Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anakusanya Watu Wake Wenye Furaha

Yehova Anakusanya Watu Wake Wenye Furaha

Yehova Anakusanya Watu Wake Wenye Furaha

‘Wakutanishe watu, wanaume na wanawake na watoto wadogo na mukaaji mugeni.’​—KUM. 31:12.

UNGEJIBU NAMNA GANI?

Kwa nini tunaweza kusema kama mikusanyiko ni vipindi vya pekee sana katika historia ya Mashahidi wa Yehova?

Ni nguvu gani ambazo Waisraeli wengi walifanya ili kuhuzuria sikukuu za kila mwaka katika Yerusalemu?

Kwa nini haupaswe kukosa hata mukusanyiko mumoja?

1, 2. Tutajifunza nini kuhusiana na mikusanyiko yetu katika habari hii?

 KWA miaka mingi, Mashahidi wa Yehova wanafanya mikusanyiko ya kimataifa na ya wilaya. Wengi kati yetu wamekwisha kuhuzuria mikusanyiko mingi kati ya mikusanyiko hiyo yenye kufurahisha, labda wamefanya hivyo kwa miaka mingi.

2 Zamani, watu wa Mungu walikuwa pia wanafanya mikusanyiko. Tutachunguza Maandiko fulani yanayozungumuzia mikusanyiko hiyo; uwe mwangalifu ili kuona namna mikusanyiko tunayofanya leo inavyopatana na ile ya watumishi wa Mungu wa kale, na ufikirie baraka tunazopata tunapohuzuria mikusanyiko hiyo.​—Zab. 44:1; Rom. 15:4.

WAKATI WA ZAMANI NA LEO

3. (a) Ni nini iliyotendeka kwenye mukusanyiko wa kwanza wa watu wa Yehova unaozungumuziwa katika Biblia? (b) Namna gani Waisraeli waliitwa ili wafike mahali pa mukusanyiko?

3 Mukusanyiko uliofanywa kwenye Mulima Sinai ulikuwa ndio mukusanyiko wa kwanza mukubwa ambao watu wa Mungu walifanya ili wafundishwe na Yehova. Ulikuwa mukusanyiko wa pekee sana katika historia ya watu wa Mungu. Mukusanyiko huo ulifurahisha sana wahuzuriaji na hawangeweza kusahau jambo hilo katika maisha yao. Hapo Yehova alionyesha Waisraeli uwezo wake wakati alipowatolea Sheria yake. (Kut. 19:2-9, 16-19; soma Kutoka 20:18; Kumbukumbu 4:9, 10.) Kuanzia wakati huo, Mungu alianza kuwatendea Waisraeli kwa njia ya pekee. Muda mufupi kisha tukio hilo, Yehova alimuonyesha Musa vyombo anavyopaswa kutumia ili kukusanya Waisraeli. Alimuambia Musa atengeneze tarumbeta mbili za feza, ambazo atakuwa anatumia ili kuita “kusanyiko lote” likutane ‘kwenye mwingilio wa hema la mukutano.’ (Hes. 10:1-4) Wazia namna watu walivyokuwa wenye furaha sana wakati walikuwa wakihuzuria mikusanyiko hiyo!

4, 5. Kwa nini mikusanyiko iliyotayarishwa na Musa na Yoshua ilikuwa ya maana sana?

4 Waisraeli walipitisha miaka 40 katika jangwa. Walipokaribia kumaliza miaka hiyo, Musa alikusanya Waisraeli wote. Mukusanyiko huo ulifanyika kwa wakati unaofaa kwa sababu taifa hilo mupya lilikuwa karibu kuingia katika Inchi ya Ahadi. Musa alitumia wakati huo muzuri ili kukumbusha ndugu zake mambo yote ambayo Yehova alikuwa amewafanyia na yale ambayo angewafanyia.​—Kum. 29:1-15; 30:15-20; 31:30.

5 Labda kwenye mukusanyiko huo, Musa aliwaelezea Waisraeli kuhusu mipango ya kawaida ya kufanywa kwa mukusanyiko na kuhusu kufundishwa kwa watu wa Mungu. Katika miaka ya sabato, ni kusema, kisha miaka saba, wakati wa Sikukuu ya Vibanda, wanaume, wanawake, watoto, na wakaaji wageni wa Israeli walipaswa kukusanyika mahali ambapo Yehova alichagua ‘ili wasikilize na kujifunza kumuogopa Yehova na kuwa waangalifu kutimiza maneno yote ya sheria.’ (Soma Kumbukumbu 31:1, 10-12.) Kwa hiyo, inaonekana wazi kwamba mwanzoni tu mwa historia ya watu wa Mungu, Yehova alipenda watu wake wakusanyike pamoja mara kwa mara ili wajifunze Neno lake na makusudi yake. Kisha Waisraeli walipata ushindi juu ya miji yote ya Inchi ya Ahadi, hata hivyo, walikuwa bado wenye kuzungukwa na mataifa ya wapagani. Kwa hiyo, Yoshua akakusanya Waisraeli wote ili kuwatia moyo washikamane na Yehova. Siku hiyo, Waisraeli wote wakafanya kiapo kwamba watamutumikia Mungu.​—Yos. 23:1, 2; 24:1, 15, 21-24.

6, 7. Ni mikusanyiko gani ambayo imekuwa ya pekee sana katika historia ya Mashahidi wa Yehova wa siku hizi, na sababu gani?

6 Katika historia ya Mashahidi wa Yehova leo, kumefanyika pia mikusanyiko ya pekee sana. Ni kwenye mikusanyiko hiyo ndipo kunatangazwa mabadiliko makubwa ambayo yametokea katika tengenezo na miangaza mipya kuhusu Maandiko fulani. (Met. 4:18) Kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu katika mwaka wa 1919 huko Cedar Point, Ohio, États-Unis, Wanafunzi wa Biblia walifanya mukusanyiko mukubwa wa kwanza. Kwenye mukusanyiko huo uliohuzuriwa na watu karibu 7 000, ilitangazwa kwamba watu wa Mungu watafanya kwa bidii kampanye ya pekee ili kuhubiri duniani pote. Katika mwaka wa 1922, mukusanyiko wa siku kenda ulifanywa mahali hapo hapo. Ndugu Joseph Rutherford, alitoa hotuba moja motomoto ili kutia moyo wahuzuriaji waendelee kuhubiri mahali pote. Aliwaambia hivi: ‘Iweni mashahidi waaminifu na wa kweli wa Bwana. Songeni mbele katika vita mupaka kila sehemu ya Babiloni ibaki ukiwa. Mutangaze ujumbe kotekote. Lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mufalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Hii ndiyo siku ya siku zote. Tazameni, Mufalme anatawala! Nyinyi ndio mawakili wake. Kwa hiyo tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mufalme na ufalme wake.’ Wote waliohuzuria, na watu wa Mungu duniani pote, walianza kuhubiri kwa bidii sana.

7 Kwenye mukusanyiko wa mwaka wa 1931, huko Columbus, Ohio, Wanafunzi wa Biblia walikubali kwa furaha jina Mashahidi wa Yehova. Kisha katika mwaka wa 1935, huko Washington, D.C., Ndugu Rutherford alifasiria maana ya ‘mukutano mukubwa unaosimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo’ kulingana na kitabu cha Ufunuo. (Ufu. 7:9-17) Katika mwaka wa 1942, katikati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu, ndugu Nathan Knorr alitoa hotuba yenye kuvutia sana yenye kichwa, “Amani​—Je, Inaweza Kudumu?” Katika hotuba hiyo, alifasiria ‘munyama-mwitu mwenye rangi nyekundu’ anayezungumuziwa katika Ufunuo sura ya 17, na akaonyesha kama kungekuwa kazi kubwa ya kuhubiri kisha vita.

8, 9. Sababu gani mikusanyiko mingine ilionekana kuwa yenye kuchangamusha moyo kabisa?

8 Kwenye mukusanyiko wenye kichwa, “Mataifa Yenye Shangwe” uliofanywa katika mwaka wa 1946 huko Cleveland, Ohio, Ndugu Knorr alitoa hotuba yenye kupendeza sana yenye kichwa, “Matatizo ya Kujenga Upya na Upanuzi.” Kuhusu hotuba hiyo, ndugu mumoja aliyehuzuria anazungumuzia namna wahuzuriaji walivyofurahi sana. Anasema: “Nilikuwa na pendeleo la kuwa nyuma ya Ndugu Knorr kwenye jukwaa mangaribi hiyo, alipoeleza mipango ya kazi ya ujenzi na mipango ya kupanua makao ya Wanabeteli na majengo ya mahali pa kuchapisha vitabu huko Brooklyn; wahuzuriaji walipiga mikono bila kuacha. Hata kama ilikuwa vigumu kutambua sura za watu, ilikuwa rahisi kuona kama watu walikuwa wenye furaha sana.” Kwenye mukusanyiko wa kimataifa huko New York City katika mwaka wa 1950, wahuzuriaji walifurahi sana kupokea Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, Biblia ya kwanza yenye usemi rahisi iliyorudisha jina la Mungu mahali pake katika Neno lake.​—Yer. 16:21.

9 Mikusanyiko mingine iliyofanywa katika inchi ambamo Mashahidi wa Yehova hapo mbele waliteswa sana na hawakuruhusiwa kuhubiri ilikuwa pia yenye kuchangamusha moyo. Adolf Hitler aliapa kwamba atawaharibu Mashahidi wa Yehova katika Alemanye, lakini katika mwaka wa 1955, Mashahidi 107 000 walikusanyika Nuremberg, mahali ambapo Hitler alizoea kukusanya maaskari wake. Wahuzuriaji wengi walilia kwa furaha! Mikusanyiko yenye kichwa, “Kujitoa kwa Mungu” ilifanywa katika Polonye katika mwaka wa 1989. Wengi kati ya watu 166 518 waliohuzuria, walitoka katika ile iliyoitwa zamani Union soviétique na Tchécoslovaquie, na katika inchi zingine za Ulaya Mashariki. Kwa wahuzuriaji fulani, ilikuwa mara yao ya kwanza kuhuzuria mukusanyiko uliokuwa na watu zaidi ya 15 ao 20. Wazia furaha ya wahuzuriaji kwenye Mukusanyiko wa Kimataifa wenye kichwa, “Ufundishaji wa Kimungu” uliofanywa huko Kiev, Ukraine, ambako watu 7 402 walibatizwa kwa siku moja; huo ulikuwa ubatizo wa kwanza wenye watu wengi katika historia ya Mashahidi wa Yehova.​—Isa. 60:22; Hag. 2:7.

10. Ni mikusanyiko gani ya pekee ambayo ungali bado unakumbuka, na kwa sababu gani?

10 Labda kuna mikusanyiko ya kimataifa ao ya wilaya ambayo ungali bado unakumbuka. Je, unakumbuka mukusanyiko wa kwanza ambao ulihuzuria ao ule ambako ulibatizwa? Mikusanyiko hiyo ilikuwa ya pekee sana kwako. Uendelee kukumbuka matukio hayo!​—Zab. 42:4.

MIKUSANYIKO YA KILA MWAKA YENYE KUFURAHISHA

11. Ni sikukuu gani zilizofanywa kila mwaka ambazo Mungu aliwaomba Waisraeli wahuzurie?

11 Yehova aliwaomba Waisraeli wakusanyike Yerusalemu ili kuazimisha sikukuu tatu kila mwaka: Sikukuu ya Keki Zisizotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma (ambayo baadaye iliitwa Pentekoste), na Sikukuu ya Vibanda. Kuhusu sikukuu hizo, Mungu aliamuru hivi: “Pindi tatu katika mwaka kila mwanamume wa kwako ataonekana mbele za uso wa Bwana wa kweli, Yehova.” (Kut. 23:14-17) Baba wengi walitambua kwamba sikukuu hizo ni za maana sana, kwa hiyo walienda huko Yerusalemu ili kuhuzuria pamoja na familia zao.​—1 Sam. 1:1-7; Lu. 2:41, 42.

12, 13. Waisraeli wengi walifanya nini ili kuhuzuria sikukuu za kila mwaka?

12 Haikuwa rahisi kwa familia nzima kufanya safari hiyo. Kwa mufano, Yosefu na Maria walilazimika kusafiri kilometre 100 kutoka Nazareti mupaka Yerusalemu. Unafikiri safari hiyo inaweza kukuchukua siku ngapi kwa muguu pamoja na watoto wadogo? Habari inayozungumuzia Yesu alipokuwa bado kijana na safari yao huko Yerusalemu inaonyesha kama watu wa familia moja na marafiki walikuwa wanafanya safari hizo wakiwa katika vikundi. Ni kweli kwamba walifurahia mambo mengi walipokuwa wanasafiri pamoja; kama vile kutayarisha chakula pamoja na kutafuta mahali pazuri pa kulala katika sehemu ambamo walikuwa wageni. Inaonekana walisafiri kwa usalama kwa sababu wazazi wa Yesu walimuachia uhuru fulani hata ikiwa alikuwa na miaka 12 tu. Hakuna mutu ambaye angesahau sikukuu hizo, zaidi sana vijana!​—Lu. 2:44-46.

13 Waisraeli walipokuwa wameenea katika sehemu mbalimbali inje ya inchi yao, wale waliokuja kuhuzuria sikukuu hizo walitoka katika mataifa mengi. Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, Wayahudi waliofurahia mambo ya kiroho na watu wa mataifa walioamini dini ya Wayahudi walifunga safari mupaka Yerusalemu; walitoka Italie, Libya, Krete, Asia Ndogo, na Mesopotamia.​—Mdo. 2:5-11; 20:16.

14. Waisraeli walipata faida gani kwa kuhuzuria sikukuu za kila mwaka?

14 Sababu kubwa iliyowachochea Waisraeli waaminifu wafunge safari na kuenda kuhuzuria sikukuu hizo ni kumuabudu Yehova pamoja na maelfu ya waabudu wengine waliofurahia mambo ya kiroho. Wale waliohuzuria walijisikia namna gani? Jibu linapatikana katika maagizo ambayo Yehova alitolea watu wake kuhusu Sikukuu ya Vibanda: ‘Utashangilia wakati wa sherehe yako, wewe na mwana wako na binti yako na mutumishi wako na kijakazi wako na Mulawi na mukaaji mugeni na muvulana asiye na baba na mujane, walio ndani ya malango yako. Siku saba utamufanyia Yehova Mungu wako sherehe katika mahali ambapo Yehova atapachagua, kwa sababu Yehova Mungu wako atakubariki katika mazao yako yote na katika kila tendo la mukono wako, nawe utakuwa na shangwe kwelikweli.’​—Kum. 16:14, 15; soma Mathayo 5:3.

TUFURAHIE MIKUSANYIKO YA SIKU ZETU

15, 16. Ulijinyima mambo gani ili uhuzurie mikusanyiko? Na ulipata baraka gani?

15 Mikusanyiko hiyo ya zamani ya watu wa Mungu inatuachia mufano muzuri leo! Hata ikiwa miaka mingi imepita na mambo mengi yamebadilika, kusudi la mikusanyiko halijabadilika. Zamani, waliohuzuria mikusanyiko walipaswa kujinyima mambo fulani ili wahuzurie. Ndugu wengi wanafanya hivyo leo. Na hawakose kupata baraka nyingi sana. Mikusanyiko hiyo ya zamani na ya leo ni vipindi vyenye kufurahisha sana kiroho na jambo hilo ni la lazima. Mikusanyiko hiyo inatutolea habari mbalimbali na kutusaidia tuelewe mambo ya maana sana ili tuendelee kulinda urafiki wetu pamoja na Mungu. Mikusanyiko inatuchochea tutumie katika maisha mambo tunayojifunza, inatusaidia tuepuke magumu, na inatutia moyo tukazie uangalifu wetu na kufuatilia mambo ambayo yatatuburudisha kiroho kuliko kufuatilia mambo ambayo yatatuchokesha.​—Zab. 122:1-4.

16 Kila mara wahuzuriaji wanazungumuzia furaha waliyopata kwa kuhuzuria mikusanyiko yetu. Ripoti moja kutoka mukusanyiko moja mukubwa uliofanywa katika mwaka wa 1946 ilisema hivi: “Lilikuwa jambo lenye kufurahisha sana kuona maelfu ya mashahidi wakiwa pamoja na wakiwa wenye kutulia. Na ilifurahisha hata zaidi kusikiliza sauti za watu kama kikundi kimoja cha wapiga muziki wakiimba kwa furaha nyimbo za Ufalme ili kumutukuza Yehova.” Ripoti hiyo inaongeza: “Biro ya Wafanyakazi wa Kujipendea ilipata wafanyakazi wengi waliofurahia kutumikia ndugu zao.” Je, wewe pia umewahi kujisikia mwenye furaha hivyo kwenye mikusanyiko ya kimataifa ao ya wilaya?​—Zab. 110:3; Isa. 42:10-12.

17. Ni mabadiliko gani yaliyofanywa kuhusu mikusanyiko?

17 Mambo fulani yamebadilika kuhusu namna mikusanyiko inavyofanywa leo. Kwa mufano, kuna wale kati yetu wanaokumbuka kwamba mikusanyiko ilikuwa inafanya siku munane! Kulikuwa vipindi vya asubuhi, vipindi vya kisha midi, na vipindi vya mangaribi. Kwenye mikusanyiko kulikuwa kila mara programu ya mahubiri. Wakati fulani programu ilikuwa inaanza saa tatu asubuhi mupaka saa tatu ya usiku. Wafanyakazi wa kujipendea walikuwa wanatumika sana ili kutayarishia wahuzuriaji chakula cha asubuhi, cha midi na cha mangaribi. Leo, mikusanyiko inafanya siku chache, na kila mutu ao kila familia inajitayarishia chakula mbele ya wakati ili kila mutu afuate vizuri programu hiyo ya kiroho.

18, 19. Ni sehemu gani za mikusanyiko ambazo unafurahia zaidi? Na sababu gani?

18 Kuna mambo fulani ya programu ya mikusanyiko ambayo kila mara tunatazamia kwa hamu na ambayo hayakubadilika. Tunatazamia kila mara kupata ‘chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa’ ambacho kinatusaidia tuelewe vizuri unabii mbalimbali wa Biblia na mafundisho mengine. Tunakipata kupitia hotuba mbalimbali na vitabu vipya vinavyotokea kwenye mikusanyiko. (Mt. 24:45) Vitabu hivyo ni vyombo vinavyosaidia mara nyingi watu wenye mioyo mizuri wapendezwe na ukweli wa Maandiko. Drama zenye kuchochea zinatia moyo vijana na watu wazima kuchunguza makusudi yao na kujilinda na mikazo inayotokana na mawazo ya ulimwengu huu muovu. Hotuba ya ubatizo pia inatutolea sisi wote nafasi ya kuchunguza tena mambo tunayotia pa nafasi ya kwanza maishani na furaha ya kuona namna wengine wanavyobatizwa ili kuonyesha kama wamejitoa kwa Yehova katika sala.

19 Bila shaka mikusanyiko ni sehemu ya maana ya ibada safi. Mikusanyiko inawasaidia watu wa Yehova wenye furaha wamutumikie kwa njia inayofaa katika siku hizi mbaya. Mikusanyiko hiyo inatutolea vitia-moyo, nafasi za kukutana na marafiki wapya, inatusaidia kupenda sana ndugu na dada zetu, na ni njia ambayo Yehova anatumia ili kubariki watu wake na kuonyesha kama anawahangaikia. Hakika, kila mumoja atapenda kupanga mambo yake vizuri ili kuhuzuria na kufaidika na kila kipindi cha kila mukusanyiko.​—Met. 10:22.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 30]

Mukusanyiko wa kimataifa katika mwaka wa 1950 huko New York City

[Picha katika ukurasa wa 32]

Mozambique

[Picha katika ukurasa wa 32]

Corée du sud