ya upainia. (Kut. 4:10; Yer. 1:6) Utafanya nini ikiwa hauna nia hiyo? Ingelikuwa vizuri kusali kwa ajili ya jambo hilo, sivyo? Bila shaka. Paulo aliwaambia waamini wenzake kama Yehova, ‘kwa ajili ya mapenzi yake mema, anatenda ndani yao ili wao wawe na nia na kutenda pia.’ (Flp. 2:13) Ikiwa unawaza kama hauna nia ya kuhubiri zaidi, muombe Yehova akupe nia hiyo na uwezo wa kufanya hivyo.​—2 Pet. 3:9, 11.

19 Noa, Musa, Yeremia, Paulo, na Yesu walikuwa wamejitoa kwa Mungu. Kwa hiyo, walitumia wakati wao na nguvu yao ili kutangaza maonyo ya Yehova. Hawakuacha mambo ya ulimwengu yawakengeushe. Mwisho wa ulimwengu huu unakaribia, kwa hiyo, sisi wote ambao tumejitoa kwa Mungu tunapaswa kuhakikisha kama tunaendelea kujikaza na kufuata mifano ya watumishi hao wa Mungu. (Mt. 24:42; 2 Tim. 2:15) Tukifanya hivyo, tutamupendeza Yehova na tutapata baraka nyingi.​—Soma Malaki 3:10.

[Maelezo ya chini]

^ Soma kitabu Mungu Asema Nasi Kupita Yeremia, ukurasa wa 104-106.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 21]

Watu hawakumusikiliza Noa

[Picha katika ukurasa wa 24]

Je, umekwisha kufikiria kwa uzito ikiwa unaweza kuwa painia wa kawaida?