Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu gani Mungu aliwaomba waabudu wake waoane kati yao tu?

Sababu gani Mungu aliwaomba waabudu wake waoane kati yao tu?

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Sababu gani Mungu aliwaomba waabudu wake waoane kati yao tu?

▪ Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli ilikuwa na amri iliyosema hivi juu ya mataifa yaliyowazunguka: ‘Usifanye mapatano yoyote ya ndoa pamoja nao. Binti yako usimupe mwana wake, wala binti yake usimuchukue kwa ajili ya mwana wako.’ (Kumbukumbu la Torati 7:3, 4) Sababu gani Mungu aliwakataza kuoana na watu wasiomuabudu?

Yehova alipenda kuwalinda Waisraeli kwa ujumla; alijua kama Shetani alitaka kuchafua ibada ya taifa lake kwa kuwachochea waabudu miungu ya uongo. Kwa hiyo, Mungu aliwaonya juu ya mataifa yaliyowazunguka kwa kusema hivi: ‘Watamugeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine.’ Kuoana na watu wasiomuabudu Mungu kungewaletea hatari nyingi. Waisraeli wangeabudu miungu mingine, Mungu hangewakubali tena na kuwalinda, na maadui wao wangewashinda kwa vyepesi. Basi, ikiwa mambo hayo yangewapata, namna gani wangetokeza Masiya aliyeahidiwa? Inaonekana wazi sababu gani Shetani alikuwa anawashawishi Waisraeli waoane na watu wasiomuabudu Mungu.

Kumbuka tena kama Mungu alihangaikia kila Muisraeli mumoja​-mumoja. Alijua kama ili kila Muisraeli apate furaha na awe na hali njema, iliomba awe na uhusiano muzuri pamoja na Mungu. Je, Yehova alikuwa na sababu nzuri ya kuwaonya juu ya hatari ya kuoana na mutu asiyemuabudu? Tuchukue mufano wa Mufalme Sulemani. Alijua vizuri onyo hili la Yehova juu ya wanawake wasiomuabudu: “Watageuza moyo wenu uifuate miungu yao.” Kwa sababu alikuwa na hekima nyingi, labda aliwaza kama jambo hilo haliwezi kumupata, na kwamba shauri hilo la Mungu halikumuhusu yeye . Kwa hiyo, akalizarau. Alipata matokeo gani? Biblia inasema hivi: “Wake zake wakaugeuza moyo wake . . . ukaifuata miungu mingine.” Hilo ni jambo lenye kuhuzunisha sana! Yehova alimukataa Sulemani, na watu wake waligawanyika kwa sababu mufalme wao hakuwa tena muaminifu.​—1 Wafalme 11:2-4, 9-13.

Watu fulani wanaweza kusema kama kuna watu ambao walioa wanawake wasiomuabudu Mungu na hawakupata matokeo mabaya. Kwa mufano, Muisraeli anayeitwa Maloni alioa mwanamuke Mumoabu anayeitwa Ruthu, na kisha mwanamuke huyo akakuwa muabudu wa Mungu. Lakini kuoa mwanamuke Mumoabu ilikuwa hatari sana. Maloni hakufanya vizuri kwa kuoa binti Mumoabu; alikufa angali bado kijana, mbele ya Ruthu kuwa muabudu wa Yehova. Kilioni, ndugu ya Maloni, alioa pia mwanamuke Mumoabu anayeitwa Orpa, ambaye aliendelea kuabudu “miungu yake.” Lakini Boazi yeye alipomuoa Ruthu, Ruthu alikuwa tayari muabudu wa Yehova. Kwa kweli, Wayahudi walimuona kuwa mutu aliyekubali kubadilisha imani yake. Ndoa ya Ruthu na Boazi iliwaletea baraka wote wawili.​—Ruthu 1:4, 5, 15-17; 4:13-17.

Je, ni jambo la hekima kuwaza kama mufano wa Maloni na Ruthu unaonyesha kama muabudu wa Yehova anaweza kuoana na mutu asiyemuabudu Yehova? Kwa kweli, kuwaza hivyo ni kama kuchukua mufano wa mutu aliyepata feza nyingi kwa kucheza muchezo wa tombola na kusema kama kucheza muchezo wa tombola ndiyo njia nzuri zaidi ya kupata feza!

Leo, Biblia inawaonya Wakristo waoane “katika Bwana tu.” Inawaonya wasifungwe “nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini.” Shauri hilo limeandikwa kwa ajili ya Wakristo wa kweli wanaotafuta kuoa ao kuolewa. Juu ya wale waliokwisha kuoana na watu wasio waabudu wa Mungu, Biblia inatoa mashauri yenye kufaa ili kuwasaidia wajue namna ya kupambana na hali hiyo ngumu. (1 Wakorintho 7:12-16, 39; 2 Wakorintho 6:14) Mashauri hayo yote yanaonyesha kama Yehova Mungu, aliyeanzisha ndoa, anataka sisi waabudu wake tuwe na furaha​—iwe tumefunga ndoa ao hapana.