Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uvumilivu wa Yehova na Yesu Unatufundisha Nini?

Uvumilivu wa Yehova na Yesu Unatufundisha Nini?

Uvumilivu wa Yehova na Yesu Unatufundisha Nini?

‘Tuone [uvumilivu wa] Bwana wetu kuwa wokovu.’​—2 PET. 3:15.

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Namna gani Yehova ameonyesha kama yeye ni muvumilivu?

Sababu gani Yesu alipaswa kuvumilia kwa muda murefu?

Tunaweza kufanya nini ili kutia nguvu uvumilivu wetu?

1. Ndugu fulani ambao wamemutumikia Yehova kwa uaminifu wanajiuliza ulizo gani?

 DADA mumoja aliyevumilia kwa uaminifu magumu kwa miaka mingi aliuliza hivi kwa unyenyekevu, “Je, mwisho utafika na ningali bado muzima?” Ndugu fulani ambao wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi wanajiuliza pia ulizo hilo. Tunangojea kwa hamu kuona ile siku ambayo Mungu atafanya vitu vyote kuwa vipya, na kuondoa magumu tunayopambana nayo leo. (Ufu. 21:5) Hata ikiwa kuna mambo mengi yanayotufanya tuamini kama ule mwisho wa ulimwengu muovu wa Shetani unakaribia sana, inaweza kuwa vigumu kungojea kwa uvumilivu siku hiyo.

2. Tutazungumuzia maulizo gani kuhusu uvumilivu?

2 Hata hivyo, Biblia inaonyesha kama tunapaswa kuwa na uvumilivu. Tutapata baraka ambazo Yehova ameahidi ikiwa tuna imani yenye nguvu na ikiwa tunangojea kwa uvumilivu wakati ambapo atatimiza ahadi zake, kama watumishi wa Yehova walioishi zamani. (Soma Waebrania 6:11, 12.) Yehova mwenyewe ni muvumilivu. Kama sivyo angekuwa amekwisha kuharibu watu wabaya, lakini anangojea wakati ambao amepanga ili kufanya hivyo. (Rom. 9:20-24) Sababu gani anavumilia hivyo? Namna gani Yesu ameiga mufano wa uvumilivu wa Mungu na ametuwekea mufano gani? Tutapata faida gani ikiwa tunaiga uvumilivu wa Mungu? Majibu ya maulizo hayo yatatusaidia kuwa na uvumilivu na imani yenye nguvu, hata ikiwa labda tunaanza kufikiri kama Yehova amekawia.

SABABU GANI YEHOVA ANAVUMILIA?

3, 4. (a) Sababu gani Yehova ameonyesha uvumilivu anapoendelea kutimiza kusudi lake kuelekea dunia? (b) Yehova alifanya nini wakati uasi ulitokea katika Edeni?

3 Kuna sababu zinazomufanya Yehova avumilie. Ni kweli kwamba Yehova ndiye aliye na mamlaka yote juu ya ulimwengu; hata hivyo, uasi uliotokea katika Edeni ulitokeza maulizo yanayohusu viumbe wake wote wenye akili. Yehova amevumilia, kwa sababu alijua kama itachukua wakati ili kujibu maulizo hayo kwa ukamili. Kwa kuwa anaelewa vizuri matendo na mawazo ya viumbe wake wa mbinguni na duniani, tuwe hakika kama anavumilia kwa faida yetu.​—Ebr. 4:13.

4 Kusudi la Yehova lilikuwa kwamba watoto wa Adamu na Eva wajaze dunia. Shetani alimudanganya Eva, na kisha Adamu alikosa kutii, hata hivyo, Mungu hakuacha kusudi lake. Mungu hakuogopa na kuanza kuchukua maamuzi haraka haraka, wala hakukasirika ao kuwaachilia wanadamu. Kuliko kufanya hivyo, alifikiria njia atakayotumia ili kutimiza yale aliyokuwa amekusudia wanadamu na dunia. (Isa. 55:11) Ili kutimiza kusudi hilo na kusaidia viumbe wake wajue kama utawala wake ndio utawala unaofaa, Yehova ameonyesha sifa ya kujizuia sana na uvumilivu. Amengojea hata maelfu ya miaka ili sehemu fulani za kusudi lake zitimie kwa njia nzuri zaidi.

5. Uvumilivu wa Yehova umetokeza baraka gani?

5 Sababu nyingine inayomufanya Yehova angojee kwa uvumilivu ni kwamba anataka watu wengi wapate uzima wa milele. Sasa anafanya mipango ili kuokoa ‘mukutano mukubwa.’ (Ufu. 7:9, 14; 14:6) Kupitia kazi yetu ya kuhubiri, Yehova anawaalika watu waje kujifunza kuhusu Ufalme wake na kanuni zake. Ujumbe wa ufalme ndio habari nzuri kuliko habari zote ambazo wanadamu wanahitaji, kwa kweli hiyo ni “habari njema.” (Mt. 24:14) Kila mutu ambaye Yehova anavuta, anaingia katika tengenezo la ulimwenguni pote. Watu walio katika tengenezo hilo ni marafiki wa kweli wanaopenda yaliyo mema. (Yoh. 6:44-47) Mungu wetu mwenye upendo anafanya hayo yote ili kuwasaidia watu hao wakubaliwe naye. Tena, kati ya wanadamu, amekuwa akichagua wale watakaotumika katika serikali ao guvernema yake ya mbinguni. Huko mbinguni, watafanya kazi ya kuwasaidia wanadamu watiifu kufikia ukamilifu na uzima wa milele. Inaonekana wazi kama hata ikiwa anangojea kwa uvumilivu, Yehova amekuwa akifanya kazi ili kutimiza ahadi zake, kwa faida yetu.

6. (a) Namna gani Yehova alionyesha uvumilivu katika siku za Noa? (b) Namna gani Yehova anaonyesha uvumilivu leo?

6 Yehova ni muvumilivu hata kama watu wanaendelea kufanya mambo ya kumuchokoza. Fikiria mambo mabaya ambayo watu walikuwa wanafanya mbele ya Garika na namna Mungu alivyoonyesha uvumilivu. Dunia ilijaa mambo ya uasherati na jeuri, na Yehova ‘aliumia moyoni mwake’ kwa sababu wanadamu walizidi tu kufanya mambo yaliyo mabaya. (Mwa. 6:2-8) Mungu hangeruhusu hali hiyo iendelee milele, kwa hiyo, aliamua kuleta garika ili kuharibu wanadamu hao wasiotii. ‘Uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja katika siku za Noa,’ Yehova alifanya mipango ili kuokoa Noa na familia yake. (1 Pet. 3:20La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo) Yehova alipoona kama wakati unafaa, alimujulisha Noa uamuzi wake na akamupatia kazi ya kujenga safina. (Mwa. 6:14-22) Zaidi ya hayo, Noa alikuwa ‘muhubiri wa uadilifu,’ alikuwa anawaonya watu kuhusu uharibifu uliokuwa karibu kutokea. (2 Pet. 2:5) Yesu alisema kama siku zetu zinafanana na siku za Noa. Yehova amekwisha kuamua ni wakati gani ataharibu ulimwengu huu muovu. Hakuna mutu anayejua ile ‘siku na ile saa’ ya mwisho. (Mt. 24:36) Leo, Mungu ametupatia kazi ya kuwaonya watu na kuwafundisha namna wanaweza kuokolewa.

7. Je, Yehova anakawia kutimiza ahadi zake? Eleza.

7 Kwa kweli, ikiwa Yehova anavumulia, hiyo haimaanishe kama hafanye lolote ao anapitisha tu wakati. Wala hatupaswe kufikiri kama hatuhangaikie. Ni kweli kwamba inaweza kuwa vigumu kuelewa jambo hilo kwa sababu tunazeeka na kuteseka katika ulimwengu huu muovu. Kwa hiyo, tunaweza kuvunjika moyo na kuanza kufikiri kama Mungu anakawia kutimiza ahadi zake. (Ebr. 10:36) Lakini, tusisahau hata kidogo kama kuna sababu fulani zinazomufanya Mungu aonyeshe uvumilivu na tusisahau kama anaendelea kutumia wakati huo kwa faida ya watumishi wake. (2 Pet. 2:3; 3:9) Tuone sasa namna Yesu pia alivyoiga uvumilivu wa Mungu.

YESU NI MUFANO MUZURI WA UVUMILIVU

8. Yesu alionyesha uvumilivu katika hali gani?

8 Yesu anaendelea kufanya mapenzi ya Mungu na amekuwa akifanya hivyo kwa maelfu ya miaka. Shetani alipoasi, Yehova aliamua kama Mwana wake muzaliwa-pekee ndiye anapaswa kuja duniani ili awe Masiya. Fikiria namna Yesu alipaswa kungojea kwa uvumilivu maelfu ya miaka mupaka wakati huo ufike. (Soma Wagalatia 4:4.) Hiyo haimaanishe kama Yesu alikuwa anangojea tu bila kufanya kazi yoyote. Yeye alikuwa anafanya kazi ambayo Baba yake alikuwa amemupatia. Mwishowe, Yesu alipofika duniani, alijua kama Shetani angemuuwisha, kama ilivyokuwa imetabiriwa. (Mwa. 3:15; Mt. 16:21) Hata hivyo, alivumilia mateso hayo mengi na kifo, kwa sababu alijua kama hayo ndiyo mapenzi ya Mungu. Hakuna mwanadamu ambaye alikuwa ameonyesha uaminifu kama ule wa Yesu. Yeye hakujifikiria mwenyewe ao kufikiria cheo chake, na hilo ni somo kwetu.​—Ebr. 5:8, 9.

9, 10. (a) Anapongojea kwa uvumilivu Yehova atende, Yesu anaendelea kufanya nini sasa? (b) Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu kalendari ya Yehova?

9 Kisha kufufuliwa, Yesu alipewa mamlaka mbinguni na duniani. (Mt. 28:18) Yeye anatumia mamlaka hayo ili kutimiza makusudi ya Yehova kulingana na kalendari ya Mungu. Yesu alingojea kwa uvumilivu kwenye mukono wa kuume wa Mungu mupaka mwaka wa 1914; wakati Mungu alipoweka maadui wake kuwa kiti cha miguu yake. (Zab. 110:1, 2; Ebr. 10:12, 13) Hivi karibuni ataharibu ulimwengu huu muovu wa Shetani. Yesu anapoendelea kungojea wakati huo, kwa uvumilivu anaendelea pia kusaidia watu wakubaliwe na Mungu na anawaongoza kwenye “maji ya uzima.”​—Ufu. 7:17.

10 Je, hauone kama Yesu ni mufano muzuri unaotusaidia kuvumilia kuhusiana na kalendari ya Yehova? Kwa kweli, Yesu alikuwa na hamu sana ya kufanya kila jambo ambalo Baba yake alimuomba afanye; hata hivyo, alikuwa anangojea wakati uliowekwa na Mungu. Kwa kuwa tunangojea pia mwisho wa ulimwengu huu muovu wa Shetani, sisi wote tunapaswa kuiga uvumilivu wa Mungu; tunapaswa kungojea uongozi wa Mungu na tusichoke kumutumikia Mungu kwa sababu ya kuvunjika moyo. Tunaweza kufanya nini ili kuiga uvumilivu huo wa Mungu?

NAMNA GANI TUNAWEZA KUIGA UVUMILIVU WA MUNGU?

11. (a) Namna gani imani inaweza kutusaidia kuvumilia? (b) Sababu gani sisi tuna sababu zaidi za kuwa na imani yenye nguvu?

11 Mbele ya Yesu kuja hapa duniani, manabii na watumishi wengine waaminifu wa Mungu walionyesha kupitia mufano wao kama hata wanadamu wasiokamilika wanaweza kuvumilia. Walivumilia kwa sababu ya imani yao yenye nguvu. (Soma Yakobo 5:10, 11.) Ikiwa hawangeamini kabisa ahadi za Yehova, ni kusema, ikiwa wangekosa imani, je wangeweza kungojea kwa uvumilivu utimizo wa ahadi hizo? Mara nyingi, walipambana na mambo yenye kuogopesha yaliyojaribu imani yao, lakini walitumaini kama hata mwisho Mungu atatimiza ahadi zake. (Ebr. 11:13, 35-40) Sisi tuna sababu nyingi zaidi za kuwa na imani yenye nguvu; Yesu anatumika leo kama ‘mukamilishaji wa imani yetu.’ (Ebr. 12:2) Alitimiza unabii na ametusaidia tuelewe vizuri makusudi ya Mungu ili tuwe na imani.

12. Tunaweza kufanya nini ili kuwa na imani yenye nguvu?

12 Tunaweza kufanya nini ili kuwa na imani yenye nguvu na uvumilivu zaidi? Ni lazima tutumie mashauri ya Mungu katika maisha yetu. Kwa mufano, fikiria sababu zinazokufanya utie Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yako. Je, unaweza kujikaza ili kutumia katika maisha yako shauri linalopatikana katika Mathayo 6:33? Labda itakuomba kutumia wakati mwingi zaidi katika mahubiri ao kuondoa mambo fulani katika maisha yako ili uwe na maisha rahisi. Usisahau namna Yehova amebariki jitihada zako mupaka leo. Labda amekusaidia kupata mutu wa kujifunza naye Biblia ao amekusaidia uwe na ‘amani yenye ubora unaozidi fikira zote.’ (Soma Wafilipi 4:7.) Kufikiria faida ambazo wewe mwenyewe umepata sababu ya kufuata maagizo ya Yehova, kutakusaidia uzidi kuwa na uvumilivu.​—Zab. 34:8.

13. Ni mufano gani unaoonyesha namna imani yetu inavyoweza kutusaidia kuvumilia?

13 Mufano wa mulimaji unaweza kutusaidia tuelewe namna imani inavyoweza kutufanya tuvumilie zaidi. Mulimaji analima, anapanda na kuvuna. Kila mara anapovuna kwa uwingi, anakuwa na uhakika zaidi, na kwa hiyo, atapanda mbegu zaidi wakati mwengine. Kwa kweli, anapopanda mbegu, ni lazima angojee kwa uvumilivu mupaka wakati wa mavuno. Lakini, hilo halitamuzuia kupanda mbegu; anaweza hata kupanda mbegu mahali pengi zaidi kuliko hapo mbele. Ana imani kama atavuna. Vilevile, tunapojifunza sheria za Yehova, tunapozitumia katika maisha yetu na kupata matokeo mazuri, imani yetu katika Yehova inaongezeka. Basi imani yetu inapoongezeka, inakuwa rahisi kwetu kungojea baraka zitakazokuja.​—Soma Yakobo 5:7, 8.

14, 15. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu mateso yanayowapata wanadamu?

14 Jambo lingine linaloweza kutusaidia kuvumilia ni kuwa na maoni yanayofaa juu ya ulimwengu na hali zetu. Jaribu kuona mambo kama Yehova anavyoyaona. Kwa mufano, fikiria namna Mungu anavyojisikia anapoona watu wakiteseka. Kwa muda murefu Mungu ameumia sana moyoni anapoona wanadamu wakiteseka; lakini huzuni hiyo haijamufanya achoke na kuacha kutenda mema. Alimutuma Mwana wake muzaliwa​-pekee “ili azivunje kazi za Ibilisi” na kuondoa mateso yote ambayo Shetani amewaletea wanadamu. (1 Yoh. 3:8) Kwa kweli, Mungu atakapoondoa mateso milele, itaonekana kama mateso tunayopata sasa yalikuwa ya muda. Kwa hiyo, kuliko kujiacha tuchoshwe na utawala huu muovu wa Shetani ao kukosa uvumilivu kwa sababu hatujue siku mwisho utakuja, acheni tuweke tumaini letu katika vitu visivyoonekana vitakavyodumu milele. Yehova ameweka siku ambayo ataondoa uovu, na atatenda bila kuchelewa.​—Isa. 46:13; Nah. 1:9.

15 Katika siku hizi za mwisho zilizo ngumu, imani yetu inaweza kujaribiwa kwa njia fulani. Kuliko kukasirika wakati tunatendewa vibaya ao wakati wapendwa wetu wanateseka, inafaa tuazimie kumutumaini kabisa Yehova. Ni kweli kwamba si rahisi kufanya hivyo kwa sababu sisi ni watu wasio wakamilifu. Hata hivyo, tunapaswa kukumbuka maneno ya Yesu yanayopatikana katika Mathayo 26:39.​—Soma.

16. Ni mawazo gani tunayopaswa kuepuka katika siku hizi za mwisho?

16 Kwa kweli, mutu anayeanza kuwa na mashaka kama mwisho unakaribia, anaweza kushindwa kuvumilia na anaweza kuanza kupanga mambo mengine katika maisha yake. Anafikiri kama mipango hiyo inaweza kumusaidia ikiwa mambo hayatendeke kama Yehova alivyosema. Kwa maneno mengine, anaweza kufikiri hivi: ‘Nitangojea ili nione kama Yehova atatimiza kabisa mambo aliyoahidi.’ Kwa hiyo, anaweza kuanza kutafuta ajulikane katika ulimwengu huu; kutafuta kuwa na feza na kuacha kutia Ufalme wa Mungu pa nafasi ya kwanza, ao kupenda kusoma masomo ya juu ili awe na maisha mazuri leo. Lakini, je, hauone kama kufanya hivyo ni alama inayoonyesha kama mutu ameanza kukosa imani? Kumbuka kama Paulo alitutia moyo tuige watumishi waaminifu waliopokea baraka za Yehova ‘kupitia imani na uvumilivu.’ (Ebr. 6:12) Yehova ameweka wakati ambapo ataharibu ulimwengu huu muovu, na hatachelewa. (Hab. 2:3) Tunapongojea mwisho, tunapaswa kuepuka tabia ya kumutumikia Yehova kama watu wasiopenda. Tunapaswa kukumbuka kama tunaishi katika siku za mwisho na kwa hiyo, tunapaswa kuhubiri kwa bidii habari njema; kazi hiyo inaweza kutuletea furaha hata sasa.​—Lu. 21:36.

FAIDA ZA UVUMILIVU

17, 18. (a) Uvumilivu unatutolea nafasi ya kufanya nini leo? (b) Tutapata baraka gani ikiwa tunavumilia?

17 Iwe tumekwisha kumutumikia Mungu kwa miezi fulani ao kwa miaka mingi, tunataka kuendelea kumutumikia milele. Uvumilivu utatusaidia tuendelee kungojea, iwe kwa muda murefu ao mufupi, mupaka wakati tutaokolewa. Yehova anatutolea nafasi ya kuonyesha kama tunatumaini kabisa maamuzi yake na kama tutabaki waaminifu kwake hata kama hilo linaweza kutuletea mateso. (1 Pet. 4:13, 14) Mungu anatutolea pia mazoezi ambayo yanaweza kutusaidia kuvumilia mupaka mwisho ili tuokolewe.​—1 Pet. 5:10.

18 Yesu amepewa mamlaka yote mbinguni na duniani, na hakuna jambo linaloweza kumuzuia asikulinde, ikiwa unataka. (Yoh. 10:28, 29) Hatupaswe kuogopa wakati ujao wala hata kifo. Wale watakaongojea kwa uvumilivu mupaka mwisho wataokolewa. Kwa hiyo, hatupaswe kuuacha ulimwengu utudanganye na kutufanya tuache kumutumaini Yehova. Lakini, tunapaswa kukomalisha imani yetu na kutumia kwa hekima wakati huu unaobaki wa uvumilivu wa Mungu.​—Mt. 24:13; soma 2 Petro 3:17, 18.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 21]

Kuiga uvumilivu wa Mungu kutakusaidia kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza na kuvuna baraka nyingi!