Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Urafiki Wao Umefanya Miaka 60

Urafiki Wao Umefanya Miaka 60

Masimulizi Kuhusu Maisha ya Watu

Urafiki Wao Umefanya Miaka 60

Mangaribi moja wakati wa kipindi cha joto ya mwaka wa 1951, wanaume vijana wane, wote wakiwa na miaka 20 hivi, walisimama katika kabine za telefone huko Ithaca, New York, États-Unis, na kuanza kuita ndugu na marafiki wanaoishi katika maeneo ya mbali ya Michigan, Iowa, na Californie. Bila shaka walikuwa na habari nzuri ya kuwajulisha!

KATIKA Mwezi wa 2, 1951, mapainia 122 walifika katika South Lansing, New York, ili kuhuzuria somo la 17 la Masomo ya Gileadi. Ndugu Lowell Turner, William (Bill) Kasten, Richard Kelsey, na Ramon Templeton walikuwa kati ya mapainia hao waliokuwa tayari kupata mazoezi ili kuwa wamisionere. Kisha muda kidogo, Lowell na Bill kutoka Michigan, Richard kutoka Iowa, na Ramon kutoka Californie walikuwa marafiki.

Miezi mitano baadaye, wanafunzi wote walifurahi sana ilipotangazwa kama Ndugu Nathan Knorr kutoka makao makubwa atakuja kuwatolea hotuba. Ndugu hao wane walipenda sana kutumikia katika inchi moja ikiwa hilo lingewezekana. Je, wakati ulikuwa umefika sasa ili wajue mahali watakapotumikia? Bila shaka, ndiyo!

Wasiwasi wa wanafunzi hao uliongezeka wakati Ndugu Knorr alipoanza kutangaza inchi ambako wanafunzi wangetumwa. Wanafunzi hao wane waliokuwa na wasiwasi lakini ambao walikuwa wametulia, walikuwa wa kwanza kuitwa kwenye jukwaa, na mwishowe waliambiwa kama watatumikia katika inchi moja! Lakini wangetumwa katika inchi gani? Wanafunzi wenzao walishangaa na kupiga mikono ilipotangazwa kama watatumwa Alemanye.

Mashahidi wa Yehova duniani pote walipendezwa sana na habari kuhusu uaminifu wa Mashahidi wenzao katika Alemanye kuanzia mwaka wa 1933 wakati Hitler alipokuwa anatawala. Wanafunzi wengi wa Biblia wanakumbuka namna walivyotayarisha mavazi na misaada mingine ili kutumia ndugu zao wa Ulaya kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu. Mashahidi wenzetu katika Alemanye walituachia mufano muzuri wa imani, ujasiri, na kumutumaini Yehova. Ndugu Lowell anakumbuka kama wakati huo alianza kufikiri hivi: ‘Sasa tutawafahamia vizuri ndugu na dada zetu hao wapendwa.’ Hii ndiyo sababu marafiki hao wane walikuwa wenye furaha sana mangaribi hiyo na walitaka kujulisha ndugu na marafiki wao kuhusu jambo hilo!

SAFARI YA KUENDA ALEMANYE

Tarehe 27 Mwezi wa 7, 1951, marafiki hao wane waliingia katika mashua iliyoitwa SS Homeland na wakaanza safari ya siku 11 kutoka East River, New York, mupaka Alemanye. Ndugu Albert Schroeder, aliyekuwa mumoja wa waalimu wa Masomo ya Gileadi na ambaye baadaye alikuwa mushiriki wa Baraza Linaloongoza, alikuwa amewafundisha maneno fulani ya kwanza​-kwanza ya Kialemand. Sasa, wakiwa katika mashua hiyo pamoja na wasafiri wa Alemanye, labda wangejifunza mambo mengi. Lakini wasafiri hao walizungumuza luga zingine za Alemanye. Hilo liliwavuruga kabisa!

Siku ya Pili asubuhi, tarehe 7 Mwezi wa 8, kisha kuvumilia kichefuchefu (hali ya kutaka kutapika), ndugu hao walifika katika muji wa Hamburg, Alemanye. Mahali pote waliona alama za vita iliyokuwa imemalizika miaka sita iliyopita. Walihuzunika sana kwa sababu ya mambo waliyoona; kisha walichukua treni usiku ili kuenda katika muji wa Wiesbaden, mahali Beteli ilipokuwa wakati huo.

Asubuhi mapema, Siku ya Tatu, walikutana na Shahidi mumoja kwa mara ya kwanza. Shahidi huyo alikuwa na jina la Kialemand; jina lake lilikuwa Hans. Yeye aliwachukua kutoka kwenye kituo cha treni na kuwapeleka kwenye Beteli, na huko aliwaacha katika mikono ya dada mumoja muzee aliyekuwa mukali kidogo na ambaye hakujua kusema Kiingereza. Hata hivyo, dada huyo alifikiri kama ndugu hao watamuelewa ikiwa anasema kwa sauti ya juu. Lakini ijapokuwa aliongeza sauti, yeye na ndugu hao wane hawakuelewana, na hilo liliwasumbua sana. Mwishowe Ndugu Erich Frost, aliyekua mutumishi wa biro ya tawi, aliwasalimu kwa uchangamfu katika Kiingereza. Mambo yalianza kuwa mazuri.

Mwishoni mwa Mwezi wa 8, ndugu hao wane walihuzuria mukusanyiko wenye kichwa “Ibada Safi.” Huo ulikuwa mukusanyiko wao wa kwanza katika Kialemand huko Francfort​-sur-le-Main. Huzurio kubwa la watu 47 432 na kuona watu 2 373 waliobatizwa, kuliwaongezea wamisionere hao bidii na tamaa ya kuhubiri. Lakini siku chache baadaye, Ndugu Knorr alionyesha kama watabaki na kutumika kwenye Beteli.

Siku zilizopita Ramon hakufurahia kuenda kutumikia kwenye Beteli ya États-Unis sababu alipenda sana kazi ya umisionere. Richard na Bill hawakufikiria hata kidogo kama siku moja wangetumika kwenye Beteli. Lakini furaha waliyopata katika mugawo wao iliwasadikisha kama Yehova ndiye anayejua kile kinachotufaa zaidi. Ni jambo la hekima kufuata uongozi wa Yehova kuliko tu kufuata tamaa zetu. Mutu akijua hivyo atafurahia kumutumikia Yehova mahali popote na katika mugawo wowote atakaopewa.

VERBOTEN!

Ndugu wengi wa Beteli ya Alemanye walifurahia sana kuwa na ndugu hao wa Amerika katikati yao sababu hilo lingewatolea nafasi ya kujizoeza kusema Kiingereza pamoja nao. Lakini siku moja katika chumba cha kulia chakula, tumaini lao lilikatizwa kwa gafula. Ndugu Frost, anayezoea kuzungumuza kwa uchangamufu, alianza kuzungumuza katika Kialemand kuhusu jambo fulani ambalo lilionekana kuwa nzito kidogo. Watu wengi walinyamaza, na kuanza kuangalia tu sahani zao. Ndugu hao waliofika hivi karibuni hawakuelewa mambo yaliyokuwa yakisemwa, lakini walianza kutambua kama mambo yaliyokuwa yakisemwa yaliwahusu. Kwa hiyo Ndugu Frost aliposema kwa sauti ya juu, “VERBOTEN!” (“Imekatazwa!”) na kurudilia maneno hayo kwa sauti yenye mukazo, ndugu hao walishikwa na wasiwasi. Walifanya nini ili ndugu huyo aseme kwa sauti ya juu hivyo?

Kisha kula, kila mutu alienda haraka katika chumba chake. Kisha siku fulani, ndugu mumoja aliwaambia hivi: “Ili mutusaidie, munapaswa kuzungumuza Kialemand. Hiyo ndiyo sababu Ndugu Frost alisema VERBOTEN, maana yake, imekatazwa kuzungumuza nanyi Kiingereza mupaka mutakapojua luga yetu.”

Familia ya Beteli ilitii haraka. Hilo liliwasaidia ndugu hao wageni wajifunze Kialemand na liliwafundisha kama kila mara shauri linalotolewa na ndugu mwenye upendo ni lenye faida kwetu, hata kama ni vigumu kulitumia mwanzoni. Shauri la Ndugu Frost lilionyesha kama alihangaikia hali nzuri ya tengenezo la Yehova na alipenda ndugu zake. * Kwa hiyo ndugu hao wane walianza kumupenda.

KUFUNDISHWA NA MARAFIKI

Marafiki wetu wanaomuogopa Mungu wanaweza kutusaidia tuwe marafiki wazuri wa Yehova. Ndugu hao wane walijifunza mambo mengi kutoka kwa ndugu wa Alemanye nao walifundishana mambo mengi. Richard anaeleza hivi: “Lowell alikuwa na ujuzi mudogo wa Kialemand lakini alizungumuza luga hiyo vizuri kuliko sisi watatu. Kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa mukubwa kuliko sisi wote, mara moja tulimuomba atusaidie na kutufundisha luga hiyo.” Ramon anakumbuka: “Kisha kufanya mwaka mumoja huko Alemanye, nilifurahi sana wakati ndugu mumoja wa Suisse alipotutolea nyumba yake ya mbao ili tupitishe mapumuziko yetu humo! Tungepitisha majuma mawili sisi pekee yetu bila kuongea Kialemand! Lakini nilisahau kama tulikuwa na Lowell. Kila asubuhi alitulazimisha tusome na kuzungumuzia andiko la siku katika Kialemand! Siku zote tulizopitisha huko alitulazimisha kufanya hivyo. Lakini tulijifunza mambo mazuri. Ni jambo la hekima kufuata uongozi wa wale wanaokujali, hata kama haukubaliane nao wakati fulani. Kuwa na maoni hayo kumetuletea faida kwa miaka mingi na kumesaidia iwe rahisi kwetu kutii uongozi mbalimbali unaotolewa na tengenezo la Yehova.”

Kila mumoja wa marafiki hao wane alijifunza kupendezwa na sifa za mwenzake, kulingana na andiko la Wafilipi 2:3 linalosema: ‘Kwa unyenyekevu wa akili [muwaone] wengine kuwa bora kuliko ninyi.’ Kwa hiyo mara nyingi wengine walimuomba Bill afanye mambo fulani ambayo hawakuwa na uwezo wa kufanya vizuri kama yeye. Lowell anakumbuka: “Ilipokuwa lazima kuchukua hatua fulani ili kushugulikia mambo fulani magumu ao yasiyofurahisha, tulimuendea Bill. Sisi tulikosa uwezo ao tuliogopa kushugulikia mambo fulani magumu, lakini Bill alikuwa na uwezo wa kuyashugulikia kwa njia iliyotufurahisha sisi sote.”

NDOA ZENYE FURAHA

Ndugu hao waliamua kuoa mumoja baada ya mwengine. Walikuwa marafiki sababu wote walimupenda Yehova na walipenda utumishi wa wakati wote, kwa hiyo waliazimia kutafuta wanawake waliokuwa tayari kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza. Utumishi wa wakati wote uliwafundisha kama kutoa kunaleta furaha zaidi kuliko kupokea na tamaa za kibinafsi hazipaswi kutuzuia kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. Kwa hiyo walichagua dada waliojiamulia wenyewe kuanza utumishi wa wakati wote. Walioa na kuwa na maisha ya ndoa yenye furaha.

Ili urafiki ao ndoa iweze kudumu, ni jambo la maana kumupatia Yehova nafasi katika urafiki huo ao ndoa hiyo. (Mhu. 4:12) Ijapokuwa baadaye bibi wa Bill na wa Ramon walifariki, wote wawili walikuwa wamejionea kwamba bibi mwaminifu anaweza kuletea bwana yake furaha na kumutegemeza. Lowell na Richard wanaendelea kutegemezwa na bibi zao. Bill alioa tena bibi ambaye angemusaidia kubaki katika utumishi wa wakati wote.

Miaka fulani baadaye, walitumwa mahali mbalimbali, zaidi sana katika Alemanye, Autriche, Luxembourg, Canada, na États-Unis. Kwa hiyo, haikuwezekana marafiki hao wane wapitishe tena wakati mwingi pamoja kama vile walivyopenda kufanya. Kila mumoja wao aliishi mbali na wengine, lakini waliendelea kupashana habari, kufurahia pamoja baraka walizopata na kufarijiana wakati wa taabu. (Rom. 12:15) Tunapaswa kupendezwa na marafiki kama hao na kuwasamini sana. Wao ni zawadi nzuri kutoka kwa Yehova. (Met. 17:17) Ni vigumu kupata marafiki wa kweli katika ulimwengu huu. Lakini kila Mukristo wa kweli anaweza kuwapata kwa uwingi. Sisi Mashahidi wa Yehova, tunafurahia urafiki pamoja na waamini wenzetu duniani pote, na zaidi ya yote, tunafurahia urafiki pamoja na Yehova Mungu na Yesu Kristo.

Marafiki hao wane wamekutana na matatizo mengi kama yale ambayo sisi wote tunakutana nayo kwa kawaida, kama vile huzuni ya kufiwa na bibi, kupambana na ugonjwa mukali, matatizo ya kuwachunga wazazi waliozeeka, matatizo ya kulea watoto na wakati huo huo kufanya utumishi wa wakati wote, woga wa kukubali mugawo mupya, na sasa wanapambana na matatizo ya uzee. Lakini wamejionea pia kwamba marafiki, wanaoishi mbali ao karibu, wanawasaidia wale wanaomupenda Yehova kupambana na kila tatizo maishani.

URAFIKI UTAKAOENDELEA MILELE

Ni jambo la kufurahisha kuona kwamba Lowell, Ramon, Bill, na Richard walibatizwa wakiwa na miaka 18, 12, 11, na 10 na wote walianza utumishi wa wakati wote wakiwa kati ya miaka 17 na 21. Walitii maneno haya ya Mhubiri 12:1: ‘Mukumbuke, sasa, Muumba wako Mukuu katika siku za ujana wako.’

Ikiwa wewe ni kijana Mukristo, kubali mualiko wa Yehova wa kuingia katika utumishi wa wakati wote. Kisha kwa sababu ya fazili zake zisizostahiliwa, unaweza kupata furaha kama ya marafiki hao wane. Unaweza kuwa mwangalizi wa muzunguko, mwangalizi wa wilaya, mwangalizi wa eneo la dunia, kutumikia kwenye Beteli, kutumika katika Halmashauri ya Tawi, kufundisha kwenye Masomo ya Huduma ya Ufalme na Masomo ya Mapainia, na kutoa hotuba kwenye mikusanyiko. Marafiki hao wane walifurahi kujua kama maelfu ya watu wamefaidika kutokana na utumishi wao! Walipata mapendeleo yote hayo sababu tu walikubali mualiko wa Yehova wa kumutumikia kwa nafsi yao yote walipokuwa vijana.​—Kol. 3:23.

Leo, Lowell, Richard, na Ramon wanatumikia tena pamoja kwenye Beteli inayopatikana sasa katika muji wa Selters, Alemanye. Jambo la huzuni ni kwamba Bill alikufa katika mwaka wa 2010 akiwa painia wa pekee katika États-Unis. Kisha miaka karibu 60 ya urafiki, kifo kilimutenganisha Bill na marafiki wake watatu! Lakini Mungu wetu, Yehova, hawezi kusahau marafiki wake. Tuko hakika kama katika Ufalme wake, urafiki wowote ambao kifo kilivunja utarudishwa.

Muda mufupi tu mbele ya kufa, Bill aliandika hivi: “Katika miaka yote hiyo 60 ya urafiki wetu, siwezi kukumbuka wakati ambapo urafiki huo ulinivunja moyo. Kila siku nimeuona urafiki huo kuwa jambo la maana sana kwangu.” Kwa kuwa wanatazamia kuendelea na urafiki wao katika ulimwengu mupya, marafiki wenzake watatu waliongeza haraka maneno haya: “Urafiki wetu utaendelea milele.”

[Maelezo ya chini]

^ Simulizi lenye kutia moyo la maisha ya Ndugu Frost lilitolewa katika Munara wa Mulinzi wa Kiingereza wa tarehe 15/04/1961, ukurasa wa 244-249.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 18]

Furaha waliyopata katika mugawo wao iliwasadikisha kama Yehova ndiye anayejua kile kinachotufaa zaidi

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 21]

“Katika miaka yote hiyo 60 ya urafiki wetu, siwezi kukumbuka wakati ambapo urafiki huo ulinivunja moyo”

[Picha katika ukurasa wa 17]

Kuanzia kushoto mupaka kuume: Richard, Lowell, Ramon, na Bill. Urafiki wao ulianzia kwenye Masomo ya Gileadi

[Picha katika ukurasa wa 18]

Juu: Ramon akiongoza Masomo ya Huduma ya Ufalme; kuume: Richard akitumika kwenye Adresografe (mashine ya kuandika adresi za watu) kwenye Beteli huko Wiesbaden

[Picha katika ukurasa wa 19]

Juu: Ndugu Frost (kuume) na wengine wakati wa ziara ya Ndugu Knorr (kushoto); kuume: Tulipokuwa kwenye mapumuziko huko Suisse katika mwaka wa 1952

[Picha katika ukurasa wa 20]

Kuanzia kushoto mupaka kuume: Richard, Bill, Lowell, na Ramon walipokutana Selters kwa ajili ya programu ya kumutolea Yehova makao mapya ya Beteli katika mwaka wa 1984

[Picha katika ukurasa wa 21]

Kuanzia kushoto mupaka kuume: Ramon, Richard na Lowell