Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tujiendeshe Kama Raia wa Ufalme wa Mungu

Tujiendeshe Kama Raia wa Ufalme wa Mungu

Tujiendeshe Kama Raia wa Ufalme wa Mungu

‘Mujiendeshe kama raia.’​—FLP. 1:27, (Maelezo yaliyo chini katika Rbi8-F).

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Ni nani wanaoweza kuwa raia wa Ufalme wa Mungu?

Unapaswa kufanya nini kuhusiana na luga, historia na sheria za Ufalme wa Mungu?

Namna gani raia wa Ufalme wa Mungu wanaonyesha kama wanapenda sheria za Mungu?

1, 2. Kwa nini shauri la mutume Paulo kwa Wafilipi lilikuwa la maana sana?

 MUTUME Paulo alitia moyo Wakristo wa kutaniko la Filipi ‘wajiendeshe kwa namna inayostahili habari njema.’ (Soma Wafilipi 1:27.) Neno la Kigiriki “jiendesheni” ambalo Paulo alitumia linaweza pia kutafsiriwa “kushiriki katika kazi ao shuguli mbalimbali za raia.” Maneno hayo yalikuwa ya maana sana kwa Wakristo walioishi katika muji wa Filipi. Kwa nini? Kwa sababu inaonekana kama muji wa Filipi ulikuwa kati ya miji ambayo wakaaji wake walipewa uraia wa Kiroma ao kukubaliwa kuwa wanainchi wa Roma. Raia wa Kiroma katika Filipi na kotekote katika Utawala wa Roma walijivunia jambo hilo, ni kusema, walijivunia kuitwa Waroma, na walilindwa na sheria za serikali ya Roma.

2 Wakristo wa kutaniko la Filipi walipaswa kujivuna kupita wanainchi wengine. Mutume Paulo aliwakumbusha kama uraia wao ulikuwa “mbinguni” kwa sababu walikuwa Wakristo watiwa-mafuta. (Flp. 3:20) Hawakuwa raia wa utawala fulani wa wanadamu, lakini walikuwa raia wa Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo walikuwa na ulinzi wa pekee na faida nyingi kuliko wengine.​—Efe. 2:19-22.

3. (a) Ni nani walio na pendeleo la kuwa raia wa Ufalme wa Mungu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Shauri la Mutume Paulo la ‘kujiendesha kama raia’ linahusu zaidi sana wale watakaotawala na Kristo huko mbinguni. (Flp. 3:20) Lakini pia, shauri hilo linahusu wale watakaoishi duniani; wale watakaotawaliwa na Ufalme wa Mungu. Sababu gani? Kwa sababu kila Mukristo, iwe ametiwa mafuta ao hapana, alijitoa kwa Mungu na anatumikia Mufalme yuleyule, ni kusema, Yehova, na anapaswa kuishi kulingana na kanuni zake. (Efe. 4:4-6) Leo, watu wanajikaza sana ili wakubaliwe kuwa raia ao wanainchi wa inchi tajiri. Je, hauone kama ni pendeleo kubwa sana kuwa raia wa Ufalme wa Mungu? Ili kutusaidia tuendelee kupendezwa na pendeleo hilo, acheni tuchunguze mambo ambayo mutu anapaswa kutimiza ili awe raia wa inchi fulani na tutayalinganisha na yale mutu anapaswa kutimiza ili awe raia wa Ufalme wa Mungu. Kisha, tutachunguza mambo matatu ambayo tunapaswa kufanya ili tustahili kuwa raia wa Ufalme wa Mungu.

MAMBO AMBAYO MUTU ANAPASWA KUTIMIZA

4. Ile luga safi ni nini, na namna gani ‘tunaiongea’?

4 Kujifunza luga. Serikali fulani za wanadamu zinawaomba wale wanaotaka kuwa raia ao wanainchi wa inchi zao wajue kwanza luga za inchi hizo. Hata kisha kukubaliwa kuwa wanainchi wa inchi fulani, watu wanajikaza ili kujua vizuri luga ya inchi hiyo. Wanaweza kujifunza kwa uharaka sarufi (grammaire) ya luga hiyo, lakini pia wanachukuwa wakati wa kujifunza namna ya kutamuka vizuri maneno ya luga hiyo. Vilevile, Ufalme wa Mungu unaomba raia wake wajifunze ile ambayo Biblia inaita ‘luga safi.’ (Soma Sefania 3:9.) Hiyo luga safi ni nini? Ni ile kweli inayopatikana katika Biblia inayozungumuzia juu ya Mungu na makusudi yake. ‘Tunaongea’ ile luga safi wakati mwenendo wetu unapatana na sheria na kanuni za Mungu. Raia wa Ufalme wa Mungu wanaweza kujifunza haraka mafundisho ya musingi ya Biblia na kubatizwa. Hata hivyo, kisha kubatizwa, watumishi wa Mungu wanapaswa kujikaza “kuongea” vizuri zaidi ile luga safi. Namna gani? Kila mumoja wetu anapaswa kupatanisha maisha yake na kanuni za Biblia ambazo amejifunza.

5. Sababu gani tunapaswa kujifunza mengi kuhusu historia ya sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova?

5 Kujifunza historia. Mutu anayetaka kuwa raia ao mwanainchi wa inchi fulani, lazima ajifunze historia ya inchi hiyo. Vilevile, wale wanaotamani kuwa raia wa Ufalme wa Mungu, wanapaswa kujifunza mengi juu ya Ufalme huo. Fikiria mufano muzuri ambao wana wa Kora walituachia. Walipendezwa sana na muji wa Yerusalemu na mahali pake pa ibada na walizungumuzia historia ya muji huo. Jambo lililowavutia sana haikuwa namna muji wa Yerusalemu na mahali pake pa ibada vilijengwa, lakini walipendezwa zaidi sana kwa sababu Yerusalemu ilikuwa ‘muji wa Mufalme mukubwa,’ Yehova; mahali pa ibada safi. Ni hapo watu walifundishwa Sheria ya Yehova. Watu walioongozwa na Mufalme wa Yerusalemu ndio Yehova alionyesha fazili zake zenye upendo. (Soma Zaburi 48:1, 2, 9, 12, 13.) Kama wana wa Kora, je, unatamani kujifunza na kuzungumuzia wengine historia ya kisasa ya sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova? Kadiri unavyoendelea kujifunza juu ya tengenezo la Mungu na namna Yehova anavyosaidia watu wake, ndivyo Ufalme wa Mungu hautakuwa jambo la kuwazia tu kwako. Kujua historia hiyo kutafanya hamu yako ya kuhubiri habari njema ya Ufalme iongezeke.​—Yer. 9:24; Lu. 4:43.

6. Kwa nini haishangaze kwamba Yehova anataka tujifunze na kutii sheria na kanuni za Ufalme wake?

6 Kuzijua sheria. Serikali za wanadamu zinawaomba wanainchi wajifunze na kutii sheria za inchi. Kwa hiyo, haishangaze kwamba Yehova anataka tujifunze na kutii sheria na kanuni ambazo zinaongoza raia wote wa Ufalme wake. (Isa. 2:3; Yoh. 15:10; 1 Yoh. 5:3) Mara nyingi sheria za wanadamu zina makosa na zinaweza kuwa na upendeleo. Lakini, “sheria ya Yehova ni kamilifu.” (Zab. 19:7) Je, tunapendezwa na sheria ya Mungu na kusoma Neno lake kila siku? (Zab. 1:1, 2) Njia moja inayoweza kukusaidia uijue sheria ya Mungu ni kujifunza sheria hiyo wewe mwenyewe. Hakuna mutu atakayejifunza sheria hizo pa nafasi yako.

RAIA WA UFALME WANAPENDA SHERIA ZA MUNGU

7. Raia wa Ufalme wanaheshimu sheria za nani?

7 Ili kubaki raia wa Ufalme tunapaswa kujua na kupenda sheria za Mungu. Raia wengi wa serikali za wanadamu wanasema kama wanakubaliana na sheria za inchi wanamoishi. Hata hivyo, wanapoona kuwa sheria fulani inawasumbua na kwamba hakuna mutu anayewaona, wanaivunja. Mara nyingi, watu hao wanataka tu “kuwapendeza wanadamu.” (Kol. 3:22) Raia wa Ufalme wa Mungu wao wanaheshimu sheria za Mungu. Tunafurahia kutii sheria hizo hata ikiwa hakuna mutu anayetuona. Sababu gani? Kwa sababu tunamupenda Yule aliyefanya sheria hizo.​—Isa. 33:22; soma Luka 10:27.

8, 9. Namna gani unaweza kujua kama unapenda kabisa sheria za Mungu?

8 Namna gani unaweza kujua kama unapenda kabisa sheria za Mungu? Namna unavyojisikia unaposhauriwa juu ya mambo ambayo unawaza yanakuangalia wewe mwenyewe, kunaonyesha kama unapenda sheria ya Mungu ao hapana. Tuchukue mufano wa mambo yanayohusu namna ya kuvaa na kujipamba. Mbele ya kuwa raia wa Ufalme, labda ulipenda kuvaa mavazi ya ovyoovyo ao mavazi yanayoamusha watu tamaa ya ngono. Upendo wako kwa Mungu ulipoongezeka, ulijifunza kuvaa kwa namna inayomuletea Mungu heshima. (1 Tim. 2:9, 10; 1 Pet. 3:3, 4) Labda sasa unaona kama unavalia vizuri. Lakini, utajisikia namna gani ikiwa muzee anakuambia kama mavazi unayopendelea kuvaa yanawakwaza wahubiri fulani katika kutaniko? Je, utamusikiliza na kutii shauri lake? Ao je, utajitetea​-tetea na kumuwekea kinyongo ao kumupinga? Sheria moja ya lazima sana ambayo raia wote wa Ufalme wanapaswa kutii ni kumuiga Kristo. (1 Pet. 2:21) Kuhusiana na Mufano wa Yesu, mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kila mumoja wetu na amupendeze jirani yake katika yaliyo mema kwa ajili ya kujengwa kwake. Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe.’ (Rom. 15:2, 3) Ili amani iendelee katika kutaniko, Mukristo anayekomaa kiroho anapaswa kuepuka bila kinyongo mambo yanayoumiza zamiri za wengine.​—Rom. 14:19-21.

9 Tuzungumuzie mambo mawili tunayopaswa kufikiria sana: namna tunavyoona mambo ya ngono na maoni yetu juu ya ndoa. Wale ambao hawajakuwa bado raia wa Ufalme wa Mungu labda hawaone ubaya wowote ikiwa mwanaume analala na mwanaume ao mwanamuke analala na mwanamuke. Pia labda hawaone hatari yoyote inayotokana na ponografia (picha na habari za ngono) na labda wanafikiri kama kufanya uzinzi na kuvunja ndoa ni uamuzi wa mutu pekee yake. Lakini, raia wa Ufalme wamekwisha kutupilia mbali mawazo ya kujifikiria mwenyewe. Ijapokuwa watu walifanya mambo hayo mbele ya kuwa Wakristo, sasa wanaona ndoa na uhusiano wa ngono kuwa zawadi kutoka kwa Mungu. Wanapenda sheria za Mungu na wanaamini kwa moyo wao wote kama wale wanaofanya mambo mapotovu ya uasherati hawastahili kuwa raia wa Ufalme wa Mungu. (1 Kor. 6:9-11) Hata hivyo, wanajua pia kama moyo ni mudanganyifu. (Yer. 17:9) Kwa hiyo, wanapendezwa na maonyo yanayowasaidia waendelee kuwa na mwenendo safi unaotegemea sheria za Mungu.

RAIA WA UFALME WANAPENDEZWA NA MAONYO

10, 11. Ni maonyo gani tengenezo la Yehova limetutolea kwa wakati unaofaa, na tunajisikia namna gani kuhusu maonyo hayo?

10 Serikali za wanadamu zinaweza kutoa maonyo fulani kuhusu vyakula na dawa vinavyoweza kuhatarisha afya ya wanainchi. Kwa kweli, vyakula vyote na dawa zote si vibaya. Lakini, ikiwa chakula fulani ao dawa fulani inaweza kuharibu afya ya wanainchi, serikali inaweza kutolea raia wake maonyo ili kuwalinda. Ikiwa serikali haifanye hivyo itaonekana wazi kama haiangaikie raia wake. Kwa hiyo, Ufalme wa Mungu pia unatutolea pa wakati maonyo fulani kuhusu mwenendo fulani na kuhusu hatari za kiroho. Kwa mufano, Internete imekuwa njia inayotumiwa sana ili kupashana habari, kufundisha na kujifurahisha ao kujiburudisha. Ni kweli kwamba tengenezo la Mungu linatumia pia Internete na kupitia njia hiyo tengenezo limetimiza mambo mengi mazuri. Hata hivyo, adresi nyingi za Internete zinaweza kuhatarisha hali yetu ya kiroho na mwenendo wetu. Adresi hizo za Internete zinazoonyesha sana mambo ya ponografia (picha na habari za ngono), ambayo kwa kweli yanahatarisha afya ya kiroho ya raia wa Ufalme wa Mungu. Kwa miaka mingi mutumwa mwaminifu ametuonya kuhusu adresi hizo za Internete. Hakika sisi raia wa Ufalme tunapendezwa kabisa na maonyo hayo ya kiroho!

11 Katika miaka ya hivi karibuni, adresi za Internete za namna ingine zimependwa sana na watu wengi na zina faida ikiwa zinatumiwa vizuri. Lakini adresi hizo zinazoitwa, adresi za Internete za kupashana habari za kipekee na marafiki, zina hatari pia. Adresi hizo zinamufanya mutu ashirikiane na marafiki wabaya. (1 Kor. 15:33) Kwa hiyo, haishangaze kwamba tengenezo la Mungu limetoa maonyo mazuri kuhusu matumizi ya adresi hizo za Internete. Je, umesoma habari zote ambazo zimechapishwa siku hizi na mutumwa mwaminifu kuhusu vituo ao adresi hizo? Ikiwa mutu anatumia adresi hizo bila kusoma kwanza habari kuhusu jambo hilo, itakuwa kutenda bila hekima. * Mutu akifanya hivyo, atakuwa kama mutu anayetumia dawa bila kusoma kwanza maagizo yanayoonyeshwa kuhusu matumizi ya dawa hiyo.

12. Kwa nini ni upumbavu kutotii maonyo?

12 Wale wasiotii maonyo yanayotolewa na mutumwa mwaminifu, kwa kweli watajiletea matatizo wao wenyewe na wataletea pia wale wanaowapenda matatizo. Ndugu na dada fulani wamejifanya watumwa wa mambo ya ponografia ao wamefanya uasherati na kisha wamejidanganya kwa kuanza kufikiri kama Yehova haone mambo wanayofanya. Ni upumbavu sana kuwaza kama tunaweza kumuficha Yehova mambo tunayofanya! (Met. 15:3; soma Waebrania 4:13.) Mungu anataka kusaidia ndugu na dada hao, na wazee wanaweza kuwasaidia. (Gal. 6:1) Serikali za wanadamu zinaweza kuamua kama mutu fulani hastahili tena kuwa raia kwa sababu ametenda mambo fulani mabaya. Vilevile, ikiwa ndugu ao dada anavunja sheria za Yehova na anakosa kutubu, Yehova atamunyanganya haki ya kuwa raia wa Ufalme wake. * (1 Kor. 5:11-13) Yehova ni mwenye rehema, kwa hiyo, wale wanaotubu na kubadilika wanaweza tena kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova na kukubaliwa tena kuwa raia wa Ufalme wake. (2 Kor. 2:5-8) Bila shaka, kumutumikia Mufalme mwenye upendo kama huyo, ni pendeleo la ajabu!

RAIA WA UFALME WANAPENDEZWA NA ELIMU

13. Namna gani raia wa Ufalme wanaonyesha kama wanapendezwa na elimu?

13 Serikali nyingi za wanadamu zinajikaza sana kuwasomesha raia zake. Zinapanga kuwe masomo ya kuwafundisha watu kusoma na kuandika na kuwafundisha kazi ya mikono. Raia wa Ufalme wanapendezwa na masomo hayo na wanajifunza kwa bidii kusoma, kuandika na hivyo wanaweza kujitegemeza kifeza. Lakini, raia wa Ufalme wa Mungu wanapendezwa hasa na elimu wanayopokea katika tengenezo la Yehova. Katika makutaniko, Yehova amechukua mipango ili kuwe masomo ya kujifunza kusoma na kuandika. Wazazi wanatiwa moyo kuwasomea watoto wao. Kila mwezi, mutumwa mwaminifu anachapisha kurasa nyingi za mafundisho yanayotegemea Biblia katika Munara wa Mulinzi na Amkeni! Ikiwa unasoma kila siku kurasa fulani, unaweza kumaliza kurasa hizo zote katika mwezi moja; kwa kufanya hivyo utaendelea kutembea pamoja na tengenezo la Yehova, njia ambayo anatumia ili kutoa elimu ya Ufalme.

14. (a) Ni mazoezi gani tunayopata? (b) Ni mapendekezo gani kuhusu Ibada ya Familia ya mangaribi umefurahia kutumikisha?

14 Kila juma, raia wa Ufalme wanapokea mazoezi mazuri kwenye mikutano ya kutaniko lao. Kwa mufano, katika kipindi cha zaidi ya miaka 60, Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi imewasaidia wanafunzi kuwa walimu wenye kujua kufundisha Neno la Mungu. Je, umejiandikisha kwenye masomo hayo? Katika miaka ya hivi karibuni, mutumwa mwaminifu ametia mukazo juu ya Ibada ya Familia ya mangaribi ya kila juma. Mupango huo unafanya familia iwe yenye kuungana sana. Je, umetumia mapendekezo yanayotolewa katika Munara wa Mulinzi na Huduma Yetu ya Ufalme kuhusu Ibada ya Familia ya mangaribi? *

15. Ni pendeleo gani kubwa kupita mapendeleo yote ambalo tunalo?

15 Raia wa serikali za wanadamu wanajaribu kuchochea wengine ili waunge mukono chama fulani cha politike, wanafanya hivyo hata nyumba kwa nyumba. Vilevile, duniani pote raia wa Ufalme pia wanaonyesha waziwazi kama wanaunga mukono kabisa Ufalme wa Mungu kwa kutangaza Ufalme huo barabarani na nyumba kwa nyumba. Kwa kweli, kama inavyoonyeshwa katika habari iliyotangulia, Munara wa Mulinzi, unaotangaza Ufalme wa Yehova, ndilo gazeti linalogawanywa sana duniani pote leo! Pendeleo kubwa kupita mapendeleo yote ni lile la kuwaelezea watu juu ya Ufalme wa Mungu. Je, unafanya kazi hiyo ya kuhubiri kwa bidii?​—Mt. 28:19, 20.

16. Namna gani unaweza kuonyesha kama wewe ni raia muzuri wa Ufalme wa Mungu?

16 Karibuni Ufalme wa Mungu ndio utakuwa serikali pekee ambayo itatawala dunia yote. Ufalme huo ndio utasimamia mambo yetu yote ya kila siku. Je, utakuwa raia muzuri wa Ufalme wa Mungu wakati huo? Sasa ndio wakati wa kuonyesha kama utakuwa hivyo. Katika kila jambo unalofanya kila siku, fanya mambo yote kwa utukufu wa Yehova na onyesha kama unajiendesha kama raia muzuri wa Ufalme wa Mungu.​—1 Kor. 10:31.

[Maelezo ya chini]

^ Kwa mufano, soma Amkeni! ya mwezi wa 7, 2011, ukurasa wa 24-27; mwezi wa 8, 2011, ukurasa wa 10-13; na mwezi wa 2, 2012, ukurasa wa 3-9.

^ Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 mwezi wa 3, 2012, ukurasa wa 30-31.

^ Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 mwezi wa 8, 2011, ukurasa wa 6-7 na Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 1, 2011, ukurasa wa 3-6.

[Maulizo ya Funzo]

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 14]

Je, unatii maonyo yanayotolewa na mutumwa mwaminifu juu ya Internete?

[Picha katika ukurasa wa 12]

Kama wana wa Kora, je, unapendezwa na ibada safi na historia yake?

[Picha katika ukurasa wa 15]

Ibada ya Familia ya mangaribi inaweza kukufanya wewe na familia yako muwe raia wazuri wa Ufalme