Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Acha Yehova Akuongoze Kwenye Uhuru wa Kweli

Acha Yehova Akuongoze Kwenye Uhuru wa Kweli

Acha Yehova Akuongoze Kwenye Uhuru wa Kweli

“[Chunguza] ndani ya sheria kamilifu iliyo ya uhuru.”​—YAK. 1:25.

UNAWEZA KUJIBU NAMNA GANI?

Ni sheria gani inayoongoza kwenye uhuru wa kweli, na ni nani wanaofaidika na sheria hiyo?

Ni nini siri ya kuwa huru kabisa?

Watu wote wanaoendelea kumutii Yehova, watapata uhuru gani?

1, 2. (a) Ni nini inayoonyesha kama katika ulimwengu leo watu hawana uhuru, na kwa nini unajibu hivyo? (b) Watumishi wa Yehova wanatazamia uhuru gani?

 TUNAISHI wakati ambao mambo kama vile pupa, kutokuheshimu sheria, na jeuri vimeongezeka sana. (2 Tim. 3:1-5) Ili kupiganisha mambo hayo, serikali ao guvernema zinatia sheria nyingi, zinaongeza vifaa na hesabu ya mapolisi, zinatumia vyombo vya kisasa kama vile kamera za kielektroniki ili kujua mambo yanayopita. Katika inchi fulani, watu wametia kengele za kielektroniki, wanafunga milango kwa makufuli mengi, na hata wamejenga kuta zenye kuwa na kura ili kulinda usalama wao. Watu wengi hawatembei tena usiku wala kuwaacha watoto wachezee inje peke yao, iwe usiku ao muchana. Kwa kweli, watu wengi hawana uhuru, na labda hali hii itazidi kuwa mbaya zaidi.

2 Katika shamba la Edeni, Shetani alidai kama ili mutu awe huru kabisa, hapashwe kumutegemea Yehova. Huo ulikuwa uongo mutupu! Kwa kweli, watu wanapokataa kuheshimu sheria za Mungu, wanateseka zaidi na zaidi. Hali hizo zinazoendelea kuwa mbaya zinawagusa pia watumishi wa Yehova. Hata hivyo, Biblia inatutolea tumaini kama siku fulani wanadamu watatoka katika utumwa wa zambi na uharibifu ili wafurahie “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Rom. 8:21) Yehova ameanza kutayarisha watumishi wake kwa ajili ya uhuru huo. Namna gani?

3. Yehova amewapa wafuasi wa Mwana wake sheria gani, na tutazungumuzia maulizo gani?

3 Mwanafunzi Yakobo anatoa jibu kwa ulizo hilo anaposema kama Yehova ametupatia “sheria kamilifu iliyo ya uhuru.” (Soma Yakobo 1:25.) Tafsiri zingine za Biblia zinaita sheria hiyo kuwa “sheria kamilifu ambayo huwapa watu uhuru” (Habari Njema Kwa Watu Wote) na “sheria kamilifu, sheria ya uhuru” (La Sainte Bible en Swahili du Zaïre). Kwa kawaida, watu wanaposikia neno sheria wanafikiria tu jambo fulani linalowafunga​-funga ili wasifanye kama wanavyopenda, hawaone kama sheria inapatana ao inatembea na uhuru. Basi, “sheria kamilifu iliyo ya uhuru” ni nini? Na namna gani sheria hiyo inatuweka huru?

SHERIA INAYOTUWEKA HURU

4. “Sheria kamilifu iliyo ya uhuru” ni nini, na ni nani wanaofaidika na sheria hiyo?

4 “Sheria kamilifu iliyo ya uhuru” si Sheria ya Musa, kwa sababu ile Sheria ya Musa ilionyesha waziwazi makosa ya Waisraeli na Kristo alitimiza sheria hiyo. (Mt. 5:17; Gal. 3:19) Basi, Yakobo anazungumuzia sheria gani? Alikuwa anazungumuzia “sheria ya Kristo,” ambayo inaitwa tena “sheria ya imani” ao “sheria ya watu huru.” (Gal. 6:2; Rom. 3:27; Yak. 2:12) Kwa hiyo, “sheria kamilifu,” inamaanisha kila jambo ambalo Yehova anataka tufanye. Wakristo watiwa​-mafuta na “kondoo wengine” wanafaidika na sheria hiyo.​—Yoh. 10:16.

5. Kwa sababu gani sheria ya uhuru si nzito?

5 “Sheria kamilifu” inatofautiana na sheria za inchi nyingi. Amri na kanuni za sheria hiyo si nzito zinaeleweka wazi na ni rahisi kufuata. (1 Yoh. 5:3) Yesu alisema: ‘Nira yangu ni laini na muzigo wangu ni mwepesi.’ (Mt. 11:29, 30) Tena, “sheria kamilifu” hiyo haina lazima ya kuonyesha malipizi ya kila kosa kwa sababu sheria hiyo inategemea upendo na haiandikwe juu ya mabamba ya mawe, lakini imeandikwa katika akili na mioyo.​—Soma Waebrania 8:6, 10.

NAMNA “SHERIA KAMILIFU” INAVYOTUWEKA HURU

6, 7. Namna gani sheria za Yehova zinatufaidi na sheria ya uhuru inatuwezesha kufanya nini?

6 Yehova amewekea watu sheria ili ziwalinde na ni kwa faida yao. Kwa mufano, fikiria sheria za asili zinazofanya tuishi; kama vile nguvu inayofanya vitu kama vile jua, mwezi ao nyota visituangukie. Watu hawanungunike eti sheria hizo zinawasonga. Lakini, wanafurahia sheria za asili wakijua kama ni kwa faida yao. Vivyo hivyo, kanuni za Yehova tunazojifunza katika “sheria kamilifu” ya Kristo ni kwa faida yetu.

7 Zaidi ya kutulinda, sheria ya uhuru inatuwezesha kutosheleza tamaa zetu zote zinazofaa bila kupata matokeo mabaya, na kwa njia inayoheshimu haki na uhuru wa wengine. Kwa hiyo, siri ya kuwa huru kabisa, ni kufanya mambo tunayopenda lakini yanayofaa; mambo yanayopatana na sifa na kanuni za Yehova. Hilo linamaanisha kama tunapaswa kujifunza kupenda mambo ambayo Yehova anapenda na kuchukia yale ambayo anachukia. Sheria ya uhuru inatusaidia kufanya jambo hilo.​—Amo. 5:15.

8, 9. Wale wanaotii sheria ya uhuru, wanapata faida gani? Toa mufano.

8 Kwa sababu hatukamilike si kwepesi kuzuia tamaa mbaya. Lakini, tunapotii kwa uaminifu sheria ya uhuru, tunaweza kufurahia tangu sasa nguvu ya sheria hiyo inayotusaidia kuwa huru kabisa. Kwa mufano, Jay alianza kujifunza Biblia na alikuwa akivuta sana sigareti. Alipojifunza kama tabia hiyo haimufurahishe Mungu, alipaswa kuamua. Je, angeendelea kuwa mutumwa wa tamaa yake ao kumutii Yehova? Ijapokuwa ilikuwa vigumu kwake kuachana na tabia ya kuvuta sigareti, Jay alichagua kumutumikia Mungu. Kisha kuachana na tabia hiyo, alijisikia namna gani? Jay alisema kama alijisikia kuwa mutu huru kabisa na mwenye furaha sana.

9 Jay alijionea mwenyewe kama uhuru ambao ulimwengu unatoa unawafanya watu ‘wakazie akili juu ya mwili,’ kwa kweli unawafanya kuwa watumwa. Lakini, uhuru ambao Yehova anatoa, unaomaanisha “kukaza akili juu ya roho,” unaweka huru na unaongoza kwenye “uzima na amani.” (Rom. 8:5, 6) Ni nini iliyomusaidia Jay kuachana na tabia yake? Hakushinda kwa nguvu zake mwenyewe lakini kwa musaada wa Mungu. Alisema hivi: “Nilijifunza Biblia kwa ukawaida, nilimuomba Yehova roho takatifu, na nilikubali musaada wenye upendo wa ndugu na dada katika kutaniko la Kikristo.” Mambo hayo yanaweza pia kutusaidia sisi sote ili kuwa na uhuru wa kweli. Namna gani?

CHUNGUZA NDANI YA NENO LA MUNGU

10. ‘Kuchunguza’ ndani ya sheria ya Mungu kunamaanisha nini?

10 Tunasoma hivi katika Yakobo 1:25: “Yeye anayechunguza ndani ya sheria kamilifu iliyo ya uhuru na ambaye hudumu katika hiyo . . . atakuwa mwenye furaha katika kuitenda.” Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “anayechunguza,” linamaanisha “kuinama ili kuangalia ndani.” Kufanya hivyo si kwepesi. Kwa hiyo, ikiwa tunataka sheria ya uhuru ichochee akili na mioyo yetu, tunapaswa kujifunza Biblia kwa bidii na kwa ukawaida, kusali, na kutafakari kabisa juu ya mambo tunayosoma.​—1 Tim. 4:15.

11, 12. (a) Namna gani Yesu alionyesha kama ni lazima kuishi kulingana na kweli? (b) Kulingana na mufano wa dada anayezungumuziwa katika kifungo, ni hatari gani ambayo vijana wanapaswa kuepuka?

11 Pia, tunapaswa kudumu ao kuendelea kutumikisha mashauri ya Neno la Mungu ili kuishi kulingana na kweli. Yesu alionyesha pia wazo hilo alipowaambia watu waliomuamini hivi: ‘Mukikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’ (Yoh. 8:31, 32) Kitabu fulani kinasema kama, neno “kujua” linalotumiwa katika andiko hili, linamaanisha pia kupendezwa na, kwa sababu “jambo ‘ambalo mutu anajua’ ni la maana sana kwake.” Kwa hiyo, tunaweza kusema kama tunaijua kabisa kweli ikiwa tunaishi kupatana nayo. Tukifanya hivyo, tunaweza kusema bila kukosea kama ‘neno la Mungu linafanya kazi’ ndani yetu; linatubadilisha kabisa na kutufanya tuonyeshe sifa za Baba yetu wa mbinguni katika maisha yetu.​—1 Tes. 2:13.

12 Ujiulize hivi: ‘Je, naijua kabisa kweli? Je, ninaishi kupatana nayo? Ao je, ningali natamani mambo ya ulimwengu ambayo yanaitwa eti “uhuru?”’ Dada mumoja aliyelelewa na wazazi Wakristo anakumbuka namna alivyojiendesha alipokuwa kijana. Aliandika hivi: “Mutu anayekomalia katika kweli, anajua kama Yehova iko. Lakini, mimi sikumujua kabisa Yehova vizuri. Sikujifunza kuchukia mambo ambayo anachukia. Sikuamini hata kidogo kama anahangaikia mwenendo wangu. Na sikuona faida ya kusali nilipokuwa katika shida. Nilitegemea akili yangu mwenyewe; ilikuwa ni upuuzi kabisa, kwa sababu sikujuwa yale niliyokuwa ninafanya.” Inafurahisha kwa sababu dada huyo alitambua baadaye kama mawazo yake yalikuwa mabaya sana, basi alifanya mabadiliko makubwa na akawa hata painia wa kawaida.

ROHO TAKATIFU INAWEZA KUKUSAIDIA KUWA HURU

13. Namna gani roho takatifu ya Mungu inatusaidia kuwa huru?

13 Andiko la 2 Wakorintho 3:17 linasema: “Mahali palipo na roho ya Yehova, pana uhuru.” Namna gani roho takatifu inatusaidia kuwa huru? Inafanya hivyo kwa kutusaidia tuwe na sifa za lazima zinazotufanya tuwe huru, ni kusema, ‘upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.’ (Gal. 5:22, 23) Haiwezekani kuwa huru bila sifa hizo, zaidi sana upendo. Ikiwa ulimwengu uko kama ulivyo leo ni kwa sababu watu hawana sifa hizo. Kisha kutaja sifa za tunda la roho, Paulo aliongeza hivi: “Hakuna sheria juu ya mambo hayo.” Alimaanisha nini kwa kusema hivyo? Paulo alimaanisha kama hakuna sheria inayoweza kuzuia ukuzi wa tunda la roho ya Mungu. (Gal. 5:18) Na ikiwa sheria fulani ingetaka kufanya hivyo, je, ingeweza? Hapana, kwa sababu mapenzi ya Yehova ni kwamba tuendelee kuonyesha sifa hizo za Kikristo zaidi na zaidi na hata milele.

14. Namna gani roho ya ulimwengu inawafanya watu kuwa watumwa?

14 Wale wanaotawaliwa na roho ya ulimwengu na wanaotosheleza tamaa zao za kimwili bila kujizuia wanaweza kufikiri kama wako huru. (Soma 2 Petro 2:18, 19.) Lakini, kwa kweli wao ni watumwa kabisa. Ndiyo sababu guvernema zinaweka sheria nyingi ili kuzuia watu wasitosheleze tamaa zao zisizofaa na tabia zao mbaya. Paulo anasema, ‘sheria huwekwa, si kwa ajili ya mutu mwadilifu, bali kwa ajili ya watu wenye kuasi sheria na watundu.’ (1 Tim. 1:9, 10) Tena, wao ni watumwa wa zambi, kwa sababu wanafanya “mambo yanayopendwa na mwili,” na mwili ni bwana asiye na huruma. (Efe. 2:1-3) Tunaweza kusema watu hao wanafanana na vidudu vinavyofuata asali iliyo katika bakuli na kisha vinashindwa kutoka humo. Watu hao wamefuata tamaa zao na kisha wanajikuta wamenaswa na zambi.​—Yak. 1:14, 15.

UHURU KATIKA KUTANIKO LA KIKRISTO

15, 16. Ni faida gani ambayo tumepata kwa sababu tumekubali kuja katika kutaniko la Kikristo, na ni uhuru gani tunaofurahia?

15 Ulipoanza kushirikiana na kutaniko la Kikristo haukuwa kama mutu anayeingia mahali fulani pa kukutana tu na marafiki ili kupitisha wakati. Lakini, ulikuja katika kutaniko kwa sababu Yehova alikuvuta. (Yoh. 6:44) Sababu gani alifanya hivyo? Je, Yehova alikuona kuwa mutu mwenye haki na anayemuogopa Mungu? Labda utajibu “Hapana kabisa.” Basi, Mungu aliona nini katika moyo yako? Aliona kama una moyo unaoweza kukubali sheria yake ya uhuru, moyo unaoweza kukubali uongozi wake muzuri. Katika kutaniko, Yehova amekulisha moyo wako kupitia mafundisho ya kweli, kwa kufanya hivyo amekuweka huru, maana yake, amekutosha katika utumwa wa mafundisho ya dini ya uongo na desturi za uongo. Tena, amekufundisha namna ya kuvaa utu mupya ili kumuiga Kristo. (Soma Waefeso 4:22-24.) Na kwa sababu umefanya hivyo, una pendeleo la kuwa kati ya watu ambao ni wao tu wanaostahili kuitwa “watu huru” duniani pote.​—Yak. 2:12.

16 Fikiria mambo haya: Unapokuwa kati ya ndugu na dada, watu wanaomupenda Yehova kwa moyo wao wote, je, unajisikia kuwa mwenye kuogopa? Je, unakuwa na wasiwasi kila mara unapokuwa pamoja nao? Unapozungumuza na waamini wenzako kwenye Jumba la Ufalme, je, unatupia-tupia jicho kwenye vitu vyako kwa sababu unawaza kama vitaibwa? Hapana! Unajisikia huru na salama. Je, unaweza kupata usalama kama huo unapokuwa na watu fulani mahali pengine? Bila shaka hapana! Jambo lingine ni hili: uhuru unaofurahia sasa kati ya watu wa Yehova ni onjo tu ya uhuru tunaongojea wakati ujao.

“UHURU WENYE UTUKUFU WA WATOTO WA MUNGU”

17. Namna gani “kufunuliwa kwa wana wa Mungu” kutawaletea wanadamu uhuru?

17 Paulo alizungumuzia uhuru ambao Yehova amewatayarishia watumishi wake watakaoishi duniani; aliandika hivi: “Uumbaji unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu.” Kisha aliongeza hivi: “Uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Rom. 8:19-21) “Uumbaji” unamaanisha wanadamu walio na tumaini la kuishi milele hapa duniani ambao watafaidika na “kufunuliwa” kwa wana wa Mungu waliotiwa mafuta na roho yake. Kufunuliwa huko kutaanza wakati Kristo atatumika huko mbinguni pamoja na “wana” hao wa Mungu ili kuondoa ubaya wote duniani na kuingiza ‘umati mukubwa’ katika ulimwengu mupya.​—Ufu. 7:9, 14.

18. Namna gani wanadamu watiifu watafikia kupata uhuru zaidi, na mwishowe watapata uhuru gani?

18 Basi wanadamu waliokombolewa watafurahia uhuru mupya ulio kamili, ni kusema, watakuwa huru na uvutano wa Shetani na mashetani. (Ufu. 20:1-3) Huo utakuwa uhuru kabisa! Kuanzia wakati huo, wafalme na makuhani 144 000 watakaokuwa pamoja na Kristo, watatumia hatua kwa hatua faida za zabihu ya ukombozi ili kuwasaidia wanadamu wawe huru kabisa mupaka wakati zambi ya Adamu na kutokamilika vitaondolewa kabisa. (Ufu. 5:9, 10) Watakapojionyesha kuwa waaminifu kiisha jaribu la mwisho, wanadamu watapata uhuru ulio kamili ambao Yehova alikusudia wanadamu wawe nao tangu mwanzo, ni kusema, “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” Jaribu kuwazia jambo hili! Itakuwa rahisi kwako kufanya mambo ambayo Mungu anataka ufanye kwa sababu mwili wako wote, moyo na akili yako vitakuwa vikamilifu na utu wako utakuwa kabisa utu ambao umefanywa kulingana na mufano wa Mungu.

19. Tunapaswa kuendelea kufanya nini leo ili tubaki katika njia inayoongoza kwenye uhuru wa kweli?

19 Je, unachunga kwa hamu siku ambayo utakuwa na “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu”? Ikiwa ndivyo, basi acha “sheria kamilifu iliyo ya uhuru” itawale akili na moyo wako. Ujifunze Biblia kwa bidii. Patanisha maisha yako na kweli na uichukue kwa uzito. Umuombe Yehova roho takatifu. Faidika kabisa na mipango ya kutaniko la Kikristo, na chakula cha kiroho ambacho Yehova anatupatia. Usiruhusu Shetani akudanganye kama alivyodanganya Eva, kwa kukufanya ufikiri kama sheria za Yehova zinakufunga-funga. Kwa kweli, Shetani anaweza kuwa mwerevu sana. Lakini, kama tutakavyoona katika habari inayofuata, tunaweza kumushinda Shetani “kwa maana sisi hatukosi kuzijua mbinu zake.”​—2 Kor. 2:11.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 9]

Je, ningali natamani sana mambo ya ulimwengu ambayo yanaitwa eti “uhuru”?

[Picha katika ukurasa wa 9]

Je, ninaishi kupatana na kweli?