Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mutu Mwenye Hekima Anatafuta ‘Ufundi wa Kuongoza’

Mutu Mwenye Hekima Anatafuta ‘Ufundi wa Kuongoza’

Mutu Mwenye Hekima Anatafuta ‘Ufundi wa Kuongoza’

Maisha yetu ni kama safari. Hata hivyo, hekima ya wanadamu haiwasaidie sana watu ili wajue namna ya kupambana na matatizo ya maisha. Wengi wamezama kwa sababu ya magumu ya maisha kama vile mashua inavyozama kwa sababu ya upepo mukali. (Zab. 107:23, 27) Kwa nini ni jambo lenye kufaa kabisa kulinganisha matatizo ya maisha na matatizo ya kufanya safari katika bahari?

Zamani, haikuwa rahisi kufanya safari katika bahari na iliomba kuwa na ujuzi wa bahari. Ili kujua kuongoza mashua katika bahari, iliomba mutu afundishwe na kapitene ao na mutu anayejua kazi hiyo vizuri. (Mdo. 27:9-11) Kwenye picha za zamani, walikuwa wakimuchapa kapitene wa mashua kuwa mutu munene kuliko wafanyakazi wengine wa mashua ili kuonyesha kama kazi yake ilikuwa ya maana sana. Ili kufanya safari katika bahari kubwa sana, wafanyakazi katika mashua walipaswa kujifunza juu ya nyota, upepo na mambo mengine yaliyokuwa yakiwasaidia wasipotee. Biblia inasema kama mabaharia fulani ni ‘wenye ufundi,’ na neno linalotumiwa hapo linaweza kumaanisha “hekima.”​—Eze. 27:8.

Leo, matatizo ya maisha yanaweza kusumbua sana kama matatizo ambayo wale waliokuwa wakifanya safari zamani katika bahari walikuwa wakikutana nayo. Ni nini kinachoweza kutusaidia?

NI WAPI MUTU ANAWEZA KUPATA UFUNDI WA KUONGOZA MAISHA

Kwa kuwa maisha ni kama safari, kama tulivyosema hapo mwanzoni, fikiria kwa uzito ukweli huu wa Biblia: ‘Mwenye hekima asikilize, ataongezewa akili, naye mutu mujuzi atajifunza uongozi.’ (Met. 1:5, 6, Verbum Bible) Maneno ya Kiebrania yanayotafsiriwa ufundi wa kuongoza yanaeleza namna kiongozi ao kapitene wa mashua ya zamani alivyokuwa akifanya. Kiongozi huyo alihitaji uwezo wa kuongoza ao kuelekeza mashua kwa ufundi.

Ijapokuwa si rahisi, tunaweza kupata ‘ufundi wa kuongoza’ na tunaweza “kufanya safari” vizuri katika maisha. Kama vile kitabu cha Methali kinavyosema, tunapaswa kutumia “hekima,” “uelewaji,” na “ufahamu.” (Met. 1:2-6; 2:1-9) Tena, tunapaswa kutafuta uongozi wa Mungu, kwa sababu hata mutu mubaya anajua ‘kuongoza,’ lakini anaongoza kwenye uharibifu.​—Met. 12:5.

Kwa hiyo, ni jambo la lazima tujifunze Neno la Mungu kwa bidii. Kufanya hivyo kutatusaidia kujua mengi juu ya Yehova na juu ya yule anayeonyesha sifa za Mungu kwa ukamilifu, Yesu Kristo. (Yoh. 14:9) Tunapata mashauri mengi yenye hekima kwenye mikutano ya Kikristo. Zaidi ya hayo, tunaweza kujifunza kutokana na mambo ambayo wengine wamejionea katika maisha, kama vile wazazi wetu.​—Met. 23:22.

FIKIRIA MBELE YA WAKATI NA UCHUKUE MIPANGO

‘Ufundi wa kuongoza’ maisha ni wa lazima sana wakati tunajikuta katika matatizo yaliyo kama maji yasiyotulia. Kushindwa kuamua jambo la kufanya wakati tunapatikana katika hali fulani ngumu kunaweza kutuvunja moyo, na kutuletea matatizo.​—Yak. 1:5, 6.

Jambo lenye kupendeza ni kwamba maneno ufundi wa kuongoza yanatumiwa pia kuhusu vita. Tunasoma hivi: ‘kwa muongozo stadi [ufundi wa kuongoza] utaendeleza vita vyako, na kwa wingi wa washauri kuna wokovu.’​—Met. 20:18; 24:6.

Kama vile askari anayejitayarisha kufanya vita, tunapaswa kufikiria mbele ya wakati na kujitayarisha juu ya jambo lolote linaloweza kuharibu uhusiano wetu na Yehova. (Met. 22:3) Kwa mufano, labda unaweza kufikiri mbele ya wakati ili kujua ikiwa utakubali kazi mupya, ao kupandishwa cheo kazini ikiwa jambo hilo linakufikia. Bila shaka, utafikiria mushahara utakaolipwa, wakati utakaopitisha ili kwenda kazini na kurudi nyumbani, na mambo mengine. Lakini, kuna mambo mengine ambayo haupaswi kusahau. Kwa mufano: Je, kazi hii inapatana na kanuni za Biblia? Saa za kazi, kama vile kazi za kugombozana; zitakuwa na matokeo gani juu ya utendaji wangu mbalimbali wa kiroho?​—Lu. 14:28-30.

Dada Loretta, alikuwa na kazi nzuri. Kompanyi yao ilipohamia mahali pengine, Loretta alipandishwa cheo. Wakubwa wa kazi walimuambia hivi: “Hii ndiyo bahati yako maishani. Tena kuna Jumba la Ufalme karibu na mahali hapo.” Lakini, tamaa ya Loretta ilikuwa ya kurahisisha maisha yake ili aweze kumutumikia Muumbaji hata zaidi. Alitambua kama kazi hiyo mupya itamufanya asiwe na wakati wa kutosha kwa ajili ya utendaji mbalimbali wa Kikristo. Kwa hiyo, alikataa kazi hiyo ijapokuwa mukubwa wake wa kazi alimuambia kama yeye ni mufanya​-kazi ambaye hawapendi kupoteza kabisa. Dada Loretta amekuwa painia wa kawaida kwa miaka 20 hivi, na anasema kwamba ikiwa alipata matokeo mazuri ni kwa sababu ya ufundi wa kuongoza mambo katika maisha yake, ni kusema, kwa kufuata mashauri ya Neno la Mungu. Amefanya urafiki wake na Yehova uwe muzuri zaidi, na amekuwa na pendeleo la kusaidia watu wengi kukubali kweli.

‘Ufundi wa kuongoza’ unahitajiwa katika familia. Kuwalea watoto ni kazi inayochukua muda murefu, na maamuzi ambayo wazazi wanachukua ili familia iwe na hali nzuri ya kiroho ao ya kimwili, yanaweza kuwa na matokeo mazuri ao mabaya juu ya familia yote wakati ujao. (Met. 22:6) Kwa mufano, wazazi Wakristo wanaweza kujiuliza: ‘Je, mazungumuzo yetu na mufano wetu vinawafundisha watoto wetu kanuni za Biblia zitakazowasaidia kupambana na matatizo watakayopata watakapokuwa wakubwa? Je, kupitia namna yetu ya kuishi, tunawafundisha kutosheka na yale waliyo nayo na kuwa na maisha rahisi ili kutia utumishi pa nafasi ya kwanza?’​—1 Tim. 6:6-10, 18, 19.

Siri ya maisha mazuri si kufuatilia miradi ya kimwili na kuwa na vitu vingi vya kimwili kama wanavyofanya watu wengi. Mufalme Sulemani alijua jambo hilo. Roho ya Mungu ilimuongoza kuandika hivi: ‘Mambo yatawaendea vyema wale wanaomuogopa Mungu wa kweli, kwa sababu walimuogopa.’ (Mhu. 8:12) Jambo hilo linaonyesha kabisa hekima ya kutafuta ‘ufundi wa kuongoza’ maisha unaotegemea Neno la Mungu.​—2 Tim. 3:16, 17.

[Picha katika ukurasa wa 30]

Ili kuonyesha kama kazi ya kapitene ilikuwa ya lazima sana walikuwa wakimuchapa munene kuliko wafanyakazi wengine wa mashua

[Picha zimetolewa na]

Su concessione del Ministero per i Beni e le Attività Culturali. Inakatazwa kwa njia yoyote kufanya kopi ya picha hii.