Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Gehazi Alipata Matatizo kwa Sababu ya Tamaa

Gehazi Alipata Matatizo kwa Sababu ya Tamaa

Uwafundishe Watoto Wako

Gehazi Alipata Matatizo kwa Sababu ya Tamaa

JE, UMEKWISHA kutamani sana kitu fulani? * Ikiwa jibu ni ndiyo, hauko peke yako. Lakini, je, utapenda kusema uongo ili upate kitu unachohitaji?— Hapana, haupaswe kufanya hivyo. Mutu anayefanya hivyo ni mutu mwenye tamaa. Acha tuone matatizo yaliyomupata mwanaume anayeitwa Gehazi kwa sababu ya tamaa yake. Gehazi alikuwa mutumishi wa Elisha, nabii wa Yehova, Mungu wa kweli.

Elisha na Gehazi waliishi zamani sana, miaka ya 1 000 hivi mbele Yesu mwana wa Mungu azaliwe hapa duniani. Elisha alifanya mambo ya ajabu sana ao miujiza kwa nguvu za Yehova! Kwa mufano, Biblia inazungumuzia mukubwa fulani wa jeshi la Siria aliyekuwa na ugonjwa mubaya wa ukoma. Ni Elisha tu ndiye alikuwa na uwezo wa kumuponyesha.

Wakati Elisha alikuwa anawaponyesha watu kwa nguvu za Mungu, hakukubali hata kidogo kulipwa feza. Unajua sababu gani?— Kwa sababu Elisha anajua kama miujiza hiyo inafanywa kwa nguvu za Yehova​—si kwa nguvu zake mwenyewe. Wakati Naamani anaponyeshwa, anafurahi sana. Kwa hiyo, anataka kumupa Elisha zawadi za zahabu, feza, na mavazi mazuri. Elisha anakataa zawadi hizo, lakini Gehazi anazitamani sana.

Kisha Naamani kuondoka, Gehazi anamufuata nyuma bila kumuambia Elisha. Gehazi anapomukuta Naamani, unajua anamuambia nini?— ‘Elisha ananituma nikuambie kama anapata wageni wawili sasa hivi. Kwa hiyo, anataka umupatie mavazi mawili ili awatolee.’

Lakini huo ni uongo! Gehazi anatunga habari hiyo ya wageni wawili. Anasema hivyo kwa sababu anapenda kupata mavazi ambayo Naamani alitaka kumupatia Elisha. Naamani hajue kama habari hiyo ni ya uongo. Kwa hiyo, anafurahi kumupatia Gehazi zawadi hizo. Naamani anamupatia hata zaidi ya vitu anavyomuomba. Unajua mambo yanayotokea kisha hapo?

Wakati Gehazi anarudi nyumbani, Elisha anamuuliza hivi: ‘Unatoka wapi?’

Gehazi anamujibu hivi: ‘Sikuenda fasi.’ Lakini Yehova alikuwa amemufunulia Elisha mambo ambayo Gehazi alifanya. Kwa hiyo Elisha anasema: ‘Huu si wakati wa kupokea feza na mavazi!’

Gehazi alikuwa amekamata feza na mavazi ambavyo havikuwa vyake. Kwa hiyo, Mungu anafanya ukoma wa Naamani umupate. Unawaza habari hii inaweza kutufundisha nini?— Jambo la lazima ambalo tunajifunza ni kwamba hatupaswe kutunga habari za uongo na kuzielezea wengine.

Sababu gani Gehazi alitunga habari ya uongo?— Ni kwa sababu alikuwa mutu mwenye tamaa. Alitamani kupata vitu ambavyo havikuwa vyake, na alisema uongo ili kuvipata. Kwa sababu ya uongo huo aliteswa na ugonjwa mubaya maisha yake yote.

Gehazi alipatwa na jambo lingine mbaya zaidi kuliko ukoma. Unajua ni jambo gani?— Mungu alimukataa na hakumupenda tena. Hatupaswe kufanya jambo lolote linaloweza kufanya Mungu atukatae! Lakini, tuwe wema na tusiwe wachoyo.

Usome katika Biblia yako

2 Wafalme 5:5, 20-27; Yuda 21;

Yohana 15:10

[Maelezo ya chini]

^ Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii (—), utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.