Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki

Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki

Kwa Ajili ya Vijana

Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki

Maagizo: Ufanye mazoezi haya mahali pa utulivu. Unaposoma maandiko, wazia kama unatazama namna matukio hayo yalivyofuatana. Ona matukio hayo akilini mwako. Sikia sauti za watu wanaozungumuziwa na ujisikie namna walivyojisikia. Fanya kama ulikuwa hapo na unaona namna mambo yanavyotendeka.

Watu wanaozungumuziwa sana katika habari hii: Ahabu, Yezebeli, Nabothi, na Eliya

Kwa kifupi: Yezebeli alimusukuma Mufalme Ahabu amuuwe Nabothi ili achukue shamba lake la mizabibu.

1 CHUNGUZA MATUKIO HAYO.​—SOMA 1 WAFALME 21:1-26.

Unawaza watu ine wanaozungumuziwa katika habari hii walikuwa watu wa namna gani?

Ahabu ․․․․․

Yezebeli ․․․․․

Nabothi ․․․․․

Eliya ․․․․․

Unawaza sauti ya Yezebeli na Ahabu katika mustari wa 5-7 ilikuwa ya namna gani?

․․․․․

Eleza fujo iliyotokea kulingana na mustari wa 13, kama unavyowazia.

․․․․․

Unawaza sauti na sura ya Eliya na Ahabu ni ya namna gani wakati wa mabishano yao yanayoelezwa katika mustari wa 20-26?

․․․․․

2 TAFUTA KUJUA ZAIDI.

Yezebeli anaonyesha sifa gani mbaya katika mustari wa 7 na wa 25?

․․․․․

Ahabu anaonyesha sifa gani mbaya katika mustari wa 4?

․․․․․

Ili kukamata shamba la mizabibu la Nabothi, ni nani wengine ambao Ahabu alilazimika kuua? (Soma 2 Wafalme 9:24-26.)

․․․․․

Ahabu alikuwa mutu wa namna gani machoni pa Yehova? (Soma tena mustari wa 25 na 26. Soma pia 1 Wafalme 16:30-33.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA JUU YA . . .

Namna Yehova alivyo tayari kuona matendo ya ukosefu wa haki.

․․․․․

Namna Yehova anavyohangaikia wale ambao wametendewa isivyo haki.

․․․․․

Namna Yehova anavyoonyesha kama yeye ni Mungu wa haki. (Soma Kumbukumbu la Torati 32:4.)

․․․․․

4 NAMNA NYINGINE UNAVYOWEZA KUTUMIA HABARI HII.

Namna gani watu fulani leo wanaweza kuonyesha roho kama ya Yezebeli? (Soma Ufunuo 2:18-21.)

․․․․․

Kama Eliya, unaweza kuonyesha moyo usio na woga katika hali gani?

․․․․․

Unaweza kuwa na uhakika gani unapoona vitendo vya ukosefu wa haki ao unapotendewa isivyo haki?

․․․․․

5 NI MAMBO GANI KATIKA HABARI HII YANAYOKUGUSA MOYO SANA, NA SABABU GANI?

․․․․․

Pendekezo: Eleza habari hii kama mutangazaji wa habari. Sema namna mambo yalivyotendeka, na ufanye kama unawauliza maulizo wale watu ine wanaozungumuziwa sana na watu wengine ambao walikuwa hapo wakati mambo hayo yalitendeka.

Ufungue www.pr418.com

Usome Biblia kwenye internete

Upakue ao kuchapisha habari hii