Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Waliongozwa na Roho Takatifu’

‘Waliongozwa na Roho Takatifu’

‘Waliongozwa na Roho Takatifu’

“Unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”​—2 PET. 1:21.

FIKIRIA MAULIZO HAYA

Namna gani ujumbe wa Mungu uliotumwa kupitia roho takatifu uliwafikia waandikaji wa Biblia?

Ni mambo gani yanayokusadikisha kama Biblia ilioongozwa na roho ya Mungu?

Unaweza kufanya nini ili uendelee kupendezwa na Neno la Mungu?

1. Kwa nini tunahitaji Neno la Mungu, Biblia?

 DUNIANI pote, watu wengi wanajiuliza maulizo haya: Tunatoka wapi? Sababu gani tuko hapa duniani? Tunaenda wapi? Kwa nini dunia iko hivi? Tunakuwa namna gani tunapokufa? Hatungekuwa na Neno la Mungu, Biblia, je, tungepata majibu ya maulizo hayo na mengine ya maana? Hatungekuwa na Biblia, tungefundishwa tu kupitia mambo tunayojionea katika maisha. Je, mambo tunayojionea katika maisha yanaweza kweli kutufundisha na kutufanya tujisikie kama mutunga-zaburi alivyojisikia kuhusu “sheria ya Yehova”?​—Soma Zaburi 19:7.

2. Ni nini inayoweza kutusaidia ili tuendelee kupendezwa na Biblia, zawadi ya lazima sana ambayo Mungu ametutolea?

2 Hata hivyo, inasikitisha kuona kama watu wengi hawana tena upendo ambao walikuwa nao hapo zamani walipojifunza kweli ya Biblia. (Linganisha na Ufunuo 2:4.) Hawaishi tena maisha yanayomupendeza Mungu. (Isa. 30:21) Tusiruhusu jambo hilo litufikie. Tunaweza na tunapaswa kuendelea kupendezwa na Biblia na mafundisho yake. Biblia ni zawadi ya lazima sana ambayo Muumbaji wetu mwenye upendo ametutolea. (Yak. 1:17) Ni nini inayoweza kutusaidia ili tuendelee kupendezwa na “neno la Mungu”? Kufikiria namna waandikaji wa Biblia walivyoongozwa na roho ya Mungu ili kuiandika, kunaweza kutusaidia. Hilo linamaanisha pia, kuchunguza mambo mengi yanayoonyesha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Kufanya hivyo kutatuchochea kusoma Neno la Mungu kila siku na kutumikisha mashauri yake katika maisha yetu.​—Ebr. 4:12.

NAMNA “WALIVYOONGOZWA NA ROHO TAKATIFU”

3. Biblia inamaanisha nini inaposema kama manabii na waandikaji wa Biblia ‘waliongozwa na roho takatifu’?

3 Biblia iliandikwa na wanaume 40 hivi, kwa kipindi cha miaka zaidi ya 1 610 kuanzia mwaka wa 1513 mbele ya Kristo mupaka mwaka wa 98 kisha Kristo. Wengine walikuwa manabii ‘walioongozwa na roho takatifu.’ (Soma 2 Petro 1:20, 21.) Maneno ya Kigiriki yanayotafsiriwa “kuongozwa na” yanamaanisha “kuchukua ao kubeba kutoka mahali fulani mupaka mahali pengine” na “yanaweza tena kumaanisha: kuchukuliwa, kusukumwa, kujiacha kuchukuliwa.” * Andiko la Matendo 27:15 linatumia usemi kama huo linapozungumuzia mashua iliyoshikwa na kuchukuliwa ao kusukumwa na upepo. Biblia inaposema kama manabii na waandikaji wa Biblia ‘waliongozwa na roho takatifu’ inamaanisha kama Mungu alizungumuza nao, aliwachochea na aliwaongoza kupitia nguvu yake ya utendaji. Kwa hiyo, mambo waliyoandika si mawazo yao, lakini ni mawazo ya Mungu. Wakati fulani, manabii na waandikaji hao hawakuelewa hata maana ya mambo waliyokuwa wakitabiri ao mambo waliyokuwa wakiandika. (Dan. 12:8, 9) Kwa kweli, “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu” na halina mawazo ya wanadamu.​—2 Tim. 3:16.

4-6. Yehova aliwatolea waandikaji wa Biblia ujumbe wake namna gani? Toa mufano.

4 Namna gani ujumbe uliotumwa kupitia roho takatifu uliwafikia waandikaji wa Biblia? Je, Mungu aliwapa maneno fulani ya kuandika ao aliwatolea tu mawazo ambayo walipaswa kuandika kwa kutumia maneno yao? Fikiria namna bwana fulani wa kazi anavyoweza kuandika barua. Ikiwa anataka barua yake iandikwe kwa maneno fulani ya pekee, anaweza kuandika barua hiyo yeye mwenyewe ao kumuambia sekretere wake aandike neno kwa neno mawazo yake. Sekretere atakapomaliza kuandika, bwana wa kazi atatia sinyatire yake juu ya barua hiyo. Wakati mwengine, bwana huyo wa kazi anaweza tu kumuambia sekretere mawazo fulani ya lazima, kisha sekretere atachagua namna ya kuandika barua hiyo, na maneno atakayotumia. Mbele ya kuituma, bwana wa kazi anaweza kuisoma na kumuambia sekretere abadili mambo fulani. Mwishowe, atatia sinyatire yake juu ya barua hiyo na yule atakayeisoma atajua kama inatoka kwa bwana huyo wa kazi.

5 Vivyo hivyo, sehemu fulani za Biblia ziliandikwa “kwa kidole cha Mungu.” (Kut. 31:18) Pia, wakati fulani Yehova alimuambia muandikaji moja kwa moja yale anayopaswa kuandika alipoona kwamba maneno fulani hayapaswe kubadilishwa. Kwa mufano, tunasoma hivi katika andiko la Kutoka 34:27: ‘Yehova akaendelea kumuambia Musa: Jiandikie maneno haya, kwa sababu ninafanya agano pamoja nawe na Israeli kupatana na maneno haya.’ Tena, Yehova alimuambia nabii Yeremia hivi: “Andika katika kitabu maneno yote nitakayokuambia.”​—Yer. 30:2.

6 Hata hivyo, mara nyingi, Mungu alitia kimuujiza katika mioyo na akili ya waandikaji mawazo kuliko maneno fulani ya pekee; hilo liliwasaidia kuchagua maneno yao wenyewe ili kuandika mawazo hayo. Andiko la Mhubiri 12:10 linasema hivi: ‘Mukutanishaji alijitahidi kutafuta maneno yenye kupendeza na kuandika maneno sahihi ya kweli.’ Mwandikaji wa Injili, Luka ‘alifuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi, kuandika hayo kwa utaratibu wenye kufuatana.’ (Lu. 1:3) Roho takatifu ya Mungu ilizuia kutokamilika kwa wanadamu kusiharibishe ujumbe wake.

7. Kutumia wanadamu ili kuandika Biblia kunaonyesha namna gani hekima ya Mungu?

7 Kutumia wanadamu ili kuandika Biblia kunaonyesha waziwazi hekima kubwa ya Mungu. Maneno hayatujulishi tu habari fulani, lakini pia namna mwandikaji anavyojisikia. Namna gani ikiwa Yehova angetumia malaika kuandika Biblia? Je, wangeweza kuandika kabisa namna watu wanavyojisikia wanapokuwa na furaha, woga, huzuni, na kuvunjika moyo? Kwa kuruhusu wanadamu wasio wakamilifu wachague maneno watakayotumia ili kuandika mawazo waliyopokea kupitia roho takatifu, jambo hilo limefanya ujumbe wa Mungu uwe wenye kugusa moyo, wenye kuonyesha namna wanadamu wanavyojisikia katika hali fulani na pia ujumbe huo hauchokeshi kwa sababu hautumie maneno yale yale.

KWA NINI TUAMINI JAMBO HILO?

8. Kwa sababu gani tunaweza kusema kama Biblia ni tofauti na vitabu vingine vya kidini?

8 Kuna ushuhuda mwingi unaoonyesha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Hakuna kitabu kingine cha dini kinachotusaidia kumujua Mungu kama Biblia. Kwa mufano, vitabu vya Wahindu vinatia ndani nyimbo za ibada za Vedi, vitabu vilivyo na maelezo yanayofasiriya nyimbo hizo, mawazo ya kifilozofia yanayoitwa Upanishadi, na hadisi za Wahindu zinazopendwa sana zinazoitwa Ramayana na Mahabharata. Kitabu Bhagavad Gita ni sehemu ya Mahabharata na kinazungumuzia maagizo juu ya mwenendo. Wabuddha wana vitabu vinavyoitwa Tipitaka (Vitabu vitatu), kitabu kimoja kinazungumuzia zaidi sana sheria na kanuni za watawa wanaume na wanawake. Kitabu kingine kinazungumuzia hasa mafundisho ya Dini ya Buddha. Kitabu cha tatu kinazungumuzia mafundisho, na mezali zilizotolewa na Buddha. Buddha hakujiita mungu, na alisema mambo machache juu ya Mungu. Maandishi ya Dini ya Confucius ni muchanganyiko wa mambo yaliyotokea zamani, sheria juu ya mwenendo, namna ya kufanya uchawi na nyimbo. Ni kweli kwamba kitabu kitakatifu cha Waislamu kinazungumuzia imani katika Mungu mumoja na kinaonyesha kama Mungu anajua mambo yote na anaweza kutabiri mambo yatakayotokea wakati ujao, lakini kitabu hicho hakizungumuzie hata jina la Mungu, Yehova, linalopatikana mahali pengi katika Biblia.

9, 10. Ni mambo gani tunayoweza kujifunza juu ya Mungu katika Biblia?

9 Vitabu hivyo vya dini vinazungumuzia mambo machache sana juu ya Mungu, lakini Biblia inatusaidia kumujua Yehova Mungu na kazi zake. Inatusaidia kuelewa sifa zake mbalimbali. Inatufundisha kama Mungu ni mwenye nguvu zote, mwenye hekima, mwenye haki, lakini pia ni Mungu anayetupenda. (Soma Yohana 3:16; 1 Yohana 4:19.) Zaidi ya hayo, Biblia inatuambia: ‘Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.’ (Mdo. 10:34, 35) Leo, kila mutu anaweza kupata Biblia. Hilo linaonyesha kama Mungu hana ubaguzi. Watu waliojifunza mambo ya luga wanaonyesha kama leo kuna luga karibu 6 700 duniani. Na wanaonyesha kama 90 % ya watu duniani wanazungumuza luga 100 kati ya luga hizo. Lakini, Biblia imetafsiriwa ikiwa nzima ao sehemu katika luga zaidi ya 2 400. Kwa hiyo, karibu kila mutu duniani anaweza kusoma sehemu ya Biblia ao yote nzima katika luga yake.

10 Yesu alisema hivi: ‘Baba yangu anaendelea kufanya kazi mupaka sasa, na mimi ninaendelea kufanya kazi.’ (Yoh. 5:17) Biblia inasema hivi: ‘Tangu wakati usio na kipimo mupaka wakati usio na kipimo Yehova ni Mungu.’ Kwa hiyo, Yehova ametimiza mambo mengi sana. (Zab. 90:2) Ni Biblia tu inayotujulisha kazi za Mungu za wakati wa zamani na za sasa na inatufunulia mambo atakayofanya wakati ujao. Tena, inatufundisha mambo yanayomupendeza Mungu na yale yanayomuchukiza, na inatuonyesha namna ya kumukaribia Mungu. (Yak. 4:8) Kwa hiyo basi, tusiruhusu mambo tunayofuatilia maishani ao mahangaiko yetu yatutenganishe na Yehova.

11. Ni nini inayoonyesha kama Biblia ina hekima nyingi na ni yenye kutegemeka?

11 Hekima nyingi na yenye kutegemeka inayopatikana katika Biblia inaonyesha pia kama kitabu hicho kilitoka kwa Mutu aliye na hekima kuliko mwanadamu. Mutume Paulo aliuliza hivi: ‘Ni nani ameijua akili ya Yehova, ndipo amufundishe?’ (1 Kor. 2:16) Andiko hilo linatukumbusha ulizo ambalo nabii Isaya aliuliza watu wa siku zake: ‘Ni nani ambaye ameipima roho ya Yehova, na ni nani kama mutu wake wa mashauri anayeweza kumujulisha jambo lolote?’ (Isa. 40:13) Bila shaka, hakuna mutu anayeweza kufanya hivyo. Kwa hiyo haishangaze kuona mutu akipata matokeo mazuri wakati anatumia mashauri ya Biblia kuhusu ndoa, kulea watoto, viburudisho, kuchagua marafiki, bidii katika kazi, kuwa mwaminifu, na kuwa na mwenendo safi. Biblia haiwezi hata kidogo kutupatia mashauri mabaya. Lakini, wanadamu hawana hekima ya kutosha ili kutoa mashauri mazuri. (Yer. 10:23) Mara kwa mara mashauri yao yanabadilika wanapotambua kama walidanganyika hapo mbele. Biblia inasema kama ‘fikira za wanadamu, ni kama pumuzi.’​—Zab. 94:11.

12. Namna gani watu wamejaribu kuiangamiza Biblia?

12 Jambo lingine lenye kuonyesha kama Mungu wa kweli ndiye aliyeiandikisha Biblia ni hili: Watu wamefanya namna yote ili kuiangamiza Biblia lakini hawakuweza. Katika mwaka wa 168 mbele ya Kristo, Mufalme wa Siria Antiokisi wa ine, alijaribu kutafuta vitabu vyote vya Sheria vilivyoongozwa na roho ya Mungu ili vichomwe. Katika mwaka wa 303 kisha Kristo, mutawala wa Roma Dioclétien, aliamuru watu wabomoe kila mahali Wakristo walikuwa wakifanyia mikutano na kuchoma Biblia zao. Hali hiyo iliendelea kwa kipindi cha miaka kumi hivi. Kisha kipindi cha kuanzia mwaka wa 1001, mapapa Wakatoliki walifanya nguvu yao yote ili Biblia isifundishwe; walikataza Biblia isitafsiriwe katika luga za watu wa kawaida. Shetani na watu wake walijaribu kuangamiza Biblia lakini walishindwa. Yehova hakuruhusu mutu yeyote aangamize zawadi yake aliyotolea wanadamu.

MAMBO AMBAYO YAMEWASADIKISHA WENGI

13. Ni mambo gani mengine yanayoonyesha kama Biblia imeongozwa na roho ya Mungu?

13 Mambo mengine yanayoonyesha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu ni haya: Biblia haijipinge, inapozungumuzia juu ya sayansi haidanganyike, unabii wake mwingi umetimia, waandikaji wake hawakuficha makosa yao, ina uwezo wa kubadili maisha ya watu, inapozungumuzia mambo ya historia, ina habari za kweli, si mambo ya kuwazia​-wazia tu, na inatoa majibu yenye kutosheleza ya maulizo yaliyo katika paragrafe ya 1. Basi, tuchunguze mambo yaliyowasadikisha watu fulani kama Biblia ni kitabu kilichotoka kwa Mungu.

14-16. (a) Ni nini iliyosadikisha Muislamu, Muhindu, na mutu anayeamini kwamba mambo ya Mungu hayawezi kujulikana, kama Biblia ilitoka kwa Mungu? (b) Ni jambo gani unalotumia katika mahubiri ili kuwaonyesha watu kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu?

14 Anwar * alikomalia katika dini ya Kiislamu katika inchi moja ya Mashariki ya Kati. Mashahidi wa Yehova walimutembelea alipokuwa akiishi kwa muda katika Amerika ya Kaskazini. Anwar anasema hivi: “Wakati huo nilikuwa sipendi dini za Kikristo kwa sababu nilikuwa nimesikia kama dini hizo zilimuanga damu nyingi sana hapo zamani, na namna watu wengi waliuawa kisha kuhukumiwa na Baraza lililokuwa likiwahukumu wale waliopinga mafundisho ya dini. Hata hivyo, nilikubali funzo la Biblia kwa sababu mimi ni mutu anayetaka kujua ukweli wa mambo.” Kisha muda fulani, Anwar alirudi kwao na hakuweza kuendeleza mazungumuzo tena na Mashahidi wa Yehova. Miaka mingi baadaye, Anwar alihamia Ulaya na huko alianza tena kujifunza Biblia. Mwishowe alisema hivi: “Nimesadiki kama Biblia ni Neno la Mungu kwa sababu ya mambo haya: unabii wa Biblia unatimia kabisa, jambo kuu la Biblia linazungumuziwa tangu mwanzo mupaka mwisho, haijipinge, na kwa sababu waabudu wa Yehova wanapendana.” Anwar alibatizwa katika mwaka wa 1998.

15 Asha ana miaka 16 na alikomalia katika familia ya Wahindu. Anasema hivi: “Nilikuwa nikisali wakati tu nilikuwa nikienda kwenye hekalu ao wakati nilikuwa na magumu, lakini sikuwaza juu ya Mungu wakati maisha yangu yalikuwa bila magumu. Lakini, Mashahidi wa Yehova waliponitembelea, maisha yangu yalibadilika kabisa.” Asha alijifunza Biblia na akaanza urafiki pamoja na Mungu. Ni nini kilichomusadikisha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu? Asha anaeleza: “Biblia ilijibu maulizo yangu yote. Ilinisaidia kuwa na imani kama Mungu yuko bila kumuona, ni kusema, bila kwenda kwenye hekalu na bila kuinamia sanamu.”

16 Paula alilelewa katika dini ya Katoliki, lakini alipokomaa, alianza kuamini fundisho linalosema kama mambo ya Mungu hayawezi kujulikana. Kisha jambo fulani likatokea. Paula anaeleza: “Siku moja nilikutana na rafiki yangu kisha miezi mingi bila kuonana naye. Wakati huo watu wengi walipenda kuwa na nywele ndefu na walipenda kutumia dawa za kulewesha. Nilipomuona, alikuwa amebadilika kabisa. Alikuwa amekata nywele zake na alikuwa mwenye furaha. Kwa hiyo, nilimuuliza: ‘Kwa nini umebadilika na umekuwa wapi?’ Aliniambia kama alianza kujifunza na Mashahidi wa Yehova na alianza kunihubiria.” Paula ambaye aliamini kama mambo ya Mungu hayawezi kujulikana alivutiwa na kukubali kama Biblia ni Neno la Mungu kwa sababu alijionea mwenyewe namna Biblia ilivyosaidia rafiki yake abadilishe maisha yake.

‘NENO LAKO NI TAA YA MUGUU WANGU’

17. Kusoma Biblia kila siku na kutafakari kunaweza kuwa na matokeo gani juu yako?

17 Biblia ni zawadi nzuri ambayo Yehova ametutolea kupitia roho yake takatifu. Furahia kuisoma kila siku, na hilo litakusaidia kuipenda na kumupenda Yule aliyeiandikisha. (Zab. 1:1, 2) Usikose kusali kila mara unaposoma ao kujifunza Biblia ili kumuomba Yehova akuongoze kupitia roho yake. (Lu. 11:13) Biblia ina mawazo ya Mungu. Kwa hiyo, kusoma Biblia na kutafakari ao kufikiri sana juu ya yale unayosoma kutakusaidia upatanishe mawazo yako na mawazo ya Mungu.

18. Sababu gani unapenda kuendelea kujifunza Biblia?

18 Kadiri ujuzi wako sahihi juu ya kweli unavyoongezeka, jikaze kuishi kulingana na yale unayojifunza. (Soma Zaburi 119:105.) Ujiangalie kupitia Maandiko kama mutu anavyojiangalia katika kioo. Ukiona kama unahitaji kufanya mabadiliko, tafazali fanya hivyo. (Yak. 1:23-25) Tumia Neno la Mungu kama upanga ili kutetea imani yako na kuondoa mafundisho ya uongo katika mioyo ya wapole. (Efe. 6:17) Unapofanya hivyo, uwe mwenye shukrani kwa kuwa manabii na wanaume waliotumiwa ili kuandika ujumbe ulio katika Biblia ‘walioongozwa kweli na roho takatifu.’

[Maelezo ya chini]

^ Dictionnaire grec-anglais ya Agano Jipya na Vitabu Vingine vya Ukristo wa mwanzo​-mwanzo.

^ Majina fulani yamebadilishwa.

[Maulizo ya Funzo]

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 29]

Soma Biblia kila siku, na utamupenda sana Yule aliyeiandikisha

[Picha katika ukurasa wa 26]

Sinyatire inaonyesha yule aliyetuma barua