Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Hamuijue ile Siku Wala ile Saa’

‘Hamuijue ile Siku Wala ile Saa’

‘Hamuijue ile Siku Wala ile Saa’

‘Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamuijue ile siku wala ile saa.’​—MT. 25:13.

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Tunapata faida gani sababu ya kutokujua wakati gani mwisho utakuja?

Namna gani watiwa-mafuta wameendelea kukesha?

Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko tayari kwa ajili ya kurudi kwa Kristo?

1-3. (a) Ni mifano gani inayoweza kutusaidia kuelewa jambo ambalo Yesu alitaka kufundisha katika mifano yake miwili? (b) Habari hii itatusaidia kujibu maulizo gani?

 WAZIA wewe ni shofere, na kwa hiyo mukubwa fulani wa guvernema anakuomba umupeleke kwenye mukutano wa maana sana. Lakini, dakika kidogo tu mbele ya kuenda kumuchukua, unatambua kama hauna esanse ya kutosha katika motokari. Mara moja unaenda haraka kununua esanse. Unapoondoka mukubwa huyo anafika. Anatazama huku na huku, hakuone. Anaona kama akikungojea atachelewa, kwa hiyo anamuomba shofere mwengine amupeleke. Kisha muda kidogo, unarudia na unakuta amekwisha kuondoka. Utajisikia namna gani?

2 Sasa tufikiri kama wewe ndiye mukubwa huyo; unataka kusafiri, lakini mbele ya kufunga safari hiyo unachagua wanaume watatu wanaostahili ili wakufanyie kazi fulani ya lazima. Unawafasiria kazi ambayo wanapaswa kufanya, na wote watatu wanaikubali kwa furaha. Lakini, unaporudi, unatambua kama ni wawili tu ndio waliotimiza kazi yao. Kisha yule ambaye hakufanya kitu anaanza kujitetea. Kwa kweli, hakujaribu hata kidogo kufanya kazi yake. Utajisikia namna gani?

3 Mifano hiyo inafanana na mifano ya Yesu ya mabikira na talanta. Yesu alitumia mifano hiyo ili kuonyesha kama katika siku za mwisho, Wakristo fulani watiwa​-mafuta wangekuwa waaminifu na wenye busara, lakini wengine wangekuwa wapumbavu. * (Mt. 25:1-30) Ili kukazia jambo alilotaka kutufundisha, Yesu alisema hivi: ‘Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamuijue ile siku wala ile saa,’ ni kusema, hatujue siku gani kabisa Mungu atamutuma Yesu kuja kuharibu ulimwengu huu wa Shetani. (Mt. 25:13) Sisi pia tunapaswa kutii shauri hilo leo. Tukiendelea kukesha kama Yesu alivyotushauri, hilo linaweza kutuletea faida gani? Ni nani walioonyesha kama waliendelea kukesha? Na tunapaswa kufanya nini sasa ili kuendelea kukesha?

FAIDA ZA KUENDELEA KUKESHA

4. Sababu gani ‘kuendelea kukesha’ hakumaanishe kubaki tu pale na kuchunga wakati ule mwisho utakapokuja?

4 Katika maisha kuna mambo ambayo yanatuomba tuheshimu wakati ili tusichelewe. Kwa mufano, kukutana na muganga, kuchukua avion, mashua ao motokari ili kusafiri. Lakini, kuna mambo mengine ambayo haiombe hata kuangalia saa, kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kumukengeusha mutu, na zaidi kunaweza kuhatarisha maisha. Kwa mufano, kuzimisha nyumba inayoungua ao kuokoa watu kisha kupita kwa matetemeko ya inchi ao mafuriko. Katika hali kama hizo zenye hatari inaomba kutenda kwa haraka; mutu haweze kusema kama atatenda kulingana na programu yake. Vilevile, kwa kuwa mwisho wa ulimwengu huu unakaribia zaidi, kazi ya kuwaonyesha watu mipango ya wokovu ambayo Yehova amechukua, ndiyo ya maana sana. Kuendelea kukesha hakumaanishe kubaki tu pale na kuchunga wakati ule mwisho utakapokuja. Kwa kweli, kuna faida tano hivi tunazopata kwa sababu hatujue kabisa siku na saa kamili ya mwisho wa ulimwengu huu.

5. Namna gani kutokujua ile siku na ile saa kunafunua mambo yaliyo katika moyo wetu?

5 Faida ya kwanza ni hii: Kutokujua siku ile mwisho utakapokuja kunafunua kabisa mambo yaliyo katika moyo wetu. Kwa kweli, kutuacha bila kujua jambo hilo kunaonyesha kama Yehova anatuheshimu kwa sababu anatuacha tutumie uhuru wetu wa kuchagua ikiwa tutabaki waaminifu kwake ao hapana. Kwa hiyo, ikiwa tunamutumikia Yehova ni kwa sababu tunamupenda, wala si kwa sababu tu tunataka kuokoka mwisho wa ulimwengu huu na kupata uzima. (Soma Zaburi 37:4.) Tunapofanya mapenzi ya Mungu tunapata furaha kabisa, na tunatambua kama anatufundisha kwa faida yetu. (Isa. 48:17) Kwa kweli, hatuzione sheria zake kuwa muzigo muzito.​—1 Yoh. 5:3.

6. Mungu anajisikia namna gani tunapomutumikia kwa sababu tunamupenda, na sababu gani anajisikia hivyo?

6 Faida ya pili: Kutokujua ile siku na ile saa kunatutolea nafasi ya kuufurahisha moyo wa Yehova. Tunapomutumikia Yehova kwa sababu tunamupenda wala si kwa sababu ya tarehe fulani ao kwa sababu tu tunataka kupata uzima wa milele, tunamusaidia Yehova amujibu adui yake Shetani anayemuzihaki na mashitaka ya uongo. (Ayu. 2:4, 5; soma Methali 27:11.) Tunapoona mateso na maumivu yote ambayo Shetani ametokeza, tunafurahia kutetea utawala wa Yehova na kukataa uongozi wa Shetani.

7. Sababu gani kuendelea kuishi maisha yasiyo ya uchoyo ni jambo lenye kuleta furaha?

7 Faida ya tatu: Kumutumikia Yehova bila kuwa na tarehe fulani katika akili yetu kunatusaidia tuendelee kuishi maisha yasiyo ya uchoyo. Leo, hata watu fulani wasiomujua Mungu wanaamini pia kama ulimwengu huu hautafanya tena siku nyingi. Wanaogopa kama kuna misiba fulani itakayoharibu ulimwengu, kwa hiyo mawazo yao ni: ‘Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.’ (1 Kor. 15:32) Lakini sisi hatuogope wakati ujao. Hatujitenge na wengine ili kufanya tu mambo yanayotupendeza sisi. (Met. 18:1) Badala yake, tunajikana wenyewe na tunafurahia kutumia wakati wetu, nguvu zetu, na uwezo wetu mbalimbali ili kuwahubiria wengine habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Soma Mathayo 16:24.) Jambo linalotuletea furaha ni kumutumikia Mungu, zaidi sana kuwasaidia wengine wamujue.

8. Ni mufano gani wa Biblia unaoonyesha kama tunapaswa kutegemea kabisa Yehova na Neno lake?

8 Faida ya ine: Kutokujua ile siku na ile saa kunatusaidia tumutegemee Yehova kabisa na kujikaza kutumia mashauri ya Neno lake katika maisha yetu. Kwa kuwa sisi ni watu wasiowakamilifu, mawazo yetu kila mara ni ya kupenda kujitegemea. Mutume Paulo aliwashauri Wakristo wote hivi: ‘Yeye anayefikiri kuwa amesimama na ajihazari kwamba asianguke.’ Watu 23 000 walikufa muda kidogo tu mbele Yoshua awaingize watu wa Mungu katika Inchi ya Ahadi. Mutume Paulo anasema kama ‘mambo hayo yaliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo.’​—1 Kor. 10:8, 11, 12.

9. Namna gani mateso yanaweza kutusafisha na kutusaidia kumukaribia zaidi Mungu?

9 Faida ya tano: Kutokujua ile siku na ile saa kunasaidia ili mateso tunayopata leo yatusafishe na kutia nguvu imani yetu. (Soma Zaburi 119:71.) Kwa kweli, siku za mwisho za ulimwengu huu ni ‘ngumu kushugulika nazo.’ (2 Tim. 3:1-5) Watu wengi wanatuchukia, kwa hiyo tunaweza kuteswa kwa sababu ya imani yetu. (Yoh. 15:19; 16:2) Ikiwa tunaonyesha unyenyekevu na kufuata uongozi wa Mungu tunapopambana na majaribu, imani yetu itasafishwa kama vile chuma inavyosafishwa kwa moto. Hatutavunjika moyo. Lakini, jambo hilo litatusaidia tumukaribie Yehova zaidi kuliko tulivyowazia.​—Yak. 1:2-4; 4:8.

10. Tunapaswa kufanya nini ili tuone kama wakati unapita haraka?

10 Wakati kupita haraka ao polepole kunategemea kile tunachofanya. Tunapokuwa na kazi mingi ya kufanya hatutakuwa na wakati wa kuangalia saa, na kwa hiyo, tutaona kama wakati unapita haraka. Vilevile, ikiwa tunatia mawazo yetu yote katika kazi ya Yehova yenye kuleta furaha, ile siku na ile saa inaweza kufika bila hata sisi kujua. Kuhusu jambo hilo, Wakristo wengi watiwa-mafuta wametuwekea mufano muzuri. Acheni turudilie mambo yaliyotokea kisha Yesu kupewa Ufalme katika mwaka wa 1914, na tuone namna Wakristo wengi watiwa​-mafuta walivyoonyesha kama walikuwa tayari na namna wengine walikosa kuwa tayari.

WALIONYESHA KAMA WALIKUWA TAYARI

11. Kisha mwaka 1914, sababu gani watiwa​-mafuta fulani walifikiri kama Bwana alikuwa mwenye kuchelewa?

11 Kumbuka mifano miwili ya Yesu kuhusu mabikira na talanta. Ikiwa mabikira ao watumwa hao wangejua wakati ambao bwana​-arusi ao bwana yao atafika, haingekuwa lazima wakeshe. Lakini hawakujua, kwa hiyo walipaswa kuwa tayari. Ijapokuwa kwa miaka mingi watiwa​-mafuta walijua kama mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka uliotiwa alama, hawakujua waziwazi ni mambo gani yangetokea. Wakati mambo hayakutokea kama walivyotazamia, ilionekana kama Bwana-arusi alikuwa mwenye kuchelewa. Ndugu mumoja alikumbuka hivi baadaye: “Watu wachache kati yetu waliamini kabisa kama tutaenda mbinguni katika juma la kwanza la Mwezi wa 10, mwaka wa 1914.”

12. Namna gani watiwa​-mafuta walijionyesha kuwa waaminifu na wenye busara?

12 Kungojea mwisho ambao haukufika lilikuwa jambo lenye kuvunja moyo sana! Zaidi ya hilo, watiwa​-mafuta waliteswa sana wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Wakati huo, kazi ya kuhubiri ilisimama na ilionekana kama watiwa-mafuta wamelala usingizi. Lakini katika mwaka wa 1919, jambo fulani liliwalamusha. Yesu alikuwa amekuja katika hekalu la Mungu la kiroho, na saa ya kufanya ukaguzi ilikuwa imefika. Kwa hiyo, watiwa​-mafuta fulani walionekana kuwa hawastahili tena kuendelea kumutumikia Bwana wao, Yesu. (Mt. 25:16) Ilionekana kama hawana bidii; walikosa kuongeza mafuta katika taa zao kama mabikira wale wapumbavu. Na kama mutumwa muvivu, hawakupenda kujitoa ili kuendeleza faida za Ufalme. Lakini, watiwa​-mafuta wengi walikuwa waaminifu na walikuwa na tamaa sana ya kumutumikia Bwana wao hata katika miaka hiyo ya vita.

13. Wakristo watiwa-mafuta walionyesha sifa gani kisha mwaka wa 1914, na wanaonyesha sifa gani leo?

13 Kisha mwaka wa 1914, Munara wa Mulinzi ulisema hivi: ‘Ndugu, wale miongoni mwetu walio na maoni yafaayo kuelekea Mungu hawavunjike moyo kuhusu mipango Yake, haizuru gani. Sisi hatukutaka mapenzi yetu wenyewe yafanyike; kwa hiyo, tulipoona kwamba jambo tulilotazamia halikutimizwa katika Mwezi wa 10, mwaka wa 1914, basi tulifurahi kwamba Bwana hakubadilisha Mupango Wake ili upatane na mawazo yetu. Sisi hatukutaka Yeye abadilishe mupango wake. Sisi tunataka tu tuweze kuelewa mipango na makusudi Yake.’ Leo watiwa-mafuta wa Bwana wangali tu wanaonyesha unyenyekevu na ushikamanifu kama huo. Hawaseme kama wanapuliziwa na roho ya Mungu, lakini wameazimia tu kufanya kazi ambayo Bwana amewaomba wafanye duniani. Na sasa leo, mukutano mukubwa wa “kondoo wengine,” Wakristo walio na tumaini la kuishi duniani wanawaiga; wanaendelea kukesha na kumutumikia Mungu kwa bidii.​—Ufu. 7:9; Yoh. 10:16.

TUONYESHE KAMA TUKO TAYARI

14. Sababu gani ni vizuri kutii maagizo tunayopewa na mutumwa mwaminifu?

14 Wakristo wa mukutano mukubwa wanaiga Wakristo watiwa-mafuta kwa kushikamana na mupango ambao Mungu anatumia ili kutoa chakula cha kiroho. Kwa kufanya hivyo, wanaonyesha kama wao pia wanaendelea kuongeza mafuta katika taa zao, ni kusema Neno la Mungu na roho yake. (Soma Zaburi 119:130; Yohana 16:13.) Kwa hiyo, wao pia wanajitayarisha kwa ajili ya kurudi kwa Kristo kwa kuwa na bidii hata katika majaribu. Kwa mufano, katika gereza moja ya Nazi, ndugu walikuwa na Biblia moja tu. Kwa hiyo walisali ili kupata chakula kingine cha kiroho. Kisha muda kidogo, walitambua kama mufungwa mumoja mupya, aliyekuwa ndugu, alificha magazeti fulani mapya ya Munara wa Mulinzi katika muguu wake wa mbao na kuyaingiza kwa siri katika gereza. Ndugu Ernst Wauer, Mukristo mutiwa-mafuta, aliyekuwa mumoja wa wafungwa hao, alisema hivi baadaye: “Yehova alitusaidia katika njia ya ajabu tukumbuke moyoni mawazo ya kuimarisha ya magazeti hayo.” Tena alisema hivi: “Siku hizi, ni rahisi sana kupata chakula cha kiroho, lakini, je, tunakisamini sikuzote? Niko hakika kwamba Yehova anawekea baraka nyingi wale wanaomutumaini, wanaobaki washikamanifu, na kula kwenye meza yake.”

15, 16. Ndugu mumoja na bibi yake walipata matokeo gani mazuri kwa sababu ya bidii yao, na mifano kama hiyo inatufundisha nini?

15 Kondoo wengine wanategemeza ndugu za Kristo kwa kufanya mengi katika kazi ya Bwana. (Mt. 25:40) Tofauti na mutumwa muovu na muvivu katika mufano wa Yesu, wanafurahia kujitoa na kufanya yao yote ili kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza. Kwa mufano, walipoalikwa ili kuhubiria watu wanaozungumuza Kishinwa wanaoishi Kenya, Jon na Masako hawakuwa hakika kama wataenda. Lakini kisha kusali na kufikiria kwa uzito hali yao, waliamua kuhamia huko.

16 Kwa sababu ya bidii yao, walipata matokeo mazuri. Walisema hivi: “Utumishi hapa unafurahisha.” Walianzisha mafunzo saba ya Biblia. Na walipata matokeo mengine mazuri. Kwa mwisho walisema hivi: “Kila siku tunamushukuru Yehova kwa kutuwezesha kuwa hapa.” Kwa kweli kuna ndugu na dada wengi ambao wameonyesha kama wanataka kufanya mengi katika kazi ya Mungu bila kujali kama mwisho utakuja wakati gani. Fikiria wengi waliosoma Masomo ya Gileadi na ambao wametumika kazi ya umisionere. Unaweza kupata habari zaidi kuhusu kazi ya umisionere kwa kusoma habari yenye kichwa “Tunafanya Yote Tuwezayo!” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15/10/2001. Unaposoma habari hiyo yenye kufurahisha kuhusu kazi ya umisionere, fikiria njia mbalimbali unazoweza kutumia ili kupanua utumishi wako kwa utukufu wa Mungu. Kufanya hivyo kutakuletea furaha.

WEWE PIA UENDELEE KUKESHA

17. Namna gani tumepata faida sababu ya kutokujua wakati mwisho utakuja?

17 Bila shaka, tumepata faida nyingi sababu ya kutokujua wakati gani mwisho utakuja. Kuliko kuvunjika moyo, tunamukaribia zaidi Yehova Baba yetu mwenye upendo tunapofanya yetu yote ili kufanya mapenzi yake. Kuweka mukono wetu kwenye jembe la ngombe, ni kusema, kufanya kwa bidii kazi ya Bwana, kumesaidia akili yetu isikengeushwe na kumetuletea furaha nyingi.​—Lu. 9:62.

18. Sababu gani tuendelee kumutumikia Mungu kwa uaminifu?

18 Siku ya hukumu ya Mungu inakaribia sana. Hakuna mumoja kati yetu anayetaka kumuhuzunisha Yehova ao Yesu. Yehova na Yesu wametupatia pendeleo nzuri katika siku hizi za mwisho, ni kusema, kuwatumikia. Hilo linaonyesha kama wanatutumainia kabisa!​—Soma 1 Timotheo 1:12.

19. Namna gani tunaweza kujitayarisha kuokoka mwisho wa ulimwengu huu?

19 Iwe tuna tumaini la kuenda mbinguni ao la kuishi katika Paradiso duniani, acheni tuendelee kufanya kwa uaminifu kazi tuliyopewa na Mungu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Hatujue kabisa kabisa siku ao saa ya siku ya Yehova, na hatuna lazima ya kujua. Tunaweza na tutaendelea kuwa tayari. (Mt. 24:36, 44) Tunaamini kabisa kama Yehova hatatudanganya ikiwa tunamutumaini na kutia Ufalme pa nafasi ya kwanza.​—Rom. 10:11.

[Maelezo ya chini]

^ Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 2012, ukurasa wa 14-18.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 26]

Hata katika hali ngumu, tafuta chakula cha kiroho

[Picha katika ukurasa wa 27]

Wakati unapita haraka tunapokuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Mungu