Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Rushwa Itaisha!

Rushwa Itaisha!

Rushwa Itaisha!

Umutumaini Yehova na kushika njia yake . . . Watu waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.’​—ZABURI 37:34.

KAMA watu wengi, je, wewe pia unawaza kama rushwa (kata-midomo) haiwezi kuepukwa na kama haiwezi kumalizika kabisa? Ikiwa unawaza hivyo, mawazo yako yanaeleweka. Tangu zamani, watu wamejaribu kila namna ya serikali ao guvernema. Lakini, hakuna hata moja ambayo imeweza kumaliza kabisa rushwa. Je, tunaweza kutumaini kama kuna wakati ambapo watu wote watatendeana kwa haki?

Inafurahisha kuona kama jibu la Biblia ni ndiyo! Inatuambia kama hivi karibuni Mungu ataondoa rushwa duniani. Namna gani? Ufalme wake ambao ni serikali ya mbinguni utaigeuza dunia kabisa. Huo ndio Ufalme ambao Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali. Katika sala ya Baba yetu, Yesu alisema hivi: “Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyiwe, duniani.”​—Mathayo 6:10, Verbum Bible.

Juu ya Yesu Kristo, Mufalme wa Ufalme huo, Biblia inatabiri hivi: ‘Atamukomboa masikini anayelilia musaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana musaidizi. Atamusikitikia mutu wa hali ya chini na masikini, naye ataziokoa nafsi za masikini. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri.’ (Zaburi 72:12-14) Hilo linatuonyesha kama Yesu anawasikilia huruma wale wanaoteswa kwa sababu ya rushwa, na kwamba ataondoa ukandamizaji! Hilo ni jambo lenye kufariji kabisa!

Ufalme wa Mungu utakaotawaliwa na Mufalme huyo mwenye nguvu na mwenye kusikilia watu huruma utaondoa rushwa duniani. Namna gani? Kwa kuondoa hivi vishawishi vitatu vinavyotokeza rushwa.

Zambi

Kwa sasa, sisi wote tunapaswa kupiganisha mielekeo ya zambi inayotuchochea kutenda kwa uchoyo. (Waroma 7:21-23) Hata hivyo, kuna watu wazuri wanaotaka kufanya mambo yaliyo sawa. Wanaamini kama damu ya Yesu iliyomwangwa ili kutukomboa ni ya bei sana, na wanaweza kusamehewa zambi zao. * (1 Yohana 1:7, 9) Watu kama hao wanaweza kufaidika na tendo kubwa la upendo wa Mungu; andiko la Yohana 3:16 linasema hivi: ‘Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa​-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.’

Mungu atawafanyia watu waaminifu jambo nzuri sana. Katika dunia mupya inayokuja, ataondoa matokeo yote ya zambi, na polepole atawarudishia watu waaminifu ukamilifu na kuwaona kuwa wenye haki. (Isaya 26:9; 2 Petro 3:13) Kisha, zambi haitachochea tena mutu yeyote kutenda isivyo haki. Wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu, rushwa haitasumbua tena wanadamu waaminifu.

Ulimwengu Muovu Ambamo Tunaishi

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba leo watu wengi wanawatesa wengine kwa makusudi. Wanawaonea watu wa hali ya chini na masikini, na wanawachochea wengine pia watende isivyo haki. Biblia inashauria watu kama hao hivi: ‘Mutu muovu aiache njia yake, na mutu mwenye mazara ayaache mawazo yake.’ Ikiwa watu kama hao wanatubu, Biblia inaahidi kwamba Mungu ‘atawasamehe kwa njia kubwa.’​—Isaya 55:7.

Lakini, jambo ambalo Mungu atafanya ni kuwaondoa tu watu hao waovu ambao hawataki kabisa kubadilika. Kupitia Ufalme wa Mungu, ahadi hii ya Biblia itatimia: ‘Umutumaini Yehova na kuishika njia yake . . . Watu waovu watakapokatiliwa mbali, wewe utaona hilo.’ * (Zaburi 37:34) Kisha kuondolewa kwa watu waovu wasiotaka kubadilika, waabudu waaminifu wa Mungu hawatasumbuka tena kwa sababu ya rushwa.

Shetani Ibilisi

Shetani Ibilisi ndiye mukubwa wa watenda zambi wagumu sana. Tunafurahi sana kujua kama hivi karibuni Yehova atamunyanganya mamlaka yote, na hataweza tena kuwashawishi watu. Mwishowe, Mungu atamuharibu milele. Adui huyo mubaya sana na mwenye kuogopesha hatawachochea tena watu kutenda vibaya.

Kwa kweli, wazo la kwamba Mungu atamaliza mambo yote yanayotokeza rushwa linaweza kuonekana kuwa ndoto tu. Lakini unaweza kujiuliza, ‘Je, kweli Mungu ana uwezo wa kuleta mabadiliko hayo? Ikiwa ana uwezo, sababu gani anakawia kufanya hivyo?’ Hayo ni maulizo mazuri na Biblia inatoa majibu yenye kufurahisha kwa maulizo hayo. * Tunakuomba uchunguze wewe mwenyewe yale ambayo Biblia inafundisha juu ya wakati ujao ulio karibu, wakati ambapo rushwa haitakuwa tena milele.

[Maelezo ya chini]

^ Ili kupata habari zingine juu ya namna tunavyoweza kusamehewa zambi kupitia kifo cha Yesu, usome sura ya 5 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ Yehova ni jina la Mungu katika Biblia.