Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Masomo Mbalimbali Yanayoongozwa na Tengenezo la Mungu Yanaonyesha Upendo wa Yehova

Masomo Mbalimbali Yanayoongozwa na Tengenezo la Mungu Yanaonyesha Upendo wa Yehova

Masomo Mbalimbali Yanayoongozwa na Tengenezo la Mungu Yanaonyesha Upendo wa Yehova

YEHOVA ni ‘Mufundishaji [wetu] Mukubwa.’ (Isa. 30:20) Upendo wake unamuchochea kufundisha na kuzoeza watumishi wake. Kwa mufano, kwa sababu ya upendo, Yehova anamuonyesha Yesu “mambo yote anayofanya yeye mwenyewe.” (Yoh. 5:20) Kwa sababu Yehova anatupenda, yeye anatupatia “ulimi wa waliofundishwa,” tunapojikaza ili kumusifu na kuwasaidia wengine.​—Isa. 50:4.

Halmashauri ya ufundishaji ya Baraza Linaloongoza inamuiga Yehova. Kwa sababu hiyo, inatumia masomo kumi ili kuwazoeza wale walio na nia na ambao hali zao zinawaruhusu kujiandikisha. Je, wewe pia unaona masomo hayo kuwa alama inayoonyesha upendo wa Yehova?

Soma kuhusu masomo hayo na maelezo ya watu fulani ambao wamekwisha kuhuzuria masomo hayo. Kisha ujiulize, ‘Namna gani ninaweza kufaidika na elimu hii inayotoka kwa Mungu?’

FAIDIKA NA MAZOEZI YA KITEOKRASI

Yehova “Mungu wa upendo,” anatutolea mazoezi yanayotusaidia kuwa na maisha yenye kusudi, kushindana na matatizo, na yanayotusaidia ili kupata furaha nyingi katika mahubiri. (2 Kor. 13:11) Kama wanafunzi wa kwanza wa Yesu, tuna vyombo vya kazi vya kutosha ili kuwasaidia wengine, “kuwafundisha kushika mambo yote” ambayo tumeamuriwa.​—Mt. 28:20.

Hata ikiwa hatuweze kuhuzuria masomo hayo yote, labda tunaweza kuhuzuria moja ao zaidi. Na tunaweza kutumikisha maagizo tuliyojifunza kutokana na mazoezi hayo ya Biblia. Pia, tunaweza kufanya utumishi wetu uwe wenye matokeo zaidi kwa kuhubiri pamoja na watumishi wa Yehova ambao wamezoezwa vizuri kwenye masomo hayo.

Ujiulize hivi: ‘Je, hali zangu zinaniruhusu nistahili kuhuzuria hata moja ya masomo hayo?’

Watumishi wa Yehova wanaliona kuwa pendeleo kutegemeza na kuhuzuria masomo hayo. Utakapopata mazoezi hayo, acha yakusaidie kumukaribia Mungu zaidi na yakupatie vyombo vya kazi ili utimize madaraka uliyopewa na Mungu, zaidi sana daraka la kuhubiri habari njema bila kupoteza wakati.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 13-17]

MASOMO MBALIMBALI YANAYOONGOZWA NA TENGENEZO LA MUNGU

Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Kusudi: Kuzoeza ndugu na dada ili wawe wahubiri na walimu wa habari njema wenye matokeo mazuri.

Muda:u Mazoezi ya kuendelea.

Mahali: Jumba la Ufalme la mahali penu.

Wanaoweza Kujiandikisha: Wahubiri wote. Pia, wengine wanaoshirikiana kwa ukawaida na kutaniko, ambao wanakubali mafundisho ya Biblia, na ambao maisha yao yanapatana na kanuni za Kikristo.

Jinsi ya Kujiandikisha: Zungumuza na mwangalizi wa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika kutaniko lenu.

Sharon ambaye amepooza kwa sababu ya ugonjwa wa mishipa ya ufahamu anasema hivi: “Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi yalinisaidia kutafuta habari katika vitabu na kutoa habari kwa njia yenye kueleweka. Nimejifunza pia kufikiria mahitaji ya kiroho ya wengine wala si yangu mwenyewe tu.”

Arnie, ambaye amekuwa mwangalizi anayesafiri kwa miaka mingi, anasema hivi: “Nilikuwa na kigugumizi na ilikuwa vigumu kwangu kuwatazama watu ninapozungumuza nao. Masomo hayo yamemaliza woga wangu na kunisaidia nijisikie kama mimi pia ni mutu wa lazima. Kupitia mazoezi haya, Yehova amenisaidia; nimejifunza jinsi ya kupumua vizuri ninapozungumuza na kukazia akili juu ya mambo ninayozungumuzia. Ninafurahia sana uwezo niliopata wa kumusifu Yehova katika kutaniko na katika mahubiri.”

Masomo ya Wanabeteli Wapya

Kusudi: Masomo haya yametayarishwa ili kuwasaidia Wanabeteli wapya watimize vizuri utumishi wao wa Beteli.

Muda: Dakika 45 kila juma kwa muda wa majuma 16.

Mahali: Beteli.

Wanaostahili Kuhuzuria: Washiriki wenye kudumu wa familia ya Beteli ao wale ambao wamejitolea na wamekubaliwa kutumikia kwenye Beteli kwa muda wa mwaka mumoja ao zaidi.

Jinsi ya Kujiandikisha: Wanabeteli wapya wanaandikishwa na Beteli.

Ndugu Demetrius, aliyehuzuria masomo hayo katika miaka ya 1980 anasema hivi: “Masomo hayo yalinisaidia kuwa na tabia nzuri ya kujifunza na yalinitayarisha vizuri ili niweze kutumikia Beteli kwa miaka mingi. Waalimu, programu ya masomo, na mashauri yanayofaa yalinisadikisha kama Yehova ananihangaikia na kama alitaka kunisaidia ili nifanye vizuri utumishi wangu wa Beteli.”

Dada Kaitlyn anaeleza hivi: “Masomo hayo yalinisaidia kukazia akili yangu mambo ya maana zaidi, ni kusema, kuwa mutu wa kiroho. Masomo ya Wanabeteli Wapya yamenisaidia nimupende sana Yehova, niipende Beteli na nilipende tengenezo la Yehova.”

Masomo ya Huduma ya Ufalme

Kusudi: Kuzoeza waangalizi wenye kusafiri, wazee, na wakati fulani watumishi wa huduma ili washugulikie vizuri madaraka yao ya uangalizi na usimamizi. (Mdo. 20:28) Kwenye masomo hayo wanajifunza namna ya kushugulikia hali, mielekeo na mahitaji ya makutaniko. Masomo hayo yanafanywa kisha miaka michache. Ni Baraza Linaloongoza ndilo linaamua wakati masomo hayo yanapaswa kufanywa.

Muda: Hivi karibuni masomo hayo yalifanywa kwa muda wa siku mbili ao mbili na nusu kwa ajili ya waangalizi wenye kusafiri, siku moja na nusu kwa ajili ya wazee na siku moja kwa ajili ya watumishi wa huduma.

Mahali: Kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu ao Jumba la Mikusanyiko linatumiwa.

Wanaostahili Kuhuzuria: Waangalizi wenye kusafiri, wazee, ao watumishi wa huduma.

Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee na watumishi wa huduma wanaalikwa na mwangalizi wa muzunguko. Ni biro ya tawi ndio inayoalika waangalizi wenye kusafiri.

Ndugu Quinn (hapa chini) anasema hivi: “Masomo hayo yanafundisha mambo mengi kwa muda mufupi, hata hivyo, yanawasaidia wazee kudumisha furaha yao na ‘kuendelea kuwa kama wanaume’ katika kazi ya Yehova. Wazee ambao wametumika kwa muda murefu na wapya, wote wanajifunza namna ya kuchunga kutaniko vizuri na kuwa wenye kuunganiswa vema ‘katika njia ileile ya kufikiri.’”

Ndugu Michael anaeleza hivi: “Masomo hayo yametusaidia kuelewa vizuri zaidi mambo tunayoamini, yametuonya kuhusu hatari za kiroho, na yametupatia mashauri yanayofaa, yanayoweza kutusaidia kutunza kundi la Mungu. Kwa kweli Yehova ni mwema kabisa kwa kutusaidia hivyo.”

Masomo ya Mapainia

Kusudi: Kusaidia mapainia ‘watimize kwa ukamili huduma yao.’—2 Tim. 4:5.

Muda: Majuma mawili.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu linatumiwa.

Wanaostahili Kuhuzuria: Wale ambao wamekwisha kuwa mapainia wa kawaida kwa mwaka mumoja ao zaidi. *

Jinsi ya Kujiandikisha: Mwangalizi wa muzunguko anaandika mapainia wanaostahili kuhuzuria na anawajulisha.

Dada Lily (kuume) anasema hivi: “Masomo hayo yamenisaidia kupambana na matatizo ninayopata katika mahubiri na katika maisha yangu. Namna yangu ya kujifunza Biblia, kuifundisha, na kuitumia katika mahubiri imekuwa vizuri zaidi kuliko zamani. Sasa nimetayarishwa vizuri ili kuwasaidia wengine, kuwategemeza wazee, na kusaidia kutaniko likomae kiroho.”

Dada Brenda, ambaye amesoma masomo hayo mara mbili, anaeleza hivi: “Masomo hayo yamenisaidia kuzama kabisa katika mambo ya kiroho, kuzoeza zamiri yangu, na kutumia uwezo wangu ili kuwasaidia wengine. Bila shaka, Yehova ni mwema!”

[Footnote]

^ Ikiwa hakuna mapainia wapya wa kutosha, mapainia fulani ambao hawakupata kusoma masomo hayo miaka tano iliyopita wanaweza kualikwa tena.

Masomo ya Wazee wa Kutaniko

Kusudi: Kusaidia wazee washugulikie vizuri madaraka yao katika kutaniko na kuwasaidia watengeneze vizuri zaidi hali yao ya kiroho.

Muda: Siku tano.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu ao Jumba la Mikusanyiko linatumiwa.

Wanaostahili Kuhuzuria: Wazee.

Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee wanaalikwa na biro ya tawi.

Wazee fulani waliohuzuria darasa la 92 la Masomo hayo katika États-Unis walitoa maelezo yafuatayo:

“Masomo haya yameniletea faida nyingi, yamenisaidia kujichunguza na kuona namna ninavyoweza kutunza kondoo za Yehova.”

“Sasa niko tayari ili niweze kuwatia wengine moyo zaidi kwa kukazia mambo makubwa ya Maandiko.”

“Nitatumia mambo niliyojifunza maisha yangu yote.”

Masomo ya Waangalizi Wasafiri na Bibi Zao

Kusudi: Kusaidia waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya wawe na matokeo mazuri zaidi katika kutumikia makutaniko na ‘wanapofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.’—1 Tim. 5:17; 1 Pet. 5:2, 3.

Muda: Miezi miwili.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi.

Wanaostahili Kuhuzuria: Waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya.

Jinsi ya Kujiandikisha: Waangalizi wasafiri na bibi zao wanaalikwa na biro ya tawi.

Ndugu Joel, aliyehuzuria somo la 1, katika mwaka wa 1999, alisema hivi: Furaha yetu kuhusu namna Yesu anavyosimamia tengenezo iliongezeka zaidi. Tuliona kama ni lazima kuwatia ndugu moyo na kusaidia kila kutaniko liwe na umoja. Masomo yalitufundisha kama hata ikiwa wakati fulani mwangalizi anapaswa kutoa shauri na kukaripia, kusudi lake kubwa ni kuwasaidia ndugu wajue kama Yehova anawapenda.”

Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi

Kusudi: Kutayarisha wazee na watumishi wa huduma wasio na bibi ili wachukue madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova. Wengi kati ya wale wanaomaliza masomo hayo wanapewa mugawo wa kutumikia mahali ambapo kuna lazima kubwa katika inchi yao. Wengine kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wako tayari kukubali hilo. Na wengine wanaweza kuwa mapainia wa pekee wa muda ili kufungua maeneo mapya na kupanua kazi ya kuhubiri katika maeneo ya mbali na maeneo yasiyogawiwa makutaniko.

Muda: Miezi miwili.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme linatumiwa.

Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu wasio na bibi walio na umri wa miaka kati ya 23 na 62 ambao wana afya nzuri na wanaotaka kutumikia mahali popote palipo na lazima kubwa. (Mk. 10:29, 30) Wanapaswa kuwa wamefanya kazi ya upainia wa kawaida kwa miaka miwili ao zaidi na kuwa wazee ao watumishi wa huduma kwa miaka miwili hivi ao zaidi bila kukatiza.

Jinsi ya Kujiandikisha: Mukutano unafanywa kwenye mukusanyiko wa muzunguko kwa ajili ya wale wanaotaka kuhuzuria masomo hayo.

Ndugu Rick, mwanafunzi wa somo la 23 katika États-Unis anasema hivi: “Kuzama katika mafundisho ya masomo hayo kumefanya roho ya Yehova inibadilishe kabisa. Yehova anapokupatia kazi fulani, anakusaidia ili uitimize. Nimejifunza kama ikiwa ninajitoa kabisa katika kufanya mapenzi ya Mungu wala si yangu, Yehova atanipa nguvu.”

Andreas, ambaye sasa anatumikia Alemanye, anaeleza hivi: “Nimejifunza kuona kama namna tengenezo la Mungu linavyofanya kazi leo ni muujiza. Masomo hayo yalinisaidia kwa sababu yalinitayarisha kwa ajili ya kazi ya wakati ujao. Tena, mifano mbalimbali ya Biblia ilinifundisha kweli hii ya musingi: Kumutumikia Yehova na ndugu zangu kunaleta furaha ya kweli.”

Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Bibi Zao

Kusudi: Kutolea ndugu na bibi zao mazoezi ya pekee ili Yehova na tengenezo lake wawatumie zaidi. Kati ya wale wanaomaliza masomo hayo, wengi wanapewa mugawo wa kutumikia mahali palipo na lazima katika inchi yao. Wengine kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wanakubali. Wanaohuzuria masomo hayo wanaweza kuwa mapainia wa pekee wa muda ili kufungua maeneo mapya na kupanua kazi ya kuhubiri katika maeneo ya mbali na maeneo yasiyogawiwa makutaniko.

Muda: Miezi miwili.

Mahali: Kwa sasa masomo hayo yanaongozwa katika États-Unis, na kuanzia Mwezi wa 9 2012, biro za tawi fulani katika dunia zitachaguliwa ili kupanga masomo hayo, kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme litatumiwa.

Wanoastahili Kuhuzuria: Ndugu na bibi zao walio na miaka kati ya 25 na 50 na wenye afya nzuri ambao hali zao zinawaruhusu kutumikia mahali popote palipo na lazima na walio na mwelekeo wa kusema: “Mimi hapa! Nitume mimi.” (Isa. 6:8) Pia, wanapaswa kuwa wameoana kwa miaka miwili hivi ao zaidi na kuwa katika utumishi wa wakati wote kwa miaka miwili ao zaidi bila kukatiza. Ndugu anapaswa kuwa muzee ao mutumishi wa huduma kwa miaka miwili hivi ao zaidi bila kukatiza.

Jinsi ya Kujiandikisha: Mukutano unafanywa kwenye mukusanyiko wa wilaya kwa ajili ya wale wanaotaka kuhuzuria masomo hayo. Ikiwa mukutano huo haufanyike katika inchi unamoishi na ikiwa unataka kuhuzuria masomo hayo, unaweza kuandikia biro ya tawi ya inchi yenu ili kupata habari zaidi.

Ndugu Eric na bibi yake Corina (hapa chini), waliohuzuria somo la 1, mwaka wa 2011 wanasema hivi: “Majuma munane hayo yalibadili maisha yetu kabisa na ni pendeleo kabisa kwa wenzi wa ndoa wanaotaka kufanya mengi katika kazi ya Yehova kuhuzuria masomo haya! Tumeazimia kuwa na maoni yanayofaa juu ya maisha, hilo litatusaidia kutumia wakati wetu kwa hekima.”

Masomo ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower

Kusudi: Kuzoeza wanafunzi ili kuwa wamisionere katika maeneo yaliyo na watu wengi, kuwa waangalizi wanaosafiri ao Wanabeteli. Kusudi ni kutia nguvu na kuimarisha kazi ya kuhubiri na biro za tawi.

Muda: Miezi tano.

Mahali: Mahali Pakubwa pa Mafundisho ya Watchtower, huko Patterson, New York, États-Unis.

Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu na bibi zao ambao wamekuwa katika aina fulani ya utumishi wa pekee, ni kusema, wamisionere ambao hawajahuzuria masomo hayo, mapainia wa pekee, waangalizi wanaosafiri, ao Wanabeteli. Wote wawili, ni kusema bwana na bibi, wanapaswa kuwa katika utumishi wa pekee pamoja kwa miaka mitatu hivi ao zaidi bila kukatiza. Wanapaswa kujua kusema, kusoma na kuandika Kiingereza vizuri.

Jinsi ya Kujiandikisha: Biro ya Tawi inaweza kuwaomba wenzi wa ndoa wajaze ombi.

Ndugu Lade na bibi yake Monique walitoka États-Unis na sasa wanatumikia Afrika. Ndugu Lade anasema hivi: “Masomo ya Gileadi yalitutayarisha kuenda mahali popote duniani, sasa tuko tayari kutumika pamoja na ndugu zetu wapendwa.”

Monique anaongezea hivi: “Ninapata furaha kubwa ninapotumia mambo ambayo nimejifunza katika Neno la Mungu. Furaha hiyo inaonyesha kama Yehova anatupenda.”

Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na Bibi Zao

Kusudi: Kusaidia ndugu wanaotumikia katika Halmashauri ya Tawi wasimamie vizuri makao ya Beteli, washugulikie makutaniko, na kazi inayofanywa na waangalizi wa muzunguko na wa wilaya. Wanajifunza pia kuhusu kazi ya kutafsiri, kuchapisha, na kusafirisha vitabu.

Muda: Miezi miwili.

Mahali: Mahali pa kubwa pa Mafundisho ya Watchtower, huko Patterson, New York, États-Unis.

Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu wanaotumika katika Halmashauri ya Tawi ao Halmashauri ya Inchi ao wengine wanaoweza kupewa migawo hiyo kisha kuhuzuria masomo hayo.

Jinsi ya Kujiandikisha: Baraza Linaloongoza linaalika ndugu hao na bibi zao.

Ndugu Lowell na bibi yake Cara, walihuzuria somo la 25, na sasa wanatumika katika Nigeria. Ndugu Lowell anasema hivi: “Nilikumbushwa kama hata kazi yangu iwe nyingi namna gani ao hata kazi yangu iwe ya namna gani, jambo la maana ni kufanya mambo jinsi Yehova anavyotaka ili kumupendeza. Masomo yalionyesha kama ni jambo la maana tuige upendo ambao Yehova anawaonyesha watumishi wake.”

Dada Cara aliongezea hivi: “Nimefikiria shauri hili: Ikiwa siweze kufasiria jambo fulani kwa urahisi, ni lazima nijifunze kwanza habari hiyo mbele ya kuifundisha wengine.”